BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,009
Date::9/6/2008
CUF kuandamana kushinikiza mafisadi EPA kufikishwa kortini
Na Kizitto Noya
Mwananchi
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimesema kitafanya maandamano nchi nzima kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani watuhumiwa wa ufisadi wa Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA).
Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba alitangaza maandamano hayo juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Temeke Mwisho jijini Dar es Salaam.
Profesa Lipumba alisema Watanzania wana haki kuihoji serikali sababu za kutowafikisha watuhumiwa hao mahakamani na wataonyesha haki hiyo kwa maandamano yatakayofanyika mwazoni mwa Oktoba mwaka huu.
"Wito wa CUF kwa serikali ni kutaka iwafikishe mafisadi mahakamani na tumepanga kufanya maandamano makubwa nchi nzima kushinikiza suala hilo katika juma la kwanza la mwezi Oktoba,'"alisea Profesa Lipumba.
Alisema maandamano hayo ambayo yatawashirikisha watu kada mbalimbali yana lengo la kushinikiza watuhumiwa wa ufisadi wa EPA wafikishwe mahakamani, warejeshe fedha walizoiba na kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.
"Pia tunahitaji tume huru ya uchaguzi ili wananchi wapate fursa ya kumchagua kiongozi wanayompenda na tutadai katiba mpya ili tuishi katika jamii inayoheshimu misingi ya demokrasia," alisema.
Profesa Lipumba alisema anaamini serikali ya CCM haiwezi kuwa makini katika kuwashughulikia mafisadi kwani imekosa uongozi bora kwa kuwakumbatia wanamtandao ambao ndio mafisadi wenyewe.
Alisema njia pekee ya kuishinikiza serikali iwashughulikie mafisadi ni maandamano yatakayowashirikisha wananchi wote ili CCM ijue kwamba jamii imechoka na utendaji wake wa kazi.
Profesa Lipumba alitaja ufisadi wa EPA, rada, Richmond na ununuzi wa ndege ya rais kuwa maeneo machache ambayo serikali imeonyesha udhaifu uwajibikaji.
Alisema hakuna sababu zinazoelezeka za serikali kuwaongezea muda watuhumiwa wa ufisadi wa EPA kurudisha fedha, kushindwa kumshughulikia mtuhumiwa wa wizi wa ununuzi wa rada na ukosefu wa umakini katika kushughulikia suala la Richmond zaidi ya kuwalinda mafisadi wanaoonekana kuwa na ushawishi mkubwa serikalini.
Profesa Lipumba alibainisha kuwa fedha za EPA ni za umma tofauti na kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwamba sio za umma na Watanzania wana haki ya kuhoji ili kujiridhisha juu ya namna zilivyochotwa na zinavyorejeshwa.
Awali akimkaribisha Profesa Lipumba, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Mbarala Maharagande alisema kama serikali inaona vyema kuwaachia huru watuhumiwa wa EPA baada ya kurejesha fedha, basi iruhusu wafungwa na mahabusu watoke rumande na gerezani wakarejeshe mali walizoiba ili wawe huru.
Alisema kitendo cha kutaka watuhumiwa EPA warejeshe mali kinakiuka misingi ya demokrasia na utawala wa sheria na kinaligawa taifa katika makundi ya walalahoi na matajiri.
CUF imetangaza maandamano hayo wiki mbili baada ya kundi la wanaharakati kutoa tangazo la kutishia kufanya maandamano nchi nzima endapo Rais Jakaya Kikwete hatawafikisha mahakamani watuhumiwa watakaoshindwa kurudisha fedha ifikapo Novemba mosi kama alivyoahidi.
Awali kundi hilo lilipanga kufanya maandamano hayo Agosti 23 mwaka huu kwa lengo la kuishinikiza serikali itangaze majina ya watuhumiwa wa ufisadi wa EPA na hatua iliyochukuliwa dhidi yao lakini ililazimika kuyasitisha baada ya polisi kutoyatambua na kutaka wafuate taratibu za maandamano.
CUF kuandamana kushinikiza mafisadi EPA kufikishwa kortini
Na Kizitto Noya
Mwananchi
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimesema kitafanya maandamano nchi nzima kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani watuhumiwa wa ufisadi wa Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA).
Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba alitangaza maandamano hayo juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Temeke Mwisho jijini Dar es Salaam.
Profesa Lipumba alisema Watanzania wana haki kuihoji serikali sababu za kutowafikisha watuhumiwa hao mahakamani na wataonyesha haki hiyo kwa maandamano yatakayofanyika mwazoni mwa Oktoba mwaka huu.
"Wito wa CUF kwa serikali ni kutaka iwafikishe mafisadi mahakamani na tumepanga kufanya maandamano makubwa nchi nzima kushinikiza suala hilo katika juma la kwanza la mwezi Oktoba,'"alisea Profesa Lipumba.
Alisema maandamano hayo ambayo yatawashirikisha watu kada mbalimbali yana lengo la kushinikiza watuhumiwa wa ufisadi wa EPA wafikishwe mahakamani, warejeshe fedha walizoiba na kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya.
"Pia tunahitaji tume huru ya uchaguzi ili wananchi wapate fursa ya kumchagua kiongozi wanayompenda na tutadai katiba mpya ili tuishi katika jamii inayoheshimu misingi ya demokrasia," alisema.
Profesa Lipumba alisema anaamini serikali ya CCM haiwezi kuwa makini katika kuwashughulikia mafisadi kwani imekosa uongozi bora kwa kuwakumbatia wanamtandao ambao ndio mafisadi wenyewe.
Alisema njia pekee ya kuishinikiza serikali iwashughulikie mafisadi ni maandamano yatakayowashirikisha wananchi wote ili CCM ijue kwamba jamii imechoka na utendaji wake wa kazi.
Profesa Lipumba alitaja ufisadi wa EPA, rada, Richmond na ununuzi wa ndege ya rais kuwa maeneo machache ambayo serikali imeonyesha udhaifu uwajibikaji.
Alisema hakuna sababu zinazoelezeka za serikali kuwaongezea muda watuhumiwa wa ufisadi wa EPA kurudisha fedha, kushindwa kumshughulikia mtuhumiwa wa wizi wa ununuzi wa rada na ukosefu wa umakini katika kushughulikia suala la Richmond zaidi ya kuwalinda mafisadi wanaoonekana kuwa na ushawishi mkubwa serikalini.
Profesa Lipumba alibainisha kuwa fedha za EPA ni za umma tofauti na kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwamba sio za umma na Watanzania wana haki ya kuhoji ili kujiridhisha juu ya namna zilivyochotwa na zinavyorejeshwa.
Awali akimkaribisha Profesa Lipumba, Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Mbarala Maharagande alisema kama serikali inaona vyema kuwaachia huru watuhumiwa wa EPA baada ya kurejesha fedha, basi iruhusu wafungwa na mahabusu watoke rumande na gerezani wakarejeshe mali walizoiba ili wawe huru.
Alisema kitendo cha kutaka watuhumiwa EPA warejeshe mali kinakiuka misingi ya demokrasia na utawala wa sheria na kinaligawa taifa katika makundi ya walalahoi na matajiri.
CUF imetangaza maandamano hayo wiki mbili baada ya kundi la wanaharakati kutoa tangazo la kutishia kufanya maandamano nchi nzima endapo Rais Jakaya Kikwete hatawafikisha mahakamani watuhumiwa watakaoshindwa kurudisha fedha ifikapo Novemba mosi kama alivyoahidi.
Awali kundi hilo lilipanga kufanya maandamano hayo Agosti 23 mwaka huu kwa lengo la kuishinikiza serikali itangaze majina ya watuhumiwa wa ufisadi wa EPA na hatua iliyochukuliwa dhidi yao lakini ililazimika kuyasitisha baada ya polisi kutoyatambua na kutaka wafuate taratibu za maandamano.