CPA/CPA/PSPTB nk vinaongeza wahitimu wasio na hela kubaki mtaani

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
Tuwaangazie wahitimu ambao husemekana wanatakiwa kuwa na sifa ya ziada. Naandika makala haya nikiwa najua uwepo wa Bodi nyingi nchini ambazo huwapa sifa za ziada wahitimu mbalimbali wa kada tofauti tofauti.

Wahasibu wakisimamiwa Bodi ya Wahasibu NBAA, ambo kuwa muhasibu mwenye sifa ya ziada utatakiwa kufanya mitihani yao na ukipata CPA (T) Basi inakuwa ni sifa ya ziada kwako kwenye soko la ajira.

Bankers wanasimamiwa na TIOB, ambao hawa hutoa CPB kwa bankers kama watafaulu mitihani yao na kuendelea kuwa mwanachama ili kujiongezea sifa ya ziada

Wagavi wanasimamiwa na PSPTB.

Hizo bodi nilizozitaja hapo zinatoa certification kwa mtu kwanza kufanya mitihani ambayo inahitaji ada, na kama mtu akishindwa basi huwa hawezi kupata cheti husika.

Ziko bodi nyingine ambazo zinahitaji uwe memba tu, kwa kulipa ada ya mwaka, bodi kama ya wahandisi, ERB, au hata hii ya walimu ambayo iliombwa kipindi fulani, najua mtaongeza bodi nyingine ambazo hudai mitihani ili kupata cheti au zile zinazotaka uwe meber tu

Hoja yangu!

Ieleweke kuwa wanafunzi wengi hutegemea mikopo kusoma masomo yao ya elimu ya juu. Bodi ya mikopo humpa mtu mkopo kwa muda ambao yuko chuoni tu! hizo bodi hazihesabiki kama ni sehemu ya chuo, hivyo mtu anayetoka chuoni hutegemea kujisomesha kwenye bodi hizo ili kupata sifa hizo za ziada.

Vitu kama CPA hugharimu si chini ya milioni kwa mitihani yake, CPB halkadhalika, hawa wengine ni zaidi ya laki mbili. Sasa mtu aliyetoka chuoni aliposomeshwa kwa mkopo anatarajia atapata wapi hela ili ajisomeshe kama sio kuongeza gap kati ya wenye nacho na wasio nacho, kwa kuwa wenye nacho wataweza kusoma na kuongeza sifa za ziada huku wasionacho wakisubiri ajira ili watumie mishahara kujipa sifa ya ziada, wakati wao wanasubiri kazi zinasema CPA is an added advantage.

Kitawafanya wasote mtaani huku wanye CPA wakipata mashavu kirahisi

Nadhani hii ni sababu nyingine ya kupunguzana

USHAURI:
Hii inaonyesha degree haitoshi kumfanya mtu aweze kuajiriwa, Je kwa nini mitihani ambayo wanaifanya katika bodi mbalimbali isiongezwe kwenye mtaala wa elimu ya Chuo Kikuu ili mtu akihitimu shahada yake anakuwa tayari yuko na sifa zote, ili kwenye soko la ajira mchuano uwe fair?

Signed!

OEDIPUS
 
Tuwaangazie wahitimu ambao husemekana wanatakiwa kuwa na sifa ya ziada. Naandika makala haya nikiwa najua uwepo wa Bodi nyingi nchini ambazo huwapa sifa za ziada wahitimu mbalimbali wa kada tofauti tofauti.

Wahasibu wakisimamiwa Bodi ya Wahasibu NBAA, ambo kuwa muhasibu mwenye sifa ya ziada utatakiwa kufanya mitihani yao na ukipata CPA (T) Basi inakuwa ni sifa ya ziada kwako kwenye soko la ajira.

Bankers wanasimamiwa na TIOB, ambao hawa hutoa CPB kwa bankers kama watafaulu mitihani yao na kuendelea kuwa mwanachama ili kujiongezea sifa ya ziada

Wagavi wanasimamiwa na PSPTB.

Hizo bodi nilizozitaja hapo zinatoa certification kwa mtu kwanza kufanya mitihani ambayo inahitaji ada, na kama mtu akishindwa basi huwa hawezi kupata cheti husika.

Ziko bodi nyingine ambazo zinahitaji uwe memba tu, kwa kulipa ada ya mwaka, bodi kama ya wahandisi, ERB, au hata hii ya walimu ambayo iliombwa kipindi fulani, najua mtaongeza bodi nyingine ambazo hudai mitihani ili kupata cheti au zile zinazotaka uwe meber tu

Hoja yangu!

Ieleweke kuwa wanafunzi wengi hutegemea mikopo kusoma masomo yao ya elimu ya juu. Bodi ya mikopo humpa mtu mkopo kwa muda ambao yuko chuoni tu! hizo bodi hazihesabiki kama ni sehemu ya chuo, hivyo mtu anayetoka chuoni hutegemea kujisomesha kwenye bodi hizo ili kupata sifa hizo za ziada.

Vitu kama CPA hugharimu si chini ya milioni kwa mitihani yake, CPB halkadhalika, hawa wengine ni zaidi ya laki mbili. Sasa mtu aliyetoka chuoni aliposomeshwa kwa mkopo anatarajia atapata wapi hela ili ajisomeshe kama sio kuongeza gap kati ya wenye nacho na wasio nacho, kwa kuwa wenye nacho wataweza kusoma na kuongeza sifa za ziada huku wasionacho wakisubiri ajira ili watumie mishahara kujipa sifa ya ziada, wakati wao wanasubiri kazi zinasema CPA is an added advantage.

Kitawafanya wasote mtaani huku wanye CPA wakipata mashavu kirahisi

Nadhani hii ni sababu nyingine ya kupunguzana

USHAURI:
Hii inaonyesha degree haitoshi kumfanya mtu aweze kuajiriwa, Je kwa nini mitihani ambayo wanaifanya katika bodi mbalimbali isiongezwe kwenye mtaala wa elimu ya Chuo Kikuu ili mtu akihitimu shahada yake anakuwa tayari yuko na sifa zote, ili kwenye soko la ajira mchuano uwe fair?

Signed!

OEDIPUS
Hapo kwenye ushauri ndo kidogo umeteleza. Kazi ya professional Board yoyote duniani ni kukupa professional skills and competences, vitu ambavyo kamwe huwez kuvipata chuoni ambapo wanakupa academic knowledge and skills. Ukiweza kutofautisha TAALUMA (ACADEMICS) na UTAALAMU(PROFESSIONALISM) nafikiri utaelewa faida za professional Boards.

Labda hoja ingekuwa ni namna gani kila institution ina-thrive to attain its goals na pia namna gani serikali na sekta binafsi inaweka zingatio la kiajira na kimaslahi relative to someone's qualifications.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi ni taaluma za hovyo sana. Nchi yetu professional qualification zimekaa kimfuno wa kuajiriwa tu, huwezi kupata professional qualification kisha ukajiajiri, labda madaktari na wahandisi na wanasheria ila hizi za fedha nbaa wanataka baada ya kufaulu cpa uhuzurie seminar zao miaka kadhaa ndio uruhusiwe kujiajiri.

Ukipata cpa na ukawa huna ajira ni sawa na darasa la 7 tu kitu unaweza ni kuchoma mahindi mtaani maana huwezi kujiajiri kwa taaluma yako. Kama utataka kujiajiri iwe nje ya taaluma yako ila kwa taaluma yako haiwezekani.

Mifumo yetu ya elimu inaridisha nyuma sana maendeleo, unasababisha umasikini na kuongeza ukosefu wa ajira, unakuta mtu msomi, qualified ila huwezi kupractise profession yako hadi miaka kadhaa.

Profession body bado wana mtazamo wa kizamani wa kimitihani. Dunia inabadilika ila huku kweti bado tunashikilia misingi iliyokwishabomoka.
 
Hapo kwenye ushauri ndo kidogo umeteleza. Kazi ya professional Board yoyote duniani ni kukupa professional skills and competences, vitu ambavyo kamwe huwez kuvipata chuoni ambapo wanakupa academic knowledge and skills. Ukiweza kutofautisha TAALUMA (ACADEMICS) na UTAALAMU(PROFESSIONALISM) nafikiri utaelewa faida za professional Boards.

Labda hoja ingekuwa ni namna gani kila institution ina-thrive to attain its goals na pia namna gani serikali na sekta binafsi inaweka zingatio la kiajira na kimaslahi relative to someone's qualifications.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hayo meneno mawili umeamua kuyatofautisha ila ni kitu kimoja,

Ngoja nikupe mfano

Mtu akisoma BA-Linguistics, ukiulizwa jamaa na profession ipi utasema ana profession gani?

Kama hana profession itakuwa ni sahihi, ila kama ana profession je, hiyo profession ameipata kwenye bodi au wapi?

NB: Bodi hutoa mitihani kupima kilekile ambacho umefunzwa shule, na hizo bodi hazina tution centres, tution centres zinajitegemea kimpango wake, Ushaur wangu ulikuja baada ya mimi kuangalia mitaala yao na kuona ni heri iongezwe shuleni ili kumtoa mtu akiwa na hizo profession kabisa
 
Back
Top Bottom