Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
CUF kungoa vigogo CCM
CUF kimeanza kujigamba wazi wazi kwa kutoa tathmini inayoitwa ya kisayansi kuonyesha kwamba, kina uhakika wa kutwaa bila jasho jingi majimbo 47 ya ubunge Tanzania Bara matokeo ambayo kinasema ni tofauti na ya Visiwani ambako kinatarajia kuzoa viti vingi vya ubunge na uwakilishi.
Mengi ya majimbo yanayotajwa ni ya Mikoa ya Lindi na Mtwara ambako duru za CUF zinasema mawaziri wawili wa Serikali inayomaliza muda wake wanaweza kuangushwa na wagombea wa chama hicho.
Mawaziri wanaotajwa kuwa hatarini ni wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara. Mkuchika ni mbunge anayemaliza muda wake na ambaye anawania tena nafasi hiyo kwenye Jimbo la Newala, mkoani Lindi.
Mwingine anayewekwa njia panda na CUF ni Hawa Ghasia, ambaye ni mbunge anayemaliza muda wake katika Jimbo la Mtwara Vijijini.
Mwingine anayewekwa njia panda na CUF ni Hawa Ghasia, ambaye ni mbunge anayemaliza muda wake katika Jimbo la Mtwara Vijijini.
Meneja wa Kampeni wa CUF, Mohamed Miraji akitoa tathimini ya chama hicho katika mahojiano ya simu kutokea Shinyanga, Jimbo la Solwa, Jumatatu wiki hii, alisema tathmini ya chama chake tangu kuanza kwa kampeni hadi sasa kuelekea ukingoni inabainisha kuwa watachukua, bila jasho, majimbo 47 Bara mbali na ya Zanzibar.
Kwa mujibu Miraj majimbo hayo wameyapanga katika kundi la A na kwamba yenye utata kidogo yamewekwa kundi B+ kwa maana kwamba huko watashinda si kwa idadi kubwa ya kura. Mbali na alama hizo za A na B+, Miraji alisema majimbo mengine 20 wameyawakea alama B.
Akifafanua alama hiyo B ambayo ni tofauti na B+, kiongozi huyo alibainisha kuwa maana ya alama hiyo ni kwamba ushindi kwa kiasi kikubwa utategemea namna CUF na wagombea husika kwenye majimbo hayo watakavyocheza karata zao dakika za mwisho.
Alama A maana yake tuna uhakika wa ushindi kwa asilimia 90, B+ tuna ushindi ambao si wa wingi mkubwa wa kura na B tunaweza kushinda kwa kutegemea tutakavyocheza karata zetu, tukicheza vibaya tunaweza kushindwa, alisema kiongozi huyo anayeongozana na mgombea urais wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.
Aliyataja majimbo ambayo tathmini yao imeyapa alama A kuwa ni Mchinga lililokuwa likiongozwa na Mudhihir Mohamed Mudhihir na Newala la Mkuchika.
Mengine ni Handeni linaloongozwa na aliyepata kuwa askari wa mwavuli Awamu ya Tatu, Dk. Abdallah Kigoda na Mtwara Vijijini linaloongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Ghasia.
Kwingine ni Tunduru Kusini ambalo limegawanywa kutoka lililokuwa Jimbo la Tunduru chini ya Mbunge wa CCM anayemaliza muda wake, Mtutura Abdallah Mtutura, jingine ni Tanga Mjini lililokuwa chini ya aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Raia, Harith Bakari Mwapachu na Lindi Mjini la Mohammed Abdulaziz.
Mengine ni Geita lilillokuwa chini ya Ernest Mabina, Liwale chini ya Hassan Chande Kigwalilo, Masasi ambalo kwa vyovyote litatoa mbunge mpya baada ya aliyemaliza muda wake, Raynald Mrope kuangushwa kwenye kura za maoni.
Kwingine ni Kondoa Kaskazini lililokuwa chini ya Zabein Mhita, Nanyumbu kwa Danstan Mkapa, Kilwa Kaskazini kwa Dk. Samson Mpanda, Rufiji lililokuwa likiongozwa na Profesa Idris Mtulya.
CUF pia imejinasibu kutwaa Jimbo la Tarime lililokuwa likiongozwa na Charles Mwera wa Chadema, ambaye kwa sasa ndiye mgombea wa CUF.
CUF pia imejinasibu kutwaa Jimbo la Tarime lililokuwa likiongozwa na Charles Mwera wa Chadema, ambaye kwa sasa ndiye mgombea wa CUF.
Jimbo la Sumve chini ya mbunge anayemaliza muda wake, Richard Ndassa nalo limetajwa na CUF kuwa sehemu salama kwa ushindi, kama ilivyo kwa Jimbo la Solwa lililokuwa likiongozwa na mbunge anayemaliza muda wake, Ahmed Ally Salum.
Mtwara Mjini chini ya mbunge anayemaliza muda wake, Mohamed Said Sinani nalo limetajwa kuangukia mikononi mwa CUF.
Alisema kampeni za mwaka huu CUF imejidhihirisha kukubalika zaidi vijijini kuliko mjini na kwamba hali hiyo inatokana na ukweli kuwa awali vyama vya Upinzani havikuwekeza maeneo hayo.