CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
Awali Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Prof. Ibrahim Lipumba alipendekeza majina ya wajumbe wawili wa Baraza Kuu kwenye Baraza hilo ili wapigiwe kura kama inavyoelekezwa na Katiba ya CUF-Chama cha Wananchi Ibara ya 96(1).
Wajumbe waliopendekezwa ni Mhe. Hamida Abdallah Khuweshil na Mhe. Haroub Mohamed Shamis na walipopigiwa kura na Baraza KuuMhe. Hamida alipata kura 27, Mhe. Haroub alipata kura 33 na kura 2 ziliharibika.
Baraza Kuu limemaliza Vikao vyake usiku wa Jana na Maazimio ya Baraza Kuu yatawekwa hadharani kupitia Mkutano na Waandishi wa Habari utakaofanyika muda utakaobainishwa baadae.