Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Inasemwa asie mwana abebe japo jiwe,kesho katika uwanja wa Kibanda uhai au kibanda maiti kama kilivyokuwa kikijulikana hapo zamani kutafanyika mkutano mkubwa wa aina yake ,waandalizi wa mkutano huo wametabiri kuwa utakuwa ni mkutano mkubwa ambao haujawahi kufanyika hapa Zanzibar au Tanganyika.
Ni mkutano ambao utawakusanya raia wa visiwa viwili vinavyoijenga Zanzibar na kuto joto lao lupitia Chama hicho cha CUF.
Mada kubwa itakayozungumzwa ni kufundishwa siasa kwa Kikwete na kuelimishwa kwa ufasaha kuhusu Zanzibar.maelfu ya wananchi wameapa kujitokeza katika mkutano huo na kusema ni mkutano ambao umekuja kwa wakati muafaka na wanaenda kusikiliza kilichomtoa kanga manyoya,kitu ambacho kimekuwa kikitolewa na kusemwa na watu kama msemo lakini kesho viongozi wa CUF watakifafanua na kujulikana hicho kilichomtoa kanga manyoya ni kipi ? Tega sikio na ili upate kisa kamili kutoka mkutanoni. Nyote mwaalikwa japo kiroho.
Ni mkutano ambao utawakusanya raia wa visiwa viwili vinavyoijenga Zanzibar na kuto joto lao lupitia Chama hicho cha CUF.
Mada kubwa itakayozungumzwa ni kufundishwa siasa kwa Kikwete na kuelimishwa kwa ufasaha kuhusu Zanzibar.maelfu ya wananchi wameapa kujitokeza katika mkutano huo na kusema ni mkutano ambao umekuja kwa wakati muafaka na wanaenda kusikiliza kilichomtoa kanga manyoya,kitu ambacho kimekuwa kikitolewa na kusemwa na watu kama msemo lakini kesho viongozi wa CUF watakifafanua na kujulikana hicho kilichomtoa kanga manyoya ni kipi ? Tega sikio na ili upate kisa kamili kutoka mkutanoni. Nyote mwaalikwa japo kiroho.