Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Wandugu, baada ya kumpata mgombea makini kutoka CHADEMA, nafikiri kwamba sasa ni wakati mzuri kwa CUF kuamua kumuunga mkono bwana huyu. Na katika kutekeleza hilo, napendekeza msemaji wa kambi ya upinzani bungeni (Rashid) awe ni mgombea mwenza. Nafkiri kuna haja ya Lipumba kuamua kujitoa katika nafasi anayotaka kugombea. Kuna haja gani ya kugombea ili hali anajua kabisa anasindikiza tu? Ni mawazo tu, tunaweza kujadili hapa, pengine hoja zetu zitamfanya Lipumba atangaze kujitoa na kumuunga mkono Dr Slaa.