#COVID19 COVID-19 is historical in Tanzania: Why don't USA, UK, EU and others copy from Tanzania how to fight against the Corona Virus?

AHSANTE SANA TLS

Chama cha kitaaluma cha mawakili na wanasheria nchini kimepita na kinapita katika nyakati mgumu

Ugumu unatokana na kuingiliwa na hata kutungiwa sheria zinazolenga kukidhoofisha

Ukifuatia kwa umakini TLS ina misimamo thabiti na kusimamia kwa dhati taaluma ya sheria, wanasheria na masilahi mapana ya umma (public interest)

Wiki chache zilizopita baraza la chama hicho lilisimama na kueleza tatizo la Corona na jinsi lilivyoathiri wanachama wake lakini pia kwa ukubwa wake katika nchi yetu na linavyoathiri jamii.

Msimamo huo hakuwa rahisi lakini ulikuwa wa lazima kwa masilahi ya chama na umma.

Ipo video nyingine kutoka kwa kiongozi wa TLS Bw.
Nshala likieleza mambo kadhaa kwa ufasaha wake bila kupendelea au kuuma maneno , bila kujikomba au kuudhi.

Katika salam zake kwa Rais Mama Samia Suluhu , TLS imeanza kwa kueleza matarajio yake kwa kiongozi huyo

TLS imeongelea umuhimu wa utawala wa sheria na kikaangazi agenda ya katiba mpya kwa nchi.

Baraza likazungumzia umuhimu wa kukumbatia sayansi katika nyakati hizi za Corona

TLS haikucha kuzungumzia vymbo vya sheria , mahakama na hata mawakili kusimamia misingi ya sheria
Orodha ya waliyonena inaendelea kwa mtazamo wa masuala ya jamii , nchi na dunia kwa ujumla wake

Kikubwa zaidi ni TLS kuutendea uma haki kwa kueleza utaratibu unaopaswa kufuatwa sasa hivi.

Wanasheria hao wamebaini uwepo wa upotoshaji wa makundi ya jamii hasa kuhusiana na katiba na kuwachanganya wananchi.

TLS ikaeleza kwa kina nini kifanyike katika wakati huu wa kihistoria kwani nchi haijawahi kupitia haya.

Ilichokifanya TLS ni kutimiza wajibu wake kwa umma na kuhakikisha unatetea masilahi mapana ya umma.

Pengine TLS kama walivyo wananchi wengine wenye uelewa walijiuliza kuhusu kikao cha baraza la mawaziri. TLS imefafanua kiapo hakivushwi bali kuhamishwa kwa kiapo kipya

Ukipata fursa ya kutazama au kusoma taarifa ya TLS kuna kitu utabaini.

Baraza hilo ni moja ya mabaraza muhimu na yanayojitambua nchini.
Pengine ule msemo wa 'mwembe wenye matunda hupopolewa mawe' unadhihirika hapa.

Kuna cha kujifunza kwa vyama vya kitaaluma nchini.
Vingi vimebaki kuwa wapiga debe bila kujua hata miriindimo ya debe hilo.

Katika nyakati ngumu za dunia kama hizi za Corona tulitegemea vyama husika kushika hatamu, kinyume chake baadhi vimegeuka kuwa matawi ya chama.

Kutenda kosa si kosa bali kurudia kosa ni kosa.

Vyama vya kitaaluma kama kile cha Madaktari( MAT), Wauguzi, Wahindisi n.k vina nafasi ya kujirekebisha na kurejea katika misingi na malengo ya uwepo wake.

Vyama hivyo vinapaswa kuiangalia TLS kama mfano na kioo.

Inasikitisha pale TLS inapokabiliana kwa ujasiri na mambo yaliyopaswa kusemwa na vyama vingine.

TLS inaweza kuwa si timilifu lakini kuna kitu cha kusema, ni chama kinachojielewa

Ahsante kwa kuitendea taaluma yenu haki na kuisadia jamii.

Tusemezane
 
Inasikitisha pale TLS inapokabiliana kwa ujasiri na mambo yaliyopaswa kusemwa na vyama vingine.

TLS inaweza kuwa si timilifu lakini kuna kitu cha kusema, ni chama kinachojielewa

Kinachoendelea sasa hivi nimechoka kushangaa na kusitikika tena.

Tulipofikia sasa hivi kifikra na kimtazamo ni kama vile tunaishi katika reality/dunia yetu wenyewe huku tunajiaminisha kwamba 2 +2=3 na sio 4!
 
Kinachoendelea sasa hivi nimechoka kushangaa na kusitikika tena.

Tulipofikia sasa hivi kifikra na kimtazamo ni kama vile tunaishi katika reality/dunia yetu wenyewe huku tunajiaminisha kwamba 2 +2=3 na sio 4!
Mwalimu , lengo la uwepo wetu ni kujaribu kusiadia jamii yetu ambayo sasa imekuwa kicheko cha dunia

Tumewauliza wenzetu hapa wanaoneza propaganda, changamoto ya kupumua ni ugonjwa gani kwa kiingereza?
Hawana jibu wanachosema ni kuwa magonjwa ya kupumua ni mengi. Hii ndio 2+2= 5

Tumewauliza kwanini Tanzania ndio Taifa pekee duniani lisilotaka chanjo?
Jibu ni kwamba chanjo zina madhara na ni lazima zichunguzwe. Tukawauliza mbona za Measles, Tetenus, DPT,, Polio n.k. tunazonunua huko kwa wazungu zinatumika kila siku? Hakuna jibu , na hapa ni 2+2=3

Wakasema tuna mbadala wa nyungu. Tumewauliza mbona kila nyumba na mtaa, kata, wilaya na mkoa una nyungu zake? Wakasema watu wa google kutoka India . 2+2= 6

Hawa ni wapiga debe ambao si rahisi kuwadharau kwasababu wanajenga hoja zinazofanana na ukweli na ni rahisi sana kuwachanganya watu.

Kituko kikubwa ni kile cha ujenzi wa mbanda ya kujifukiza katika kitovu cha tiba nchini MNH na Mloganzila

Halafu kuna togwa na Mtindi umetengenezwa na watu wameanishwa kwa dhati kabisa ni matibabu ya Corona
Anayeeneza propaganda hizo ni msomi mbobevu.

Kwasasa kuna tatizo jingine la watu kutojua maana na tofauti za norms, tradition , Culture na Law
Tutalifafanua hili

Na bado watu hawakubali ukweli hata pale unapojidhihiri. Kwanini watu hawajali kuvaa mask na social distancing? Yaani hili nalo ni gumu . Hapa ndipo 1 + 1 = 11 .
 
Wanaohoji kwamba chanjo hazijafanyiwa tafiti za kutosha hivyo tuzikatae wako tayari kujifukiza na kunywa michanyato ya tangawizi ambayo hakuna tafiti hata moja imefanywa kuhusu ubora wake!
 
Mwalimu , lengo la uwepo wetu ni kujaribu kusiadia jamii yetu ambayo sasa imekuwa kicheko cha dunia

Tumewauliza wenzetu hapa wanaoneza propaganda, changamoto ya kupumua ni ugonjwa gani kwa kiingereza?
Hawana jibu wanachosema ni kuwa magonjwa ya kupumua ni mengi. Hii ndio 2+2= 5

Tumewauliza kwanini Tanzania ndio Taifa pekee duniani lisilotaka chanjo?
Jibu ni kwamba chanjo zina madhara na ni lazima zichunguzwe. Tukawauliza mbona za Measles, Tetenus, DPT,, Polio n.k. tunazonunua huko kwa wazungu zinatumika kila siku? Hakuna jibu , na hapa ni 2+2=3

Wakasema tuna mbadala wa nyungu. Tumewauliza mbona kila nyumba na mtaa, kata, wilaya na mkoa una nyungu zake? Wakasema watu wa google kutoka India . 2+2= 6

Hawa ni wapiga debe ambao si rahisi kuwadharau kwasababu wanajenga hoja zinazofanana na ukweli na ni rahisi sana kuwachanganya watu.

Kituko kikubwa ni kile cha ujenzi wa mbanda ya kujifukiza katika kitovu cha tiba nchini MNH na Mloganzila

Halafu kuna togwa na Mtindi umetengenezwa na watu wameanishwa kwa dhati kabisa ni matibabu ya Corona
Anayeeneza propaganda hizo ni msomi mbobevu.

Kwasasa kuna tatizo jingine la watu kutojua maana na tofauti za norms, tradition , Culture na Law
Tutalifafanua hili

Na bado watu hawakubali ukweli hata pale unapojidhihiri. Kwanini watu hawajali kuvaa mask na social distancing? Yaani hili nalo ni gumu . Hapa ndipo 1 + 1 = 11 .
Mkuu ndio maana nimesema tumeamua kutembea katika dunia na reality yetu wenyewe.

Tunahoji barakoa feki toka kwa mabeberu lakini wakati huo huo tunapokea condoms toka kwa mabeberu hao hao.

Tunahoji chanjo ambazo hazijafanyiwa utafiti lakini wakati huo huo tunajifukiza nyungu na kubugia kila aina ya dawa za kienyeji ambazo hakuna anayeweza kukuonesha tafiti zilizofanywa kuhusu ubora wake. Kwani tunashindwa nini kuagiza na kuzifanyia utafiti kwanza kabla ya kuruhusu matumizi?

Tunasema ni ugonjwa wa changamoto za kupumua au pneumonia huku tunashindwa kuelezea kwa kina jinsi unavyoambukiza, hatari zake na jinsi ya kujikinga badala yake tunatoa majibu mepesi kwa maswali magumu.

Upimaji tumeugeugeuza kuwa dili ya kupiga $100 kwa kila msafiri huku mwananchi akiachwa ajihangaikie mwenyewe... kinachotusaidia ni kwamba hatutoi data lakini reality ni kwamba covid inatutikisa sana tu!
 
Mkuu ndio maana nimesema tumeamua kutembea katika dunia na reality yetu wenyewe.
Jambo hili limetudhalilisha na kuwa hadithi ya dunia. Fikiria kuwa Somalia nchi iliyotawanyika na ambayo kusimama katika foleni iwe ya sukari au unga ni 'risk' kwasababu bomu linaweza kulipuka, leo wamekubaliana na sayansi na wamechanja watu wao. Somalia!

Sisi tunasema hazijafanyiwa utafiti. Nimewauliza proponents wa hizi theory za nyungu na anti-vaxxers akina Mlenge na Wacha1, vaccines zinazotumika nchi kwasasa zilifanyiwa utafiti na nani na lini?
Nikawauliza kwanini wasiombe samples tutumie mamlaka zetu za madawa na viwango kufanya uchunguzi?
Hawana jibu!
Tunahoji barakoa feki toka kwa mabeberu lakini wakati huo huo tunapokea condoms toka kwa mabeberu hao hao.
Tena leo watoto wamechanjwa na chanjo kutoka Ubeberuni. Hakuna anayehoji wanahoji ya Corona
Tunapokea ARV kutoka ubeberuni, hakuna anayehoji tunahoji chanjo
Tunatumia Iphone kutoka ubeberuni, hawahoji hilo. n.k.
Tunahoji chanjo ambazo hazijafanyiwa utafiti lakini wakati huo huo tunajifukiza nyungu na kubugia kila aina ya dawa za kienyeji ambazo hakuna anayeweza kukuonesha tafiti zilizofanywa kuhusu ubora wake. Kwani tunashindwa nini kuagiza na kuzifanyia utafiti kwanza kabla ya kuruhusu matumizi?
Na nyungu zinatofautiana kutoka nyumba hadi nyingine, mtaa hadi mwingine, kata mkoa na Wilaya
Kumbe basi hatuna formula ya nyungu, lakini tupo mstari wa mbele kuhoji ubora wa chanjo wa kisayansi!!

Hakuna anayetuambia Togwa na Mtindi zimefanyiwa utafiti lini na zimekuwa published wapi duniani.
Tunahoji chanjo imepatikana haraka, hatuhoji hizo za Togwa na Mtindi Lishe zilichukua muda gani
Tunasema ni ugonjwa wa changamoto za kupumua au pneumonia huku tunashindwa kuelezea kwa kina jinsi unavyoambukiza, hatari zake na jinsi ya kujikinga badala yake tunatoa majibu mepesi kwa maswali magumu.
Tumeuliza changamoto ya kupumua ni ugonjwa gani? Hakuna kitu kama hicho na kila ugonjwa umeaanishwa kitaalamu. Changamoto ya kupumua inaletwa na nini, inasambaa vipi na inatibiwaje, hakuna anayeeleza
Yaani tunafukia vichwa mchangani tukijidanganya adui hatuoni. Sisi ni Mbuni wa ajabu sana duniani.
Upimaji tumeugeugeuza kuwa dili ya kupiga $100 kwa kila msafiri
Halafu mashine ya kupimia imetoka ubeberuni. Kulikuwa na jitihada za kudhalilisha mashine hizo kwa mafenesi na oil. Kisayansi mashine za kufanya analysis zina 'spec na zinakuwa calibrated'
Kinyume na specifications unapata kitu kinaitwa false positive au false negative n.k.
Sasa kama mashine hizo hazifai, tuonyeshwe zilizotengenezwa nchini kama SIDO n.k.
huku mwananchi akiachwa ajihangaikie mwenyewe... kinachotusaidia ni kwamba hatutoi data lakini reality ni kwamba covid inatutikisa sana tu!
Hapa ndipo nilimweleza Mlenge kuna kukosa moral compass na ku embrace moral decay
Mwananchi wa kawaida anaambiwa nyungu, kumbe kuna mahali wana ventilators na Oxygen cylinders

Kuna mabanda ya kufukiza MNH na Mloganzila halafu kuna taasisi wanazotibiwa watu wengine.

Kuficha takwimu kulilenga kupunguza hadhithi za madhara. Mfano, TEC walitoa takwimu za watu wao.
TLS nao, hilo likaonekana mwiba . Sababu kubwa ni kuficha ukubwa wa tatizo lakini haitusaidii

Bila takwimu huwezi kusema chochote, lakini pia unafungua milango ya kusema chochote.
Kwa mfano mtu akisema watu 500K wamekufa utakataa vipi? Yeye atakuuliza takwimu zako za kupinga zake zipo wapi. Huu ni mkakati wa ajabu sana in the end watu wanajua kutokana na maumivu wanayokabiliana nayo
 
WAZIRI WA 'NYUNGU' AVAA BARAKOA

Jana Waziri wa zamani aliyehusika na uhamasishaji wa nyungu akiita kwa majina nyungu season 2 au 3 alionekana akiwa amevaa barakoa nyeusi. Hii ilikuwa katika kujikinga na Corona kutokana na mikusanyiko ya watu.

Kitendo hicho ni chema kinachoonyesha kujali. Kuvaa barakoa kuna maana kuu mbili
1. Kujikinga na maambukizi kama yapo kutoka kwa watu wengine
2. Kuwakinga wengine ikiwa una maambukizi yasiyodhahiri ' asymptomatic'

Kilichoshangaza kidogo katika hili ni kuona waziri yule yule aliyehubiri nyungu kwa nguvu sana leo amevaa barakoa bila kuwaambia wapika nyungu kuhusu 'u-turn' kutoka nyungu season hadi barakoa. Kulikoni?

Tumeeleza katika uzi huu mambo mawili, kwanza, kile kilichoitwa 'moral compass' ambapo ni uwezo wa kuamua klilichosahihi au la katika mazingira fulani na pili ' mora decay ' ambayo ni ukosefu wa maadili ya kiroho

Kama Mh Waziri alijua kwamba barakoa ni muhimu alipaswa kuwaambia watu hivyo.
Kinachoonekana ni waziri kujua kilichosahihi na kisicho lakini hakuwa mkweli kuchelea mkate wake

Ikifika hapo ndipo ukosefu wa maadili ya kiroho unapokuja '' moral decay'' kwamba pengine kwa maelezo yake ya kupotosha akijua anafanya hivyo kuna watu wamemfuata na hakuna anayejua nini kiliwatokea

Hapo napo tunahamia kwenye suala jingine, la kutojali ubinadamu ' disregard for humanity''
Kwamba ifanyike tu naitapita kama ilivyopita wimbi la kwanza.

Kauli hii ya Mlenge tuliilani sana kwa kusema maisha ya binadamu ni asilimia 100 bila kujali amefariki mtu au watu. Uhai wa mtu mmoja ni 100%

Tulieleza hapo nyuma kwamba kama kuna chanjo na ipatikane na watu waamue kutumia au kutotumia.

Kitendo cha kuamua tu hakuna chanjo ni kuwanyima wanaotaka haki wakati huo huo na watu hao hao wakipanga haki za nyungu, kusali na maombi kwa wengine si cha kiungwana .

Ugonjwa wa Covid-19 upo na watu wanaugua na kupoteza maisha. Nchi za dunia zinafuata sayansi na Tanzania si kisiwa. Masuala ya kiimani ni ya watu binafasi. Matumizi ya vitu au tiba zisizothibitishwa ni moral decay.

Kuchanganya siasa na sayansi kuna tatizo kubwa la kutojali maisha ya watu '' disregard for humanity''

Hili la waziri ni funzo ! lakini pia tujiulize tunahitaji muda gani wa kujifunza zaidi?
Tunahitaji ushahidi upi ili tuamini gonjwa lipo na linaua?

Kuna tatizo gani hatuvai barakoa au social distancing ili kujikinga na kuepusha madhara?
 
Let us point out clearly for those just tuning in!

1. About Masks

Myth:
Wearing mask is the only way to protect one from Coronavirus. Forcing everyone to wear a mask, it is a highlight of a caring national administration.
Reality: In science, there are debates as to the effectiveness of masks. See



2. About Lockdown

Myth:
Locking down healthy populations is the only way to protect them from COVID-19. A caring administration locks down its population.
Reality: Lockdowns may be more harmful. See



3. About Social Distancing

Myth:
Social Distancing is the only way to protect yourself and others from COVID infection in social situations.
Reality: Social Distancing may not be as effective as it is touted to be. See



4. About COVID-19 Vaccines
Pana hii video ya kichochezi imekuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii Tanzania hivi karibuni...


View attachment Uchochizi.mp4
SOURCE: a viral social-media video
 
Mlenge umerejea mkuu na kwa kasi ya ajabu maana sioni kama umeelewa

Ni hivi utatafuta video za kila aina lakini Virus ina prove watu wrong in so many ways.

Kuna waliokejeli kama Mh mmoja aliyesema '' Covid-19' tuheshimiane kama maradhi mengine
Naona wiki hii Waheshimiwa wakiwemo watangaza na wapiga debe wa nyungu wanavaa Masks !

Kuna mtu kanitumia kitaarifa katika kisimu changu cha Nokia na ki-link kutoka gazeti moja la huko ulaya sijui kama ni kweli au la . Kigazeti kinaitwa Bloomberg wakisema Wasafiri wa Tanzania wanaongoza kwa 'variants' za Corona , na hii ni utafiti wa kisayansi. Hebu jaribu ku google utuletee hapa maana kisimu cha Nokia sina uhakika nacho

Kwasasa vuta subira baada ya siku 14 kuanzia tarehe za 20 kuendelea kutakuwa na mengi, nani anajua ? Ni mwenyezi mungu aliyetupa akili lakini mark my words.
 
Mlenge umerejea mkuu na kwa kasi ya ajabu maana sioni kama umeelewa

Ni hivi utatafuta video za kila aina lakini Virus ina prove watu wrong in so many ways.

Kuna waliokejeli kama Mh mmoja aliyesema '' Covid-19' tuheshimiane kama maradhi mengine
Naona wiki hii Waheshimiwa wakiwemo watangaza na wapiga debe wa nyungu wanavaa Masks !

Kuna mtu kanitumia kitaarifa katika kisimu changu cha Nokia na ki-link kutoka gazeti moja la huko ulaya sijui kama ni kweli au la . Kigazeti kinaitwa Bloomberg wakisema Wasafiri wa Tanzania wanaongoza kwa 'variants' za Corona , na hii ni utafiti wa kisayansi. Hebu jaribu ku google utuletee hapa maana kisimu cha Nokia sina uhakika nacho

Kwasasa vuta subira baada ya siku 14 kuanzia tarehe za 20 kuendelea kutakuwa na mengi, nani anajua ? Ni mwenyezi mungu aliyetupa akili lakini mark my words.
Nguruvi3 ,

Nipo JF tu mbona, nimejaa tele ka pishi la mchele!

Looks like kama kipo kitu mnafurahia! Mtu yeyote apambanaye na Kovid kwa mbinu tofauti nanyi, mnamuandika kwenye bad books zenu!

Hao uliowasikia kwenye Nomkia ya kitochi, muvu yao was not unexpected, na kama sikosei tuliipredict katika uzi huuhuu.

Wanatikisa kibiriti cha timu mpya waone kama na wao watamarch in lockstep with the Global you-know-who. Dont'cha know?
 
Nipo JF tu mbona, nimejaa tele ka pishi la mchele!
Umetoweka mkuu, lakini inaeleweka ulipigwa na electric shock hasa ukizingatia maneno ya yule bwana '' Covid-19 ' ikubali kuishi na sisi kama magonjwa mengine au iondoke. Well, virus hana akili , hasikii wala haoni anatenda tu.
Matokeo yake yapo wazi, haichagui wajihi wala wasifu .Ni virus haihitaji mjadala wa kukubalika au kukataliwa.
Looks like kama kipo kitu mnafurahia! Mtu yeyote apambanaye na Kovid kwa mbinu tofauti nanyi, mnamuandika kwenye bad books zenu!
Dunia na wanasayansi hawapambani solo na virus anayezaliana kwa mabilion kwa dakika.

Dunia ina concerted effort kukabiliana na virus na si suala la miujiza au kubahatisha.

Mungu amewapa wanadamu akili, wenzetu wanazitumia kutafuta dawa na chanjo si kugeuka matutusa

Kuna bahati nasibu za pesa na kamari, hakuna bahati nasibu ya maisha ya watu! hakuna ! huo ni upuuzi
Tanzania ni sehemu ya dunia lazima tushirikiane na dunia na kwamba kama ni Mungu ni wa wote

Hivi kuna nani Mkatoliki zaidi ya Papa anayevaa masks na social distancing?
Kuna utakatifu zaidi ya Makka ambako sasa huendi kuhiji bila chanjo?

Tanzania lazima tuwe part of the solution na siyo problem! kwa mwendo tulio nao wa kuchemsha majani ambako kume prove failure hata kwa wapiga debe, hatuna budi kujirudi na kurejea katika international platform na kuwa players katika concerted effort. Tusigeuke misukule wala tusikubali kufanywa misukule kwa gharama za maisha ya watu wetu. Tumepoteza watu wengi na tunaendelea kupoteza!
Hao uliowasikia kwenye Nomkia ya kitochi, muvu yao was not unexpected, na kama sikosei tuliipredict katika uzi huuhuu.

Wanatikisa kibiriti cha timu mpya waone kama na wao watamarch in lockstep with the Global you-know-who. Dont'cha know?
Well, ni wale wale wanaotengeneza mashine za kupimia Corona ambapo Tanzania inatoza Dola 100.
Kwamba hauamini utafiti wao lakini tunaamini mashine zao! ha ha ha
Ni wale wale wanaotengeneza Polio, Mumps, Rubella, Measles , Tetanus, Diptheria , hepatitis Vaccines

Tanzania hatujatengeneza chanjo yoyote ile isipokuwa zile Togwa na Mitindi ambayo wao hawanywi wanakimbizwa kwa matibabu mengine, wakipona wanataka sisi tunywe kitu kisichothibitisha kisayansi wala hakitumiki na hata ka nchi kamoja ka Africa.

Tumejaribu kunywa Togwa la Madagascar hakuna anayejua matokeo yake.Huko Malagasi watu wamekufa sana kwa upuuzi nasi tukaona ni vema kwenda kuazima ujinga kwa muda.

Watu wetu wanakufa kwasababu hatutaki chanjo kwa chuki binafsi tu!

Tunawanyima watu access ya chanjo kwasababu zisizo na kichwa wala miguu.

Dunia yote ikiwemo majirani wapo na dunia sisi '' Tumejaribu kuonja sumu kwa kulamba'' imekula kwetu big time! sasa ni wakati tutie akili na kusimama kidete kudai chanjo

Asiyetaka chanjo ruksa lakini tusimnyime fursa anayetaka.
Tuna vita moja tu ya Corona, hatuna vita nyingine na wala tusitafute sababu! tumechekwa sana sasa basi
 
Dunia yote ikiwemo majirani wapo na dunia sisi '' Tumejaribu kuonja sumu kwa kulamba'' imekula kwetu big time! sasa ni wakati tutie akili na kusimama kidete kudai chanjo.

Tuna vita moja tu ya Corona, hatuna vita nyingine na wala tusitafute sababu! tumechekwa sana sasa basi
Mkuu Nguruvi3, asante sana kwa juhudi zako katika kuelimisha hii jamii ya watu wasio na uelewa wa kutosha na kwa kweli kiwango cha juu cha uvumilivu kinahitajika ambacho sisi wengine, kwa bahati mbaya, hatuna...hongera sana tu!
 
Let us point out clearly for those just tuning in!

1. About Masks

Myth:
Wearing mask is the only way to protect one from Coronavirus. Forcing everyone to wear a mask, it is a highlight of a caring national administration.
Reality: In science, there are debates as to the effectiveness of masks. See



2. About Lockdown

Myth:
Locking down healthy populations is the only way to protect them from COVID-19. A caring administration locks down its population.
Reality: Lockdowns may be more harmful. See



3. About Social Distancing

Myth:
Social Distancing is the only way to protect yourself and others from COVID infection in social situations.
Reality: Social Distancing may not be as effective as it is touted to be. See



4. About COVID-19 Vaccines
Pana hii video ya kichochezi imekuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii Tanzania hivi karibuni...


View attachment 1735140
SOURCE: a viral social-media video
Hizi ni cheap excuses kwamba njia zilizoshauriwa na wataalamu wa afya (mask & social distance) kwamba hazifai. Hii imeshakuwa proven over and over again kwamba it works na wote walioleta ubishi imewagharimu maisha ya watu wengi sana.

Hatuna moral authority yoyote ya kudai kwamba tumefanya vizuri kwenye mapambano dhidi ya covid wakati hatukusanyi data!
 
Hizi ni cheap excuses kwamba njia zilizoshauriwa na wataalamu wa afya (mask & social distance) kwamba hazifai. Hii imeshakuwa proven over and over again kwamba it works na wote walioleta ubishi imewagharimu maisha ya watu wengi sana.

Hatuna moral authority yoyote ya kudai kwamba tumefanya vizuri kwenye mapambano dhidi ya covid wakati hatukusanyi data!
Unamaanisha wanaovaa maski na kufanya sosho distensi hawafi kwa korona?
 
Hizi ni cheap excuses kwamba njia zilizoshauriwa na wataalamu wa afya (mask & social distance) kwamba hazifai. Hii imeshakuwa proven over and over again kwamba it works na wote walioleta ubishi imewagharimu maisha ya watu wengi sana.

Hatuna moral authority yoyote ya kudai kwamba tumefanya vizuri kwenye mapambano dhidi ya covid wakati hatukusanyi data!

Uingereza wamezuiwa kutoka nchini mwao kwenda nje ya nchi, labda kwa sababu chache zilizoorodheshwa, vinginevyo faini...

Unataka TZ nasi tufanye hivyo. Right?
 
Mkuu Nguruvi3, asante sana kwa juhudi zako katika kuelimisha hii jamii ya watu wasio na uelewa wa kutosha na kwa kweli kiwango cha juu cha uvumilivu kinahitajika ambacho sisi wengine, kwa bahati mbaya, hatuna...hongera sana tu!
Mkubwa , tunajaribu japo kwa mawazo. Tunapoteza watu kwasababu zisizo na kichwa wala miguu.

Tumebadilika ! si Tanzania ya Mlima Kilimanjaro na Serengeti bali Tanzania ya ''Corona deniers''
Tumekuwa cheko na burudani ya dunia

Miaka ya 1978? Mwalimu Nyerere alihutubia Taifa kuhusu Ugonjwa wa Cholera( Kipindupindu). Ugonjwa huu haukuwepo Tanzania bali uliletwa kutoka India.

Mwl alianzisha kampeni za Usafi na kuieleza dunia tuna tatizo, tusaidiwe! Misaada ikamiminika kutoka kila kona.Mwl aliita Cholera hakuwahi kusema ''changamoto ya kinyesi''

Mwaka jana juzi dunia ikasema kuna Corona na inaua. USA ya Trump wakapuuzi kama alivyofanya Bosenero wa Brazil na wengine wamelipa gharama kubwa.
Juzi Brazil watu 4,000 wamefariki kwa siku moja.Kuna takwimu

Sisi haturejea historia ya Mwalimu Nyerere kuuambia ulimwengu tupo pamoja.
Tumeamua kupuyanga kivyetu bila kuwa na clear direction tunakwenda wapi.

Tumezuia kusema Corona ili tusijali Masks , social distancing au vaccine.
Tukafukia vichwa mchangani kama mbuni, kila tukisimama hatuoni wenzetu hata wanaotuambia. Imekula

Changamoto ya kupumua ni kitu gani?
Serikali isiyo na dini (secular) ika azima majoho ya maaskofu na kanzu za masheikh kuhubiri.

Tukageukia miti shamba tukinywa mivinyo ya matunda kama tunaugua utapiamlo!

Tukawa wapiga ramli huenda ni vita nyingine na si Virus

Na mwisho tukajenga mabanda mazuri sana na kutengeneza misufuria kwa kile kilichoitwa Nyungu,
Tukaita nyungu season II, au nyungu plus, leo wapiga debe wanavaa masks ! wanaogopa , nyenyere wameingia uchagoni na bwala limeingia ruba.

Tuiangukie dunia, tuiambie tumemalizana na changamoto ya kupumua tunaungana na mataifa kupambana na COVID-19.

Tuagize chanjo kwa wanaotaka '' wasiotaka hata wakifa hawatakufa wote'' alituambia mpendwa wetu.

Alshabab wa Somalia wamesitisha mashambulizi kutoa fursa ya chanjo, sisi tujisikie fedheha!

Taifa lililoongoza ukombozi wa Afrika sasa linaongoza kwa madogori , mitishamba na mapambio.

Tunahitaji chanjo hatuhitaji kamati za maprofesa! tunahitaji kuagiza jana si kesho

Nanyi wapambe tusikilizeni '' Mbuzi kala Mkeka wapambe mtakalia nini"
 
MALAGASI (MADAGASCAR) YAPIGA 'U-TURN'

VIRUS HANA SIMILE, KUNGURU MJANJA HUEPUSHA UBAWA WAKE

Kuna taarifa ya BBC ikieleza Malagasi kukubali matumizi ya Vaccine na inashirikiana na dunia ya watu

Rais wa nchi hiyo Bw Nirina Rajeolina alitangaza ugunduzi wa dawa ya COVID-9 aliyoiitwa Covid-Organics ambayo ni mithili ya chai iliyotengenezwa kwa mchanyato wa mazao kadhaa yanayopatikana duniani

Nchi hiyo ikajitoa shirika la Afya Duniani kwa kuchelea shirika halitambui dawa eti kwasababu tu imetengenezwa katika bara hili lenye vituko la Afrika.

Kwamba, Rajeolina alitaka walimwengu watumie madawa bila ithibati ya kisayansi akiamini u tu i yanatibu

Rajeolina hakuwa peke yake, Tanzania ilituma ndege kubwa na Waziri wa mambo ya nje kuichukua dawailiyotengenezwa barani Afrika na Waafrika wenyewe bila kuingiliwa na mataifa au Mabeberu

Ilichukua muda mfupi hali ilibadilika mjini Antananarivo kwa wananchi kupukutika mithili ya nyenyere waliopukutwa katika nguzo ya nyumba ya majani. Watu walifariki sana wakiwa wanakunywa Covid organics

Kwa Tanzania , mshirika wa Covid wa Madagascar hakuna anayejua shehena ya Covid Organics ilitumika kwa kundi gani na matokeo gani. Pamoja na tambo za kwenda kuichukua kwa midege hakuna habari zaidi

Hakuna anayeweza kueleza kwa uyakinifu ikiwa Madagascar nao waliwahi kutifikia Tanzani ili tubadilishane uzoefu wa mavumba ya nyungu na utaalam wa kujenga mabanda kama yale ya Muhimbili.

Pengine matukio kadhaa yamemshawishi Rais Rajeolina wa Madagascar kuamini kuwa tatizo zima la Covid ni la kisyansi na si kisiasa au kihisi kama yeye na washirika wake walivyoweza kuw

Rajeoilina ameona ni wakati muafaka wa kujinusuru yeye na Taifa lake kwa kuungana na dunia ya wajuvi
Rais Narina ameelewa kuwa maagizo yake na matakwa yake binafsi yamepelekea madhara kwa watu wake

Madagascar imejirudi sasa inataka vaccines, mitishamba , madogori, misufuria na hisia hazikuisaidia nchi hiyo zaidi ya kuumiza watu ambao pengine walikuwa tayari kununua vaccine kwa gharama kubwa kunusuru maisha yao.

Katika kipindi hiki cha Kwaresma kuelekea pasaka kuna maandiko yasemayo
'Heri ya waaminio kwa kusikia kuliko kuona''. Je, Rajeolina amefikiwa na neno la roho !
 
MALAGASI (MADAGASCAR) YAPIGA 'U-TURN'
VIRUS HANA SIMILE, KUNGURU MJANJA HUEPUSHA UBAWA WAKE
Madagascar imejirudi sasa inataka vaccines, mitishamba , madogori, misufuria na hisia hazikuisaidia nchi hiyo zaidi ya kuumiza watu ambao pengine walikuwa tayari kununua vaccine kwa gharama kubwa kunusuru maisha yao.
Rais Rajeolina mjanja sana. Yawezekana yeye hata kuionja hakuthubutu ila alijua wajinga wametamalaki miongoni mwetu na kweli kwa namna walivyoubugia huo ushombwe sina hamu. Kwa mbali nakumbuka kikombe cha babu na barabara ya kuelekea Loliondo ilivyochongwa haraka haraka ndani ya saa 24...masikini Wadanganyika, we never learn.
 
Back
Top Bottom