CUF, NCCR, TLP waliwaunga mkono CHADEMA kudai TUME HURU na kugoma kwao

eliesikia

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
787
755
Madai ya KATIBA mpya na TUME HURU ni madai ya upinzani wote.. Lakini wengine wameshachoka ndio maana CUF, NCCR wameamua kuwaachia CHADEMA ambao wamepata bahati ya kuwa wengi bungeni na sasa harakati na matunda ya CHADEMA yataonekana kuinufaisha kambi nzima ya upinzani na wananchi.. Pamoja na wanaharakati wa haki za binadamu ambao wote wanadai hili.....
Kutoka bungeni ni sahihi katika siasa??? Njia hii ni ya kiungwana au maandamano ndio uungwana????

1. Rejea kule CUBA wabunge walishawahi kutoka wakati Fidel Castro anaongea kwa minajili ya kutokubaliana nae na utawala wake wa kijeshi...
2. Marekani walishwahi kutoka nje kwenye mkutano baada ya kiongozi wa Iran kuanza kuongea kwa minajiri ya kutokubaliana nae
3. Iran waliwahi kutoka nje kwa minajiri ya kukataa Marekani kuingilia nchi za kiislamu
4. Rejea nchi mbalimbali na nyingine juzijuzi tuuu wametoka nje kuonyesha kutokukubaliana, India, Malaysia(mwaka 2008 kuhusu DNA bill ), Pakistan, Japan, South Africa(Zuma insult), Zambia(Electroral bill), Kuwait, Gambia, iraqi(residaa reelect), Sri Lanka na nchi nyingine nyingi...


TAFAKURI:
Kama wewe ni mtu wa kawaida na una uelewa mkubwa wa siasa kutoka nje ni siasa pia kwa kuwa unaonyesha jinsi gani unataka meza ya maelewano iharikishwe... Mimi nakwambia hivi kama CUF wasingekuwa watawala Zanzibar wao ndio wangeongoza msafara.. Kwa kuwa madai ya tume isiyo huru hata wao Pamoja na Lipumba wamekuwa wakilalamikia toka 1995...
Hata hao NCCR nao waliwahi kufungua kesi mahakamani kudai tume huru ya uchaguzi... Kusema kweli sio jambo la kushangaza kabisa...
Kilichotokea pale ni lazima kila mtu na jamii ya kimataifa itamshauri Jk kuingia meza ya makubaliano ili uchaguzi ujao uwe huru na wa haki.. JK asiteue tena refa wa uchaguzi kama tulivyozoea...
CUF, NCCR, TLP, UDP kama wanaongea siasa bila vitendo ni ajabu sana... Wakati mwingine ni lazima uonyeshe uhitaji wa hali ya juu wa kile unachokitaka na si vinginevyo...

Kuna watu wanadai njia iliyotumika si sahihi??? Waniambie wanayoona ni sahihi ni ipi!!! Kama una hoja mbadala toa si kupondea ya mwenzako.. Mimi naona hapa kuna umbwe kubwa la fikra na ukungu mkubwa wa kufikiri... Watu wengi kwa sababu ya ushabiki tunakuwa masikini wa mawazo mbadala.. Kama CHADEMA wamekosea nieleze njia gani ni bora toka 1990 ilipoanza mikakati ya katiba mpya pale Karimjee nadhani ambapo National committee for Constitutional Reform(NCCR) iliundwa..
Tuachie mawazo mbadala na harakati zitendeke.. CHADEMA walituma watu wa IT kuchunguza mtambo wa NEC siku hiyohiyo ukagoma mbele yao.. NEC ikawaihidi watawa feedback ukitengenezwa.. Cha ajabu walipata barua ya tar 28 okt ikafika 8 novemba.. Kwa nini NEC walifanya hivi??Jibu mwenyewe.

Mimi naomba CCM na JK wachukulie haya kwa mustakabali wa nchi yetu.. Kikwete kama atakubali Constitution Reform basi atakumbukwa zaidi kuliko watangulizi wake.. Na mataifa ya nje yatampongea kama mwenzie Mwai Kibaki.. Asiangalie kama CCM itaanguka au laaah... Kwa kuwa ameahidi vitu na anao uwezo wa kutekeleza basi CCM itabaki lakini vinginevyo lazima wataanguka... Wasiogope kwa minajili hiyo lakini watende haki... Siku zote haki humweka mtu huru!!!

Nawasilisha
Eliesikia
 
Naunga mkono hoja 100%. Wakikataa katiba mpya na damu ikamwagika 2015 wajue kuwa watawajibika. Hongera CHADEMA kwa mikakati ya AMANI mliyoamua kufuata. Narudia tena muendelee kwa amani kabisa. Nafikiri hao CCM na JK wanasubiri ncha ya upanga ndio amani ipatikane, wanafikiria hata kuandaa maandamano ya kuipinga CHADEMA. Katiba mpya lazima ipatikane by ANY MEANS NECESSARY.

Nawasilisha.
 
:eek::teeth::A S-alert1::A S crown-1:yaah its gud:teeth::teeth::teeth::teeth::A S crown-1::redfaces::bump:naunga mkono hoja
 
Amini nawaambia inahitaji nia ya kweli kwa wabunge kuwatumikia wananchi kwa ukweli kabisa.

Tabia inayoonyeshwa na wabunge wa vyama vya upinzani inatokana na rushwa state corruption to be specific. Wabunge wengi wakishafika pale amabo wasio nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi ni rahisi sana kuwa upande wa serikali kwa sababu ya maslahi wanayopata.

Ikumbukwe kuwa wengi wa wapinzani ni watu ambao wamekuwa wanahangaikia maisha. Hivyo exposure ya mihela ya ubunge ni rahisi kuwapotezea malengo.
 
Kwanza naunga mikono yote miwili hoja ya katiba mpya. Kwa sababu itatoa dira ya tume huru ya uchaguzi, msajili huru wa uchaguzi na haki zaidi ya kidemkrasia na la zaidi kumpunguzia madaraka RAIS. JK anapaswa kujua kuwa kwa katika miaka yake mitano hakuna mema anayoweza kujivunia kama kumbukumbu kwa watanzania. Amepata nafasi nyingine na wapinzani wake wanasema amepata kwa KUCHAKACHUA! Namshauri atumie fursa hii kuondoka na jina zuri na kufuta giza lililomtanda kwamba yeye ni mtetezi wa MAFISADI. Anaweza kufanikisha kuacha taswira mpya kwa watanzania na kuacha kumbukumbu ya MILELE katika historia ya Tanzania endapo ataanzisha na kufanikisha kuandikwa KATIBA mpya na 2015 nchi ikafanya uchaguzi kwa katiba mpya. Namshauri JK asihofu kuanguka kwa ccm, bali aangalie uhai wa TANZANIA YETU.
 
Madai ya KATIBA mpya na TUME HURU ni madai ya upinzani wote, Good comment
 
Hoja isijadiliwe imepita.
Sijui kwa kudai haki ikifikia wabunge wanapigana bungeni, Maneno yatakuaje?
 
Back
Top Bottom