CUF kuandamana nchi nzima

2. Nimesoma neno kwa neno rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM ambayo ilishakubaliwa na kamati zote mbili. Suala la serikali ya pamoja linapaswa kutekelezwa kabla ya mwaka 2010.
3. Nimesoma ripoti ya Kamati ya CCM iliyopeleka Butiama kwa ajili ya Kamati Kuu na baadaye halmashauri Kuu; ukweli ni kuwa hoja ya kura ya maoni haikuzuka kikaoni- iliandaliwa kabla kwa pendekezo la Karume na kukubaliwa na wanakamati. Pamoja na uzuri wa dhana ya kura za maoni, lakini nia(motive) yake hapa si nzuri! Kwa serikali ambayo haifanyagi referendum katika masuala muhimu kihistoria kama Muungano, Katiba, Mfumo wa Vyama vingi, kumuundoa Rais wa Zanzibar kama makamu wa Rais(ambalo lilikuwa ni suala katika makubaliano mama ya muungano); inatia shaka serikali kama hiyo itakapo suala la kura za maoni Zanzibar. Ni Kikwete huyu huyu ambaye alipokwenda Kenya hakutaka wakina Raila na Kibaki wafanye kura za maoni, akata wasaini makubaliano na kuyatekeleza. Wakati wa kuibwa kwa kura hakuitishwa kura za maoni, kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa, lakini kosa moja linaweza kutoa ishara ya kosa lingine! Kwa ujumla ukiisoma ripoti hii ya Kamati ya CCM; ukisoma na Barua ya Mwisho ya Makamba; utagundua kuwa Makamu Mwenyekiti Msekwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete- hawakusema kweli wakati wakieleza mchakato wa Maazimio ya NEC ya CCM na Matokeo yake!
4. Nilikuwepo Diamond Jubilee jana na nimemsikiliza Lipumba toka mwanzo mpaka mwisho. Nilichokielewa ni kwamba CCM imekuwa ikiwatapeli CUF toka baada ya uchaguzi, ikiwafanyia unafiki wa hali ya juu- CUF nayo kwa upande wake ilikuwabali ku-give in too much; ikakubali ghilba za aina zote ikiwa na matumaini makubwa kwamba Kikwete yuko genuine! Na kwa kiasi kikubwa mambo yote haya yalifanyika kwa siri ya pande mbili; kwa mategemeo makubwa ya CUF kwamba pengine serikali ya mseto ingetokea. Kumbe CCM wakati wote ilikuwa ikiweka kadi chache mezani na nyingine nyingi zaidi kuzificha chini ya meza.Ukiangalia mtiririko wa matukio katika hii miaka mitatu kuhusu Zanzibar utagundua ama Rais Kikwete anafanya unafiki wa hali ya juu wa kisiasa, au ni kiongozi dhaifu katika CCM kama mwenyekiti anayezidiwa nguvu na makundi mengine ndani ya chama chake. Kwa vyovyote vile, hali hii ikiachwa bila panga kuitwa panga na si kisu kikubwa ni ishara mbaya kwa utangamano wetu kama taifa haswa kwa kuwa kwa sasa CCM ndicho chama tawala!
5. Tunaungana mkono na CUF katika hili, kwani kitisho cha demokrasia mahali Fulani ni kitisho cha demokrasia mahali pote. Maandamano ya jumamosi, hayapaswi kuwa maandamano ya CUF, yanapaswa kuwa maandamano ya umma! Ama hakika, uwongo una mwisho- lakini ukweli unapaswa husimama milele, na ukweli hauna itikadi. CUF wanaweza kuwa walijikwaa mahali Fulani katika mchakato huu; lakini sasa ni wakati wa kutazama mbali zaidi, kutazama picha kubwa zaidi- CCM ikiwachwa ikapita katika hili, itandelea kuacha na ufisadi mwingine ukatawala kwenye RICHMOND, BOT nk na hatimaye kuweka misingi ya ufisadi wa kudumu zaidi katika uchaguzi mkuu 2010. Hatupaswi kuacha utadamuni wa ufisadi, usanii wa kisiasa, uchezeaji wa haki, na wananchi kukaaa pembeni kama watazamaji na wanyooshaji vidole kuendelea katika taifa letu. Ni wakati mwingine wa kuandelea kuchukua hatua!
JJ

PS:
• Mwenye Hotuba ya Jana ya Lipumba atuwekee hapa tafadhali
• Mwenye rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM iliyokubaliwa na kamati za pande mbili aiweke hapa pia tafadhali

John Mnyika;

Inasikitisha sana kuunga mkono wenzenu kurudi back to sqaure one; wakati walikuwa wanaelekea kwenye makubaliano... Najua hii ni sawa kwako na akina Lipumba kwa sababu hakuna unachokosa tukirudi nyuma tena...! Ni waZanzibar wanatamani mjadala huu uendelee uishe.... wewe na propaganda zako munaona kwamba muafaka utapatikana mtakosa ya kutokea kwenye majukwaa mshindwe kwa jina... na mlegee kabisa...



Ni uzembe wa hali ya juu sana tatizo la miaka mingi kulifanya la emergency kama ilivyokuwa Kenya... I'm sorry there must be a problem of IQ somewhere...

Kenya haikushauriwa kwenda kwa Wananchi kwa kura ya maoni kwa sababu mazingira hayo yangeleta machafuko zaidi...(hili lilisemwa wazi hata sisi tusiokuwa tuna-practise siasa kama wewe tulijua hilo)

Watu kama John Mnyika kweli ndio mwanasiasa wa kukabidhiwa nchi kwa uchambuzi wako dhaifu kiasi hiki.

Ati Kikwete ni dhaifu... unafahamu maana ya Rais na maana ya Mwenyekiti wa Chama... You seem not to be serious at all... Kama munaburuzwa na Mbowe CCM kuna vichwa huwezi buruza tu ndugu yangu... NEC ya CCM imesheheni watu makini mkuu!!!

Narudia tena kwa kuwa hakututumia kura ya maoni huko zamani... hata sasa ambapo demekrasia ni dhana muhimu ya utawala bora tusitumie... huu ni uvivu wa kufikiri...


Alafu ulazima wa kufanya kabla ya 2010 ni upi.... mimi nadhani katiba yes itabadilishwe kabla 2010 ili baada ya uchaguzi serikali ya mseto ndio iundwe...
 
Kasheshe and the company:

Labda nianze kwa kusema kwamba inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana kuitetea CCM ya leo. Hii ni kwa sababu kujaribu kuwatetea CCM utakuwa unajaribu kupingana na ukweli na hamna kitu kigumu kama kupinga ukweli.

Sasa twende nyuma kidogo. Sababu za kuunda serikali ya mseto huko Zanzibar ni za kihistoria na zinazingatia mazingira halisi ya kisiasa na kijamii huko. Baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi tulirejea tena kwenye historia ambapo hakuna uchaguzi unaoweza kutoa clear winner. Hakuna chama chenye uwezo wa kushinda outright majority huko Zanzibar katika urais na katika bunge. This is a fact today and it is also a historical fact. Kwa hiyo kwa mazingira haya una options mbili tu Zanzibar; ambazo ni:

i) ama uwe na serikali ya mseto ikishirikisha vyama vyote viwili katika serikali ama

ii) urudi katika mfumo wa chama kimoja

Najua baadhi ya wahafidhina katika CCM wangependelea zaidi option no. 2. Hata hivyo hakuna njia tena ya kurudi huko. Again this is a fact. Ni kwa sababu hii hata Mwalimu Nyerere, ambao CCM wanadai wanamuenzi, akashauri kwamba lazima Zanzibar kuwe na serikali ya mseto. Mwalimu Nyerere alisema wazi kabisa kuwa swala la kuamua serikali ya mseto ni la viongozi. Tatizo lenu wana CCM mnayachukua ya Nyerere yale yanayowapendeza tu!

Sasa ni namna gani unafikia serikali serikali ya mseto ni jambo, kama alivyosema Nyerere, linalohitaji uongozi kuliko kura ya maoni. Pengine ni hapa ambapo baadhi yetu tunafikiri kwamba Rais wetu ni mwoga wa kufanya maamuzi magumu na pia anaogopa kufanya makosa. Sasa wataalamu wa uongozi wa kisiasa wanakwambia ukiwa na kiongozi anayeogopa kuchukua maamuzi mazito na anayeogopa kufanya makosa ujue ni kiongozi dhaifu-wao wanasema hiyo ni dalili kubwa kuliko zote za incompetence in leadership.

Nasema hili ni jambo ambalo linahitaji uongozi kwa sababu kura yeyote ya maoni itakuwa na pande mbili. Wana CCM wahafidhina akina Karume and company watasema hatuhitaji, wakati CUF watasema tunahitaji. Kwa hiyo utaona kwamba at the end of the day matokeo ya kura ya maoni yatakuwa hayana tofauti na kura ingine yeyote ile katika uchaguzi wa kawaida. Ndio maana mimi nakushangaa sana unapomdharau Lwaitama katika hoja yake hii. Kimsingi kwa kumdharau Lwaitama kwa hoja yake hii unawadharau wengi akiwemo Mwalimu Nyerere. Ungeacha ushabiki na ukatulia kidogo ungegundua Lwaitama alikuwa right na wewe ndio hasa tunaopaswa tukushangae.

The bottlem line: kinachosumbua Zanzibar, ambayo pia itajitokeza bara vyama vya upinzani vikipata nguvu, ni sense of entitlement kwenye leadership. CCM wanaamni kwamba ni wao tu wenye haki ya kutawala huko na sio mwingine. Kwa hiyo zote hizi ni danadana ili tufike uchaguzi wa 2010 halafu tuanze tena mzunguko huu. Na hili linathibitishwa na kauli zako hapa na zile za FMES pale anaposema kwamba CCM Zanzibar wanawajibika kuwatete weusi wenzetu (this couldn't be more ridiculous!).

Naamini Kikwete alikuwa anamaanisha katika hotuba yake kule Dodoma katika nia yake ya kutaka kutatua mgogoro wa Zanzibar. Tatizo la Kikwete ni naivety anayoonyesha. Yeye alikurupuka kutoa hotuba ile ili apate sifa bila kujua hali halisi ya mgogoro ule. Alipaswa kujua katika swala hili la Zanzibar nafasi yake kama Rais wa Jamhuri haiwezi kuwa kubwa bila kuwa-take on board viongozi wenzake katika CCM Zanzibar. Hata hivyo imetusaidia, blessing in disguise, kuthibitisha yale tuliyokuwa tunayajua kwamba Rais wetu ni dhaifu kwa kiwango kwamba hana hata uwezo wa kuwashawishi wenzake katika CCM kwa yale anayofikiri ni mema kwa nchi.
 
Kwa hiyo kwako wewe hapa wa kulaumiwa ni CUF na sio Kikwete ambaye aliahidi kuwa atahakikisha kunakuwa na muafaka zanzibar bila kujali nani mwenye makosa?

Wote ni wa kulaumiwa kwa sababu wanaonekana wanatuchezea mchezo wa siasa. CCM hawakuwa na sababu ya kutoibua suala la kura ya maoni wakati wa mazungumzo, waliliweka kama mtego kwa CUF ili ku-delay implementation ya makubaliano.
Kwa upande mwingine, ilitarajiwa kuwa kwa kuwa XCUF ndiyo iliyokuwa na malalamiko mengi, isingeruhusu masuala kama yasijadiliwe kwenye mazungumzo. Ilitakiwa kuwa na ajenda timilifu ambayo ingewahakikishia kuwa wanacoveer KILA KITU MUHIMU ili kuepuka na usanii kama huu unaofanywa sasa.
Inaonekana labda waliacha makusudi ili wafanye wanayofanya sasakama njia ya kujiongezea nguvu ya kisiasa
 
Kasheshe and the company:

Labda nianze kwa kusema kwamba inahitaji ujasiri wa hali ya juu sana kuitetea CCM ya leo. Hii ni kwa sababu kujaribu kuwatetea CCM utakuwa unajaribu kupingana na ukweli na hamna kitu kigumu kama kupinga ukweli.

Sasa twende nyuma kidogo. Sababu za kuunda serikali ya mseto huko Zanzibar ni za kihistoria na zinazingatia mazingira halisi ya kisiasa na kijamii huko. Baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi tulirejea tena kwenye historia ambapo hakuna uchaguzi unaoweza kutoa clear winner. Hakuna chama chenye uwezo wa kushinda outright majority huko Zanzibar katika urais na katika bunge. This is a fact today and it is also a historical fact. Kwa hiyo kwa mazingira haya una options mbili tu Zanzibar; ambazo ni:

i) ama uwe na serikali ya mseto ikishirikisha vyama vyote viwili katika serikali ama

ii) urudi katika mfumo wa chama kimoja

Najua baadhi ya wahafidhina katika CCM wangependelea zaidi option no. 2. Hata hivyo hakuna njia tena ya kurudi huko. Again this is a fact. Ni kwa sababu hii hata Mwalimu Nyerere, ambao CCM wanadai wanamuenzi, akashauri kwamba lazima Zanzibar kuwe na serikali ya mseto. Mwalimu Nyerere alisema wazi kabisa kuwa swala la kuamua serikali ya mseto ni la viongozi. Tatizo lenu wana CCM mnayachukua ya Nyerere yale yanayowapendeza tu!

Sasa ni namna gani unafikia serikali serikali ya mseto ni jambo, kama alivyosema Nyerere, linalohitaji uongozi kuliko kura ya maoni.


Kitila and the company (unlimited)!

Mpaka hapo tuko pamoja!!!

Tatizo tu hujaelewa mpaka sasa kwamba vyama vyote vinakubaliana serikali ya Mseto... come back please from wherever you are!!!

I repeat vyama vyote vimekubaliana serikali ya mseto...

Kama political science inasema muafaka/agreement inanaletwa na shinikizo la kiongozi then I'm lost.
 
Nasema hili ni jambo ambalo linahitaji uongozi kwa sababu kura yeyote ya maoni itakuwa na pande mbili. Wana CCM wahafidhina akina Karume and company watasema hatuhitaji, wakati CUF watasema tunahitaji. Kwa hiyo utaona kwamba at the end of the day matokeo ya kura ya maoni yatakuwa hayana tofauti na kura ingine yeyote ile katika uchaguzi wa kawaida. Ndio maana mimi nakushangaa sana unapomdharau Lwaitama katika hoja yake hii. Kimsingi kwa kumdharau Lwaitama kwa hoja yake hii unawadharau wengi akiwemo Mwalimu Nyerere. Ungeacha ushabiki na ukatulia kidogo ungegundua Lwaitama alikuwa right na wewe ndio hasa tunaopaswa tukushangae.

Kura hizo hazitakuwa hivyo na wala sitegemei ziwe hivyo especially kwa sababu vyama vyote vinasema kwamba kimsingi vimekubaliana serikali ya mseto... wanachotaka kutoka kwa wananchi ni Endorsement... nyinyi wana demokrasia hamuitaki hii ama kweli wasomi munaturudisha kwenye ujima!!!

Kwa hakika Dr. Lwaitama namheshimu sana lakini kwa hili ni la vitabuni as opposed na vitu ambavyo vitatokea on the ground...

Kumbuka sio CCM bara, wala visiwani watawezasimama kwenye majukwaa kupinga kura ya Maoni... Haviwezi fanya hivyo wakati watakuwa wametia sahihi... what they need is endorsement....

Comon Kitila amka mkuu... forget about books kidogo... just use logic, umesoma hesabu nakuaminia
 
Kura hizo hazitakuwa hivyo na wala sitegemei ziwe hivyo especially kwa sababu vyama vyote vinasema kwamba kimsingi vimekubaliana serikali ya mseto... wanachotaka kutoka kwa wananchi ni Endorsement... nyinyi wana demokrasia hamuitaki hii ama kweli wasomi munaturudisha kwenye ujima!!!

Kwa hakika Dr. Lwaitama namheshimu sana lakini kwa hili ni la vitabuni as opposed na vitu ambavyo vitatokea on the ground...

Kumbuka sio CCM bara, wala visiwani watawezasimama kwenye majukwaa kupinga kura ya Maoni... Haviwezi fanya hivyo wakati watakuwa wametia sahihi... what they need is endorsement....

Comon Kitila amka mkuu... forget about books kidogo... just use logic, umesoma hesabu nakuaminia

Kasheshe, acha utani. Kama ingekuwa ni rahisi hivyo kwamba inahitajika endorsement tu kusingekuwa na mabishano ya masaa nane kwenye mkutano wa HKT ya CCM huku Butiama. Ni kwamba kuna watu ndani ya CCM huko Zanzibar hawakubaliani na hili jambo na itakapokuja kwenye kura za maoni watakampeni upande wa pili.

Mkuu, hakuna kura ya maoni ya endorsement msipotoshe wananchi. Kama issue ingekuwa ni endorsement baraza la wawakilishi Zanzibar lingefanya kama ilvyofanyika huko Kenya. Hapa kinachotafutwa ni kama kile walichofanya Kenya kuhusu katiba mpya na Zimbabwe kuhusu Ardhi ambako kote kulikuwa na rigorous campaign.

Mkuu, utaongea sana katika hili lakini what you are trying to do is to try to, unconvicingly, justify the unjustifiable!
 
Kasheshe, acha utani. Kama ingekuwa ni rahisi hivyo kwamba inahitajika endorsement tu kusingekuwa na mabishano ya masaa nane kwenye mkutano wa HKT ya CCM huku Butiama. Ni kwamba kuna watu ndani ya CCM huko Zanzibar hawakubaliani na hili jambo na itakapokuja kwenye kura za maoni watakampeni upande wa pili.

Mkuu, hakuna kura ya maoni ya endorsement msipotoshe wananchi. Kama issue ingekuwa ni endorsement baraza la wawakilishi Zanzibar lingefanya kama ilvyofanyika huko Kenya. Hapa kinachotafutwa ni kama kile walichofanya Kenya kuhusu katiba mpya na Zimbabwe kuhusu Ardhi ambako kote kulikuwa na rigorous campaign.

Mkuu, utaongea sana katika hili lakini what you are trying to do is to try to, unconvicingly, justify the unjustifiable!
Tatizo ninyi wapinzani munatamani muwe madarakani... mustakabali wa Zanzibar hauko ndani yenu kabisa...shida yenu ni kuingia madarakani...

Suala la Baraza la wawakilishi ni dhahiri litaingia mahali pake ambapo ni kwenye kuibadilisha katiba... hilo halina shaka... hata kidogo...

Tofautisha mazingira ya Kenya na Tanzania msomi wetu... na mchambuzi wetu makini...

Wapeni nafasi kamati ya muafaka waendelee... mwisho watuambie wameshindwa kuafikiana au wameafikiana.... sasa bado hawajamaliza... kila mtu amekuwa kwenye kamati... du, ama kweli Tanzania penda sana longolongo...

Acheni kupiga ramli zenu kwamba ati wananchi wa Zanzibar wengi hawataka serikali ya mseto... kwani wao ndio viongozi wakikosa uwaziri unawaadhiri... ni jambo la wazi viongozi wengine wa CCM watapinga lakini majority wananchi wataunga mkono..

Ramli zenu nyingi zimekuwa za uongo... hii pia ni uongo....

1. Hivi si ninyi mnaosema siku zote kwamba Maalimu anashinda anapokonywa tu ushindi wake.... kwa hoja hii si kunatakiwa tu, msimamizi tumalize mambo?

2. Si mulisema mzee wa Kiraracha alishinda uchaguzi 1995?

3. Si mulisema JJ aliibiwa kura Ubungo...
 
1. Sitapenda kujadili historia ya Zanzibar, asili ya mtanziko wa kisiasa huko; lakini mimi naomba nichangia suala la principle tu hapa- kwamba pande mbili zimekaa zimajadiliana na kukubaliana mambo Fulani Fulani; baadaye upande mmoja umeanza kwenda tofauti. It's a political problem, that needs a political solution.
2. Nimesoma neno kwa neno rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM ambayo ilishakubaliwa na kamati zote mbili. Suala la serikali ya pamoja linapaswa kutekelezwa kabla ya mwaka 2010.
3. Nimesoma ripoti ya Kamati ya CCM iliyopeleka Butiama kwa ajili ya Kamati Kuu na baadaye halmashauri Kuu; ukweli ni kuwa hoja ya kura ya maoni haikuzuka kikaoni- iliandaliwa kabla kwa pendekezo la Karume na kukubaliwa na wanakamati. Pamoja na uzuri wa dhana ya kura za maoni, lakini nia(motive) yake hapa si nzuri! Kwa serikali ambayo haifanyagi referendum katika masuala muhimu kihistoria kama Muungano, Katiba, Mfumo wa Vyama vingi, kumuundoa Rais wa Zanzibar kama makamu wa Rais(ambalo lilikuwa ni suala katika makubaliano mama ya muungano); inatia shaka serikali kama hiyo itakapo suala la kura za maoni Zanzibar. Ni Kikwete huyu huyu ambaye alipokwenda Kenya hakutaka wakina Raila na Kibaki wafanye kura za maoni, akata wasaini makubaliano na kuyatekeleza. Wakati wa kuibwa kwa kura hakuitishwa kura za maoni, kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa, lakini kosa moja linaweza kutoa ishara ya kosa lingine! Kwa ujumla ukiisoma ripoti hii ya Kamati ya CCM; ukisoma na Barua ya Mwisho ya Makamba; utagundua kuwa Makamu Mwenyekiti Msekwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete- hawakusema kweli wakati wakieleza mchakato wa Maazimio ya NEC ya CCM na Matokeo yake!
4. Nilikuwepo Diamond Jubilee jana na nimemsikiliza Lipumba toka mwanzo mpaka mwisho. Nilichokielewa ni kwamba CCM imekuwa ikiwatapeli CUF toka baada ya uchaguzi, ikiwafanyia unafiki wa hali ya juu- CUF nayo kwa upande wake ilikuwabali ku-give in too much; ikakubali ghilba za aina zote ikiwa na matumaini makubwa kwamba Kikwete yuko genuine! Na kwa kiasi kikubwa mambo yote haya yalifanyika kwa siri ya pande mbili; kwa mategemeo makubwa ya CUF kwamba pengine serikali ya mseto ingetokea. Kumbe CCM wakati wote ilikuwa ikiweka kadi chache mezani na nyingine nyingi zaidi kuzificha chini ya meza.Ukiangalia mtiririko wa matukio katika hii miaka mitatu kuhusu Zanzibar utagundua ama Rais Kikwete anafanya unafiki wa hali ya juu wa kisiasa, au ni kiongozi dhaifu katika CCM kama mwenyekiti anayezidiwa nguvu na makundi mengine ndani ya chama chake. Kwa vyovyote vile, hali hii ikiachwa bila panga kuitwa panga na si kisu kikubwa ni ishara mbaya kwa utangamano wetu kama taifa haswa kwa kuwa kwa sasa CCM ndicho chama tawala!
5. Tunaungana mkono na CUF katika hili, kwani kitisho cha demokrasia mahali Fulani ni kitisho cha demokrasia mahali pote. Maandamano ya jumamosi, hayapaswi kuwa maandamano ya CUF, yanapaswa kuwa maandamano ya umma! Ama hakika, uwongo una mwisho- lakini ukweli unapaswa husimama milele, na ukweli hauna itikadi. CUF wanaweza kuwa walijikwaa mahali Fulani katika mchakato huu; lakini sasa ni wakati wa kutazama mbali zaidi, kutazama picha kubwa zaidi- CCM ikiwachwa ikapita katika hili, itandelea kuacha na ufisadi mwingine ukatawala kwenye RICHMOND, BOT nk na hatimaye kuweka misingi ya ufisadi wa kudumu zaidi katika uchaguzi mkuu 2010. Hatupaswi kuacha utadamuni wa ufisadi, usanii wa kisiasa, uchezeaji wa haki, na wananchi kukaaa pembeni kama watazamaji na wanyooshaji vidole kuendelea katika taifa letu. Ni wakati mwingine wa kuandelea kuchukua hatua!
JJ

PS:

• Mwenye Hotuba ya Jana ya Lipumba atuwekee hapa tafadhali
• Mwenye rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM iliyokubaliwa na kamati za pande mbili aiweke hapa pia tafadhali

Haya matatizo ya Zanzibar Ni uroho wa madaraka na kutokua na dhamira njema kwa wananchi pia kwa nchi.

Ndio maana utaona focus zao zote za watu wasio na nia njema hua wakati wa uchaguzi tu,watatumia gharama/maisha ya watu ili tu wapate njia ya kutekeleza nia yao mbaya.

Suluhu ya Zanzibar ni Rahisi mno ila kwa vile wote watafuta madaraka na wasivyo na nia ya nchi yao na wananchi wao bali mabwana wao watafanya kila hila kuwatumia wananchi ili wafikie malengo yao.

CUF na CCM kama wanania njema kwa nchi na wazanzibari ,mimi nafikiri wangekubaliana hivi ktk muafaka wao-
wabadirishe kifungu ktk katiba ya ZANZIBAR na MAWAZIRI wateuliwe kutoka wananchi wakawaida wasiwe WABUNGE(WAWAKIRISHI),nusu watoke pemba na nusu watoke ugunja.
Hapo ukisikia watu wanauliwa ama wanaandamana kwa ajiri ya CUF ama kutembelea ulaya wanashitakiana basi tatizo litakua sio siasa.
Kwanini CUF hawataki kupropose njia hii?? Kwani mpaka CUF iingie madarakani ndio matatizo ya Pemba yataisha????
 
[QUOTE
Kumbuka sio CCM bara, wala visiwani watawezasimama kwenye majukwaa kupinga kura ya Maoni... Haviwezi fanya hivyo wakati watakuwa wametia sahihi... what they need is endorsement....

Comon Kitila amka mkuu... forget about books kidogo... just use logic, umesoma hesabu nakuaminia[/QUOTE]

lakini Mkuu, hivi umefikiria iwapo kwenye kura ya maoni wananchi wakisema hawataki serikali ya mseto itakuwaje?
Of course itakuwa ni verdict nzuri na kuwaona waliokaa kujadiliana kuwa ni wapumbavu kupendekeza jambo ambao wananchi hawalitako. lakini kwa nini kabla hawajapendekeza serikali ya mseto wasiwaulize wananchi wanataka nini?
 
Kasheshe and the company:..............
Sasa twende nyuma kidogo. Sababu za kuunda serikali ya mseto huko Zanzibar ni za kihistoria na zinazingatia mazingira halisi ya kisiasa na kijamii huko. Baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi tulirejea tena kwenye historia ambapo hakuna uchaguzi unaoweza kutoa clear winner. Hakuna chama chenye uwezo wa kushinda outright majority huko Zanzibar katika urais na katika bunge. This is a fact today and it is also a historical fact. Kwa hiyo kwa mazingira haya una options mbili tu Zanzibar; ambazo ni:

i) ama uwe na serikali ya mseto ikishirikisha vyama vyote viwili katika serikali ama

ii) urudi katika mfumo wa chama kimoja

Najua baadhi ya wahafidhina katika CCM wangependelea zaidi option no. 2. Hata hivyo hakuna njia tena ya kurudi huko. Again this is a fact. Ni kwa sababu hii hata Mwalimu Nyerere, ambao CCM wanadai wanamuenzi, akashauri kwamba lazima Zanzibar kuwe na serikali ya mseto. Mwalimu Nyerere alisema wazi kabisa kuwa swala la kuamua serikali ya mseto ni la viongozi. Tatizo lenu wana CCM mnayachukua ya Nyerere yale yanayowapendeza tu!

Sasa ni namna gani unafikia serikali serikali ya mseto ni jambo, kama alivyosema Nyerere, linalohitaji uongozi kuliko kura ya maoni.
Nasema hili ni jambo ambalo linahitaji uongozi kwa sababu kura yeyote ya maoni itakuwa na pande mbili. Wana CCM wahafidhina akina Karume and company watasema hatuhitaji, wakati CUF watasema tunahitaji. .
Mheshimiwa Kitila, ili uyasarifu masuala hayo ,ya Zanzibar inabidi uwe mvumilivu kidogo,uulize mengi uyajuwe, ndipo ufanye uchambuzi wako wa kitaalamu. Hali iliyopo sasa hivi ya Upemba na Uunguja haikuvurumka wakati vinaanzishwa vyama vingi. Ilikuwa ni kabla ya hapo mara tu baada ya Seif na genge lake kufukuzwa na CCM (wakati wa Chama kimoja kule Dodoma) na katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyokuwa chini ya Mh. Idriss Abdulwakil (ambapo Seif alipoteza Uwaziri Kiongozi, na Duni Ukatibu Mkuu katika Afisi ya Waziri Kiongozi) Seif na genge lake wakaanzisha Kundi la kisiasa la kiharamia (wakati wa Chama Kimoja ilikuwa illegal) lilojulikana kuwa ni KAMAHURU. Hili ndilo chimbuko la siasa za chuki za Upemba na Uunguja ambazo zinatutesa leo hii. Wakati wa kuanzishwa kwa vyama vingi KAMAHURU wakatumia fursa hiyo kwa kupitia mgongo wa Mzee Mapalala (mwenye busara). Huyo Mzee aliachana nao baada ya kujua nini hasa dhamira ya Seif na genge lake ambalo lilijitumbukiza katika Chama chake na Kuunda hiyo Civic United Front iliyopo sasa. Dhana ya kurejesha hadithi hizo za siasa za kabla ya Mapinduzi ilikuwa ni gear ya CUF kuwachota wafuasi kutoka Pemba na wachache waliopo Zanzibar Mjini ambao wana asili ya Kiarabu na Kingazija, pamoja na Wahafidhina (wenye asili ya Kiarabu) walioko Mashariki ya Kati na Nchi za Ulaya. Katika option za kufuatwa ni hiyo ya kwanza, kwani ya pili (Chama kimoja) haina nafasi katika maendeleo ya jamii ya leo. Kwa mantiki hiyo ndiyo maana CCM inasimama kidete kuona kwamba tunakuwa na Serikali shirikishi iliyo madhubuti iliyosimama katika misingi ya Katiba, Sheria, Haki, na kukubaliwa na wadau wote. Siyo Mseto kama unavyozungumzwa na CUF na mashabiki wao. Hivyo Ndivyo Ilivyo.
 
Haya matatizo ya Zanzibar Ni uroho wa madaraka na kutokua na dhamira njema kwa wananchi pia kwa nchi.

Ndio maana utaona focus zao zote za watu wasio na nia njema hua wakati wa uchaguzi tu,watatumia gharama/maisha ya watu ili tu wapate njia ya kutekeleza nia yao mbaya.

Suluhu ya Zanzibar ni Rahisi mno ila kwa vile wote watafuta madaraka na wasivyo na nia ya nchi yao na wananchi wao bali mabwana wao watafanya kila hila kuwatumia wananchi ili wafikie malengo yao.

CUF na CCM kama wanania njema kwa nchi na wazanzibari ,mimi nafikiri wangekubaliana hivi ktk muafaka wao-
wabadirishe kifungu ktk katiba ya ZANZIBAR na MAWAZIRI wateuliwe kutoka wananchi wakawaida wasiwe WABUNGE(WAWAKIRISHI),nusu watoke pemba na nusu watoke ugunja.Hapo ukisikia watu wanauliwa ama wanaandamana kwa ajiri ya CUF ama kutembelea ulaya wanashitakiana basi tatizo litakua sio siasa.
Kwanini CUF hawataki kupropose njia hii?? Kwani mpaka CUF iingie madarakani ndio matatizo ya Pemba yataisha????

Shabash!!! Panapo mazungumzo Bwana suluhu inakuja tu. Unaona muelekeo wa Mheshimiwa Mkamap hivi sasa. Huo ni msimamo bora, why the Honorable Seif Sharif Hamad can't borroww a leaf from you. Hata akiizengea ile nafasi ya Unaibu Rais -1 inayopendekezwa nin sawan tu wadau watamkaribisha. Anaweza kuwa na point atakaporejea tena kwenye meza ya makubaliano kuitafuta suluhu ya kweli.
 
Wacheni kwenda mbali wakati tatizo la Zanzibar linajulikana na kila mtu hata CCM wenyewe wanalijua hilo ,yaani ukiwakuta wametulia na wako katika mudi wa kibindamu ,utawasikia wakisema CUF hatuwawezi na huu ni ukweli ambao mbali ya kuwa utakuwa mwenye bahati kuusikia ukitoka kwenye vinywa vyao lakini kama ni mtu na utu wako unakupa fikra za kiutu basi utahisi tu kuwa CCM haiwawezi CUF katika uchaguzi zinazotumika ni nguvu na ubabe wa kutumia polisi na majeshi ,natumai hilo wengi wenu mnalijua ,so far ushahidi wa karibuni kule katika Jimbo la Kiteto ,mbona mnakuwa na sahau au ndio uzee wa akina Msuya unawatembelea,hivyo ndivyo CCM inavyotamba lakini hawana kitu si Unguja si Pemba na si Kigoma Tanga na sehemu zingine,msikae hapa na kupoteza mida zenu kwa mambo ambayo CCM wanataka kuyaficha,ukweli CCM imeshapoteza kila sehemu ya Zanzibar kama inavyojulikana waliobaki ni wahafidhina.
Sasa hapa mtalonga sana lakini kinachojitokeza ni kuwa Wazanzibar maisha yao ni taabani sana sana ,fahamu tu Zanzibar hakuna viwanda kama huku Tanzania Bara ,wanategemea biashara za hapa na pale na kuletewa fedha za matumizi kutoka kwa majamaa zao na ndugu walioko nje na hata hivyo hazisaidii kitu ni kiasi cha kupitisha siku tu na kwa wale wafanyao kazi serikalini mshahara ni wa vuta nikuvute ukitahamaki imeshapita miezi miwili wanaofanya kazi serikalini wanalijua hilo,kwa kweli maisha yao ni ya kubabaisha babaisha na kukopa na madeni mengi.
Kwa mpenda amani yeyote yule atahitaji kuona Zanzibar inapata uongozi unaotokana na ridhaa za wananchi ,hivo kama kweli Watanzania au nyie mnaotoa mada za kichochezi na kuonyeshana vidole au kutiyana vidole machoni basi Zanzibar inahitaji Uchaguzi ambao utakuwa wa haki na huru ,jambo ambalo halijawahi kufanywa tokea uchaguzi wa vyama vingi uanzishwe.
Uitishwe Uchaguzi au na tuseme CUF watupilie mbali hoja hizi za miafaka irudi na lao jipya ,ambalo litaungwa mkono na kila mpenda amani ambae ataweza kuridhika kuwa ikiwa itafanywa hivyo na kutekelezwa basi hakuna atakaekuja kama mbogo kuwa ameibiwa au polisi wamikimbia na masanduku ya kura.
Jambo moja ambalo litairudisha Zanzibar katika amani ni kutumia nyenzo za umoja wa Mataifa katika kuendesha uchaguzi wa Zanzibar ,kuanzia uandikishaji mpaka upigaji kura na matangazo yake ,uendeshwe uchaguzi chini ya umoja wa Mataifa au tuseme kwa lugha inayofahamika Uchaguzi wa Zanzibar uendeshwe na kusimamiwa na umoja wa Mataifa UN maana hata AU unaweza ukaingia kasoro ,waletwe watu hapa hawafahamu hata kiswahili wala kiingereza.Yaani watu waendeshe kampeni zao kusini na mashariki ule mtindo wa kusema chama fulani hakikubaliki seheme fulani kwa hiyo kisiende kufanya mkutano wa kampeni hilo lisiwepo ,mtu afanye mkutano wake hata ikiwa atakuwa yeye na meza matuta na minazi lakini hakunyimwa haki ya kufanya mkutano.
Kwa kuhitimisha na kumalizia ni kuutaka uongozi wa CUF na Wa CCM ili kumaliza pata shika hizi ambazo zimepachikwa jina kuwa ni za kihistoria hivyo kunahitajika historia nyengine ambayo itafuta dhana hii potofu kuwa Wazanzibari wana matatizo tokea zamani ,wakubali wote kwa pamoja na watie saini kuwa uchaguzi wa 2010 usimamiwe na vyombo vya United nation na si vinginevyo .Kila mtu atulize roho yake.
 
Kasheshe, acha utani. Kama ingekuwa ni rahisi hivyo kwamba inahitajika endorsement tu kusingekuwa na mabishano ya masaa nane kwenye mkutano wa HKT ya CCM huku Butiama. Ni kwamba kuna watu ndani ya CCM huko Zanzibar hawakubaliani na hili jambo na itakapokuja kwenye kura za maoni watakampeni upande wa pili.

Mkuu, hakuna kura ya maoni ya endorsement msipotoshe wananchi. Kama issue ingekuwa ni endorsement baraza la wawakilishi Zanzibar lingefanya kama ilvyofanyika huko Kenya. Hapa kinachotafutwa ni kama kile walichofanya Kenya kuhusu katiba mpya na Zimbabwe kuhusu Ardhi ambako kote kulikuwa na rigorous campaign.

Mkuu, utaongea sana katika hili lakini what you are trying to do is to try to, unconvicingly, justify the unjustifiable!
Mimi nakubalkiana kabisa na Kasheshe. Ni kweli Vyama vyote vinakubaliana na Mseto (Serikali ya mchanganyiko,shirikishi)CUF wanafurahia wasirikishwe katika hali ya hivi sasa,na hivyo kuchukua nafasi ya Uwaziri Kiongozi. Kwa mujibu wa Katiba ya hivi sasa (na sheria zilizopo, na taratibu za kiutawala) Waziri Kiongozi ana madaraka makubwa, ni msaidizi wa Rais kwa kila hali (kwa kweli anakasimu sehemu kubwa ya madaraka ya Rais) Katika hali ya sasa ambapo wanatoka Chama kimoja ni sawa, lakini ikiwa vyama tofauti kutakuwa na kasheshe hapo katika kutekeleza majukumu yao. Rais atapata shida (iwe anatoka CCM au anatoka CUF-Seif Sharif baada ya uchaguzi wa 2010) Sasa basi ndiyo maana CCM wamekuja na maboresho hayo ya Manaibu wawili kumretain (Naibu 2 ambaye atatoka chama kimoja na Rais- na atamkaimu Rais katika dharura, ataongoza shughuli za Serikali katika Baraza la wawakilishi), ambaye atakuwa anayakasimu kwa kiwango fulani madaraka ya Rais, lakini ni sawa kwa sababu ni mtu kutoka Chama cha Rais(kilichoshinda). Vile vile atakuwepo Naibu Rais-1, atafanyakazi ya kutengeneza hiyo dhana ya Serikali Shirikishi katika kuwahudumia wadau. Lipo Baraza la usulihishi hapo liotaundwa kuwaweka katika mstari viongozi hao endapo watakuwa wanazozana katika harakati za kupigania maslahi ya wadau. Sasa hapo huo uhafidshina wa CCM Zanzibar uko wapi? Wewe usishughulike na wajumbe wa CCM Zenj kukamaa katika vikao hivyo vya CCM. Wao hawataki mseto katika mazingira ya mfumo wa sasa unaoweka Waziri Kiongozi. Ukikubali mfumo mbadala, huna haja ya hata kuwashawishi wao wataimba mseto mpaka kwenye mipasho ya taarab.
 
Mimi nakubalkiana kabisa na Kasheshe. Ni kweli Vyama vyote vinakubaliana na Mseto (Serikali ya mchanganyiko,shirikishi)CUF wanafurahia wasirikishwe katika hali ya hivi sasa,na hivyo kuchukua nafasi ya Uwaziri Kiongozi. Kwa mujibu wa Katiba ya hivi sasa (na sheria zilizopo, na taratibu za kiutawala) Waziri Kiongozi ana madaraka makubwa, ni msaidizi wa Rais kwa kila hali (kwa kweli anakasimu sehemu kubwa ya madaraka ya Rais) Katika hali ya sasa ambapo wanatoka Chama kimoja ni sawa, lakini ikiwa vyama tofauti kutakuwa na kasheshe hapo katika kutekeleza majukumu yao. Rais atapata shida (iwe anatoka CCM au anatoka CUF-Seif Sharif baada ya uchaguzi wa 2010) Sasa basi ndiyo maana CCM wamekuja na maboresho hayo ya Manaibu wawili kumretain (Naibu 2 ambaye atatoka chama kimoja na Rais- na atamkaimu Rais katika dharura, ataongoza shughuli za Serikali katika Baraza la wawakilishi), ambaye atakuwa anayakasimu kwa kiwango fulani madaraka ya Rais, lakini ni sawa kwa sababu ni mtu kutoka Chama cha Rais(kilichoshinda). Vile vile atakuwepo Naibu Rais-1, atafanyakazi ya kutengeneza hiyo dhana ya Serikali Shirikishi katika kuwahudumia wadau. Lipo Baraza la usulihishi hapo liotaundwa kuwaweka katika mstari viongozi hao endapo watakuwa wanazozana katika harakati za kupigania maslahi ya wadau. Sasa hapo huo uhafidshina wa CCM Zanzibar uko wapi? Wewe usishughulike na wajumbe wa CCM Zenj kukamaa katika vikao hivyo vya CCM. Wao hawataki mseto katika mazingira ya mfumo wa sasa unaoweka Waziri Kiongozi. Ukikubali mfumo mbadala, huna haja ya hata kuwashawishi wao wataimba mseto mpaka kwenye mipasho ya taarab.

CUF hawautaki mseto hata kuuona hiyo ndio imeshatoka wandugu ,na ndio mnaona kasi wanayoondokea CUF kama mnasema ni chama cha wapemba basi ndio hivyo hao hawasikii kitu tena ,mtabaki njooni tukae wameitega CCM na CCM imetegeka ,CUF ni wakali wa siasa,maana wameshaondoka na kila mtu na kuwawacha CCM mapepe ,sasa hivi kila kona ya dunia ina mawazo ya kuwa CCM ndio mbaya na huna pa kupita. Nasema hilo jambo ndio limeshatoka ,walala hoi wanasema imetoka hio !!!
 
1. Sitapenda kujadili historia ya Zanzibar, asili ya mtanziko wa kisiasa huko; lakini mimi naomba nichangia suala la principle tu hapa- kwamba pande mbili zimekaa zimajadiliana na kukubaliana mambo Fulani Fulani; baadaye upande mmoja umeanza kwenda tofauti. It’s a political problem, that needs a political solution.
2. Nimesoma neno kwa neno rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM ambayo ilishakubaliwa na kamati zote mbili. Suala la serikali ya pamoja linapaswa kutekelezwa kabla ya mwaka 2010.
3. Nimesoma ripoti ya Kamati ya CCM iliyopeleka Butiama kwa ajili ya Kamati Kuu na baadaye halmashauri Kuu; ukweli ni kuwa hoja ya kura ya maoni haikuzuka kikaoni- iliandaliwa kabla kwa pendekezo la Karume na kukubaliwa na wanakamati. Pamoja na uzuri wa dhana ya kura za maoni, lakini nia(motive) yake hapa si nzuri! Kwa serikali ambayo haifanyagi referendum katika masuala muhimu kihistoria kama Muungano, Katiba, Mfumo wa Vyama vingi, kumuundoa Rais wa Zanzibar kama makamu wa Rais(ambalo lilikuwa ni suala katika makubaliano mama ya muungano); inatia shaka serikali kama hiyo itakapo suala la kura za maoni Zanzibar. Ni Kikwete huyu huyu ambaye alipokwenda Kenya hakutaka wakina Raila na Kibaki wafanye kura za maoni, akata wasaini makubaliano na kuyatekeleza. Wakati wa kuibwa kwa kura hakuitishwa kura za maoni, kosa moja haliwezi kuhalalisha kosa, lakini kosa moja linaweza kutoa ishara ya kosa lingine! Kwa ujumla ukiisoma ripoti hii ya Kamati ya CCM; ukisoma na Barua ya Mwisho ya Makamba; utagundua kuwa Makamu Mwenyekiti Msekwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete- hawakusema kweli wakati wakieleza mchakato wa Maazimio ya NEC ya CCM na Matokeo yake!
4. Nilikuwepo Diamond Jubilee jana na nimemsikiliza Lipumba toka mwanzo mpaka mwisho. Nilichokielewa ni kwamba CCM imekuwa ikiwatapeli CUF toka baada ya uchaguzi, ikiwafanyia unafiki wa hali ya juu- CUF nayo kwa upande wake ilikuwabali ku-give in too much; ikakubali ghilba za aina zote ikiwa na matumaini makubwa kwamba Kikwete yuko genuine! Na kwa kiasi kikubwa mambo yote haya yalifanyika kwa siri ya pande mbili; kwa mategemeo makubwa ya CUF kwamba pengine serikali ya mseto ingetokea. Kumbe CCM wakati wote ilikuwa ikiweka kadi chache mezani na nyingine nyingi zaidi kuzificha chini ya meza.Ukiangalia mtiririko wa matukio katika hii miaka mitatu kuhusu Zanzibar utagundua ama Rais Kikwete anafanya unafiki wa hali ya juu wa kisiasa, au ni kiongozi dhaifu katika CCM kama mwenyekiti anayezidiwa nguvu na makundi mengine ndani ya chama chake. Kwa vyovyote vile, hali hii ikiachwa bila panga kuitwa panga na si kisu kikubwa ni ishara mbaya kwa utangamano wetu kama taifa haswa kwa kuwa kwa sasa CCM ndicho chama tawala!
5. Tunaungana mkono na CUF katika hili, kwani kitisho cha demokrasia mahali Fulani ni kitisho cha demokrasia mahali pote. Maandamano ya jumamosi, hayapaswi kuwa maandamano ya CUF, yanapaswa kuwa maandamano ya umma! Ama hakika, uwongo una mwisho- lakini ukweli unapaswa husimama milele, na ukweli hauna itikadi. CUF wanaweza kuwa walijikwaa mahali Fulani katika mchakato huu; lakini sasa ni wakati wa kutazama mbali zaidi, kutazama picha kubwa zaidi- CCM ikiwachwa ikapita katika hili, itandelea kuacha na ufisadi mwingine ukatawala kwenye RICHMOND, BOT nk na hatimaye kuweka misingi ya ufisadi wa kudumu zaidi katika uchaguzi mkuu 2010. Hatupaswi kuacha utadamuni wa ufisadi, usanii wa kisiasa, uchezeaji wa haki, na wananchi kukaaa pembeni kama watazamaji na wanyooshaji vidole kuendelea katika taifa letu. Ni wakati mwingine wa kuandelea kuchukua hatua!
JJ

PS:
• Mwenye Hotuba ya Jana ya Lipumba atuwekee hapa tafadhali
• Mwenye rasimu ya makubaliano ya CUF na CCM iliyokubaliwa na kamati za pande mbili aiweke hapa pia tafadhali

Ahsante Mnyika kwa hili,

Unajua kadri ninavyosoma maelezo ya wenzetu wa ccm hapa, utadhani kuwa makubaliano ni CUF ndiyo wanakiuka kumbe ni ccm ndiyo wanabadilisha mchezo na magoli kila mwaka.

Kikwete rudi toka Comoro uokoe nchi yako mzee!
 
John Mnyika;

Inasikitisha sana kuunga mkono wenzenu kurudi back to sqaure one; wakati walikuwa wanaelekea kwenye makubaliano... Najua hii ni sawa kwako na akina Lipumba kwa sababu hakuna unachokosa tukirudi nyuma tena...! Ni waZanzibar wanatamani mjadala huu uendelee uishe.... wewe na propaganda zako munaona kwamba muafaka utapatikana mtakosa ya kutokea kwenye majukwaa mshindwe kwa jina... na mlegee kabisa...



Ni uzembe wa hali ya juu sana tatizo la miaka mingi kulifanya la emergency kama ilivyokuwa Kenya... I'm sorry there must be a problem of IQ somewhere...

Kenya haikushauriwa kwenda kwa Wananchi kwa kura ya maoni kwa sababu mazingira hayo yangeleta machafuko zaidi...(hili lilisemwa wazi hata sisi tusiokuwa tuna-practise siasa kama wewe tulijua hilo)

Watu kama John Mnyika kweli ndio mwanasiasa wa kukabidhiwa nchi kwa uchambuzi wako dhaifu kiasi hiki.

Ati Kikwete ni dhaifu... unafahamu maana ya Rais na maana ya Mwenyekiti wa Chama... You seem not to be serious at all... Kama munaburuzwa na Mbowe CCM kuna vichwa huwezi buruza tu ndugu yangu... NEC ya CCM imesheheni watu makini mkuu!!!

Narudia tena kwa kuwa hakututumia kura ya maoni huko zamani... hata sasa ambapo demekrasia ni dhana muhimu ya utawala bora tusitumie... huu ni uvivu wa kufikiri...


Alafu ulazima wa kufanya kabla ya 2010 ni upi.... mimi nadhani katiba yes itabadilishwe kabla 2010 ili baada ya uchaguzi serikali ya mseto ndio iundwe...

Kasheshe,

Mzee wangu vipi leo, wengi hapa tumejua kilichotokea Butiama. Wengi hapa tumejua kuwa CUF na CCM walikubaliana kwenye kikao cha muafaka na kwenye meza ya marudiano na vyama vyote vikapeleka makubaliano kwenye vikao vya chama. Yaliyotokea ni kama ifuatavyo:

1. CUF wakapitisha rasimu ya makubaliano hence report ya BBC
2. CCM wakakataa mambo Butiama na wakataka kuanza maigizo.

Hii spinning ya kuwageuzia CUF inaweza kufanikiwa kule kijiji cha matembele lakini sio jambo forums.
 
Tatizo ninyi wapinzani munatamani muwe madarakani... mustakabali wa Zanzibar hauko ndani yenu kabisa...shida yenu ni kuingia madarakani...

.......

Shida yenu ni kuingia madarakani?
Kasheshe, hivi kuna chama cha siasa ambacho hakina malengo ya kushika hatamu za nchi? Naona hapa wewe ndio unalose it na sio Kitila?
 
Shabash!!! Panapo mazungumzo Bwana suluhu inakuja tu. Unaona muelekeo wa Mheshimiwa Mkamap hivi sasa. Huo ni msimamo bora, why the Honorable Seif Sharif Hamad can't borroww a leaf from you. Hata akiizengea ile nafasi ya Unaibu Rais -1 inayopendekezwa nin sawan tu wadau watamkaribisha. Anaweza kuwa na point atakaporejea tena kwenye meza ya makubaliano kuitafuta suluhu ya kweli.

CCM ndio wanavuruga makubaliano ya amani zanzibar na sio CUF. Nimesikitishwa sana na statement hapa kuwa CCM zanzibar ipo kulinda masilahi ya weusi, hii ni below standard wana ccm acheni kutafuta sababu ya kumwaga damu kwa chuki za kibaguzi!
 
CCM ndio wanavuruga makubaliano ya amani zanzibar na sio CUF. Nimesikitishwa sana na statement hapa kuwa CCM zanzibar ipo kulinda masilahi ya weusi, hii ni below standard wana ccm acheni kutafuta sababu ya kumwaga damu kwa chuki za kibaguzi!

Hapo wanawadanganya wenzao wakiamini watawakomboa lakini wanaporudi kwenye mishahara mpaka ipite miezi mitatu maji umeme ni kwenye nyumba za wahafidhina tu,mahospitali ndio hivyo mende wamewashinda kunguni ,usije ukajaribu kufungua droo unaweza ukaona upo katika kideo kwa mende wanavyohangaika kutafuta nafasi ya kukaa.Maana wangejiuliza iweje raisi mkewe awe ni muarabu bibi wa raisi muhindi ,hapa ndipo walipo wahafidhina wakiwakusanya wafanyakazi wa serikali na wanafunzi ndipo mkutano unapotimia la si hivyo basi watabaki na meza matuta na minazi wakiihutubia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom