CUF haina cheo cha mwanasheria mkuu wa chama, aliyetiwa bei asijikweze kutaka kujinenepesha mnadani

Ngoja hama hama iwakute Cuf visiwani.

Zanzibar ndio chimbuko la siasa za upinzani Tanzania tokea kuanza mfumo wa vyama vingi 1992, ndio walioifundisha Tanzania bara siasa za upinzani
Kama utakumbuka Zanzibar Fatma Maghimbi aliwahi kuwa mbunge JMT kwa ticket ya CUF, akina Juma Othman waanzilishi wa CUF wakasaliti chama wakaingia ccm lakini angalia CUF ndivyo ilivyopiga hatua kila miaka inavyosonga mbele mpaka leo hii ambapo ni tishio kubwa kuliko Chadema kule Bara. Ndio mana yanafanyika hayo wakidhani watafanikiwa kwa kiwango hicho.

Zanzibar si limbukeni wa ajira za ccm ni watu maskini lakini wenye msimamo unaondelea. CCM wa zanzibar na Tanzania Bara wanaelewa hivyo.
 
Zanzibar si limbukeni wa ajira za ccm ni watu maskini lakini wenye msimamo unaondelea. CCM wa zanzibar na Tanzania Bara wanaelewa hivyo.
Dominos effect ni hulka ya mwanadamu ngoja hautaamini macho na masikio yako.
 
Hapa pana point muhimu sana ya kuiangalia na ni advantage kubwa sana kwa CUF dhidi ya kesi ya Lipumba.

Ikiwa CCM na vyombo vya dola vinamkubali Lipumba kama ni mwenyekiti halali wa CUF baada ya kujipachika cheo hicho zaidi ya mwaka mmoja baada ya kujiuzulu, inakuwaje wanampokea MTATIRO kuwa mwanachama wa CCM dakika tu baada ya kujiuzulu. Jee kww Mtatiro na wengine suala la.kukubaliwa na kikao cha chama haiwahusu? Au CCM inakubali mwanachama wake kuwa na kadi za vyama vyengine tofauti kwa wakati mmoja? Kwa sababu kutokana na msimamo wa CCM na vyombo vya dola, unabakia kuwa mwanachama wa CUF mpaka kikao cha chama kibariki kujiuzulu kwako. Lini kikao kilikaa kubariki kujiuzulu kwa Mtattiro na Naibu Meya?

Naomba kufafanuliwa kuhusu hili suala?
 
Shetani hajawahi kumshinda Mungu hata mara moja , nimegundua una roho nyepesi sana ! hii cuf unayoiandika hapa imeacha kila cheo kule Zanzibar kuanzia udiwani , uwakilishi hadi urais ili kupigania haki , Maalim Seif hatishwi na hawa wenye njaa , ukiwa na akili hata ya kuendea uwani tu utajua anachokifanya lipumba hakina maisha , anatumikishwa kwa muda mfupi na atahamia ccm siku yoyote .
Uzuri siku hazigandi, tutadanganyana mwishi wa siku muda ndio unaamua. This is 2018, 2020 si mbali na uzuri mimi si wa CUF nayaangalia yajayo.
 
Swali kwa wana CUF kati ya Lipumba na Mtatiro nani msaliti wa chama?
 
Shetani hajawahi kumshinda Mungu hata mara moja , nimegundua una roho nyepesi sana ! hii cuf unayoiandika hapa imeacha kila cheo kule Zanzibar kuanzia udiwani , uwakilishi hadi urais ili kupigania haki , Maalim Seif hatishwi na hawa wenye njaa , ukiwa na akili hata ya kuendea uwani tu utajua anachokifanya lipumba hakina maisha , anatumikishwa kwa muda mfupi na atahamia ccm siku yoyote .
Lakini Mwenyekiti wa hiyo Kamati iliyoundwa na Maalim tayari mguu mmoja uko-Ccm..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa pana point muhimu sana ya kuiangalia na ni advantage kubwa sana kwa CUF dhidi ya kesi ya Lipumba.

Ikiwa CCM na vyombo vya dola vinamkubali Lipumba kama ni mwenyekiti halali wa CUF baada ya kujipachika cheo hicho zaidi ya mwaka mmoja baada ya kujiuzulu, inakuwaje wanampokea MTATIRO kuwa mwanachama wa CCM dakika tu baada ya kujiuzulu. Jee kww Mtatiro na wengine suala la.kukubaliwa na kikao cha chama haiwahusu? Au CCM inakubali mwanachama wake kuwa na kadi za vyama vyengine tofauti kwa wakati mmoja? Kwa sababu kutokana na msimamo wa CCM na vyombo vya dola, unabakia kuwa mwanachama wa CUF mpaka kikao cha chama kibariki kujiuzulu kwako. Lini kikao kilikaa kubariki kujiuzulu kwa Mtattiro na Naibu Meya?

Naomba kufafanuliwa kuhusu hili suala?
Kuacha uanachama si kujiuzulu, uanachama si cheo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom