CRDB, fanyieni kazi tatizo la business transactions, nmeshindwa kupata huduma

Kila siku mtandao hakuna leo nimeshindwa kutuma pesa Mtandao. Hii benki hopeless.

Hili neno kwa CRDB limeshakuwa kama wimbo wao wa kazi. Kila ukienda Bank yao utakuatana na hii habari "mtandao upo chini". Mbona mitandao ya bank zingine haiendi chini. Wao wanaweza wana nini kiasi kwamba ninyi mmeshindwa, mnabaki kubahatisha.

My advice: Employ competent people who can serve your clients to their satisfaction otherwise you will lose them.
 
Charles Kimei wa CRDB, Nehemia Mchechu wa NHC na Ramadhan Dau wa NSSF ni mapacha watatu wa awamu ya Nne ambao ndio walikuwa think tank ya JK

You can call them "think tank" ya JK or whatever; the three were the facilitators of Kikwete's looting of the country!!! JIWE amefanya busara sana kuwatimua bila kuwapeleka Lupango kama alivyomfanyia Kitilya!!! Kuna tetesi kuwa tawi la CRDB Kimei alilojenga CHATTO kujipendekeza kwa Jiwe limefungwa kwani hakuna biashara!!!
 
CRDB haijaanza huo ushamba leo. Toka Kimei yupo hapo wamekuwa wanafanya mambo ya kishamba vilevile.

Ni kweli kuwa IT department ya CRDB in a matatizo. Juzi nilifungua website yao na kukuta tangazo la declaration of dividends; as a shareholder nilitaka kuthibitisha kama AGM ilibariki utowaji wa hilo gawio. Nikashangaa kuwa lile bandiko lao sio sahihi na wanatarajia kuwa na AGM virtually because of coven-19 at a later date,hivyo the dividend payment might be at the end of June!!! I talked to one senior officer of the bank about the anomaly in their website, he promised to talk to responsible officials in order to rectify the problem!!!

Uzembe kule CRDB sio IT department peke yake nadhani hata ofisi ya Corporation secretary ina mapungufu mengi; kumbuka hawa ndio wanaoshuhulika na sharaeholders lakini hawahakikishi kuwa correct information is posted on the website.!!!
 
CRDB haijaanza huo ushamba leo. Toka Kimei yupo hapo wamekuwa wanafanya mambo ya kishamba vilevile.

Nakumbuka 2013, niliwaomba wa-activate card yangu kufanya online transaction. Wakanijazisha forms.

Nilifuatilia ile form mwezi mzima wananipiga kalenda. Nikahamia Standard Chartered Bank. Toka siku hiyo sijajutia.

Leo hii unaweza fungua account kwa App ya SC bila kwenda bank. Na kila kitu ukaattach hapohapo. Haya mambo Crdb hawawezi.

Crdb na Nmb ni benki local, zina wafanyakazi wanaowaza kilocal zaidi.
Standard chartered wako njema unafungua akaunti hata kwa APP wamenibamba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo tayari wamesha kukosesha deals kibao na kukuingizia hasara ya kutosha.. Tunakazi kubwa sana kama taifa ya kumshinda adui ujinga na umasikini
 
Kimei kutengeneza ukabila crdb hana legacy ya kumkumbuka.

Crdb caribu heads wote wa idara, sections and branches utakuta ni ndugu zake/wakaskazini wenzake.

A country with over 50m people kupendelea watu wa kanda yako pekee ni ujinga ambao hauna mfano.
kwani hao sio watanzania ? hawana vigezo ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo tayari wamesha kukosesha deals kibao na kukuingizia hasara ya kutosha.. Tunakazi kubwa sana kama taifa ya kumshinda adui ujinga na umasikini
Wababaishaji Sana hawa Jamaa ipo siku watakutana na kichaa bobu atawasue. Najua wanaweza kumudu gharama za wanasheria nguli but image Yao itachafuka cause Jamaa anaweza kushirikisha na media. Kesi ikawa knaripotiwa kwenye media kwamba crdb wamezingua
 
Kila siku mtandao hakuna leo nimeshindwa kutuma pesa Mtandao. Hii benki hopeless.
Hao jamaa wa CRDB niliomba wan activate na sim banking, hhaahahahah miezi mitatu sasa kila siku wanasema nenda kwenye ATM ujihudumie, mara ya mwisho kadi ikamezwa. Nilikuwa moshi mjini pale eti wameweka na katangazo kuwa fanya transactions haraka hakara ukichelewa kadi itamezwa, amini usiamini nilichelewa kidogo na kweli kadi ikamezwa. Hopeless kabisa hao jamaaa.
 
Siamini kama crdb wamekuwa wababaishaji kiasi hiki...

Miezi miwili iliyo pita nilijaza fomu ya kujiunga na online purchasing...

Nikaambiwa nitatumiwa Temporary Access code ndani ya masaa 24. Zikapita siku mbili sijatumiwa hiyo namba, nikamwambia kuulizia kulikoni. Kama kawaida Yao wakaomba namba ya akaunti, namba SITA za Mwanzo za kwenye card number yangu na namba nne za Mwisho. Nikafanya kama walivyo agiza then nikaaambiwa after 24 hours nitatumiwa namba..

Two days later number bado haijatumwa. Nikaamua kwenda makao makuu.
.
wakachukua details zangu nikaaambiwa nitatumiwa namba baada ya masaa 24.

siku tatu zikapita bila majibu. Nikapiga simu.. nikaambiwa Tena ntatumiwa namba baada ya masaa 24..

seven hours later nikatumiwa temporary access code...

Kwenda kwenye website Yao nikafanya kama walivyo elekeza..

Sehemu ya majina yangu nikajaza jina la Mwanzo na la mwisho Kwa herufi kubwa then nikaweka na hiyo temporary access code Yao..

Baada ya Ku click, ikaleta majibu Password and names do not match.

Nikajaribu mara ya pili, password and names do not match.


mara ya tatu nikaambiwa the service has been suspended.

nikapiga simu nikaambiwa ntatumiwa access code nyingine after two hours.

after two hours HAKUNA namba iliyo tumwa, kupiga simu nikaambiwa after twenty four hours natumiwa namba..

toka mwezi wa tatu mwishoni mpaka WA huu WA SITA majibu NI Yale Yale..

Watu wengi wanawalalamikia crdb kuhusu huduma hii.

crdb badilikeni SASA... Vunjeni kitengo chenu cha IT ni wababaishaji mno..

watu tunashindwa kufanya business transactions Kwa sababu ya uzembe na ubabaishaji wa IT experts wenu.


personally nimevunja account yangu ya crdb.

hela zote nimehamishia Standard Chartered Bank..

sijui NI wateja wenu wangapi watakuwa wamefanya hivi.

yani watu wenu wa it wanafanya mambo kienyeji Sana. Like seriously!!! Yani hawawezi kufanya majukumu Yao mpaka uwapigie kuwakumbusha?

This is too unprofessional. Enzi za Kimei hakukuwaga na ubabaishaji kama huu.

IT EXPERTS wa Standard Chartered Wana kitu gani ambacho IT experts WA Crdb hawana?

how comes nimeenda Standard Chartered nimefungua account, Kasi ilivyo kuwa activated nikaenda kujiunga na huduma ya online purchasing na imekuwa activated ndani ya siku moja?


Nitamshauri vp MTU anaetaka kujiunga na huduma ya online purchasing akafungue akaunti Crdb wakati Standard Chartered wapo?

Hata ngombe Hawezi kuyapeleka Makinda yake kwenda kunywa maji kwenye kisima chenye maji masafi wakati anajua mahali kilipo kisima chenye maji masafi.

Dunia ya sasa karibu kila kitu kinafanyika online..Taasisi kubwa kama crdb inakuwa na experts wanao fanya ubabaishaji kwenye kitengo muhimu kama hicho inakuwa haimake sense..

Kwa usumbufu mlio nifanyia mngeufanya Kwa mtu kama Mtikila am sure as hell huko mahakamani kungekua na jalada linalosomeka MTIKILA Vs CRBD.

Angewashtaki for the breach of contract

crdb lifanyieni kazi Tatizo haraka iwezekanavyo.

asanteni na kwaherini

Nilijaribu hii huduma 2016 mpaka nikakata tamaa ikabid nifungue account bank nyngne tu sasa juzi kat nimeona kadi ya crdb nikasema nijaribu tena hii huduma ila hz kasumba mkuu hata siziwez ngoja nifungue bancABC ile card bila account tu
 
Bank imeshavaa kaptula, huyu aliyechukua nafasi ya Kimei hamna kitu kabisa
 
Crdb Nmb Tpb - Usithubutu kutumia hizi bank kwenye online purchasing. Utajuta

Benki za kutumia kwenye online purchasing ni ABC na Exim ndo wako vizuri. Equity wako vizuri kwenye payment (one way payment) ila usiitumie ku receive hela wana usumbufu kwenye kupata hela kutoka online.

~ Experienced user

Equity wanasumbua kupokea hela toka lini!?
Mimi nina mwaka wa 3 napokea kupitia equity sijawahi pata tatizo lolote!
 
CRDB is a local bank,full of people from nothern part of tanzania.Hata mikopo yao ni ovyo kabisa wanakwapua nssf za watu as if hiyo mikopo haina bima.Kimbia haraka kutoka kwenye hii local bank,wanaoperate chini ya kiwango cha kibubu.
kwahiyo unamaanisha wale wazee wa mbege kazi imewashinda?
 
ha ha ha ha ume nikumbusha
CRDB Bank ilikua n moja ya bank niliyo kua naikubali saaana sana yani kias kwamba nilipo maliza tu Adv nilifungua kwa mara ya kwanza A/c crdb na mkopo wang wa chuo wote ulikua unapita crdb na hata kazi yang ya kwanza mshahara nilikua napokelea crdb

Sasa kipindi iki mambo ya Online Purchasing ndo yame pamba moto nili amua nitumie pia bank yang hii kwa ajili ya miamala ya aina hii
kila niki enda tawini kuunga hiyo huduma nafata taratibu zote lakin nilikua sifanikiwi siku wahi hata kutumiwa hzo Access code mpaka leo hii zaid ya miaka 7 natumia hii bank

Nilkuja Fungua Acc ya SKRILL nika i link na Card yang ya Visa kuna muamala uli paswa ufanyike kisha nitume zile transaction details kwa skrill team ili ku verify acc yang eeeh nime fika Reception nawaeleza nime fanya muamala skrill nahitaji Bank Statement

Staff ana niuliza Skrill ndo nn? nika muelekeza kisha akapiga simu kwa Back office kuna mteja wa Skrill apa nashindwa muhudumia jamaa sijui walimpa jibu gani lakin inshort sikupata msaada wowote toka kwao ndo nikawa najiuliza hivi hizi Bank zetu ndo zipo Local hivi hata Online wallets hawazijui?


kama Crdb mna soma apa basi mjitahidi kuendana na mabadiliko ya tech mambo mapya kila siku yana ongezeka hii ni karne ya Sayansi na teknolojia wazeee
 
Back
Top Bottom