CRDB Visa Card: Utata wa matumizi yake mtandaoni

Manitoba

JF-Expert Member
Jul 8, 2008
240
9
Kama una CRDB Visa Card, na ulikuwa unafikiria kuitumia kwenye internet, basi usithubutu kutia sahihi kuiwezesha kutumika mtandaoni (ila kama tu unajua unachokifanya).

CRDB wametoa card mpya zenye nembo ya visa, ambayo wanatangaza kwamba unaweza kununulia vitu mtandaoni. Inaonekana kama ni bonge la wazo mpaka pale utakapogundua jinsi gani zisivyo salama hata kiduchu.

Mtu yeyote mwenye namba ya kadi yako, pamoja na vile vinamba vitatu vya "usalama" vilivyo nyuma, anaweza kuitumia hiyo kadi yako kwenye mtandao bila tatizo lolote. Kwa hiyo ukiitumia kwenye tovuti ambayo si salama, basi ni kama umegawa namba yako kwa watu wengine kujihudumia.

Pia ukiisahau kadi yako mezani, na mtu/rafiki yako/mtoto wako mtukutu/mpenzi wako/secretary wako akapata mda wa kunakili pembeni hizo namba zako, basi pia inakuwa imekula kwako.

Kama ulikuwa unafikiria ile pin yako, basi sahau maana haina kazi kwenye mtandao.

Address Verification
Unaweza ukawa unajiuliza mbona kuna watumiaji wengi tu wa credit cards duniani na wasiwe na wasiwasi hivyo?

Moja ya njia ambayo huwa inatumika kupunguza wizi wa kutumia kadi za wengine ni kufanya uhakiki wa anuani. Kiasi kwamba mtu akiweka oda ya kitu basi oda yake itakubaliwa na kadi kutumika ikiwa tu anuani ya ambapo vitu vya kwenye oda hiyo vitatumwa ni sawa na anuani ya mwenye kadi.

Kwa CRDB hii feature wameifinya, kiasi kwamba mtu yeyote duniani anaweza kutumia kadi yako na kununua na kutuma vitu vyake sehemu yoyote duniani anavyotaka.

Paypal
Kutumia site kama www.paypal.com inaweza kusaidia kuondoa uwezekano wa mtu kukuibia namba za kadi yako online.

Kujiunga kadi yako na paypal sio tatizo, tatizo ni jinsi ya paypal kuihakiki kwamba kweli ni ya kwako.

Paypal wanachofanya ni kukuchaji fedha kidogo (wastani wa 2,000TZS), halafa katika muamala huo wanaweka namba ya siri fulani. Sasa wewe inabidi uangalie statement yako kutoka benki, uione hiyo namba, halafu uwape paypal. Assumption hapo ni kwamba hakuna mtu mwingine anaweza kuona statement yako zaidi ya wewe.

Sasa ndani ya paypal unaweza ukakamilisha taratibu. Ukija CRDB ili kupata tu details za hiyo transaction, jasho litakutoka. Inaweza ukadhani ni kitu simple tu kupata details za transaction (hata mimi nilifikiria hivyo), lakini amini usiamini utashangazwa :) ... Nimefanya si chini ya trip 10 kwenda CRDB kwa ishu hiii, usihesabu simu, na nimetoka kupiga nyingine sasa hivi ... lol ...

Ningetakiwa niwe nimeshakata tamaa ila tu nataka tu nifuatilie mpaka mwisho waniambie inawezekana au haiwezekani.

Ila kama huu ndio utaratibu, sioni ni jinsi gani wataweza kuwahudumia wateja hata 100 tu wanaotaka kujiunga na paypal. Achilia mbali kwamba hawa watu 100 inabidi wapige kwata CRDB more that 10 times, halafu wawe wanapiga simu mara kwa mara kuwakumbushia CRDB case zao. Na mara nyingi watu unaoongea nao CRDB hata hawaelewi unazungumzia nini.

Makubaliano yako na CRDB ni soo
Ili kuiruhusu kadi yako kutumika online, itabidi utie saini makubaliano yako na CRDB, ambayo yanavipengele ambavyo vinaiondolea CRDB jukumu lolote la kukuhakikishia usalama wako unpotumia kadi yako kwenye mtandao. Kwa hiyo ukiwa online na kadi yako, jua you are on your own.

Kwa watumiaji wengine duniani kuna taratibu za jinsi ya mtu kupinga kuchajiwa transaction ambazo hujazifanya wewe. Na kuna taratibu za jinsi gani utarudishiwa pesa zako.

Mpkataba wa CRDB hauoneshi kama kuna kitu kama hicho. Kwa hiyo mtu akipata details za kadi yako, siku zote itakuwa inakula upande wako.

Kwa hiyo baada ya kuutia saini tu nimehakikisha kadi yangu haiondoki machoni pangu, na pia nahakikisha akaunti hiyo ya CRDB haina vijisenti vingi ... mpaka ntakapomaliza hii exercise. :)

Hitimisho
Sasa hivi unaweza kutumia kadi yako ya CRDB kwenye mtandao, lakini you do it at your own risk, tena risk kubwa tu.

Kinachonitisha ni kwamba kama kadi yako imewezeshwa kutumika kwenye internet, mtu hana haja ya kukuibia kadi nzima kwa sababu utashtuka, utaripoti, na kadi itafungwa. Anachotakiwa kufanya ni kupata namba za kadi zilizopo mbele, na vile vijinamba vitatu vilivyopo nyuma ya kadi, na inakula upande wako kimya kimya.

Kama umeiwezesha kadi yako kutumika kwenye mtandao, na kama vijinsenti vyako kwenye akaunti yako sio vidogo, na kama huwezi kuitunza details za kadi kiasi hicho, ni vyema ungewaambia waizibe isitumike kwenye mtandao ... or u may have to learn the hard way.
 
Katika hali kama hii ni vipi wadau watahamasika kununua hisa za CRDB wakati ikiingizwa katika soko la hisa? Hizi ni weaknesses ambazo bila ya kutafutiwa ufumbuzi zita-cast a shadow of doubt kwa customers kama pesa yao iko safe. Can U please educate me on this?
 
Kuna wakati server ya crdb inayohusiana na hiyo ili crash watu wa nchi nyingi za asia walikuwa wanatoa pesa tu kwa wale waliokuwa wanajua jamaa walikaa kama siku 4 hivi mpaka mtaalamu wao walipokuja toka majuu

walahi kazi ipo nakwambia
 
Wadau naomba mtufahamishe vizuri, je ni wakati gani unapoweza ama kuruhusu au kuzuia kadi yako kuweza kutumika mtandaoni je nipale unapo apply for the new card au wakati wa kuichukua? nimeomba kadi crdb baada ya niliyokuwa nayo ku-expire.
 
Katika hali kama hii ni vipi wadau watahamasika kununua hisa za CRDB wakati ikiingizwa katika soko la hisa? Hizi ni weaknesses ambazo bila ya kutafutiwa ufumbuzi zita-cast a shadow of doubt kwa customers kama pesa yao iko safe. Can U please educate me on this?

Wanaangalia kama benki inapata faida mwanawane. Na inapata faida. Kumbuka pesa zikiibwa hapo, ni zako ndio zimeubwa, wewe ndio umepata hasara sio wao ... tena wao watakuwa wametengeneza mapata kidogo kwa transaction hiyo ya wizi ... sasa sioni kwa nini hata wewe usiende wekeza huko :)
 
Wadau naomba mtufahamishe vizuri, je ni wakati gani unapoweza ama kuruhusu au kuzuia kadi yako kuweza kutumika mtandaoni je nipale unapo apply for the new card au wakati wa kuichukua? nimeomba kadi crdb baada ya niliyokuwa nayo ku-expire.

Walipoanza haya mambo ya kadi kutumika mtandaoni, ilikuwa kwamba unapewa kadi ikiwa tayari kutumika mtandaoni.

Nadhani baada ya kugundua hizo loopholes ndio wakaweka utaratibu wa kukusainishe wewe makubaliano ambayo yanaiondolea CRDB wajibu wowote wa kukuhakikishia usalama wako, na hivyo hata ukiibiwa ni juu yako.

Kwa hiyo ukipata kadi yako mpya hutaweza kuitumia mtandaoni mpaka usaini kale kamkataba kao. Kwa hiyo uko salama mpaka pale utakapotia saini kale kamkataba kalikokaa upande.
 
Nafikiri inategemea. Nimetumia mara kadhaa na hakuna shaka, na jamaa wengi nawajua wanatumia bila shaka. Kwa kufananisha, nimewahi ona mtu hapo Norway kapata kwenye account yake 6 billions NKR ikiwa inatoka na makosa ya Kibenki na vivyo hivyo kule Sweden kuna jamaa wa Moscow (Mrusi) alilamba zaidi ya SKR equivalent to USD 2 ml bila wenyewe kushtuka kwa mwaka mzima kwa kucheza na Credit Cards. Huyu Mrusi mpaka leo anatafutwa huku akiendeleza huo uzandiki. Zingine nyingi zinafahamika.

CRDB VISA CARD haiwezi kuwa tofauti na hizi incidences. Ni pro and cons za technology. technology Inaweza kukubamiza au kukunyanyua.
 
Thanks Manitoba, itakuwaje kutumia kadi yako kwa single transactions-yaani ukitaka kununua kitu kwenye mtandao unacharge akaunti yako na fedha zile tu zinazohitajika?
Nimeona wengine wanatumia mtindo huu, imekaaje hapo mkuu!
 
Nafikiri inategemea. Nimetumia mara kadhaa na hakuna shaka, na jamaa wengi nawajua wanatumia bila shaka. Kwa kufananisha, nimewahi ona mtu hapo Norway kapata kwenye account yake 6 billions NKR ikiwa inatoka na makosa ya Kibenki na vivyo hivyo kule Sweden kuna jamaa wa Moscow (Mrusi) alilamba zaidi ya SKR equivalent to USD 2 ml bila wenyewe kushtuka kwa mwaka mzima kwa kucheza na Credit Cards. Huyu Mrusi mpaka leo anatafutwa huku akiendeleza huo uzandiki. Zingine nyingi zinafahamika.

CRDB VISA CARD haiwezi kuwa tofauti na hizi incidences. Ni pro and cons za technology. technology Inaweza kukubamiza au kukunyanyua.

Mzee mimi nadhani wanao-design hizi technologies huwa wanashirikisha sana akili. Kama tungekuwa sisi basi ndio tungesema hivyo kirahisi tu kwamba "Inaweza kukubamiza au kukunyanyua". Lakini wenzetu wanashirikisha akili na kujitahidi kuhakikisha kuwa technolojia inasaidia zaidi kuliko inavoumiza.

Sasa naomba nikupe fact mbili tatu ambazo pengine zitakubadili mawazo.

Kwa wenzetu interests za mwenye kadi zinakuwa protected. Kwengine kunakuwa na jinsi ambayo mwenye kadi anaweza kuilalamikia transaction ambayo hakufanya yeye, na issuer wa card yake akaissue kitu chaitwa "charge back" ambapo mwenye kadi anarudishiwa pesa yake, na mtua huduma anakatwa hiyo pesa.

Kwenye sehemu zenye utaratibu huu, anayeumia ni mtoa huduma na si mwenye kadi. Kwa hiyo hayo mabilioni unayoyatolea macho ni hasara zaidi kwa mtoa huduma kuliko kwa mwenye kadi.

Utaratibu huo unahakikisha kwamba mtoa huduma anajiridhisha kwamba hiyo kadi ni halali na mtumiaji wake ni halali. Na njia za kufanya hivyo kwa kutumia technolojia hiyo hiyo zipo, na zinatumika huku duniani: si mapambo.

Tofauti ya CRDB card hapa nikwamba mtu akitumia card yako ya CRDB, na ukaona transaction ambayo hukuifanya wewe, huna pa kulalamika. Maana yake CRDB ni kama wanasema ukiibiwa ni shauri yako. Yaani inawezekana hata kumtafuta mwizi wasikusaidie. :) Wakati kwa wenzetu ukiibiwa aliyesaidia wizi ndio anabanwa.

Umeona hiyo tofauti?
 
Thanks Manitoba, itakuwaje kutumia kadi yako kwa single transactions-yaani ukitaka kununua kitu kwenye mtandao unacharge akaunti yako na fedha zile tu zinazohitajika?
Nimeona wengine wanatumia mtindo huu, imekaaje hapo mkuu!

Kutumia card ya CRDB kwenye mtandao ni wazo zuri. Na CRDB inabidi wapongezwe kwa hatu hiyo.

Ninachosema hapa ni kwamba CRDB wamejitoa kwenye tatizo lolote litakalotokea kwa matumizi ya kadi yako. Kitu ambacho ni tofauti na kwa wenzetu kwa jinsi ninavyofahamu mimi.

Hiyo inafanya matumizi ya hii card yawe na risk zaidi. Yaani hata kama kosa ni lakwao bado hakuna wa kukusaidia.

Kwa mfano ukinunua kitu online halafu kwa bahati mbaya anayekuuzia akatoa fedha zaidi ya zile alizotakiwa kutoa. Halafu kwa bahati mbaya akawa anasuasua kukurudishia fedha zako. Hapo utakuwa huna jinsi ila kukubali umeliwa kimachomacho. Lakini kwa wenzetu kuna taratibu za kupinga transaction ambayo si sawa au si halali, na mwenye kadi waweza kurudishiwa pesa ambazo hukutakiwa kukatwa. Kwa CRDB inaonekana hakuna kitu kama hicho.

Sisemi kwamba CRDB wanatakiwa waweke utaratibu kama huo. Ila nasema wewe mtumiaji ujue hali ilivyo, usije ukang'atwa siku ndio ukaanza kutoa macho na kuwa mkali na CRDB.
 
Mimi nimetumia huduma hii kwa miezi sita na mpaka sasa sijapata matatizo na ukweli inarahisisha sana transactions zako. Zaidi ya kununua, unaweza pia ku-transfer pesa kwenda kwa mtu mwingine.
Cha muhimu angalau ukumbuke kila siku kuingia mtandaoni na kuangalia salio lako.
Mwanzo mgumu ila am confident "we" are progressing.
 
Je kuna haja ya kuomba ushauri wa baraza la walaji? hii ndio kazi yao kumlinda mlaji. Mimi naona kuna haja ya kushirikisha baraza hili na si kukaa kimya.
 
Mimi nimetumia huduma hii kwa miezi sita na mpaka sasa sijapata matatizo na ukweli inarahisisha sana transactions zako. Zaidi ya kununua, unaweza pia ku-transfer pesa kwenda kwa mtu mwingine.
Cha muhimu angalau ukumbuke kila siku kuingia mtandaoni na kuangalia salio lako.
Mwanzo mgumu ila am confident "we" are progressing.

Kwa hili CRDB wamepiga hatua, ila nafikiri cost ya hii kitu itakuwa ni kubwa zaidi ya Benefit. Cha kufanya kwa wale wenye kutaka huduma hii ni bora kuwa na account mbili yaani Moja ni kwa ajili ya transaction za online, unahamisha pesa na kufanya transactions on spot, hapo hapo. Nyingine ni kuhifadhia pesa kama una wasiwasi
 


Cha kufanya kwa wale wenye kutaka huduma hii ni bora kuwa na account mbili yaani Moja ni kwa ajili ya transaction za online, unahamisha pesa na kufanya transactions on spot, hapo hapo. Nyingine ni kuhifadhia pesa kama una wasiwasi

Ni kweli kabisa. Hii itaondoa wasiwasi wa kwamba unaibiwa au watu wanachezea account yako.
 
Sielewi kwa nini CRDB wameifinya hiyo feature ya address, kwa kufanya hivi wenye account zetu tumekuwa more exposed to fraud. Au ndio wanataka kuutangazia ulimwengu mzima kuwa- watanzania hatuna address?
Nisingemshauri mtu yoyote kutumia hii huduma for the time being hadi pale kutakapokuwa na uhakika kwamba kuna 100% protection kwa wateja na Bank iko tayari kuwa responsible pale ambapo kutatokea 'ufisadi'.
 
Mzee mimi nadhani wanao-design hizi technologies huwa wanashirikisha sana akili. Kama tungekuwa sisi basi ndio tungesema hivyo kirahisi tu kwamba "Inaweza kukubamiza au kukunyanyua".

Nakubaliana nawe. Ninaposema inaweza kukubamiza kwa mfano wa hizi Crdit Cards, ni pale ambapo unaweza ibiwa! Wanaibiwa wengi sana duniani. Ila lengo lake ni kurahisisha mambo kama ilivyo.


Tofauti ya CRDB card hapa nikwamba mtu akitumia card yako ya CRDB, na ukaona transaction ambayo hukuifanya wewe, huna pa kulalamika. Maana yake CRDB ni kama wanasema ukiibiwa ni shauri yako. Yaani inawezekana hata kumtafuta mwizi wasikusaidie. :) Wakati kwa wenzetu ukiibiwa aliyesaidia wizi ndio anabanwa.


Mimi hapo sioni tofauti. Kwani katika mazingira yote uliyoweka, hakuna sehemu ambayo Insuarer wa CC yako anawajibika kukulipa (compensation). Every transaction done is at your own risk.Nadhani unafahamu kwanini licha ya Bank kukupatia ATM Card wewe, wenyewe kama Bank huwa hawatakiwi kuijua na hawawezi? Suala la kubanwa kama unvyoliongelea ni la kawaida, unaweza pata pesa yako au usipate!. Naongelea losses hapa.

Naamini CRDB iko sawa sawa na tutafika kule wengine waliko. Mtoto asipochafuka unadhani atajuaje kucheza mpira wa miguu?
 
Mimi nimetumia huduma hii kwa miezi sita na mpaka sasa sijapata matatizo na ukweli inarahisisha sana transactions zako. Zaidi ya kununua, unaweza pia ku-transfer pesa kwenda kwa mtu mwingine.
Cha muhimu angalau ukumbuke kila siku kuingia mtandaoni na kuangalia salio lako.
Mwanzo mgumu ila am confident "we" are progressing.

Sawa kaka.

Sisemi kwamba wewe ndio ulivyo, ila sisi tuna kawaida sana ya zima moto. Kwa sababu inafanya kazi, basi kheri. Yakianza kutokea matatizo, unaona kama muujiza na kulalama kwa nini benki yako haikulindi. Lakini pengine mtu ungejua ukweli ulivyo, mtu ungejua risks ziko wapi na ungekuwa makini zaidi na unachokifanya.

Sielewi kwa nini CRDB wameifinya hiyo feature ya address, kwa kufanya hivi wenye account zetu tumekuwa more exposed to fraud. Au ndio wanataka kuutangazia ulimwengu mzima kuwa- watanzania hatuna address?
Nisingemshauri mtu yoyote kutumia hii huduma for the time being hadi pale kutakapokuwa na uhakika kwamba kuna 100% protection kwa wateja na Bank iko tayari kuwa responsible pale ambapo kutatokea 'ufisadi'.

Sadakta! Ndio maana nikasema, "usithubutu ila tu kama unajua unachokifanya".

Wasiwasi wangu mkubwa ni kwamba kwa jinsi CRDB wanavyoitangaza kama vile hakuna risk yoyote, watu watazikurupukia na wengi wataumia.

Bottom line is, know what you are doing.

Mzee mimi nadhani wanao-design hizi technologies huwa wanashirikisha sana akili. Kama tungekuwa sisi basi ndio tungesema hivyo kirahisi tu kwamba "Inaweza kukubamiza au kukunyanyua".

Nakubaliana nawe. Ninaposema inaweza kukubamiza kwa mfano wa hizi Crdit Cards, ni pale ambapo unaweza ibiwa! Wanaibiwa wengi sana duniani. Ila lengo lake ni kurahisisha mambo kama ilivyo.


Tofauti ya CRDB card hapa nikwamba mtu akitumia card yako ya CRDB, na ukaona transaction ambayo hukuifanya wewe, huna pa kulalamika. Maana yake CRDB ni kama wanasema ukiibiwa ni shauri yako. Yaani inawezekana hata kumtafuta mwizi wasikusaidie. :) Wakati kwa wenzetu ukiibiwa aliyesaidia wizi ndio anabanwa.


Mimi hapo sioni tofauti. Kwani katika mazingira yote uliyoweka, hakuna sehemu ambayo Insuarer wa CC yako anawajibika kukulipa (compensation). Every transaction done is at your own risk.Nadhani unafahamu kwanini licha ya Bank kukupatia ATM Card wewe, wenyewe kama Bank huwa hawatakiwi kuijua na hawawezi? Suala la kubanwa kama unvyoliongelea ni la kawaida, unaweza pata pesa yako au usipate!. Naongelea losses hapa.

Naamini CRDB iko sawa sawa na tutafika kule wengine waliko. Mtoto asipochafuka unadhani atajuaje kucheza mpira wa miguu?

Kweli huoni tofauti? Umeshasikia kitu kinaitwa "Charge Back"? Kama hujawahi basi ndio maana huoni tofauti.
Soma kidogo hapa: Chargeback - Wikipedia, the free encyclopedia

Ukweli ni kwamba kwa wenzetu interest za mwenye kadi zinalindwa, wakati hapa CRDB imejitoa jukumu lolote la kufanya hivyo. Yaani kwa CRDB kukiwa na transaction ya makosa au fraudulent transaction, basi ndio umeuwawa. Kwa wenzetu kunakuwa na taratibu za jinsi gani ya ku-complain, na hata kurudishiwa pesa zako. Kwa CRDB hakuna, kama huamni kasome kale kamkataba. "Every transaction done is at your own risk" ni statement inayoweza kutolewa na CRDB na issuer wengine wasiojali maslahi ya mwenye kadi kabisa.

Mzee bado huoni tofauti?

Kweli kufika tutafika. Lakini wakiendelea kuwa na customers wanaokubali wasiwe na rights namna hiyo kila kitu namna hiyo, basi twawezafika tukiwa tumechelewa kiaina.

Ngoja labda nikupe sababu kwa nini wenzetu wanaona kuna umuhimu wa kuweka kitu kama "Charge Back" tena mpaka kwenye sheria zao.

Mantiki sio tu kumlinda mtu na pesa zake tu. Ni kwamba usipoweza kuwa-assure watu kwamba they are safe, in the long run wengi wata-opt-out. Na ukiwa na wengi hawaingiii kwenye hiyo system, ndio tutakuwa tunachelewa hivyo kufika.

Halafu pia kuwepo kwa "Charge Back" kunamfanya mtoa huduma kuchukua steps kuhakikisha kwamba CC/DB ni halali, na pengine mtumiaji ni halali. Hizi steps zipo tayari, na watu wanazitumia. Ukiondoa "Charge Back", mtoa huduma hatakuwa na incentive yoyote kuhakiki kwamba matumizi ya CC/DB ni halali.

Kama huelewi hilo wewe subiri pale makampuni ya ki-tz yatakapo anza kutoa huduma online, na kucharge kwa kutumia hiyo Visa card ya CRDB. Naweza nikakwambia kitakachotokea. Either watu hawatatumia hizo huduma, ama CRDB watabadili hako kamkataba.

Kuna mzee wangu mmoja aliniambia kuona mbele si kazi, hata mbuzi anaona mbele. Kuona mbali ni issue.

<rant>
Pengine tujitahidi kuepuka kuweka statement za jumla jumla ambazo hatuna uhakika nazo, ili mradi tu kusupport argument zatu.
Unapoweka statement kama "hakuna sehemu ambayo Insuarer wa CC yako anawajibika kukulipa (compensation)", halafu kukakosekana mtu wa kuonyesha kwamba umekosea, unakuwa umepotosha wengi baba.
</rant>
 
Last edited:
Pengine tujitahidi kuepuka kuweka statement za jumla jumla ambazo hatuna uhakika nazo, ili mradi tu kusupport argument zatu.
Unapoweka statement kama "hakuna sehemu ambayo Insuarer wa CC yako anawajibika kukulipa (compensation)", halafu kukakosekana mtu wa kuonyesha kwamba umekosea, unakuwa umepotosha wengi baba.



Mkuu, inaonyesha wewe umesome tu kwenye shule kuhusu credit cards. Mimi siyo mtalaamu wa uchumi wala mtu wa banki, ila nimetumia CC kadhaa. Labda siwezi kueleza zaidi kwa sababu hiyo. Ila kuhusu wizi kwa credits cards na compensation unaweza check hapa upate info zaidi ya ile niliyokupatia. <http://en.wikipedia.org/wiki/Credit_card_fraud>
Huyu jamaa pamoja na huyu <http://www.securityfocus.com/news/11493> wanakuambia kuwa ni hela nyingi sana zinaibiwa Duniani kwa CC kila mwaka. Hao wote si CRDB. SOma kwa makini sana.


Hatubishani ila tunaongelea kwa uzoefu wa kutumia na si kusoma shule na pia kupeana ujumbe kwa kutumia experience. Siwateti CRDB kwa namna yoyote ile na CRDB hawawezi kufanana na Inter-national companies za America au Europe za CC. Pia pamoja na kuwa kuna hiyo disclamer kwa CRDB nimewahi fanya makosa ya k-transaction kwa tune ya equivalent ya 500,000TSHS. Nili-report international Banking section pale CRDB TZ wakarekebisha in three days.

Ila ninasema kwamba wako sawa sawa kulingana u-TZ kule. Wata-improve tu service zao with time. Sio muda wa kuanza kwaponda kuwa wao nyuma na hawajali rights za wateja wao. Kuna banks kadhaa za SEA zina masharti magumu sana na nilishangaa sana jinsi wateja wanavyo-chargiwa services a hizo benks ukifananisha na Europe au TZ na jinsi wanavyolalamika sana. Lakini bankers wana sababu.

Tujitahidi kupenda home na vitu vya home. Vilivyo majuu havikushuka. Vilianza hivi hivi.

Take home message: Shule ina umuhimu wake. Ila uzoefu wa siku nyingi una umuhimu zaidi. Rubani aliyekuwa trained kuendesha Boeings za abiria mwaka jana, hawezi kuanza na 747-400 immediately. Lazima aanzie chini kwenye 737-200 kwanza!
 
Tehe tehe sisi wa vijijini tumepona maaan tumezoea kupanga foleni ya NMB, VISA wapi na wapi? Asante kwa taarifa incase tumepata na sisi fulsa hiyo tutakuwa makini.
 
Nakushukuru sana Manitoba. Wahenga walisema, ukiona mwenzio ananyolewa, nawe tia maji. Kinga ni bora kuliko kutibu. Nawashauri wenzangu wote tunaotumia kadi hii ya CRDB tuwe makini, tusipuuzie kwani kilio kitakuwa mjukuu wetu. CRDB nao wanatakiwa kujibu maswali wanayoulizwa na wateja wao kuhusu usalama wa matumizi ya kadi hii, kwani kukaa kimya nako kunatoa mwanya kwa wateja wao na watu wengine kusema wanayoona yanawafaa
 
Back
Top Bottom