CUF kuandamana nchi nzima

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
Leo Mwenkyekiti wa CUG, Prof Ibrahim Lipumba ameunguruma katika ukumbi wa Diamond Jubilee na kutoa msimamo wa chama hicho kuhusiana na masuala ya muafaka.

Kwanza CUF imempa masharti JK ili kunusuru mwafaka huo.

Wamemtaka aidha, CCM isaini makubaliano kama yalivyokuwa kabla haijatumbukiza kipengere cha kura ya maoni, au awakutanishe Maalim Seif na karume wajadiliane la kufanya kama ambayo aliwakutanisha Odinga na Kibaki kule Kenya.

Asuipofanya hivyo, kitakachotokea CUF imesema isilaumiwe.

Kwa kuonyesha nguvu yake, chama hicho kimesema kimeandaa maandamano yatakayofanyika mikoa yote nchini na wanaanzia Z'Bar Jumamosi ijayo wakiwashikirisha viongozi wakuu wa vyama vilivyo kwenye ushirikiano.

Wakitoka Zenji, wanahamia mkoa mwingine.

Tujiandae kwa mabomu ya machozi?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom