COVID-19: Nani mkweli kati ya Serikali yetu na Ubalozi wa Marekani? Je, Tanzania tunawaogopa sana Wamarekani? Kwanini waseme uongo huu waachwe?

Wanabodi,

Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa, huja na makala fikirishi, elimishi na hamasishi uzalendo za "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo hutolewa kwa mfumo wa maswali, makala ya leo ni kuhusu utoaji wa taarifa za Corona, COVID-19: Nani Mkweli Kati ya Serikali Yetu na Ubalozi wa Marekani?!. Jee Tanzania Tunawaogopa Sana Wamarekani?!. Kwanini Wamarekani Waseme Uongo Mkubwa kama Huu halafu Waachwe tuu hivi hivi?!.

Nimesoma with disbelief hii taarifa ya leo ya ubalozi wa Marekani, kwanini ubalozi unatoa taarifa ya uongo kuhusu hali ya COVID-19 nchini kwetu na wanaachwa hivi hivi?!, Jee hawa Wamarekani tunawaogopa?.

Taarifa yenyewe inapatikana hapa kwa wale wa kimombo
Tanzania International Travel Information

Kama rais Magufuli juzi kasema Corona imepungua, jana Waziri Ummy kathibitisha kwa data, leo Marekani inaibuka na kesema hizo taarifa zinazotolewa na viongozi wetu ni taarifa za uongo, na kutusingizia serikali yetu inaficha data, nani mkweli na nani muongo?.

Kwanini Wamarekani waseme uongo waachwe?!. Kama serikali yetu itawanyamazia hawa Wamarekani bila kuwaonya au kuwachukulia hatua yoyote kwa uongo wao, then waelewa wataelewa nani ni muongo kweli na nani ni mkweli, na pia huu utakuwa ni uthibitisho kuwa Mmarekani tunamuogopa, hata utusingizie uongo gani sisi, tunanyamaza tuu!.

Tanzania na rais wetu Magufuli na serikali yetu tumekuwa tukisingiziwa uongo mwingi na sometimes hata kutukanwa na kudhalilishwa na media za nje, lakini tunanyamaza ama kwa kuwapuuza, ama kwasababu Tanzania kwa sasa hatuna watu wenye the capacity kujibu tuhuma kama za The Economist, lakini enzi za Kikwete, aliposingiziwa na balozi wa Marekani kuwa amehongwa suti, Ikulu yetu haikunyamaza, baada ya kupiga kelele humu, Marekani walikanusha.

Lakini sasa leo rais wetu anasema ukweli, kesho Waziri wetu wa Afya anasema kweli, halafu kesho yake, ubalozi uliopo hapa hapa Tanzania unaibuka na taarifa za uongo kuonyesha serikali yetu inaficha ukweli!, ukificha ukweli maana yake unachoripiti ni uongo!. Sasa huu uongo unaosemwa nchini, na ubalozi fulani, usipokanushwa, itaamaanisha ama tunawaogopa Wamarekani, ama tunachoelezwa na serikali yetu ni .. na wanayoyasema Wamarekani ndio ukweli wenyewe, ilaikitokea hawa Wamarekani ni waongo, swali linabaki "Hivi hawa Wamarekani wanatutakia nini?!. Kwanini watutungie uongo na kuueneza dunia nzima?. What is their motive behind and what do they wish to achieve?.

Paskali


Hili wala siyo jambo kubwa kivile; ni suala la Wamarekani kujihami... labda tungewauliza data zao labda wao wana namna nyingine ya kujua idadi ya wagonjwa nchini nje ya taratibu za serikali...
 
Hili wala siyo jambo kubwa kivile; ni suala la Wamarekani kujihami... labda tungewauliza data zao labda wao wana namna nyingine ya kujua idadi ya wagonjwa nchini nje ya taratibu za serikali...
Bora tuendelee kukaa kimya. Maana wakiamua kuweka hizo njia tutashindwa hata kuchutama.

Umemuelewa Paschal kwa huyo mwanahabari aliyekufa na kuzikwa.?

Sie kama Jamhuri tumekubaliana kuwa hakuna corona wala hatuhitaji kumthibitishia mtu.
 
Kwa sababu hupimi, huwezi kujua kiwango cha maambukizi. Kwa sababu unasema wanaosikia dalili wajifukize majumbani kwao, huwezi kujua hata idadi ya wanaojifukiza. Halafu unasema maambukizi yamepungua, unatumia kigezo gani? Ramli za wapiga bao?

Taarifa zetu haziaminiki kwa kiwango chochote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ukitangaziwa wamekufa 200 itakusaidia nini? Utaenda kuwafufua?
Serikali imeshasema ugonjwa upo tuchukue tahadhari full stop
COVID ipo lakini sio ugonjwa special sana hadi tuutukuze. Kuna magonjwa mengi kila dakika yanaua watu wengi tu na maisha yanaendelea.
Kwenye hii COVID namuunga mkono raisi Magufuli
Hapo hata mimi nashangaaga sana upewe idadi ya waliokufa ujawe hofu au? ukawafufue
 
Dunia nzima mambukizi ya covid yanaongezeka, Tanzania tu ndio nchi pekee duniani imefanikiwa kutokomeza covid 19? ??? CCM komeni kutumia gonjwa hili kisiasa na kuhadaa wananchi, brewing a disaster.
 
Wafanyakazi wamenyimwa nyongeza na promotions nyingi na ambazo ni haki zao kiutumishi. Hawawezi kuficha taarifa kwa maslahi ya kisiasa. Kazi ipo kwa upendeleo hakuna anayeweza kuwa mwaminifu bila maslahi
 
Dunia nzima mambukizi ya covid yanaongezeka, Tanzania tu ndio nchi pekee duniani imefanikiwa kutokomeza covid 19? ??? CCM komeni kutumia gonjwa hili kisiasa na kuhadaa wananchi, brewing a disaster.
Tukisema tupime watu kama wanavyofanya wengine ni kweli tutaona maambukizi yanaongezeka ila sijui kufanya hivyo kutatoa mchango gani kutofautisha na hali iliyokuwepo sasa?
 
Tukisema tupime watu kama wanavyofanya wengine ni kweli tutaona maambukizi yanaongezeka ila sijui kufanya hivyo kutatoa mchango gani kutofautisha na hali iliyokuwepo sasa?
Tatizo wananchi wamaacha kuchukua tahadhari aina yeyote baada uongozi wa nchi kuwahadaa ugonjwa umetokomezwa.
 
Tatizo wananchi wamaacha kuchukua tahadhari aina yeyote baada uongozi wa nchi kuwahadaa ugonjwa umetokomezwa.
Unataka kuniambia kwamba wananchi wanaona ndugu zao wanaumwa corona na hadi kufa ila wao wanasikiliza serikali inavyowahadaa kuwa corona imetokomezwa?
 
Mambo kama haya ni kawaida sana katika vita ya kiuchumi, Marekani yupo kimasilahi kupitia siasa zake.
Ujasusi unaeleza watu wabaya hujivika ngozi za kondoo, wema upendo na kusaidia hasa misaada kwa jamii au Taifa japo nyuma ya pazia ni watu hatari sana ( USA).

Ukweli ambao wengi hawaufahamu ni kuwa wamarekani wengi wana maisha magumu sana hasa kwenye public services kama vile hospitali na Mashule huduma zao ni mbovu tena mbovu sana tofauti na private services.(wapo vizuri wamiliki ni hao mabepari wanao tupa misaada).
zaidi wanatumia vyombo vya habari kam BBC. N.k kusambaza propaganda kwa mataifa kama yetu kwao hakuna uhuru wa vyombo vya habari kuripoti matatizo ya kwao (hili lipo wazi).

Kwa akili za kawaida sio kwamba USA wanatupa msaada bali wanataka kunufaika kupitia misaada na mikopo wanayotoa.
Hiki USA wanacho kifanya, mkuu Pascal Mayalla ni ajenda za kisiasa( wanatuchafua kisiasa) hapa sio corona kuna mambo yao
No mercy under capitalism.
Hivi Kuna watu mna akili za ajabu Sana, Vita ya uchumi ndio nini?
Mikopo ya kujenga reli,umeme mnawategemea wao (IMF,WB)
Kulisha dawa waginjwa HIV)AIDS,chanjo za watoto,umeme b jijini,barabara,afya,kujenga madarasa n.k fedha zinatoka kwao kwa mikopo au ufadhili!

Makusanyo na mapato ya ndani yanatosheleza mishahara na gharama nyingine za uendeshaji serikali.
Waache watoe tahadhali kwa raia wao, sisi tunaficha udhaifu na takwimu. Na Vita ya uchumi isiwe kichaka Cha kuficha udhaifu wa serikali
 
Wazungu hawajawahi kuongopa mjomba
Mkuu Erythrocyte, Mhe. Tundu Lisu aliposema "tumepata Rais wa ajabu sana" nilimuona Tundu Lisu hana adabu na anamkosea adabu Rais wetu. Lakini majuzi aliposimama kuwahutubia watz kuwa Covid19 imeisha tz na Bunge likapitisha azimio la kumpongeza kuimaliza Corona hapa Tanzania, wakati huo huo nikiona marafiki wakifa kwa changamoto za kupumua nilishangaa sana. Ni wiki ya tatu sasa napona taratibu kutoka katika mateso makali ya maumivu na changamoto za kupumua. Lakini haikuwa Covid19, kwani kwa mjibu mamlaka Corona virus haipo Tz.
 
Mkuu Erythrocyte, Mhe. Tundu Lisu aliposema "tumepata Rais wa ajabu sana" nilimuona Tundu Lisu hana adabu na anamkosea adabu Rais wetu. Lakini majuzi aliposimama kuwahutubia watz kuwa Covid19 imeisha tz na Bunge likapitisha azimio la kumpongeza kuimaliza Corona hapa Tanzania, wakati huo huo nikiona marafiki wakifa kwa changamoto za kupumua nilishangaa sana. Ni wiki ya tatu sasa napona taratibu kutoka katika mateso makali ya maumivu na changamoto za kupumua. Lakini haikuwa Covid19, kwani kwa mjibu mamlaka Corona virus haipo Tz.
Swala la corona kusema kwamba halipo, ni kujidanganya, lakini kusema pia lipo na linatisha Tanzania Napo pia ni kujidanganya!

Corona ipo Ila haina mamlaka yake katika Taifa la wacha Mungu Tanzania, wenye kuamini tu ndio wanaendelea kujichanganya kila mahali, hawana hofu, wenye hofu inawala vichwa vibaya sana
 
Back
Top Bottom