Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Wapenzi wa CUF, acheni kudanganya watu kwani mwaka jana Chadema hawakuweka mgombea Ubunge katika Wilaya ya Igunga. Waliogombea Ubunge Igunga walikuwa wawili tu - ROSTAM AZIZI ABDULRASOOL wa CCM aliyepata kura 35,674 na LEOPOLD LUCAS MAHONA wa CUF aliyepata kura 11,321.
Na katika kinyang'anyiro cha Uraisi Wilayani Igunga, pamoja na uchakachuaji uliofanyika Kikwete wa CCM alishinda kwa kura 34,090 akifuatiwa na Dr. Slaa wa Chadema kura 8,874 na Prof. Lipumba akawa wa tatu kwa kura 3,181. Ukitafakari kidogo utagundua mgombea Ubunge wa CUF anamzidi mgombea Uraisi wa CUF kwa kura zaidi ya 8,000 (see ?)
Hata hivyo Chadema waliweka wagombea Udiwani kwenye kata mbali mbali Wilayani Igunga na waliweza kushinda maeneo fulani tofauti na CUF iliyoambulia sifuri. Swali - huo umaarufu wa CUF Igunga unatoka wapi ?
Na katika kinyang'anyiro cha Uraisi Wilayani Igunga, pamoja na uchakachuaji uliofanyika Kikwete wa CCM alishinda kwa kura 34,090 akifuatiwa na Dr. Slaa wa Chadema kura 8,874 na Prof. Lipumba akawa wa tatu kwa kura 3,181. Ukitafakari kidogo utagundua mgombea Ubunge wa CUF anamzidi mgombea Uraisi wa CUF kwa kura zaidi ya 8,000 (see ?)
Hata hivyo Chadema waliweka wagombea Udiwani kwenye kata mbali mbali Wilayani Igunga na waliweza kushinda maeneo fulani tofauti na CUF iliyoambulia sifuri. Swali - huo umaarufu wa CUF Igunga unatoka wapi ?