COVID-19 ni ushahidi kuwa Madaktari na Manesi ni kada zinazostahili kulipwa vizuri sana na pengine kuliko kada zingine zote

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Kabla sijaenda mbali katika uandishi wa bandiko hili,naomba niweke wazi kuwa mimi sio daktari wala nesi bali nina fani tofauti kabisa ila nimesukumwa na ukweli ulio wazi juu ya ugumu na hatari iliopo katika kutumikia kada hizi mbili hasa ya udaktari.

Tukirudi kwenye mada,hali ya ugonjwa huu wa corona huko Marekani na Ulaya kwa sasa na hatari inayowakabili watumishi wa sekta ya afya katika mataifa hayo na mengine duniani ni ushahidi tosha kuwa kada hizi mbili ni kada muhimu na nyeti sana katika huu ulimwengu kuliko kada zingine zote.

Japo ni kweli karibu kila kada/kazi ina risk zake,lakini sidhani kama kuna kada ina high risk kama hizi kada mbili na hasa yanapotokea majanga ya maradhi ya mlipuko kama ilivyo corona kwa sasa.

Kwa mfano, wakati hivi sasa watu tunaogopa hata kusogeleana huku tukiwa hatuna hata uhakika kuwa mwenzangu huyu ana virusi,madaktari na manesi na wafanyakazi wengine katika kada hii wao hawana option zaidi ya kulazimika kuwahudumia wagonjwa licha ya hatari kubwa waliyonayo.

Yaani kwa kifupi, it is matter of death or life.

Mbali na pandemic kama hii ya corona,hata wanapohudumia wagonjwa wa magonjwa mengine,kama vile kuwafanyia upasuajj wagonjwa au kina mama wajawazito wenye magonjwa hatari ya kuambukiza kama vile HIV, n.k. bado wanakuwa kwenye risk kubwa tu ya wao kuambukizwa magonjwa haya hivyo hizi kada ni kada zinazofanya kazi katika mazingira ya hatari karibu kila siku katika utumishi wao.

Naelewa katika mafunzo yao wanafundishwa namna zote za kujikinga na maradhi au hatari inayoweza kuwakabili katika utendaji wao wa kazi,ila bado hawa ni binadamu wanaoweza kufanya makosa kama wafanyavyo watu wengine waliko katika fani na kada tofauti ila tofauti hapa ni kuwa wao makosa yao ynaweza kugharimu maisha yao mbali na ya mgonjwa,

Kwa mfano, hivi sasa teyari kuna madaktari kadhaa wameripotiwa kufa kutokana na kuwahudumia wagonjwa wa corona huku ulaya na bila shaka bado wataendelea kufa kama ilivyokuwa kwenye ebola na magonjwa mengine.

Kuna watu wanaweza kusema kada ya ualimu ndio muhimu na inayostahili kulipwa vizuri kuliko hata kada ya udaktari kwasababu bila mwalimu huwezi kupata daktari, lakini wanasahau uhai wa mtu ukipotea, hakuna namna unaweza kuurejesha na hakuna asiegopa kifo hata kwa wanajeshi waliko vitani.

Naelewa kazi ya jeshi ni ngumu na ya hatari lakini ni heri mwanajeshi anaepambana na adui anaeonekana kwa macho kuliko nesi au daktari anaepambana au ku-deal na adui asionekane kwa macho kama huyu COVID-19 na wengine wengi.
.
Hivyo,natoa wito kwa serikali kutazama upya maslahi ya kada hizi kama walivyofanya kwa watumishi wa TRA enzi za utawala wa Mkapa lakini nawataka na hawa madaktari na manesi nao wawe na utu na pia wajali na kuthamini wagonjwa.

Hata kama wanalipwa risk allowance, mishahara ya tofauti ni muhimu sana kwa hizi kada na msisahau shule ya udaktari ni pasua kichwa.

Pichani ni dakatri wa kichina aliejulikana kwa jina la Doctor Lie Wenliang alietoa tahadhari kwa mara ya kwanza juu ya uwepo wa ugonjwa wa korona na ambae alifariki kwa ugonjwa huo nchini China:

1585171718265.png
 
Kuongeza mshahara ndio kutazuia vifo?

Kila kada inaumuhimu wake ni kheri kubalance kila upande na kuleta matokeo sahihi katika jamii.
mbunge anaegonga meza na kukuna kitambi na kupayuka maneno ysiyokuw na tija kw taifa analipw vizuri daktari ambae ikitoke hudum zote nchininzinafungwa kwa sabbu y janga fulani basi hudam yke itakuw ya mwisho kufungwa kwa sababu ya umuhimu wake. walipwe vizuri nami nakazia
 
Sijasoma uzi wako kwa sababu umeshindwa kuweka point ulioikusudia badala yake umezunguka wee.

Ila acha nichangie.

Kila kazi ina umuhimu wake hasa zinapotokea nyakati fulani fulani.

Sasa hivi unaona daktari wanapiga kazi hasa ni kweli kwa sababu kuna tatizo linalohusiana na wao ndo mana unasema hivyo.

Pakitokea vita hapa mkuu utasema askari ndo walipwe zaidi kwa kazi yao ngumu kwa sababu ukiona wanavyosuguana risasi utaogopa mkuu.

Tatizo sio adui kuonekana au kutoonekana mkuu tatizo ni adui ana madhara gani ?

Mtu kwenye vita anakufa hana mguu wala mkono wakati mwana corona anakufa ana ndevu zake na kitambi kinene mkuu.

Corona ni ugonjwa mbaya sana ila hauthibitishi kulipwa madaktari vizuri zaidi ya wengine, hiyo ni katika kazi yao na umuhimu wao unaonekana sasa hivi kwa sababu kuna janga limetokea linawahusu secta yao ya afya.

Likitokea linalohusu sekta ya ulinzi hapa usiwe mchoyo kusema askari walipwe zaidi kwa kazi wafanyazo.usicheze na vita wewe ya mapambano ya silaha.

Sikatai Daktari ni muhimu sana mkuu

Ila suluhisho sio kuongeza mishahara walipwe zaidi,suluhisho ni kuajiri wengi ili huduma iwe pana.kulipa mshahara mkubwa daktari huku wagonjwa ni wengi kuliko madaktari inakuwa haina maana yeyote itabakia kusemwa aaah wanalipwa vizuri lakini kuna impact gani kwa jamii ?

Huu sio wakati unaothibitisha daktari kulipwa zaidi,bali huu ni wakati unaothibitisha kuwa tunahitaji madaktari na wauguzi wengi zaidi Nchi kwa ajili ya huduma bora.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mbunge anaegonga meza na kukuna kitambi na kupayuka maneno ysiyokuw na tija kw taifa analipw vizuri daktari ambae ikitoke hudum zote nchininzinafungwa kwa sabbu y janga fulani basi hudam yke itakuw ya mwisho kufungwa kwa sababu ya umuhimu wake. walipwe vizuri nami nakazia
Mfano Mnyika, Jacob, Lema na Kibajaj......full vitambi!
 
Kama si mwalimu aliyemfundisha basi za huo udaktar au unesi unadhani kungekuwa kuna yeye cha msingi ni kwamba kila fani na kila kada zinategemeana hakuna bora kuliko nyingine. Bila mpharmacia na lab technician huyo daktar anaweza fanya kazi yake?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kama umelenga kada yote kwa ujumla kidunia ila hapa tanzania ni watu wenye majivuno mnoo hawatimizi kama zao kwa ufanisi, majibu mabovu hawana ushirikiano mzuri kwa kweli. huku ukimshikisha pesa mnaenda dawa ila si wazalendo.
Kabla sijaenda mbali katika uandishi wa bandiko hili,naomba niweke wazi kuwa mimi sio daktari wala nesi bali nina fani tofauti kabisa ila nimesukumwa na ukweli ulio wazi juu ya ugumu na hatari iliopo katika kutumikia kada hizi mbili hasa ya udaktari.

Tukirudi kwenye mada,hali ya ugonjwa huu wa corona huko Marekani na Ulaya kwa sasa na hatari inayowakabili watumishi wa sekta ya afya katika mataifa hayo na mengine duniani,ni ushahidi tosha kuwa kada hizi mbili ni kada muhimu na nyeti sana katika huu ulimwengu kuliko kada zingine zote.

Japo ni kweli karibu kila kada/kazi ina risk zake,lakini sidhani kama kuna kada ina high risk kama hizi kada mbili na hasa yanapotokea majanga ya maradhi ya mlipuko kama ilivyo corona kwa sasa.
ne
Kwa mfano, wakati hivi sasa watu tunaogopa hata kusogeleana huku tukiwa hatuna hata uhakika kuwa mwenzangu huyu ana virusi,madaktari na manesi na wafanyakazi wengine katika kada hii wao hawana option zaidi ya kulazimika kuwahudumia wagonjwa licha ya hatari kubwa waliyonayo.

Yaani kwa kifupi, it is matter of death or life.

Mbali na pandemic kama hii ya corona,hata wanapohudumia wagonjwa wa magonjwa mengine,kama vile kuwafanyia upasuajj wagonjwa au kina mama wajawazito wenye magonjwa hatari ya kuambukiza kama vile HIV, n.k. bado wanakuwa kwenye risk kubwa tu ya wao kuambukizwa magonjwa haya hivyo hizi kada ni kada zinazofanya kazi katika mazingira ya hatari karibu kila siku katika utumishi wao.

Naelewa katika mafunzo yao wanafundishwa namna zote za kujikinga na maradhi au hatari inayoweza kuwakabili katika utendaji wao wa kazi,ila bado hawa ni binadamu wanaoweza kufanya makosa kama wafanyavyo watu wengine waliko katika fani na kada tofauti ila tofauti hapa ni kuwa wao makosa yao ynaweza kugharimu maisha yao mbali na ya mgonjwa,

Kwa mfano, hivi sasa teyari kuna madaktari kadhaa wameripotiwa kufa kutokana na kuwahudumia wagonjwa wa corona huku ulaya na bila shaka bado wataendelea kufa kama ilivyokuwa kwenye ebola na magonjwa mengine.

Kuna watu wanaweza kusema kada ya ualimu ndio muhimu na inayostahili kulipwa vizuri kuliko hata kada ya udaktari kwasababu bila mwalimu huwezi kupata daktari, lakini wanasahau uhai wa mtu ukipotea, hakuna namna unaweza kuurejesha na hakuna asiegopa kifo hata kwa wanajeshi waliko vitani.

Naelewa kazi ya jeshi ni ngumu na ya hatari lakini ni heri mwanajeshi anaepambana na adui anaeonekana kwa macho kuliko nesi au daktari anaepambana au ku-deal na adui asionekane kwa macho kama huyu COVID-19 na wengine wengi.
.
Hivyo,natoa wito kwa serikali kutazama upya maslahi ya kada hizi kama walivyofanya kwa watumishi wa TRA enzi za utawala wa Mkapa lakini nawataka na hawa madaktari na manesi nao wawe na utu na pia wajali na kuthamini wagonjwa.

Hata kama wanalipwa risk allowance, mishahara ya tofauti ni muhimu sana kwa hizi kada na msisahau shule ya udaktari ni pasua kichwa.

Pichani ni dakatri wa kichina aliejulikana kwa jina la Doctor Lie Wenliang alietoa tahadhari kwa mara ya kwanza juu ya uwepo wa ugonjwa wa korona na ambae alifariki kwa ugonjwa huo nchini China:


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama si mwalimu aliyemfundisha basi za huo udaktar au unesi unadhani kungekuwa kuna yeye cha msingi ni kwamba kila fani na kila kada zinategemeana hakuna bora kuliko nyingine. Bila mpharmacia na lab technician huyo daktar anaweza fanya kazi yake?


Sent using Jamii Forums mobile app

Unakosea sana mkuu. Kufikiri hivyo...
huwezi mfananisha mwalimu na daktari wote wanaumuhimu wao,lakini kwenye mwaswaala ya kimaslahi daktari anastahili zaidi, mleta uzi ametazamia kwenye sehemu ya risk wanazokutana nazo..mwalimu anakutana na risk gani?,mafua kutokana na vumbi la chaki?, mphamasia anakutana na risk gani ukilinganisha na daktari?,
 
Kila kada inategemea nyenzake. Sisi sote ni mwili mmoja wenye viungo tofauti.

Ili wafanyakazi wa afya waweze kufanya kazi zao vizuri wanahitaji msaada wa miundombinu ya maji, umeme, vifaa, ulinzi, sheria, n.k. ambavyo wanavipata kutoka kada nyingine.

Hali ni hiyohiyo kwa walinzi, walimu, wahandisi, wachuuzi, wanasiasa, wanasheria, wakulima, n.k. Hivyo, sote tunategemeana na hatupaswi kujenga dhana ya kada moja kuwa bora kuliko nyingine.

Kwenye afya moja ya vitu vinavyofundishwa ni kumjengea mtoa huduma sense of humanity. Sasa hii hauwezi kuwa nayo kama utajiona wewe ni bora kuliko mwingine.
 
Kila kada inategemea nyenzake. Sisi sote ni mwili mmoja wenye viungo tofauti.

Ili wafanyakazi wa afya waweze kufanya kazi zao vizuri wanahitaji msaada wa miundombinu ya maji, umeme, vifaa, ulinzi, sheria, n.k. ambavyo wanavipata kutoka kada nyingine.

Hali ni hiyohiyo kwa walinzi, walimu, wahandisi, wachuuzi, wanasiasa, wanasheria, n.k. Hivyo, sote tunategemeana na hatupaswi kujenga dhana ya kada moja kuwa bora kuliko nyingine.

Kwenye afya moja ya vitu vinavyofundishwa ni kumjengea mtoa huduma sense of humanity. Sasa hii hauwezi kuwa nayo kama utajiona wewe ni bora kuliko mwingine.

Nakubaliana na wewe mkuu...
 
Neno hili halipendeki lkn ndio ukweli. Hizo kazi ulizozitaja ni za WITO .

Maana yake , malipo yoyote unayokadiria kwa kazi hizo hayastahili.

Kila mtenda kazi anaumuhimu wake kwa nafasi yake na kwa wakati wake.
 
Back
Top Bottom