Elections 2010 CUF sasa yairarua CHADEMA Igunga; Hamad Rashid Mohamed asema CHADEMA sio chama cha kitaifa

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Majira News


Mbunge wa Lindi kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Bw. Salum Baruani akihutubia wananchi wa Kijiji cha Ngwamashimba wilayani Igunga wakati wa mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona jana.
*Yadai haijakomaa kisiasa, si cha kitaifa

Na Peter Mwenda, Igunga

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimewataka wananchi wa Igunga kutokipigia kura Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kuwa si chama cha kitaifa na hakijakomaa kisiasa.

Hayo yalisemwa na Mbunge wa Wawi, Bw. Hamad Rashid Mohamed, wakati akimnadi mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo, Bw. Leopold Mahona katika viwanja vya Barafu mjini hapa.

Mbunge aliwahi kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni kabla ya Bw. Freeman Mbowe wa CHADEMA kuchukua nafasi hiyo, alidai kuwa chama hicho hakijakomaa kisiasa ndiyo maana kinajihusisha na vitendo vya vurugu ikiwemo kumwaga tindikali, kupiga risasi na mengine na kwamba hiyo inaonesha hakiwezi kuleta maendeleo ya wananchi.

Alisema chama hicho kina ubinafsi, ndiyo maana kilijitenga bungeni na kuunda umoja wa wabunge wa CHADEMA peke yao tofauti na wakati alipokuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni ambapo alishirikisha wabunge wa vyama vyote vya upinzani wakiwemo wa chama hicho bila ubaguzi.

Alidai sera za CHADEMA hazina tofauti za CCM ambao wanagawa madaraka kwa watoto wao, ndugu na jamaa badala ya kufuata utaratibu wa uongozi katika jamii.

Bw. Rashid aliyewasili mjini hapa juzi na helkopta ya CUF kujumuika na wabunge wengine wa chama hicho hivyo kufanya idaid yao kufikia 20, alisema chama chake ni cha kitaifa ambacho kina viongozi pande zote za muungano.

“Makamu wa Rais Zanzibar ni Katibu Mkuu wa CUF, sisi wabunge wa Zanzibar tumekuja kwa gharama zetu kumsaidia mwenzetu aingie bungeni kuwakomboa watu wa Igunga, niambieni CHADEMA kuna kiongoi gani Zanzibar,” alihoji Bw. Rashid.

Alisema wananchi wa Igunga wakitaka maendeleo ya kweli wamchague, Bw. Mahona kuwa mbunge kwa kuwa wana kila sababu ya kufanya hivyo ili kubadilisha maisha yao.

Naye Meneja Kampeni wa mgombea wa CUF, Bw. Antony Kayange, alisema wapiga kura wasipoteze muda kukipigia kura CCM kuwa wanakumbuka kumleta Waziri wa Ujenzi, Bw. John Magufuli kuwaongopea.

Alisema anawadaganya kujenga daraja la mto Mbutu ambalo limeahidiwa kujengwa miaka mingi iliyopita bila ahadi hiyo kutimizwa.

“Huyu Magufuli amekuwa madarakani kwa miaka 11 mbona hata siku moja hakufikiria kuja Igunga angalau kuona kero za wananchi, leo anakuja kudanganya kujenga daraja la Mbutu huo ni uongo, msikubali kurubuniwa kupigia kura CCM,” alisema Bw. Kayange.

Naye Naibu Katibu wa CUF Tanzania Visiwani, Bw. Ismail Jussa, alisema wananchi wa Igunga wasikubali kudanganywa na vyama vingine kwa kuwa wataendelea kukabiliana na matatizo waliyonayo bila kupata ufumbuzi.

Alisema katika majimbo ambayo CUF inaongoza yana maendeleo makubwa kutokana na kuwa na uwezo mkubwa kujenga hoja za wananchi na kuziwasilisha serikalini kufanyiwa kazi.

Mgombea ubunge Bw. Mahona akiomba kura kwa wananchi alisema kamwe hatakimbia jimbo lake kama wanavyofanya wabunge wengine bali atatumia muda wake mwingi kuwatumikia wananchi wa Igunga.


http://majira-hall.blogspot.com/2011/09/cuf-sasa-yairarua-chadema-igunga.html#http://majira-hall.blogspot.com/2011/09/cuf-sasa-yairarua-chadema-igunga.html#
 
CHADEMA waliweka wabunge Zanzibar lakini hawakuchaguliwa ndio sababu hiyo CHADEMA sio chama kitaifa?

Kwahiyo CUF kimekuwa chama cha kitaifa 2010 baada ya kupata mbunge Lindi?

Hawajui kuwa Chadema wana wabunge 3 wa kuteuliwa toka Zanzibar na Pemba? si Utaifa huo?
 
Majira News



Mbunge wa Lindi kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Bw. Salum Baruani akihutubia wananchi wa Kijiji cha Ngwamashimba wilayani Igunga wakati wa mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona jana.

*Yadai haijakomaa kisiasa, si cha kitaifa

Na Peter Mwenda, Igunga

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimewataka wananchi wa Igunga kutokipigia kura Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kuwa si chama cha kitaifa na hakijakomaa kisiasa.

Hayo yalisemwa na Mbunge wa Wawi, Bw. Hamad Rashid Mohamed, wakati akimnadi mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo, Bw. Leopold Mahona katika viwanja vya Barafu mjini hapa.

Mbunge aliwahi kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni kabla ya Bw. Freeman Mbowe wa CHADEMA kuchukua nafasi hiyo, alidai kuwa chama hicho hakijakomaa kisiasa ndiyo maana kinajihusisha na vitendo vya vurugu ikiwemo kumwaga tindikali, kupiga risasi na mengine na kwamba hiyo inaonesha hakiwezi kuleta maendeleo ya wananchi.

Alisema chama hicho kina ubinafsi, ndiyo maana kilijitenga bungeni na kuunda umoja wa wabunge wa CHADEMA peke yao tofauti na wakati alipokuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni ambapo alishirikisha wabunge wa vyama vyote vya upinzani wakiwemo wa chama hicho bila ubaguzi.

Alidai sera za CHADEMA hazina tofauti za CCM ambao wanagawa madaraka kwa watoto wao, ndugu na jamaa badala ya kufuata utaratibu wa uongozi katika jamii.

Bw. Rashid aliyewasili mjini hapa juzi na helkopta ya CUF kujumuika na wabunge wengine wa chama hicho hivyo kufanya idaid yao kufikia 20, alisema chama chake ni cha kitaifa ambacho kina viongozi pande zote za muungano.

“Makamu wa Rais Zanzibar ni Katibu Mkuu wa CUF, sisi wabunge wa Zanzibar tumekuja kwa gharama zetu kumsaidia mwenzetu aingie bungeni kuwakomboa watu wa Igunga, niambieni CHADEMA kuna kiongoi gani Zanzibar,” alihoji Bw. Rashid.

Alisema wananchi wa Igunga wakitaka maendeleo ya kweli wamchague, Bw. Mahona kuwa mbunge kwa kuwa wana kila sababu ya kufanya hivyo ili kubadilisha maisha yao.

Naye Meneja Kampeni wa mgombea wa CUF, Bw. Antony Kayange, alisema wapiga kura wasipoteze muda kukipigia kura CCM kuwa wanakumbuka kumleta Waziri wa Ujenzi, Bw. John Magufuli kuwaongopea.

Alisema anawadaganya kujenga daraja la mto Mbutu ambalo limeahidiwa kujengwa miaka mingi iliyopita bila ahadi hiyo kutimizwa.

“Huyu Magufuli amekuwa madarakani kwa miaka 11 mbona hata siku moja hakufikiria kuja Igunga angalau kuona kero za wananchi, leo anakuja kudanganya kujenga daraja la Mbutu huo ni uongo, msikubali kurubuniwa kupigia kura CCM,” alisema Bw. Kayange.

Naye Naibu Katibu wa CUF Tanzania Visiwani, Bw. Ismail Jussa, alisema wananchi wa Igunga wasikubali kudanganywa na vyama vingine kwa kuwa wataendelea kukabiliana na matatizo waliyonayo bila kupata ufumbuzi.

Alisema katika majimbo ambayo CUF inaongoza yana maendeleo makubwa kutokana na kuwa na uwezo mkubwa kujenga hoja za wananchi na kuziwasilisha serikalini kufanyiwa kazi.

Mgombea ubunge Bw. Mahona akiomba kura kwa wananchi alisema kamwe hatakimbia jimbo lake kama wanavyofanya wabunge wengine bali atatumia muda wake mwingi kuwatumikia wananchi wa Igunga.

Huyo hamadi bila kuitaja chadema hawezi kujenga hoja kwani anajua kwa kuitaja chadema ndio anapata attention.
Naona marupurupu ya kiongozi wa upinzani bado yanamtoa roho.
Mwenziye Mbowe hana shida na hayo marupurupu ndio maana hata shangingi alilirudisha.
Poor hamadi, anazidi kwisha.
 
Kumjadili Hamad ni sawa na kutaka tuanze kumjadili Nape hapa .Hamad is dead walking mind alidhani CUF na udini inaweza lolote .Hawa ni wa kupuuza .Waache waige kupanda helikopta then wapotee .
 
Mimi ninachoona ni vyama kukosoana bila ya kuwaeleza wananchi mipango ya maendeleo.
Kukosoa na kulaumu ni rahisi, kwani hutumii nguvu (pengine hata akili) kwa kukosoa bali bla bla bla!
Nasikitika kuwa vyama vimepoteza muda bure kukosoana, kukashifiana na kupigana badala ya kushughulikia maendeleo.
Pamoja na yote, nina hakika wana Igunga wana akili za kutosha kumjua nani mbaya wao. Ninachowaomba watumie haki yao ya kura kupata haki yao ya maendeleo.
 
Mfa maji siku zote haishi kutapatapa, hana cha kuwaambia wananchi kuhusu chama chake na jinsi gani kitainua maisha ya walala hoi Igunga? Poor him.
 
Majira News


Mbunge wa Lindi kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Bw. Salum Baruani akihutubia wananchi wa Kijiji cha Ngwamashimba wilayani Igunga wakati wa mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea wa chama hicho, Bw. Leopold Mahona jana.

*Yadai haijakomaa kisiasa, si cha kitaifa

Na Peter Mwenda, Igunga

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimewataka wananchi wa Igunga kutokipigia kura Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kuwa si chama cha kitaifa na hakijakomaa kisiasa.

Hayo yalisemwa na Mbunge wa Wawi, Bw. Hamad Rashid Mohamed, wakati akimnadi mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo, Bw. Leopold Mahona katika viwanja vya Barafu mjini hapa.

Mbunge aliwahi kuwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni kabla ya Bw. Freeman Mbowe wa CHADEMA kuchukua nafasi hiyo, alidai kuwa chama hicho hakijakomaa kisiasa ndiyo maana kinajihusisha na vitendo vya vurugu ikiwemo kumwaga tindikali, kupiga risasi na mengine na kwamba hiyo inaonesha hakiwezi kuleta maendeleo ya wananchi.

Alisema chama hicho kina ubinafsi, ndiyo maana kilijitenga bungeni na kuunda umoja wa wabunge wa CHADEMA peke yao tofauti na wakati alipokuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni ambapo alishirikisha wabunge wa vyama vyote vya upinzani wakiwemo wa chama hicho bila ubaguzi.

Alidai sera za CHADEMA hazina tofauti za CCM ambao wanagawa madaraka kwa watoto wao, ndugu na jamaa badala ya kufuata utaratibu wa uongozi katika jamii.

Bw. Rashid aliyewasili mjini hapa juzi na helkopta ya CUF kujumuika na wabunge wengine wa chama hicho hivyo kufanya idaid yao kufikia 20, alisema chama chake ni cha kitaifa ambacho kina viongozi pande zote za muungano.

“Makamu wa Rais Zanzibar ni Katibu Mkuu wa CUF, sisi wabunge wa Zanzibar tumekuja kwa gharama zetu kumsaidia mwenzetu aingie bungeni kuwakomboa watu wa Igunga, niambieni CHADEMA kuna kiongoi gani Zanzibar,” alihoji Bw. Rashid.

Alisema wananchi wa Igunga wakitaka maendeleo ya kweli wamchague, Bw. Mahona kuwa mbunge kwa kuwa wana kila sababu ya kufanya hivyo ili kubadilisha maisha yao.

Naye Meneja Kampeni wa mgombea wa CUF, Bw. Antony Kayange, alisema wapiga kura wasipoteze muda kukipigia kura CCM kuwa wanakumbuka kumleta Waziri wa Ujenzi, Bw. John Magufuli kuwaongopea.

Alisema anawadaganya kujenga daraja la mto Mbutu ambalo limeahidiwa kujengwa miaka mingi iliyopita bila ahadi hiyo kutimizwa.

“Huyu Magufuli amekuwa madarakani kwa miaka 11 mbona hata siku moja hakufikiria kuja Igunga angalau kuona kero za wananchi, leo anakuja kudanganya kujenga daraja la Mbutu huo ni uongo, msikubali kurubuniwa kupigia kura CCM,” alisema Bw. Kayange.

Naye Naibu Katibu wa CUF Tanzania Visiwani, Bw. Ismail Jussa, alisema wananchi wa Igunga wasikubali kudanganywa na vyama vingine kwa kuwa wataendelea kukabiliana na matatizo waliyonayo bila kupata ufumbuzi.

Alisema katika majimbo ambayo CUF inaongoza yana maendeleo makubwa kutokana na kuwa na uwezo mkubwa kujenga hoja za wananchi na kuziwasilisha serikalini kufanyiwa kazi.

Mgombea ubunge Bw. Mahona akiomba kura kwa wananchi alisema kamwe hatakimbia jimbo lake kama wanavyofanya wabunge wengine bali atatumia muda wake mwingi kuwatumikia wananchi wa Igunga.

CUF inahubiri ukanda na uzanzibari wakati CCM ikihubiri UDINI kuwatenganisha watu kulingana na dini zao wakati chadema wakizungumzia sera na jinsi watakavyowasaidia wananchi katika matatizo yao waliyonayo kama alivyosema ZITTO kuwaondolea kero nyingi ikiwemo kupiga marufuku michango isiyo na manufaa kama walivyofanya singida mashariki kwa Tundu mwana wa Lisu.
 
Hamadi Rashid ni mwehu,wao wamefunga ndoa na ccm,hivyo alitaka cdm nao waingie kwenye hiyo ndoa?Hamadi utaifa unao usema hapo hauelewe. Kwani cdm si wanao wabunge wa kuteuliwa toka nzn? We unataka nini haswa?Fisi maji mkubwa we.mlafi mkubwa sana wa madaraka wewe,toka wakunyime uongozi wa kambi rasmi unachuki sana we kizee cha kale,kula jeuri yako.
 
CUF maji ya shingo... wanasindikiza tu uchaguzi na wakati kila mtu anajua hawawezi kuchukua... wanapoteza ela za bure tu bora wangeenda kufanya maendeleo huko waliko chaguliwa.. mpambano igunga ni kati ya CCM na CHADEMA.. na CDM ndio kinachopewa nafasi ya juu kuliko vyote
 
CUF ni chama cha kidini,ukimuondoa mtatiro ambaye naye naona siku hizi ana SIJIDA,kuna kiongozi gani mwingine ambaye sio muislamu,CUF hawana hata mbunge mmoja wa dini ya kikristu,ni chama cha waarabu.
 
Hamadi Rashid ni mwehu,wao wamefunga ndoa na ccm,hivyo alitaka cdm nao waingie kwenye hiyo ndoa?Hamadi utaifa unao usema hapo hauelewe. Kwani cdm si wanao wabunge wa kuteuliwa toka nzn? We unataka nini haswa?Fisi maji mkubwa we.mlafi mkubwa sana wa madaraka wewe,toka wakunyime uongozi wa kambi rasmi unachuki sana we kizee cha kale,kula jeuri yako.

punguza ukali mkuu! anatafuta umaarufu, teh teh teh teh!
 
Ndio siasa zetu za Tanzania, mwenzako akimwaga ugali wewe unamwaga mboga!
 
hamadi rashid atia huruma, maalim seif naye du! wapemba wenzie wamezama melini kizembe yeye anakata whisky ikulu zenji, hajaongeza uwajibikaji serikali hata chembe!
 
CHADEMA waliweka wabunge Zanzibar lakini hawakuchaguliwa ndio sababu hiyo CHADEMA sio chama kitaifa?

Kwahiyo CUF kimekuwa chama cha kitaifa 2010 baada ya kupata mbunge Lindi?

Hawajui kuwa Chadema wana wabunge 3 wa kuteuliwa toka Zanzibar na Pemba? si Utaifa huo?
Maji na mafuta daima ujitenga!jamaa wa CCM B wa pumba hawajambo!
 
CUF =CCM siwezi kushangaa wakiungana kuishambulia chadema, sasa huyu naye amekuja kumnadi mgombea au amekuja kuiponda CHADEMA?Hizi ni siasa za kitoto kabisa acheni kulopoka upuuzi, mwageni sera zenye tija kwa wananchi,ongeleeni maendeleo mtawafanyia nini wananchi,ACHENI UJINGA.
 
hamadi rashid atia huruma, maalim seif naye du! wapemba wenzie wamezama melini kizembe yeye anakata whisky ikulu zenji, hajaongeza uwajibikaji serikali hata chembe!
Wewe wacha uongo waislamu hawanywagi Whisky!!
 
Kumjadili Hamad ni sawa na kutaka tuanze kumjadili Nape hapa .Hamad is dead walking mind alidhani CUF na udini inaweza lolote .Hawa ni wa kupuuza .Waache waige kupanda helikopta then wapotee .

Huyo anaendelea kuziota posho alizokuwa akipata alipokuwa KUB, ndio maana haishi kumtaja mbowe.

Hata hivyo cuf kujaribu kupambana na chadema badala ya ccm si habari tena kwa kuwa wao ni wanandoa lazima wapigane tafu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom