CUF, NCCR, TLP, UDP siasa ya Tanzania basi tena, CHADEMA tumaini la watanzania

Sir R

JF-Expert Member
Oct 23, 2009
2,175
298
Tumebakiwa na chama kimoja tu cha upinzani Tz, CDM tumaini la watanzania.

Vyama vingine wamekwama, viongozi wao wanatumiwa na chama tawala na serikali wakati wa kampeni.
Lakini watu wameshaanza kuwatambua hilo . Uchaguzi wa Igunga ni mfano mzuri.

Ushauri: CDM andaeni operesheni maalum ya kushiriki shughuli za maendeleo kama vile Usafi wa mazingira, kujitolea kutengeneza barabara vijijini. Kuwalipia wanafunzi wasio na uwezo wa kulipa ada.

Wabunge wa CDM watembelee taasisi mbalimbali kama shule za misingi, sekondari, wahamasishe wanafunzi kusoma kwa bidii ili kujenga maisha yao ya baadae.

Viongozi wa CDM maeneo mbalimbali waandaa mafunzo maalum kuhusu ujasiriamali. zaidi yalenge wanawake na vijana.

Hayo yote yakifanyika, CDM itakuwa imejitambulisha kwa wananchi kwa njia ya vitendo zaidi amabyo yana impact kwenye maisha ya wananchi.

Wasihangaike na CCM, watu watajua la kufanya wakati wa uchaguzi.

CDM kazi ianze mara moja.
 
Back
Top Bottom