#COVID19 COVID-19 is historical in Tanzania: Why don't USA, UK, EU and others copy from Tanzania how to fight against the Corona Virus?

Nguruvi3, umepatwa na nini? Mbona umekaa kimipashomipasho aisee? Mpaka narudia mara mbilimbili kusoma Username yako kuhakiki.
Hoja zako zaweza kujitegemea pasipo mipasho na bezo za ajabu ajabu, kwa sasa zinaonekana kuwa ni msukumo wa chuki ba kinyongo binafsi.

Jitafakari Upya Mkuu.
Hapana ! hoja zangu zipo wazi

1. Kuzuia upotoshaji kuhusu Corona na Chanjo
Kwanza, Corona ni ugonjwa na ni pandemic. Ni tatizo la dunia na si vita ya aina yoyote ile
Pili, tunahitaji mbinu za sayansi kukabiliana na maradhi. Sala, Maombi na mapambio ni mali binafsi
Tatu, conspiracy theory zinazoenezwa kuwadanganya wananchi tutazipinga kwa nguvu zote
Nne, kuwaeleza wasomaji nini hasa kinaendelea katika ulimwengu katika zama hizi za ugonjwa hatari

2. Kudai haki ya chanjo
Kwamba, kama raia wa dunia tuna haki ya kupewa fursa ya chanjo. Si lazima kwa mtu, kukataa chanjo ni haki ya mtu. Haki hiyo ndiyo inayotoa haki ya watu kudai chanjo. Ni haki na si hisani ya mtu kwa utashi wake tu

Afya ni suala la mtu binafsi na haliamuliwi na mamlaka au idara yoyote au mtu mmoja tu kwa hisia zake
Mbona hatuoni serikali ikisimami watu wakubali au wakatae operesheni ?

Nafahamu kibwagizo cha mbuzi kala mkeka knaudhi hasa kwa washabiki walioaminishwa ujinga nao pasi kufikiri wakauchukua kama ukweli. Ni kero kwa waliopewa kazi ya kupotosha umma !

Ndiyo maana nasema tumechekwa sana duniani ! tunaita ugonjwa wa dunia changamoto ya kupumua kwa kuhofia mtu na si afya zetu. Tunakataa sayansi kumpendeza mtu na si kuponya nafsi zetu.

Msomi katika kiwango cha juu anaposema lishe ni dawa ya corona, hapo tukimsema itakuwa mipasho?
Msomi anapotengeneza dawa leo India wanaumia na hawezi kuipeleka ni mipasho kweli?

Hivi hukuona balozi wa Japan akikabidhi choo cha sekondari kwa mkuu wa Wilaya. Katika hali hii tunawezaje kuhoji chanjo ya virus tusiowaona ikiwa hatuwezi kufukua ardhi na kuweka mashino. Ni mipasho hiyo kweli!

Tumekubali kulishwa majani eti ni dawa kwasababu tu kuna mtu kaamua.
Tukaambiwa kuna dawa zetu ambazo huwezi kupeleka katika nchi yoyote jirani miongoni mwa mataifa 8 yanayotuzunguka. Tukaaminishwa mchachai unaponya.

Tukaambiwa garlic, pepper zinaponya, leo wahindi wanaokula vitu hivyo hali ni tete

Lakini mkuu, siku zote silaumu huwa natoa maangalizo.
Kabla ya ATC kusitisha safari sisi tulisema wiki nyingi kabla
Tukaeleza hatari ya kutotoa elimu kwa umma, wao wakaja siku nyingi baadaye

Ni hayo mkuu, uwe na amani nipo kama nilivyokuwa
 
INDIA HALI NI MBAYA

WHO, Mataifa makubwa na madogo yameelekeza nguvu zao nchini India ambapo kwa hakika hali ni mbaya sana

Kuna upotoshaji eti ' hofu' inaua zaidi ya Corona. Kauli hizi ni za ajabu, ukitazama hali iliyopo India inashangaza kumsikia mtu akisema hakuna haja ya kupeana hofu.

Ukweli unabaki kuwa ukweli kwamba Corona imeshambulia dunia, kuanzia Italy, UK, Brazil, South Africa, Marekani , China na Spain n.k. Kila inapotua na variants, eneo inaathirika kikamilifu. Ndivyo ilivyo kwa India

Kusema kwamba India kuna matatizo si kutia hofu ni ukweli tu. Picha, video n.k zinaueleza ukweli huo

Hofu kubwa iliyotanda duniani ni kusambaa kwa variant ya India na hofu ya pili ni kuwa variant hiyo kufanya mutations na kuja kivingine.

Hofu hii ni kubwa zaidi kwa nchi ambazo mifumo ya Afya ni mibovu, nchi zilizokataa sayansi na nchi zisizotumia chanjo. Yanayotokea India yanaweza kutokea popote pale duniani

Kuna taarifa kwamba variant ya India imeshatua Kenya na Uganda. Kama ni kweli, kuna tatizo linalotunyemelea

Kuna kitu kinaitwa 'latent period' kikaamanisha kipindi cha kuambukizwa ugonjwa hadi dalili kujitokeza

Kutokana na kuingiliana wasafiri wamesambaza virus duniani na kinachoendelea sasa ni latent period

Hili ni tatizo kwa nchi ambazo ;Hazikuchukua hatua za kuchanja Raia wao
Kuna ushahidi chanjo si tu inazuia maambukizi bali pia inapunguza makali ya maambukizi

Pili, nchi ambazo zimechelewa kuchukua hatua kama za kufunga usafiri na nchi zilizoathirika kama India

Kuendelea kuchukua tahadhari, kutoa elimu ya tahadhari na kuwaeleza wananchi ukweli ni hatua za muhimu sana katika kujiandaa endapo itatokea tusivyotarajia. Kuficha ukweli kwa hoja za ''kutotia' watu hofu ni kujipumbaza

Maandalizi ya vifaa kama Oxygen ni muhimu. Hii haimaanishi kuna tatizo au tunatarajia tatizo bali ni hatua za lazima katika kujiandaa (preparedness)

Kwamba, kwanini hatujafikiria chanjo ni kukiuka haki za raia. Haki ya mtu kutotaka chanjo ni sawa sawa na ya mtu anayetaka chanjo. Kamati zipi na zinatafuta nini ikiwa dunia inayotuletea chanjo toka uhuru imeridhia!

Ukweli unabaki kuwa ukweli, tulipotezwa!
 
Hakuna Haki ya kupata kila UNACHOKITAKA, bali kile UNACHOPASWA KUPATA.

Serikali ipo kuratibu na kujua kipi hasa raia wake WANAPASWA KUPATA na kuhakikisha wanakipata.

Wasomi wetu mnatuangusha, mnaishi usomi wenu kama Imani/Dini, mnatumika kutudunisha nanyi mkijikweza katika maarifa batili, na mkijionea fahari hilo.

Tusipotoshe, laa wajukuu wetu watatulilia makaburini kwa tamaa zetu leo.
 
Hakuna Haki ya kupata kila UNACHOKITAKA, bali kile UNACHOPASWA KUPATA.

Serikali ipo kuratibu na kujua kipi hasa raia wake WANAPASWA KUPATA na kuhakikisha wanakipata.

Wasomi wetu mnatuangusha, mnaishi usomi wenu kama Imani/Dini, mnatumika kutudunisha nanyi mkijikweza katika maarifa batili, na mkijionea fahari hilo.

Tusipotoshe, laa wajukuu wetu watatulilia makaburini kwa tamaa zetu leo.
Mkuu,

Hoja ya kwamba Serikali ipo kuratibu na kujua kipi hasa raia wake WANAPASWA KUPATA na kuhakikisha wanakipata haimaanishi pia kufikiri kwa niaba ya raia. Bado raia ana nafasi kubwa kuisimamia serikali kufanya yale yanayopaswa kufanywa kwa ustawi wao.... ndio maana ya kauli mbiu ya government of the people by the people ikimaanisha kwamba serikali inawajibika kwa raia wake na sio the other way around.

Pengine ungelitendea haki andiko lako kwa kufafanua wasomi wanatuangusha kwa namna gani? Maarifa batili ni yepi? Mbona haya tunayoita maarifa batili na usomi tunayatumia ipasavyo kulinda afya zetu kwenye nyanja nyingine kama kunywa maji yaliochemshwa, kulala kwenye chandarua, kutumia kondomu lakini kwenye suala hili ya covid ndio imekuwa kigugumizi? Shida iko wapi?
 
Hakuna Haki ya kupata kila UNACHOKITAKA, bali kile UNACHOPASWA KUPATA.
Kauli hii ingetoka kwa Mkenya, Mmarekani, Mwingereza au Mnigeria ningeshangaa
Ikitoka kwa Mtanzania ni sawa sawa kwasababu hata mshahara wake, Mtanzania ataomba

Kuna fadhila na Haki. Siku zote Raia anapata haki hapati fadhila. Ni mlipa kodi na mwajiri
Kutaka chanjo ni haki kama haki ya kuchemsha majani au kushinda uwanja wa Taifa kwa mapambio

Unapoiongelea haki lazima usimame na 'unachotaka' siyo unachopaswa .

Serikali ipo kuratibu na kujua kipi hasa raia wake WANAPASWA KUPATA na kuhakikisha wanakipata.
Kinachoelezwa si uratibu, ni uchunguzi. Swali, tunachunguza nini zaidi ya mataifa mengine ambayo yamemaliza kuchanja? Sisi tuliojenga mabanda ya kufukiza Hospitalini ndio wa kuchunguza chanjo ?
Sisi tuliokwenda kutafuta maji ya mchachai ndio wa kuchunguza vaccine?
Sisi tulitengeneza mvinyo wetu usio na kazi yoyote ndio wa kuchunguza vaccine inayotumiwa na dunia?
Sisi tunaoamini mapambio kupambana na virus ndio wa kuchunguza vaccine?

Lakini, tunachunguza nini ikiwa tunachanja watoto wetu kila siku na chanjo kutoka huko huko! hivi kama ni kudhuru hapo pa watoto si ndipo pakuanzia kumaliza kizazi!
Tunachunguza nini ikiwa dawa zote tunaagiza nje hata dawa za kusafishia maji ya Ruvu zinatoka huko?
Wasomi wetu mnatuangusha, mnaishi usomi wenu kama Imani/Dini, mnatumika kutudunisha nanyi mkijikweza katika maarifa batili, na mkijionea fahari hilo.
Maarifa ni sayansi si haya tuliosukumiziwa kichwani, kwamba, tunaweza kupambana na Virus kwa mapambio

Huko Maka na Rome tulikochukua maarifa mengine wanatumia sayansi.
Tusipotoshe, laa wajukuu wetu watatulilia makaburini kwa tamaa zetu leo.
Tusipotoshwe kuita ugonjwa changamoto ya kupumua. Tusipotoshwe kuamini Virus wanapandikizwa kwa vita ya uchumi. Tusipotoshwe kuchemsha majani tu kwasababu kuna mtu anataka hivyo.
Ipo siku wajukuu watajiuliza walikuwa na wazee wa aina gani!
 
Mkuu,

Hoja ya kwamba Serikali ipo kuratibu na kujua kipi hasa raia wake WANAPASWA KUPATA na kuhakikisha wanakipata haimaanishi pia kufikiri kwa niaba ya raia. Bado raia ana nafasi kubwa kuisimamia serikali kufanya yale yanayopaswa kufanywa kwa ustawi wao.... ndio maana ya kauli mbiu ya government of the people by the people ikimaanisha kwamba serikali inawajibika kwa raia wake na sio the other way around.
Pengine ungelitendea haki andiko lako kwa kufafanua wasomi wanatuangusha kwa namna gani? Maarifa batili ni yepi? Mbona haya tunayoita maarifa batili na usomi tunayatumia ipasavyo kulinda afya zetu kwenye nyanja nyingine kama kunywa maji yaliochemshwa, kulala kwenye chandarua, kutumia kondomu lakini kwenye suala hili ya covid ndio imekuwa kigugumizi? Shida iko wapi?
Ahsante!

Leo watoto wanachanjwa DPT(Diptheria , Pertussis and Tetanus), halafu kuna Measles, Rubella, Polio etc
Huko hatusikii mbwembwe za uchunguzi, ikija COVID kuna uchunguzi. Kigugumizi cha nini?
Hakuna anayeeleza kwanini leo watoto wachanjwe halafu vaccine ya Corona iwe na tatizo

Vaccine ya Corona ni haki yetu, anayetaka apate, asiyetaka ni haki yake aachwe.
Hili la mtu kufikiri kwa niaba ya Raia ni makosa. Nani amempa kibali cha kufikiri na kuzuia corona lakini hana kibali cha operesheni za moyo na kichwa? Kwanini Corona?
 
Mbona kwenye UKIMWI tunasema wazi kwamba ugonjwa ni hatari na unaua? Hii sio kujaza wananchi hofu?
 
Mbona kwenye UKIMWI tunasema wazi kwamba ugonjwa ni hatari na unaua? Hii sio kujaza wananchi hofu?
Halafu tumepokea ARV za $B 5. Hatukusikia kuhoji

Si uliona walificha data na kuzuia takwimu ili wakisimama wasema hakuna anayefariki!
 
Mkuu mwalimu.

Ni kweli raia wanayo nafasi kubwa ya kusimamia serikali juu yanayopaswa kufanywa juu ya Ustawi wao. Huo ni Wajibu wa kila RAIA, na ni haki yake ya msingi kabisa.
Ninachosemea hapa si kila KIPASWACHO kupata raia basi ndicho WATAKACHO. Raia wanaweza kukataa kile wanachopaswa, lakini halitabadili utendekaji wake(kwa werevu) Raia pia wanaweza KUTAKA wasichopaswa, na halitafanyika.

Serikali ni lazima ipitie MATAKWA ya raia wake kuyachakata vile inavyopaswa, na kisha kufanya Utendaji ambao unaweza kuwa ni kinyume au sawa na hayo matakwa.

Kusema serikali ni lazima iwajibikie kila watakacho raia wake ni Upotoshaji. Haijawahi kuwepo serikali ya namna hiyo, maana isingeishi.

Usomi Batili ni ule unaotaka na kulazimisha watu waamini kuwa, HAKUWEZI kuwa na juzi na maarifa yaliyo nje ya Mfumo huo wa usomi. Hakuna sayansi iliyo nje ya Sayansi hii ya Leo. Walivyo na hila na mipango michafu vichwani mwao, chochote kilicho nje ya sayansi yao, hukipima kwa vigezo vya sayansi zao na kukibatilisha na kukipa laana kabisa. Yaani ni kukataa kuwa hakuna maisha ndani ya maji kwa sababu wewe ukitoswa huwezi kuishi, hutaki kabisa kuambiwa juu ya samaki. Huu ni Ulimbukeni mkubwa sana, Ni Utumwa.

Mkuu, hicho unachokiita mafanikio ni Ubatili. Umejaribu kutafuta mifano dhaifu ambayo sijui ni kwa makusudi au bahati mbaya, umeficha disasters ya hiyo sayansi ya Leo.... Why hukutaja Dawa za Uzazi wa mpango na madhara yake, why hukutaja mionzi hospital, why hukutaja mafanikio ya GMO seeds? Unayaficha kulinda nini?
Kila leo magonjwa yanaongezeka, kila leo ukali wa magonjwa unaongezeka. Inaanza kama UTI, utapewa dawa kuilea mpaka ikomae iwe PID,utaendelea kupewa Dawa kuirutubisha ili ikomae na mwishowe saratani. UNAITAJE HAYO KUWA NI MAFANIKIO? Ni kwa faida ya Nani?

Tuna macho na kutazama, lakini hatuoni. Tumesoma na tunaweza kutamka vema scientific research... Hao ni Wapotoshaji, Wanatumika kutetea Ubatili wakijivunia Wingi wa mikaratasi tupu vichwani. Ni wasomi na Usomi Ubatili.

Inakera sana!
 
Mkuu Nguruvi3.

Unachopaswa ni Unachostahili, kulingana na mazingira na nyakati mahususi.

Matakwa ya MTU kamwe hayawezi kuwa haki, haushi katika upweke. TUNAFUNGAMANA. Uachopaswa kupata, ni kile kitakachoheshimu na kulinda mahusiano sahihi katika Mafungamano yenu. Hicho kinaweza kuwa ni Kinyume na MATAKWA yako.

Hivi ni kwanini dhana ya Haki mnaibebabeba tu kirahisirahisi, na kuzisema kiholelahole tu mbele za watu!? Huwa mnapima athari zake? Luna anayeweza kutamka hadharani kuwa KILA UNACHOKITAKA NI HAKI YAKO, HIVYO CHUKUA AU DAI?

Sijasema serikali inaratibu ujio wa chanjo, nimetamka kuwa wajibu wa serikali ni kuratibu maisha ya raia wake kiujumla, katika hilo kuchunguza, kupima na kutathimini ni sehemu ya majukumu yake.


Mkuu, siombei mabaya, ila ikitokea kuna jamaa yako amepata fracture yoyote, nitafute nikuambie ambako utashuhudia Ukuu wa Sayansi iliyo nje ya Mifumo iliyopo, na kamwe haiwezi kupimwa nayo.

Punguzeni Bezo na Kujitusi.
 
Kila siku nauliza swali, kujiridhisha na nini? Unaletewa chanjo za EPI kila siku. Leo kipi kigeni?
Maprofesa wetu si hawa wanaokunywa mchaichai! Si hawa wa ugunduzi wa Covidol ha ha ha OMG
India wana shida, kwanini hampeleki Mpiji, Covidol na NIMRcafe?

Hivi watalaam wetu si hawa wanaojenga mabanda ya kufukiza.
Tena tukaambiwa Garlic na pepper inakinga dhidi ya Covid, well! India wanakula sana!!!

Mataifa yote duniani yanapiga chanjo isipokuwa Tanzania kwasababu ya ushamba tu !

Tunajengewa vyoo vya shule na ubalozi wa Japan halafu tunahoji chanjo

Chanjo iletwe asiyetaka shauri yake, wapo waliokaidi uwepo wa Corona, well!

Wapambe enzi za kulishwa ujinga na kukumbatia ushamba zimepita!
FYI Watanzania ie Babu zetu waliishi miaka mingi bila hizo dawa unazozipigia chapuo. Fahamu kitu kimoja miti shamba ni tiba bora, hata hizo dawa unazofikiria wazungu wanatengeneza zinatokana na mimea. Sio kila kitu bora kaleta mzungu ni cha kukumbatia. Wahenga walisema ''Elimu ni ufunguo wa maisha.''
 
INDIA HALI NI MBAYA

WHO, Mataifa makubwa na madogo yameelekeza nguvu zao nchini India ambapo kwa hakika hali ni mbaya sana

Kuna upotoshaji eti ' hofu' inaua zaidi ya Corona. Kauli hizi ni za ajabu, ukitazama hali iliyopo India inashangaza kumsikia mtu akisema hakuna haja ya kupeana hofu.

Ukweli unabaki kuwa ukweli kwamba Corona imeshambulia dunia, kuanzia Italy, UK, Brazil, South Africa, Marekani , China na Spain n.k. Kila inapotua na variants, eneo inaathirika kikamilifu. Ndivyo ilivyo kwa India

Kusema kwamba India kuna matatizo si kutia hofu ni ukweli tu. Picha, video n.k zinaueleza ukweli huo

Hofu kubwa iliyotanda duniani ni kusambaa kwa variant ya India na hofu ya pili ni kuwa variant hiyo kufanya mutations na kuja kivingine.

Hofu hii ni kubwa zaidi kwa nchi ambazo mifumo ya Afya ni mibovu, nchi zilizokataa sayansi na nchi zisizotumia chanjo. Yanayotokea India yanaweza kutokea popote pale duniani

Kuna taarifa kwamba variant ya India imeshatua Kenya na Uganda. Kama ni kweli, kuna tatizo linalotunyemelea

Kuna kitu kinaitwa 'latent period' kikaamanisha kipindi cha kuambukizwa ugonjwa hadi dalili kujitokeza

Kutokana na kuingiliana wasafiri wamesambaza virus duniani na kinachoendelea sasa ni latent period

Hili ni tatizo kwa nchi ambazo ;Hazikuchukua hatua za kuchanja Raia wao
Kuna ushahidi chanjo si tu inazuia maambukizi bali pia inapunguza makali ya maambukizi

Pili, nchi ambazo zimechelewa kuchukua hatua kama za kufunga usafiri na nchi zilizoathirika kama India

Kuendelea kuchukua tahadhari, kutoa elimu ya tahadhari na kuwaeleza wananchi ukweli ni hatua za muhimu sana katika kujiandaa endapo itatokea tusivyotarajia. Kuficha ukweli kwa hoja za ''kutotia' watu hofu ni kujipumbaza

Maandalizi ya vifaa kama Oxygen ni muhimu. Hii haimaanishi kuna tatizo au tunatarajia tatizo bali ni hatua za lazima katika kujiandaa (preparedness)

Kwamba, kwanini hatujafikiria chanjo ni kukiuka haki za raia. Haki ya mtu kutotaka chanjo ni sawa sawa na ya mtu anayetaka chanjo. Kamati zipi na zinatafuta nini ikiwa dunia inayotuletea chanjo toka uhuru imeridhia!

Ukweli unabaki kuwa ukweli, tulipotezwa!
India kulikuwa na lock down kama sikosei. Twambie mkuu wao walikosea wapi? BTW India ndio manufacturer wa viwanda vingi vya dawa kwa bei ya chee kutoka USA na Europe.
 
SOMO KUTOKA INDIA

Taarifa ya Wizara ya Afya Tanzania katika mabandiko hapo nyuma imesisitiza 'serikali inaweza kudhiti COVID-9' .

India nchi iliyoathirika sana na wimbi linaloendelea la Corona inakabiliwa na tatizo mawili makubwa
Tatizo la muda mfupi na la dharura ni upatikanaji wa 'Oxygen'
Tatizo la pili ni vaccination kwa mamilioni ya watu ili kudhibiti ugonjwa kama ilivyofanyika nchi za Magharibi

Mfumo wa Healthcare wa India upo juu ukilinganisha na wa kwetu ndiyo maana tunapeleka Wagonjwa wetu.

Mfumo wa usambazaji wa hewa ya Oxygen katika nchi zilizoendelea ni '' Central' kwa maana,kuna mtungi mmoja mkubwa kama ile ya vituo vya mafuta, halafu wodi za wagonjwa zimeunganishwa ''system' na mfumo huo.
Hivyo mgonjwa anapata Oxygen akiwa katika kitanda na ipo switch ndogo ya kuunganisha hewa

Kuna wakati California ilikabiliwa na tatizo la Oxygen kwasababu ya ongezeko la Wagonjwa.
Hata hivyo tatizo hilo lilitatuliwa mara moja kutokana na mifumo imara ya usambazaji

Kwa Tanzania, mfumo wetu ni ule wa kutumia mitungi ya Oxygen.
kwamba mgonjwa mmoja na mtungi mmoja. Kwa Wagonjwa 200 basi utahitaji mitungi 200 ( 200 O2 cylinders)

Ndicho kinatokea India kwasasa na nchi zilizoendelea zinapeleka misaada ya mitungi kwa ndege na Oxygen katika matanki kwa njia nyingine ikiwemo reli na meli

Kuna Hospitali moja ya ''Badra' nchini india iliyokuwa na Wagonjwa 230 katika ICU. Oxygen ilikwisha na ilichukua dakika 80 kupata tena kwa maana ya supply kufika. Katika kipindi hicho watu 12 walipoteza maisha.
Fikiria hivi kwa Saa 1 na Dakika 20 watu 12, je ingekuwa saa 6 au 8 au 10 nini kingetokea!!

Mwaka jana wakati wimbi linavuma Tanzania kulikuwa na ''taarifa'' za ndugu kuhaha kutafuta mitungi ya Oxygen.

Ilifika mahali '' ikasema rushwa' ilitumika . Katika mazingira ya ugonjwa rushwa ni jambo la hatari hasa ikiwa 'against' asiye na uwezo. Hayo yalisemwa na tuyaache kama yalivyo, lakini, tulishuhudia mengi

Ni kwa mantiki hii tunajiuliza ikiwa serikali imejiandaa kwa njia zote.

Kuna tofauti ya kudhibiti ugonjwa inayosema na Serikali na kukabiliana na ugonjwa ''emergency' unapotokea.

Kudhibiti ugonjwa ni long term plan, kukabiliana na ugonjwa ni 'emergency'

Badala ya kuendeleza zogo la kijinga la lishe, mitishamba na madogori ya asili na kienyeji, wizara ya Afya itafakari ikiwa Hospitali zina uwezo wa kutoa Oxygen na ikiwa nchi inaweza kuzalisha Oxygen katika high demand

Tunayasema haya si kwa kutisha watu, wala haina maana wimbi la India laja! la hasha

Kuna kitu kinaiitwa 'preparedness' kwamba unajiandaa kwa dharura hata kama haipo katika njia yako

Wapambe waliosimama kiambazani watasema 'tusitishe watu'', wanasahau mbuzi hakuwatisha ! kala mkeka
Hujaanza kuimba huo wimbo leo, Wacha kuweka porojo, zile maiti za kuzika usiku zimeishia wapi?
 
Hujaanza kuimba huo wimbo leo, Wacha kuweka porojo, zile maiti za kuzika usiku zimeishia wapi?
Unakumbuka lile tamk '' watu wasizike usiku kutoka kwa yule bwana''
Unakumbuka lile tamko la yule mama wa maembe '' si lazima watu wasafirishe'
 
India kulikuwa na lock down kama sikosei. Twambie mkuu wao walikosea wapi? BTW India ndio manufacturer wa viwanda vingi vya dawa kwa bei ya chee kutoka USA na Europe.
India waliweka lockdown wakaondoa kwasababu ya watu kukataa. Wimbi likapita salama kama ilivyokuwa Tanzania

Wimbi la pili likaanza Tanzania, ndio hadi tukapa 'tangazo la kutozika usiku' . India walikuwa salama

Majuzi watu 25,000 wakajaa Ganjes river huku zaidi ya 50K wakihudhuria mikutano ya Narendra Mod
Wakaacha kila tahadhari wakifurika kila mahali, well kianchoendelea ujaua ni nini

By the way 'wameanza kuvaa masks' teh teh teh. Leo umeona?
 
Weka ushahidi mkuu, Wacha mambo ya kuokoteza story!
Kwani tumenunua ARV lini na kwa kiasi gani? Teh teh

By the way kuna 'Bilioni 27'' za EU za Covid. Sikusema mimi ni EU Parliament.

Ha ha ha , tukienda huko itabidi tuite wasihusika, teh teh OMG
 
Back
Top Bottom