CUF wafuata mkia wa CHADEMA kuwaunga mkono maandamano nchi nzima

Kaazi kweli kweli yaani kwako wewe historia na sia za Tanzania zimeanzia 2010 baada ya Dr. Slaa kugombea urais umesahau kuwa CUF ndiyo mwanzilishi wa siasa za maandamano kwenye nchi hii hadi mwenyekiti wake Prof. Ibrahimu Haruna Lipumba (Mnyamwezi) akavunjwa mkono. Na Cuf ikafikia kuitwa ngangari huku polisi wakijiita ngunguri. Ama kweli taifa limepokea wapiga kura wapya wengi sasa nimeamini..

Haya sasa! Wameanza kugombea maandamano! Tuliyasisi sisi enzi zile hata tukaitwa sijui nani vile? Sijui Prof. wetu ndie mwanzilishi wa siasa za maandamano! Wizi mtupu! Si juzi mlikuwa mnayapinga nyie kwa ushawishi wa magamba na baadhi ya viongozi wenu wa maisha ya ahera kwamba yanavunja amani, mara hii yamegeuka lulu ghafla?

Hapo kwenye red/bold kama usemavyo ni kweli kabisa taifa limepokea wapiga kura wapya. Waliokuwa wananyonya enzi zenu muflisi za ngunguri na ngangari ambazo hata thinking capacity yenu ilikuwa ndogo ndio vijana na wapiga kura makini na mahiri wa leo na ni viongozi na taifa la kesho. Heko watoto na vijana wa Tanzania. Sasa hivi tunataka hoja za kujenga taifa na sio siasa za shari na udini.
 
huu nao ni ujinga wa kisiasa kama sio upumbavu. hata wakiuawa wayu wangap kwa kuwa tu inaaminika ni wafuasiw a chadema basi cuf hawaandamani kupinga wala hawawaungi mkono chadema katika kupinga, akiuawa mmoja tu anayesadikiwa kuwa mwanachama wa cuf utasikia,,, aaa kumbe chadema wao sahihi!!... mazezeta haya!! ndo yanaamka sasa na kubaini uvunjwaji wa haki za binadamu baada ya mtu wao kuuawa. kumbe hata mtu wa ccm akiuawa na ccm wataamka!

siasa gani hizi hadi watu mtu wako auawe ndo ujue thamani ya binadamu na ukatili wa polisi? ina maana tanzania ya leo chama kinapanua domo lake pale tu mwanachama wao anapouawa?

nashauri chadema wajitokeze katika maandamano yatakayoitishwa na cuf kulaani mauaji haya ili kuonyesha kuwa chadema wanalaani mauaji ya raia yanayofanywa na polisi bila kujali itikadi za kisisa na hapo watadhihirisha ukomavu wao na kupata crediti zaidi katika harakati zao za kutetea haki za binadamu

MKUKI KWA MCHUNGU, KWA BINADAMU NGURUWE. cuf mlikuwa wapi siku zote???? mshadai talaka kwa ccm?? kama bado daini kwanza ndo mtuambie habari za maandamano.
 
Huu ndo unafiki ambao tunahitaji kuupiga vita hapa nchini. Waswahili wanasema kama watu wanajenga nyumba moja hakuna haja ya kugombania fito. Walianza kuwapiga vijembe wenzao tukadhan ni kwa sababu ya ndoa yao. Walidhan kutoa ilani yao ya uchaguzi ndo mambo yatawanyookea. Inabidi nao waombe radhi na napenda niwashauri wajaribu kufanya mambo yao ya wengine wawaachie hao wengine.....!

Wote wanaopenda haki wayalaani matukio ya polisi kuuwa raia hovyo, bila kujali kama hao raia ni wakristo, waislam, wanachama wa CCM, CHADEMA, CUF hata wasio kuwa na vyama. Tabia hii haikubaliki kabisa.
 
Back
Top Bottom