#COVID19 Covid-19 itatumaliza, Wizara ya Afya imekaa kimya kama vile haipo

Mazoezi hutaki,
Kuvaa barakoa hutaki,
Kunawa mikono hutaki,
Kukaa umbali wa mita moja na nusu kati yako na wenzako hutaki,
Kupiga nyungu hutaki unaona ni ujadi,
Kutumia tiba mbadala ya matangawizi na marimao huwezi
Basi chanja hutaki,
Epuka misongamano hutaki,
Serikali ikuambie lipi jipya ambalo hujasikia?
 
Ugonjwa wa covid 19 au uviko unaenea kwa kasi nchini.wizara ya afya utadhani haipo.hakuna jitihada zozote zinazofanywa na wizara hii kuhamasisha wananchi kujikinga na huu ugonjwa wa corona covid-19.

Tayari leo Simba Sports club ishapoteza mmoja wa viongozi mashuhuri ambaye siku chache alihojiwa na kusema wazi anaugua covid 19. Sasa mtu kama huyu maarufu keshachanyikana na watu wangapi? Kaambukiza wangapi? Jamani tunalichukulia kimzaha suala la huu ugonjwa wa covid 19, itafika siku tutakuwa hatuna budi kukaa nyumbani maana hata makazini hakutakalika.

Kuna tabu au tatizo lipi kwa wizara bila kujali lawama,shutuma n.k kupiga marufuku mikusanyiko yote iwe ya mipira hasa simba na yanga, mikutano ya kiinjili, mihadhara ya kiislamu, matangazo ya kibiashara, upigaji muziki unaokusanya watu, mikutano ya hadhara ya vyama n.kNYIE WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII INABIDI MCHUKUE UAMUZI MGUMU.
Askofu gwajiboy aishaipasuapasua
 
Kosa la serikali ni kusema chanjo ni hiari
Hata isingesema, mwisho wa serikali upo nje ya mwili wangu, kunipa vitu nisivyotaka hakuna wa kunilazimisha kuingiza takataka na kemikali chini ya ngozi yangu, nasema Big No!
Ninyi mnaotaka kufuata kila inachotaka serikali ifuateni ninyi...ndani ya mwili wangu marufuku.
Kumamae zenu mnaotaka kutu enslave
 
Unaonaje ukakaa tu lockdown mwenyewe ndani ya nyumba yako? Au unataka wizara ije ikulazimishe?
Nashangaa!! Tunalazimishana kwenye makanuni ya corona, mimi huwa nashangaa sana mtu anaponiambia vaa barakoa, na nyoko nyoko nyingine za Uviko...kama mtu una hofu na kifo jipige lockdown mwenyewe, tusipangiane, kila mtu ana maamuzi na maisha yake, hata nikitaka kujiua sasa hivi natafuta sumu ya panya nakunywa nakufa, maisha ni yangu niachwe hivi hivi
 
Tuzidi tu kuchukua tahadhari na kuomba Mungu inakuja MU variant ambayo ni ressistant kwa chanjo.
 
Back
Top Bottom