CUF waishambulia CHADEMA

nickname

JF-Expert Member
Dec 20, 2009
544
147
ALIYEKUWA kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni katika Bunge lililopita, Hamad Rashid Mohamed amewashambulia viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kuwataka wawe na msimamo na wafanye uamuzi kisiasa kama watu wazima.

Hamad amewatuhumu Chadema kuwa wabaguzi kwa kuwa walitaka kushirikiana na Chama Cha Wananchi (CUF) kuunda kambi hiyo lakini walidhamiria kuvitenga vyama vingine ya upinzani.


Mbunge huyo wa Wawi (CUF) alimewaeleza waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, wao (CUF) hawana shida ya vyeo kwa kuwa waliwahi kuwa na madaraka makubwa kuliko ya kwenye hiyo kambi ya upinzani bungeni.


Amewataka viongozi wa Chadema wawe ‘matured' na watambue pia gharama za kisiasa za kutomtambua Rais Jakaya Kikwete.


Kwa mujibu wa Hamad, CUF wana msimamo, waliwahi kufanya uamuzi mgumu na wakautekeleza hivyo Chadema wajifunze kwao (CUF).


Alisema, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alimfuata akamueleza nia ya kushirikiana na CUF kuunda kambi ya upinzani bungeni lakini kwa kuvitenga vyama vingine vyenye wabunge katika Bunge hilo.


Hamad amesema, alikataa wazo la Mbowe na akampa ushauri ambao hadi sasa hajautekeleza.


Mwanasiasa huyo amesema, CUF wanataka kambi ya upinzani bungeni ushirikishe vyama vyote vya upinzani, Chadema hawataki.


Hamad amesema, viongozi wa Chadema wamemkwaza Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, hivyo waende wakazungumze nao wayamalize.


Source: Basil Msongo, HabariLeo, Dodoma; Tarehe: 18th November 2010
 
Jamani kumbe CHADEMA wana maadui wengi ,CUF wanakeraa sana ,toka waunde serikali(waolewe) na CCM wana nyodo sana.Sijui mimba inawasumbua?? Khaa!!!!!!!!:angry:
 
Sijui wengine mmepokeaje taarifa hii, tutaona mtakavyochangia.

Mimi nilipoipokea tu moja kwa moja nikatafuta sentensi ambapo Hamadi ataeleza ni kanuni gani ya bunge ambayo CHADEMA wameivunja. Hakuna hata sentensi moja. Ni tatizo, kubwa tu la CUF.

Kuna ugonjwa mbaya unaoanzia hata kwenye jamii na kuendelea hadi kwenye makundi makubwa ya kitaifa kama vyama. Ugonjwa huo uko hivi: tunajua kwamba fulani anaweza kufanya jambo fulani tulipendalo kwa hiari yake na utashi wake tu.

Lakini badala ya kumuomba na kumuacha hiari yake na utashi wake vimsukume kufanya tupendalo kale ka-ugonjwa kanatusukuma tumshinikize hadi ile hiari yake igeuke kuwa kama lazima.

Ukweli unabaki palepale kwamba kelele hata kama ni za dunia nzima haziwezi kugeuza jambo la hiari kuwa la lazima. Tukifanikiwa kulilazimisha na hivi vishinikizo vyetu basi huo nao ni ufisadi mwingine wa kupora hiari ya mtu\chama na kuifanya lazima.

Ndicho wanachokifanya wenzetu hawa bahati nzuri Hamad haelezi kuwa kama CHADEMA waliwahi kushinikiza hiari kama wao sasa hivi.

Tumejadili kanuni za bunge kuhusu hili na hapa tuzisome tena vifungu vyake:

14(2):
Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia 12.5 ya Wabunge wote.

14(3):
Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya Wabunge wasiopungua 12.5% ya Wabunge wote.

14(4):
Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimoja ambavyo kila kimoja kina Wabunge 12.5% au zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kuliko vingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwili au zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya 12.5%, Wabunge wa vyama vinavyohusika watachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibu watakaokubaliana wenyewe.

15(1):
Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

15(2):
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateua Wabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.
 
ALIYEKUWA kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni katika Bunge lililopita, Hamad Rashid Mohamed amewashambulia viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kuwataka wawe na msimamo na wafanye uamuzi kisiasa kama watu wazima.

Hamad amewatuhumu Chadema kuwa wabaguzi kwa kuwa walitaka kushirikiana na Chama Cha Wananchi (CUF) kuunda kambi hiyo lakini walidhamiria kuvitenga vyama vingine ya upinzani.

Mbunge huyo wa Wawi (CUF) alimewaeleza waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, wao (CUF) hawana shida ya vyeo kwa kuwa waliwahi kuwa na madaraka makubwa kuliko ya kwenye hiyo kambi ya upinzani bungeni.

Amewataka viongozi wa Chadema wawe ‘matured' na watambue pia gharama za kisiasa za kutomtambua Rais Jakaya Kikwete.

Kwa mujibu wa Hamad, CUF wana msimamo, waliwahi kufanya uamuzi mgumu na wakautekeleza hivyo Chadema wajifunze kwao (CUF).

Alisema, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alimfuata akamueleza nia ya kushirikiana na CUF kuunda kambi ya upinzani bungeni lakini kwa kuvitenga vyama vingine vyenye wabunge katika Bunge hilo.

Hamad amesema, alikataa wazo la Mbowe na akampa ushauri ambao hadi sasa hajautekeleza.


Mwanasiasa huyo amesema, CUF wanataka kambi ya upinzani bungeni ushirikishe vyama vyote vya upinzani, Chadema hawataki.

Hamad amesema, viongozi wa Chadema wamemkwaza Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, hivyo waende wakazungumze nao wayamalize.

Source: Basil Msongo,HabariLeo ,Dodoma; Tarehe: 18th November 2010

- Well, hii ni nothing but cheap politics halafu you wonder who is immature here Mwenyekiti wa Chadema aliyeongea naye huyu kiongozi wa CUF in private, au huyu kiongozi wa CUF aliyeyaleta mambo ya Private kwenye Public? Sasa unaunda vipi umoja wa Upinzani bungeni na viongozi kama hawa wasioelewa kutenganisha maana ya ishus za private na ishus za public!

- I mean mambo kama haya yataishia kurudisha nyuma tu momentum ya ari ya wananchi waliyoionyesha kwenye huu uchaguzi kwamba wanataka mabadiliko, sasa kama CUF hawaelewi basi dawa ni kuachana nao tunachotaka ni upinzani wa kweli bungeni ili taifa liweze kunufaika na uwajibikaji utakaoletwa na Upinzani kweli bungeni hata kama ni mdogo, maana sasa itakwua nguvu ya hoja zaidi kuliko uwingi wa wabunge wa chama,

- CUF someni mabadiliko ya nyakati wananchi hawana tena muda wa kupoteza na hizi habari zisizo na anything good kwa taifa, zaidi tu ya kutafuta cheap popularity ambayo kama imeshindikana kupatikana kwenye kura, haiwezi kupatikana kwa kulumbana kwenye public na wapinzani wengine!, it stinks!


William.
 
Hamad anaposema gharama ya kutomkubali Jk anamaanisha hakubaliani na chadema kutomtambua jk.
Amesahau cuf hawakumtambua Karume kama rais kwa muda mrefu mpaka walipo laghaiwa na ccm ndipo wakamkubali.
Hamad ni mnafki na anataka chadema waonekane wabaya kwa kutofanya jambo la hiari.

La zaidi Hamad aseme wapi chadema imevunja kanuni ya kuanzisha kambi ya upinzani, aanzie hapo.
 
Jamani kumbe CHADEMA wana maadui wengi ,CUF wanakeraa sana ,toka waunde serikali(waolewe) na CCM wana nyodo sana.Sijui mimba inawasumbua?? Khaa!!!!!!!!:angry:
tusiwe blinds kwenye hili... Lazima tuelewe ukweli kabla ya kudhani CUF hawana point

Much as we seek for changes, it has to be very systematic and sophisticated... nadhani kuna haja ya CHADEMA ku-take things slow and cut off drama ili wajipange upya, including kujenga kambi ya upinzani

Nakumbuka niliuliza kuhusu kambi ya upinzani, nikaambiwa kwamba CHADEMA ndio walikua na haki ya kufanya, lakini naamini kama wangeamau kukaribisha wapinzani wote, hilo lingeleta maana zaidi na ile courtesy ingezaa imani ndani ya upinzani

Najifunza hayo masiasa because i am for changes lakini nadhani kuna tatizo kidogo... haiwezekani wewe tu ndio uchukiwe na kila mtu

Having said that, nashauri wakuu chadema wakae chini na wa-shut down media for three months kupunguza impurities and reach out to wapinzani ili kujenga upya upinzani
 
- Well, hii ni nothing but cheap politics halafu you wonder who is immature here Mwenyekiti wa Chadema aliyeongea naye huyu kiongozi wa CUF in private, au huyu kiongozi wa CUF aliyeyaleta mambo ya Private kwenye Public? Sasa unaunda vipi umoja wa Upinzani bungeni na viongozi kama hawa wasioelewa kutenganisha maana ya ishus za private na ishus za public!

- I mean mambo kama haya yataishia kurudisha nyuma tu momentum ya ari ya wananchi waliyoionyesha kwenye huu uchaguzi kwamba wanataka mabadiliko, sasa kama CUF hawaelewi basi dawa ni kuachana nao tunachotaka ni upinzani wa kweli bungeni ili taifa liweze kunufaika na uwajibikaji utakaoletwa na Upinzani kweli bungeni hata kama ni mdogo, maana sasa itakwua nguvu ya hoja zaidi kuliko uwingi wa wabunge wa chama,

- CUF someni mabadiliko ya nyakati wananchi hawana tena muda wa kupoteza na hizi habari zisizo na anything good kwa taifa, zaidi tu ya kutafuta cheap popularity ambayo kama imeshindikana kupatikana kwenye kura, haiwezi kupatikana kwa kulumbana kwenye public na wapinzani wengine!, it stinks!


William.

Loud and clear... CUF wameamua kuwa wanafiki... lakini cha maana ni chadema kurudi kambini na kupanga upya mambo yao

Thanks for the post
 
HIYO HABARI YENYEWE NAONA UMEITOA KWENYE GAZETI LENYE KINYESI CHA NGURUWE HABARI LEO GAZETI LINALONAJISIWA KILA KUKICHA,JANA MHARIRI WAKE KAANDIKA TAHARIRI YAKE AKISEMA HIVI chadema acheni kurudisha maendeleo ya watanzania nyuma. JAPO KUWA SINA KIPATO CHA KUNUNUA GAZETI NA MAGAZETI NAYASIKILIZIA YAKISOMWA REDIONI.NALICHUKIA HABARI LEO KAMA MATAPISHI
 
Habari leo linasomwa na wa2 wakarne ya kumi na nane na kumi na tisa sisi wa karne ya 21 tunasoma mwanahalisi rai na raia mwema,redio tunasikiliza bbc citizen kenya n.k,kwenye net jf fb n.k.sasa ukiniletea habari kutoka gazeti la mafisadi tena linalopinga mabadiliko nakuona mpuuzi tena ****,cuf ccm ni vyama vya kidini na kikabila vina ufuasi kwa waislam na waswahili tu. Nani ana haja ya kusikiliza upuuzi wa hamadi rashidi jumlisha lipumba mara mbatia sawasawa gawanya na lyatonga mrema sawasawa na ccm ya kanali kikwete.
 
Habari leo linasomwa na wa2 wakarne ya kumi na nane na kumi na tisa sisi wa karne ya 21 tunasoma mwanahalisi rai na raia mwema,sasa ukiniletea habari kutoka gazeti la mafisadi tena linalopinga mabadiliko nakuona mpuuzi tena ****,cuf ccm ni vyama vya kidini na kikabila vina ufuasi kwa waislam na waswahili tu. Nani ana haja ya kusikiliza upuuzi wa hamadi rashidi jumlisha lipumba mara mbatia sawasawa gawanya na lyatonga mrema sawasawa na ccm ya kanali kikwete.
 
Habari leo linasomwa na wa2 wakarne ya kumi na nane na kumi na tisa sisi wa karne ya 21 tunasoma mwanahalisi rai na raia mwema,cuf ccm ni vyama vya kidini na kikabila vina ufuasi kwa waislam na waswahili tu. Nani ana haja ya kusikiliza upuuzi wa hamadi rashidi jumlisha lipumba mara mbatia sawasawa gawanya na lyatonga mrema sawasawa na ccm ya kanali kikwete.
 
Jamani kumbe CHADEMA wana maadui wengi ,CUF wanakeraa sana ,toka waunde serikali(waolewe) na CCM wana nyodo sana.Sijui mimba inawasumbua?? Khaa!!!!!!!!:angry:
Hapa the main point ni kwamba Kafri hawezi kuwa mbele lazima awe mkiani, kama alivyofanyiwa muasisi wa CUF, kwa hiyo hapa ni kwamba CUF hawawezi kuungana na kafiri wataungana na wale ambao hawajakata tamaa na akhera CCM, maana viongozi wa juu ni Waislaam na mwislaam humuunga mkono mwislaam,,,,,Chunguza uone ukweli ndiyo huo
 
Kama ni kweli haya ni maneno ya bwana Hamad basi ni kakurupuka na kakosa busara. Naanza kudoubt kama kweli ana stahili sifa zote alizo kuwa akimwagiwa kama kiongozi wa upinzani. Lakini kwa vile CUF sasa hivi wana muafaka (makubaliano) na CCM na kwa vile wamepewa baadhi ya vyeo kule visiwani tutegemee objectivity toka kwa baadhi ya viongozi wa CUF kupungua especially wale viongozi wakuu.

Kwanza Mh. Hamad ana bidi atambue kitu kimoja. Inabidi atambue kwamba kikatiba Chadema ina ruhusiwa kuunda uongozi wa upinzani bungeni bila kushirikisha chama chochote kingine. Kwa hiyo chama chochote kitakacho alikwa na Chadema kujiunga nacho ni kwa mapenzi ya Chadema wenyewe. Sasa Hamad ana chukulia kama ni haki.

Pili ukiangalia idadi ya wabunge vyama vingine vilivyo pata huoni hata maana ya kuwaingiza kwenye uongozi rasmi wa upinzani Bungeni. Chama kina mbunge mmoja au wawili kita badilisha nini haswa ukizingatia CCM ina more than 50%? Hao wabunge wa vyama vingine (ukiachilia CUF) wange kuwa wana hitajika kuvusha idadi ya upinzani kuvuka asilimia 50 ningeelewa ila kwa sasa kuli hitahika ushirikiano wa vyama vikuu viwili vya upinzani.

Tatu ni kwamba siyo lazima uwe kwenye shadow cabinet kuwa mpinzani na kuleta upinzani wa kweli bungeni. Hao wabunge wawili watatu waliobaki bado wana weza kuleta changamoto nje ya baraza la kivuli humo bungeni. Kama kweli wana taka sauti zao kusikika basi wata sikika tu!

Swala la kujiuliza ni je kwa nini Hamad ana nga'ngania Chadema washirikishe vyama vingine Bungeni lakini haja wahi kutamka (as far as I know) na kudai kwa nini CCM haishirikishi vyama vingine kwenye serikali yao (ukiachilia mbali SMZ)? Mimi nadhani Hamad ana tambua kwamba kuwa na muafaka na CCM ZNZ na kuwa kwenye kambi ya upinzani Bungeni SMT itakua contradictory kwa maana kwa upande mmoja wata kuwa part of the government na kwa upande mwingine wata kuwa part of the opposition.Nadhani Hamad na CUF wana tafuta tu visingizio vya kuto kuji husisha na upinzani wakiogopa kuvuruga muafaka.
 
Cuf = ccm.

Kwa kiasi fulani you are right mkuu. Sasa CUF itaface identical crisis. Ita wezaje kutumikia mabwana wawili? Zanzibar wata kuwa sehemu ya serikali ila Muungano wao ni upinzani. Sasa wana jikuta katika position mbaya sana kisiasa kwa maana viongozi wa CUF wanabidi wapunguze sana makali yao ya upinzani bara ili kulinda maslahi yao Zanzibar. Hasara watakayo ipata ndiyo hiyo kuonekana CCM.

Sasa wana jikuta kwenye lose-lose situation:
1.CCM ikiboronga basi hata wao CUF kwenye uchaguzi wa 2015 hawata kuwa na nguvu ya kuongea haswa huko Zanzibar. Wata toa wapi moral authority ya kukosoa serikali wakati na wao wata kuwa sehemu ya serikali? Wata jitenganishaje na makosa ya CCM?

2. Hata CCM ifanye vizuri hamna atake ona haja ya CUF kwa maana wata waona ni wale wale kwa hiyo ni bora hata kuwapa CCM waendelee kuliko kuwapa CUF uongozi.

Nawaambieni wakuu CUF imejiweka mahara pabaya sana. In the short run baadhi ya viongozi wao ambao wame kuwa wakililia madaraka miaka nenda rudi wata pata vinafasi lakini in the wrong run wana kiua chama. It is sad that CUF is showing a lack of vision and judgement.
 
Kama ni kweli haya ni maneno ya bwana Hamad basi ni kakurupuka na kakosa busara. Naanza kudoubt kama kweli ana stahili sifa zote alizo kuwa akimwagiwa kama kiongozi wa upinzani. Lakini kwa vile CUF sasa hivi wana muafaka (makubaliano) na CCM na kwa vile wamepewa baadhi ya vyeo kule visiwani tutegemee objectivity toka kwa baadhi ya viongozi wa CUF kupungua especially wale viongozi wakuu.

Kwanza Mh. Hamad ana bidi atambue kitu kimoja. Inabidi atambue kwamba kikatiba Chadema ina ruhusiwa kuunda uongozi wa upinzani bungeni bila kushirikisha chama chochote kingine. Kwa hiyo chama chochote kitakacho alikwa na Chadema kujiunga nacho ni kwa mapenzi ya Chadema wenyewe. Sasa Hamad ana chukulia kama ni haki.

Pili ukiangalia idadi ya wabunge vyama vingine vilivyo pata huoni hata maana ya kuwaingiza kwenye uongozi rasmi wa upinzani Bungeni. Chama kina mbunge mmoja au wawili kita badilisha nini haswa ukizingatia CCM ina more than 50%? Hao wabunge wa vyama vingine (ukiachilia CUF) wange kuwa wana hitajika kuvusha idadi ya upinzani kuvuka asilimia 50 ningeelewa ila kwa sasa kuli hitahika ushirikiano wa vyama vikuu viwili vya upinzani.

Tatu ni kwamba siyo lazima uwe kwenye shadow cabinet kuwa mpinzani na kuleta upinzani wa kweli bungeni. Hao wabunge wawili watatu waliobaki bado wana weza kuleta changamoto nje ya baraza la kivuli humo bungeni. Kama kweli wana taka sauti zao kusikika basi wata sikika tu!

Swala la kujiuliza ni je kwa nini Hamad ana nga'ngania Chadema washirikishe vyama vingine Bungeni lakini haja wahi kutamka (as far as I know) na kudai kwa nini CCM haishirikishi vyama vingine kwenye serikali yao (ukiachilia mbali SMZ)? Mimi nadhani Hamad ana tambua kwamba kuwa na muafaka na CCM ZNZ na kuwa kwenye kambi ya upinzani Bungeni SMT itakua contradictory kwa maana kwa upande mmoja wata kuwa part of the government na kwa upande mwingine wata kuwa part of the opposition.Nadhani Hamad na CUF wana tafuta tu visingizio vya kuto kuji husisha na upinzani wakiogopa kuvuruga muafaka.
The big issue here ni Udini tu, naamini kama chadema viongozi wangekuwa akina Abdallah, Mohammed wangekubali na si swala la muafaka hapa mkuu.
 
The big issue here ni Udini tu, naamini kama chadema viongozi wangekuwa akina Abdallah, Mohammed wangekubali na si swala la muafaka hapa mkuu.

Huwa sikimbiliagi kusema kitu fulani ni udini mkuu. Kuna mambo ukiya angalia juu juu utadhani ni udini ila it's deeper than that. Tukubali ukweli kwamba CUF kuwa sehemu ya serikali ya CCM Zanzibar kutaipa wakati mgumu CUF kushirikiana na vyama vya upinzani kwenye Bunge la Muungano. Wata wakosoaje?

Pia sababu nyingine ninayo weza kutoa ni labda wivu mkuu. CUF ndiyo walikua chama kikuu cha upinzani kwa muda mrefu na huyu bwana Hamad ndiyo aliye kuwa kiongozi wa upinzani kwenye Bunge la tisa. Kwa hiyo ina wezekana kuna friction fulani kati ya hivi vyama kwa kimoja kujiona ndicho chama kipya kuu (na CHadema ina haki ya kufikiria hivyo) na CUF kujalibu kujionyesha kwamba wao bado wana nguvu. Hapa ni tatizo la transition of oppositional power kutoka CUF kwennda Chadema. CUF hawataki kuachia na Chadema ina demand the respect it deserves.
 
Huwa sikimbiliagi kusema kitu fulani ni udini mkuu. Kuna mambo ukiya angalia juu juu utadhani ni udini ila it's deeper than that. Tukubali ukweli kwamba CUF kuwa sehemu ya serikali ya CCM Zanzibar kutaipa wakati mgumu CUF kushirikiana na vyama vya upinzani kwenye Bunge la Muungano. Wata wakosoaje?

Pia sababu nyingine ninayo weza kutoa ni labda wivu mkuu. CUF ndiyo walikua chama kikuu cha upinzani kwa muda mrefu na huyu bwana Hamad ndiyo aliye kuwa kiongozi wa upinzani kwenye Bunge la tisa. Kwa hiyo ina wezekana kuna friction fulani kati ya hivi vyama kwa kimoja kujiona ndicho chama kipya kuu (na CHadema ina haki ya kufikiria hivyo) na CUF kujalibu kujionyesha kwamba wao bado wana nguvu. Hapa ni tatizo la transition of oppositional power kutoka CUF kwennda Chadema. CUF hawataki kuachia na Chadema ina demand the respect it deserves.
Muasisi wa CUF ni nani? na kwa nini alitolewa? wakapangwa Wale wasiokata tamaa na akhera. It implies the same mkuu wa CCM na Mkuu wa CUF ni waislaam hawawezi kuangushana. Lakini kwa Chadema wakuu ni kina nani?... We dont need to go to school to know this
 
Muasisi wa CUF ni nani? na kwa nini alitolewa? wakapangwa Wale wasiokata tamaa na akhera. It implies the same mkuu wa CCM na Mkuu wa CUF ni waislaam hawawezi kuangushana. Lakini kwa Chadema wakuu ni kina nani?... We dont need to go to school to know this

Mkuu tukiangalia hivyo na tukienda down that road utaanza kuona kwamba wote wana makosa. Maana CUF wanaonekana ni Waislamu na Chadema Wakatoliki/Wachaga. Udini upo na ukabila upo sikatai. Hata katika hali ya kawaida mtu ukiwa na nafasi uka kutana na mtu wa kabila lako au dini yako una kuta ni rahisi zaidi kuwasaidia ila haimaanishi wewe ni mkabila au mdini.

Ila mkuu hamna haja ya mimi na wewe kubishana. Unaweza kuwa sahihi kusema udini umechangia nami nasema muafaka nao kwa kiasi kikubwa umechangia. Mbona wakati CUF ndiyo wameunda baraza kivuli bunge lililo pita wali washirikisha Chadema? Wakati huo udini haukuepo? Kwa mantiki hilo swala la kwanza linalo kuja kichwani mwangu ni kwamba it's not a matter of "udini" per se bali inferiority complex inayo izuia CUF kuwa chini ya Chadema kwenye baraza kivuli ndani ya Bunge.
 
Back
Top Bottom