CUF na siasa za jino kwa pengo.....

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,032
79,015
Wajameni mie nashangaa hawa wenzetu wenye kuongelea muungano wa vyama vya upinzani katika chaguzi na kuishi maisha ya usaliti; Je, watafanya hivi mpaka lini? Hebu tujiulize CUF wanasema ati Upinzani usimamishe mgombea mmoja wakati hawajaonyesha kivitendo hata pale ambapo CHADEMA si Mpinzani yaani katika yale majimbo yaliyo chini ya CHADEMA na ilihali tumeona sehemu kadha wa kadha sehemu ambapo CHADEMA haijasimamisha Wabunge, ilitoa support kwa CUF na hata katika madiwani (pale chama kingine cha upinzani kinapokubalika zaidi)! Sasa huu unafiki unatoka wapi? Juzi hapa CHADEMA kama chama kilichotimiza vigezo vya kuunda upinzani iliwasiliana na CUF wakiwaeleza nia yao ya kutaka kushirikiana, naskia ikatoka command toka visiwani ati waungane na TLP, UDP na NCCR-Mageuzi! jamani at least NCCR-mageuzi naweza sema wanadamu changa ila wanaangushwa na Mwenyekiti wao, ila TLP nao jamani? hata UDP nina wasi pia na Cheyo, ila nashukuru kwa kumpigia Marando! Kuongeza unafki uliokubuhu kwa hawa CUF (CCM B) wakahaidi kumuunga mkono Bw Mabele Marando; cha kushangaza woote wakapigia CCM uspika! Je tunapata picha gani? Mapandikizi kushoto na kulia sio? Jamani nashukuru kwa CHADEMA kuliona hilo...hawa watu wamenunuliwa kaeni nao chonjo! nia yao ni kuwasambaratisha hawana nia dhabiti na wala hawajui maana ya neno upinzani! vijiba vya roho vinawasumbua babu! hata mtoto wa vidudu atakuambia Marando was more qualified kuchukua kiti cha uspika zaidi ya mama Makinda by far ila hawa wenzetu wakaamua kumpigia kura wa CCM A angalieni tu CCM A hawamuangalii mtu usoni wanapotaka kukutoa roho (kukuisraili)... ?? lets wait and see na huo urafiki wa mashaka wa CCM A na B! utaishia wapi? meanwhile endelezeni zile itikadi zenu za jino kunako Pengo waana ile jino kunako jino ni marehemu siku mingiiiiiiiiiiiiiiii!
 
Unacho ongelea ni tetesi tu!, cuf ni wapinzani wa kweli hata dunia inajuwa, chadema ndio kwanza mnajifunza so msikilize aliyekutangulia kuona juwa, acheni kujifanya mnaweza, hamuwezi bila ya kushirikiana, tatizo lipo chadema sio cuf.
 
Hivi vyama vya upinzani visiungane, ili kuleta upinzani mzuri kwa nchi. Kuwa na strong two parties ni mbaya kwa taifa, kwa sababu italeta chuki zisizo za msingi kwa nchi. Angalia Marekani ilivyojaa na chuki, yote kwa sababu ya strong two parties.
 
Unacho ongelea ni tetesi tu!, cuf ni wapinzani wa kweli hata dunia inajuwa, chadema ndio kwanza mnajifunza so msikilize aliyekutangulia kuona juwa, acheni kujifanya mnaweza, hamuwezi bila ya kushirikiana, tatizo lipo chadema sio cuf.
wacha weee..real revolutionaries hawawezi pigia kura CCM ni kuwasaliti wale wanachama wenu 17 waliopoteza maisha wakiwapigania uchaguzi uliopita! kama kweli mnajua mlichokifnya mnge-abstain voting basi na ingeweza kueleweka kidogooo... kwamba kupiga kura kunakinzana na utashi na matakwa yenu katika ustawi wa upinzani! Lakini hii ya kupigia kura CCM; huniambii kitu tena kwanza hairuhusiwi maana inakinzani na ustawi wa chama chenu bungeni; mbaya zaidi ukiangalia walioshindana yaani Makinda vs Marando! CUF imepigia kichuguu ikauacha Mlima Kilimanjaro (qualification-wise)! what CUF did was shooting on its own foot yaani more than double standards kwa ufupi CUF si wapinzani dhana nzima ya kuhadaa umati ilikuwa kutimiza matakwa ya Lipumba na Seif kupata madaraka kwa bahati mbaya huku Bara Lipumba si riziki na Maalim hayuko radhi kuendelea kusubiri yakheee yaumiza matumbo! sasa ndo tunaona true colours za CUF!
 
Hivi vyama vya upinzani visiungane, ili kuleta upinzani mzuri kwa nchi. Kuwa na strong two parties ni mbaya kwa taifa, kwa sababu italeta chuki zisizo za msingi kwa nchi. Angalia Marekani ilivyojaa na chuki, yote kwa sababu ya strong two parties.
Kwa mujibu wa itikadi za visiwani za Maalim sio?... baada ya kushindwa huko visiwani then hakuna Muungano! Na ulioombwa Bungeni? Kwa maoni yangu kama Upinzani walitakiwa kuwa pamoja ili kuweza kuhimili mikiki ya CCM sasa kwa vile CUF ni CCM B sasa hizi kila muswaada utapita maana automatically watapata outright 2/3 kuufanya muswaada kuwa sheria Haki ya Mungu presidential term limit iko njiani kuondolewa na vitu vingine kama mahakama ya kadhi na OIC zitapita kiulaiiini!
 
Back
Top Bottom