Upepo wa kisiasa kisiwani Pemba unazidi kutoridhisha baada ya vitendo vya hujuma za wazi vinazidi kuongezeka kila kukicha,safari hii matawi ya vyama vya CUF na CCM yakiteketenzwa kwa moto na watu wasiojulikana. Haya ni maandalizi tu ya kuelekea uchaguzi mwakani? Je uchaguzi wenyewe utakuwaje mwakani? Wiki iliopita tulishuhudia zoezi la uandikishaji kusimama kwa ajili ya vurugu. Wakulaumiwa NANI? Tunafanya nini kuzuia vurugu kama hizi?