Elections 2015 CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake

Wanabodi, baada ya kutangazwa tarehe ya uchaguzi wa visiwani Zanzibar,

Kuna watu wanadhani Chama cha Wananchi CUF, kina hiyari kushiriki uchaguzi huo au kutoshiri, as if kushiriki uchaguzi wa marudio ni jambo la hiyari!, watakuwa wanajidanya!. CUF hakina option yoyote ya kuamua ama ishiiki ama isishiriki, kwa sababu ushiriki wa uchaguzi wa marrudio sio option bali ni lazima kwa sababu kila kitu kiko vile vile kam,a mwanzo!.

Wenye option ya kuamua kushiriki au kutoshiriki ni wapiga kura, ndio wanaweza kuamua ama kujitokeza kushiriki kupiga kua, au kususa kupiga kura, na mgombea hata kama atapata kura moja ya ndio, ndio atatangazwa mshindi!, hivyo kupiga kura au kutopiga kura ndio bado ni option!, iwapo CUF itatangaza kususia uchaguzi huo, tangazo hilo ndilo litakuwa tangazo rasmi la kifo rasmi cha kilichokuwa Chama cha Wananchi CUF, kwa sababu majina ya wagombea wa CUF tatakuwepo kwenye karatasi za uchaguzi na hawatachaguliwa, hivyo kuipatia CCM ushindi wa mezani, ikiwemo kuivunja ngome ya CUF kule Pemba, kwa CCM kuvitwaa viti vyote vya Uwakilishi Zanzibarr na Pemba, ambapo pia huo ndio utakuwa mwisho wa SUK na CCM kutawala peke yake na kuhitimishwa kwa kifo rasmi cha chama cha wananachi, CUF!.

Nakiri kupandisha uzi huu kufuatia bandiko la mwana jf huyu
Zanzibarr sio nchi bali ni sehemu ya JMT, dhima ya muungano, ni undungu wa asili kati ya watu wa Tanganyika na Zanzibar, lakini sababu halisi ya muungano ni kuipatia Zanzibar ulinzi na usalama, Zanzibar haina polisi wala jeshi, hivyo jukumu la ulinzi na usalama wa Zanzibar, sio jukumu la Zanzibar, ni jukumu la JMT!. Hivyo CUF washirriki au wasuse, it will make no diference kwa sabau jukumu la ulinzi na usalama wa Zanzibar, ni jukumu la serikali ya JMT, chini ya Amiri Jeshi Mkuu, Drr. Jojm Pombe Magufuli.

Uchaguzi umetangazwa, utafanyika kwa amani na utulivu, mshindi atapatikana kwa haki, atatangazwa, ataapishwa na kuunda SUK nyingine, kwa uhuru kabisa bila`wasiwasi wowote!.

Hata hivyo kushiriki uchaguzi kugombea nafasi yoyote ni hiyari, pia kuamua kutokushiriki katika uchaguzi pia ni hiyari, sambamba na kujiandikisha kupiga kura ni hiyari, kutokujiandikisha pia ni hiyari, na kujiandikisha kupiga kura na kutokupiga kura pia ni hiyari, zote hizo ni demokrasia.

Kitendo cha CUF kushiriki uchaguzi wa mwanzo kunaifanya CUF ni lazima ishiriki uchaguzi wa maudio sio kwa hiyai bali kwa lazima. Hapa hakuna choice. Na iwapo CUF watasusana uchaguzi wa marudio, kususa huko kutakuwa ni kususa batili. kutakao ipatia CCM ushindi wa mezani, tena this time CCM itashinda viti vyote vya uwakilishi Unguja na Pemba, na huu ndio utakuwa mwisho rasmi wa CUF. Kamwe CUF isikubali kuingia katika mtego wa kususia uchaguzi wa marudio!.

Kikweli JK alikuwa ni mpole sana, hivyo Zanzibar imemchezea sana hadi kumtia vidole machoni katika yale mabadiliko batili ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 2010. John Pombe Magufuli, hii ni namba nyingine, huyu sio mtu wa mchezo mchezo au kuchezewa kama JK, hivyo CUF kama wanadhani watasusa na kubembelezwa, this time watakuwa wame bugi step, sasa hapa ni kazi tuu!.

Tutaulinda muungano kwa gharama yoyote!.

Pasco
Mkuu uko sawia,wasiposhiriki watakuwa wamejiweka mlalo wa mende,ni vyema wakaliangalia hili kwa makini.
 
Pasco, naomba kupingana nawe. Chama chochote kina option ya kujitoa kwenye ugombea wa nafasi fulani. CUF wanaweza kuiandikia tume na kujitoa kwenye uchaguzi. Pia,SUK inaundwa na mshindi wa kwanza na wa pili, CUF wasipokuwepo kuna chama kitakachofuatia kwa kura, hata kama kwa kura kumi. Kuvunjwa kwa ngome ya CUF pemba hiyo ni ndoto,kutokuwepo kwenye uchaguzi hakutaondoa harakati za kisiasa za CUF Zanzibar,wataendelea! 2005-2010,wawakilishi wa CUF walisusia Vikao vyote vya BW, haikuwafuta kwenye ramani ya siasa, and it was the same as if they had not participated in the election. Leo wamemtimua aliyekuwa mgombea kupitia ADC, Hamad Rashid, je! Ataebdelea kuwa mgombea?
Mkuu uchaguzi wa marudio ni kila kitu ni kama kilivyokuwa mwanzo, hakuna kubadili chochote wala hakuna kujitoa, unless litokee jambo linaloitwa force majeure, mfano kifo cha mgombea, uchaguzi jimbo hilo utaahirishwa na kufanywa uchaguzi mdogo!.

Hakuna cha kuandika baua, hakuna cha kujitoa, wala kususa!, bali kuna uhuru wa kupiga au kutokupiga kura!.

Pasco
 
...slippery slope argument!..kwamba CUF isiposhiriki ndo kifo chake!??..,si kweli!
...swali la msingi ni lile lile tu:je huu uchaguzi wa marudio ni halali/batili?...jibu la swali hili ndo litasadifu maamuzi ya ama kushiriki au kutoshiriki kwa CUF na mustakabali wa uhai wake pia ikibidi!
 
Mwaka 1964 wazanzibar walikuwa hawajui ya kwamba watanganyika wamejikushanya maeneo ya tanga wakipanga mikakati ya kuivamia zanzibar,ni miaka 54 sasa wazanzibar wameelewa ni nani adui yao.
 
Tutaulinda muungano kwa gharama yoyote!.

Pasco

Hata kama unatoa ushauri sidhani kama unahaki ya kumalizia kama ulivomalizia eti "Tutaulinda muungano kwa gharama yoyote!." Huu ni upunguani wa fikra. Zanzibar ilikua dola yenye silka na tamaduni zake kujidai kuropokwa maneno eti CUF walimtia vidole machoni JK kwa kuwachia kufanya mabadiliko ya katiba mwaka 2010 inatupa imani na kututhibitishia CHUKI ULIZONAZO DHIDI YA ZANZIBAR na watu wake. Kamwe Zanzibar haitakua Kilimanjaro au Mwanza! ilikua nchi, bado ni nchi na itaendelea kuwa nchi, japo watu kam wewe unojiita pasco unaonesha CHUKI NA NYOYO ZA FITNA KWA ZANZIBAR, INSHAAALAH ipo siku historia itajirudia. Kumbukeni hata Mwingereza ametawala Dunia kwa karne na karne lakini yako wapi! YAGUJU, CHUKI ZENU WATANGANYIKA JUU YA ZANZIBAR IPO SIKU SITAKWISHA HATA KAMA NI BAADA YA KARNE, ZANZIBAR IPO SIKU ITAKWAMUKA TU.
Umeandika kwa hasira sana ndugu yangu. Hukumelewa Pasco

Pasco anakariri kauli za viongozi waliopita akiwemo Magufuli 'Tutalinda muungano kwa gharama yoyote''

Ukisoma maelezo yake, anashadidia hoja zake kwa kauli hiyo

Hukumuelewa, muombe radhi na wakati mwingine ujaribu kuangalia kauli kutoka 'angle'tofauti
 
Mi nawashauri wazanzibari wakapige kura, nyingi sana kiasi kwamba hata wakitaka kuchakachua ishindikane,watashinda tena ,halafu ccm acheni uoga mpeni seif zanzibar,hana uwezo wa kuvunja muungano na akijaribu si apewe kama za jumbe tu,tunahitaji kupumzika tuachane na migogoro isiyo na kichwa wala miguu,zanzibar ilishakufa kitambo kama Ilivyokufa tanganyika nashangaa watu wanataka kufufua maiti! mkae mkielewa kuna nchi moja tu jmt ,hivyo vyeo mnavyogombania ni hisani tu na hapo ndipo linapoanzia tatizo,nawashauri ccm mpeni seif hicho kiti akizengua vunja kabisa na serikali,na hakuna serikali 3 wala 2 unda serikali moja tupumzike!
 
ur wrong mr.
pale cuf ikikubali kushiriki inapigwa buubaa,..
bora waendelee na msimamo wa kutoshiriki had mwisho2,..
jk c mtu mzuri
ashaandaa sumu zake na benja mkpa na sheni kupiga machanga ya macho,..cuf hata wafanyaje hawataweza kuzuia wizi
wa ccm.,...
ni bora wasimamie msima wa kutoshiriki,.,.
 
Suala la Zanzibar ni gumu sana na halipo katika level ya kujadiliwa na msukuma wenzangu Pasco, hili lipo kwenye level ya wana diplomasia kama kina membe, mahigi ila sio Balozi Seif Ally Iddy
 
Kwa kipindi kirefu sana nimekuwa nakupa respect kubwa sana Pasco na kukuona kuwa miongoni ya Great Thinkers wa kutukuka humu JF.

Lakini kwa bandiko lako hili nimelazimika kukushusha hadhi to the very very lowest level.

Kwanza naamini hakuna mtu yeyote anayeweza kupinga jambo hili including wewe Pasco mwenyewe kuwa Katiba ya nchi ndiyo sheria mama na inapaswa kila mtu aitii na ndiyo mantiki ya kila kiongozi kabla hajakabidhiwa madaraka anaapa kuitii.

Sasa nataka nikuulize maswali machache Pasco:

1. Jecha alipoufuta uchaguzi wa Oktoba 25 alisema anaufuta kutokana na mamlaka aliyo nayo kwa mujibu wa sheria. Sasa kwa kuwa majukumu ya ZEC yameainishwa ndani ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Tunaomba Mkuu Pasco ututajie ni Ibara ipi ndani ya Katiba hiyo inayompa mamlaka Mwenyekiti wa ZEC tena bila kushirikisha makamishna wrnzie wa ZEC kuufuta uchaguzi huo?

2.Sote tulimsikia Jecha siku anaufuta uchaguzi ule tarehe 28/10/2015 akisema kuwa uchaguzi huo utarejewa ndani ya siku 90 ambayo ndiyo matakwa ya kisheria. Sasa tunaomba mkuu Pasco utueleze je tarehe 20/03/2016 iliyopangwa kufanyika uchaguzi huo bado ni ndani ya siku 90 ambazo Jecha huyo huyo alisema wazi kuwa ndipo utarejewa ili kutekeleza matakwa ya kisheria?

3. Hivi itawezekanaje uchaguzi huo wa marejeo usimamiwe na Jecha huyo huyo ambaye alidai Tume yake ya uchaguzi hawaelewani hadi waliwahi kutwangana ngumi? Hivi Tume ya aina hiyo inawezaje kuwa na credibility ya kusimamia jukumu zito kama hilo la uchaguzi mkuu ambalo ni la uhai wa Taifa letu?

4. Sote tunafahamu kuwa tokea atangaze kufutwa kwa uchaguzi wa Oktoba 25 Jecha alipelekwa mafichoni hadi ameibuliwa jana kufanya hiyo 'special task' na kurejea tena mafichoni. Sasa swali langu kwa Pasco, je Jecha atatusimamia uchaguzi huu wa marejeo kwa kutumia 'remote control' akiwa huko mafichoni?

5. Swali langu la mwisho kwa Pasco. Hivi ina maana nchi yetu ina kikundi kidogo cha watu ambao wanaruhusiwa kuisigina Katiba ya nchi wanavyotaka? Akiwemo huyo Jecha Salim Jecha ambaye anaisigina Katiba anavyotaka bila kuchukuliwa hatua yoyote? Au hayo yanafanyika kwa hicho Pasco ulichokiita kuulinda Muungano wa Tanzania kwa gharama yoyote?!
 
Mkuu Pasco, heshima kwako. Nakiri you're a good satirist. Watu wengi hawajazoea uandishi wa "satire" hivyo wanachokozeka kirahisi na kuja juu bila kuelewa maana halisi ya kinachosemwa. Kuna ambao kweli wameamini kuwa na wewe ni mmoja wa wale waliopania "kuyalinda mapinduzi kwa gharama yoyote"!

Pamoja na tasnifa uliyoonyesha, si kweli kwamba CUF hawana hiyari kujitoa na si kweli kwamba wakijitoa ndio kifo chao. Lakini ni kweli kwamba wana mtihani mkubwa.

Wakijitoa watakuwa wamelinda msimamo wao na kusimamia kanuni ya demokrasia makini. Na hii itakuwa na matokeo makubwa zaidi kama wananchi wengi watawaunga mkono kwa kususia uchaguzi huo wa marudio na kuufanya udorore sana.

Wakishiriki watakuwa "wamegeuka jiwe". Heshima ya chama itaenda chini. Kikubwa zaidi hawawezi kushinda uchaguzi ambao mwenyekiti wa ZEC ndiye mwenye kauli ya mwisho na nyuma yake imeshadhihirika kuwa anadhibitiwa na vyombo vya dola. Victory is certainly out of question.
 
Suala la Zanzibar ni gumu sana na halipo katika level ya kujadiliwa na msukuma wenzangu Pasco, hili lipo kwenye level ya wana diplomasia kama kina membe, mahigi ila sio Balozi Seif Ally Iddy
Mtajadili mpaka linii ? Tunataka action diplomasia ina limit,hao kina membe si walikuwepo serikalini?Zanzibar si ya kujadili ni ya action, kama alivyo fanya karume alijadiliana na shamte majadiliano hayakufanikiwa then ikafata action! Nataka kusema zanzibar inamtaka mtu kama magufuli mtu wa action,kwamba haya jamani njia ni hii hakuna tena majadiliano tumesha jadiliana sana,wapemba na wa unguja hawaelewani what u expect ? Imekua kama isidingo
 
Ile inayoitwa busara ya Maalimu au CUF ndiyo matokeo ya kurudiwa kwa uchaguzi! Sio rahisi watu ambao mfumo wao wa maisha/utafutaji wao unategemea serikali kwa takribani nusu karne wakaachia madaraka kiurahisi. Chukua mfano wabunge waliodumu karibu miaka 20 bungeni leo hii wakishindwa kurudi bungeni maisha yao yanakuwa mabaya kama hawakuwa wanavuna mamilioni ya bure miaka 20. Vipi makatibu, wenyeviti wa chama, makada wa chama ambao kwa mfumo wetu huwezitofautisha chama na serikali wanaishi kwa kutegemea serikali sio chama leo wakaepembeni?. Vipi wakuu wa wilaya, mikoa, wakurugenzi??? CUF ilihitji kwenda mbele ziidi kile kinachoitwa busara. Sio kila japo linahitaji busara!! Hata hivyo busara ingeshinda kama pande zote zingekuwa na busara!!! Isitoshe busara ilitumiaka miakachaguzi zote zilizopita ambapo inasemekana CUF ilikuwa inashinda lakini haikufanikiwa!!! Iweje mwaka huu tena busara ile ile iliyoshindwa awamu karibu 5 ifanikiwe uchaguzi huu??.
 
ur wrong mr.
pale cuf ikikubali kushiriki inapigwa buubaa,..
bora waendelee na msimamo wa kutoshiriki had mwisho2,..
jk c mtu mzuri
ashaandaa sumu zake na benja mkpa na sheni kupiga machanga ya macho,..cuf hata wafanyaje hawataweza kuzuia wizi
wa ccm.,...
ni bora wasimamie msima wa kutoshiriki,.,.
Imagination! Wonders! kama unajua kuna wizi ndio ukomae usiibiwe sio kususa ukisusa wenzio wara
 
Imagination! Wonders! kama unajua kuna wizi ndio ukomae usiibiwe sio kususa ukisusa wenzio wara
kma cuf ikikubali iwe na uhakika wa ulinzi na usimamizi,...wa uhakikaa mkuu
na show ya ulinzi iwe cuf% kubwa kuliko fisiem
au kma kukataa bora ikatae100%isipige kula kabisa,..
Fisiem matapeli
 
kma cuf ikikubali iwe na uhakika wa ulinzi na usimamizi,...wa uhakikaa mkuu
na show ya ulinzi iwe cuf% kubwa kuliko fisiem
au kma kukataa bora ikatae100%isipige kula kabisa,..
Fisiem matapeli
Ndio hiyo niliosema ushajua mpinzani wako ni tapeli na mwizi lazima ujipange haswa sio kususa
 
Back
Top Bottom