#COVID19 COVID-19 is historical in Tanzania: Why don't USA, UK, EU and others copy from Tanzania how to fight against the Corona Virus?

India waliweka lockdown wakaondoa kwasababu ya watu kukataa. Wimbi likapita salama kama ilivyokuwa Tanzania

Wimbi la pili likaanza Tanzania, ndio hadi tukapa 'tangazo la kutozika usiku' . India walikuwa salama

Majuzi watu 25,000 wakajaa Ganjes river huku zaidi ya 50K wakihudhuria mikutano ya Narendra Mod
Wakaacha kila tahadhari wakifurika kila mahali, well kianchoendelea ujaua ni nini

By the way 'wameanza kuvaa masks' teh teh teh. Leo umeona?
Geresha tu hiyo, don't read that story. Tanzania is safe asikudanganye mtu. Rais ana malengo yake anataka waone yupo serious.
 
FYI Watanzania ie Babu zetu waliishi miaka mingi bila hizo dawa unazozipigia chapuo. Fahamu kitu kimoja miti shamba ni tiba bora, hata hizo dawa unazofikiria wazungu wanatengeneza zinatokana na mimea. Sio kila kitu bora kaleta mzungu ni cha kukumbatia. Wahenga walisema ''Elimu ni ufunguo wa maisha.''
Wewe unajifunza haya leo ! Mimi nimetumia sana hiyo mitishamba lakini kuna mpangilio wake
Sio kuwaambia watu wachemshe majani hovyo. Dawa asili si kuvamia mitu mimea na kuwaambia watu watumie

Hawa wazungu wanatengeneza vaccines na mtoto akifikisha miaka 5 tayari amepata DPT, Polio, Measles
Halafu ukisafiri kuna Yellow fever, Dengue, Rubella n.k
Katika hizo hakuna hata moja inayotengenezwa Africa achilia mbali Magu , Muheza au Geita

Hii internet ni ya wazungu teh teh teh

Mkubwa, tulia tu mbuzi kala mkeka !
 
Kwani tumenunua ARV lini na kwa kiasi gani? Teh teh

By the way kuna 'Bilioni 27'' za EU za Covid. Sikusema mimi ni EU Parliament.

Ha ha ha , tukienda huko itabidi tuite wasihusika, teh teh OMG
Unalishwa matongo pori na wewe unakula tu? Weka hata link basi tuone ili tufahamu hayo unayochema ni ya kweli. Au unataka kila story ya BBC au CNN tuikubali kichwa kichwa? Tanzania hadi hivi sasa ugonjwa wa corona sio tishio kama wewe na washabiki wenzako wanavyotaka tuamini. Watanzania wengi wanakufa kwa magonjwa mengine na siyo hayo mafua sijui nini au corona etc. khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee.
 
Wewe unajifunza haya leo ! Mimi nimetumia sana hiyo mitishamba lakini kuna mpangilio wake
Sio kuwaambia watu wachemshe majani hovyo. Dawa asili si kuvamia mitu mimea na kuwaambia watu watumie

Hawa wazungu wanatengeneza vaccines na mtoto akifikisha miaka 5 tayari amepata DPT, Polio, Measles
Halafu ukisafiri kuna Yellow fever, Dengue, Rubella n.k
Katika hizo hakuna hata moja inayotengenezwa Africa achilia mbali Magu , Muheza au Geita

Hii internet ni ya wazungu teh teh teh

Mkubwa, tulia tu mbuzi kala mkeka !
Internet bila madini ya Afrika haifanyi kazi. Kumbe unakubali miti shamba inafanya kazi sasa hiyo elimu umepata ya nini kama unakiri mambo ambayo ni obvious?
 
Geresha tu hiyo, don't read that story. Tanzania is safe asikudanganye mtu. Rais ana malengo yake anataka waone yupo serious.
Yes , tunamtakia heri Mh Rais SSH

Uzuri ni kuwa Rais ana appreciate uwepo wa tatizo na analisema kama lilivyo

Tumeondoka kule kwa changamoto ya kupumua na vita ya uchumi. Virus na vita ? wapi na wapi
 
Internet bila madini ya Afrika haifanyi kazi.
Madini tunawapelekea , hatuna mitambo ya kuchimbia
Kwahiyo tunachimba halafu tunampelekea mzungu dollar atulete mashine teh teh teh

Sisi tunadanganyana vita ya uchumi. Weeee! Virus anakula mapafu halafu yunasema vita ya uchumi! my foot
 
Yes , tunamtakia heri Mh Rais SSH

Uzuri ni kuwa Rais ana appreciate uwepo wa tatizo na analisema kama lilivyo

Tumeondoka kule kwa changamoto ya kupumua na vita ya uchumi. Virus na vita ? wapi na wapi
Umesoma latest report ya Moody kuhusu Tanzania economy?
 
Mkuu Mwalimu
Huyo alikuwa mpinga mask , Vaccines, kufukiza majani, na social distancing. Alikuwa anahubiri kula maembe na mananasi kisha kukimbia na vibuyu vya maji barabarani kama dawa ya COVID-19 . Leo tunashangaa sijui kipi kimemsibu hadi kubadili msimamo na kurudia sayansi aliyoisigina. Ni kiongozi wetu wa Wizara husika
 
Mkuu Nguruvi3.

Unachopaswa ni Unachostahili, kulingana na mazingira na nyakati mahususi.

Matakwa ya MTU kamwe hayawezi kuwa haki, haushi katika upweke. TUNAFUNGAMANA. Uachopaswa kupata, ni kile kitakachoheshimu na kulinda mahusiano sahihi katika Mafungamano yenu. Hicho kinaweza kuwa ni Kinyume na MATAKWA yako.
Mkuu, kuna matakwa ya aina tofauti. Kuna matakwa tu kama matakwa kwasababu mtu anataka.

Kuna matakwa yaliyojengwa katika misingi, haya ndiyo ninayozungumzia. Matakwa yaliyojengwa juu ya maelewano na ufungamano wetu sote katika jamii. Tukayaweka matakwa hayo katika haki na kuyaanisha katika sheria za nchi. Freedom of speech si hisani ni takwa langu chini ya katiba. Kama ilivyo pia kwa takwa la mtu kuamua afya yake. Kwa anayetoka Hospitali akatibiwe nyumba pengine kufia huko anatimiza takwa lake la kuamua maisha yake kama yule anayesaini kufanyiwa operesheni ya kichwa.
Serikali haionekani popote pale katika maamuzi kama haya! ni maamuzi binafsi kwa matakwa ya watu

Kupata chanjo ni takwa langu la msingi la haki. Ikiwa basi hatuwezi kupata chanjo kwasababu za kijamii, basi tupewe fursa ya mashirika kuagiza chanjo ili wanaotaka kama ilivyo kwa wasiotaka watimize matakwa yao
Ikiwa chanjo haina madhara kwa jamii isipokuwa ni hiari ya mtu, hakuna sababu ya kuzuia, ni kunyima haki
Hivi ni kwanini dhana ya Haki mnaibebabeba tu kirahisirahisi, na kuzisema kiholelahole tu mbele za watu!? Huwa mnapima athari zake? Luna anayeweza kutamka hadharani kuwa KILA UNACHOKITAKA NI HAKI YAKO, HIVYO CHUKUA AU DAI?
Dhana ya haki ni rahisi kwasababu ipo kiasili zaidi kuliko ilivyo! Kwa bahati mbaya kuna mataifa, Tanzania ikiwemo watu wake wamepumbazwa kiasi cha kuomba HAKI.

Haki haiombwi na wala haipatikani katika silver plate. Haki inatakiwa na kudaiwa.

Kwa miaka kadhaa Watanzania walipoteza haki ya kuzungumza wanaamini kuna mtu aliyebeba haki hiyo.

Wanaamini serikali ni 'dude' linaloratibu haki zao na kwamba dude hilo halipaswi kuguswa, kuulizwa au kuhojiwa.

Watu hao wataomba haki na madhara yake ni watu kuomba mishahara iongezwe May 1 bila kujua wana HAKI ya kujadiliana na Mwajiri wao Serikali kupitia vyama vya Wafanyakazi.

Watanzania wanaomba haki.
Wameaminishwa na imetitia katika bongo zao kwamba haki ni jitu kubwa lisilosemwa kirahisi.
Sijasema serikali inaratibu ujio wa chanjo, nimetamka kuwa wajibu wa serikali ni kuratibu maisha ya raia wake kiujumla, katika hilo kuchunguza, kupima na kutathimini ni sehemu ya majukumu yake.\
Ni Watanzania tu wanaoamini serikali inapaswa kuratibu maisha yao. Huu nao ni ututusa kama ule wa kudai haki.

Serikali ina ukomo na wala haipaswi kujua una nini chumbani mwako.

Ni kwa msingi huo, ukikosa chakula na mwanao akafa kwa njaa, utakodi gari ya kwenda kuhifadhi mwili, kulipia gharama za mazishi. Hayo utayafanya peke yako si serikali itakayokusaidia.

Ni kwa mfano huo, watu wanaokufa kwa Corona serikali haihusiki, mitaani tunachanga pesa kusafirisha au kuzika wapendwa wetu.

Ikiwa ni hivyo basi vipi serikali ituzie tusifaidike na huduma iliyothibitishwa na Dunia kuwa ni muhimu katika kipindi hiki?
Punguzeni Bezo na Kujitusi.
Ungesema haya kwa wale walioamini kuwa Virus ya Corona inayoshambulia system za mwili na mapafu ni vita ya uchumi. Wanaoamini mchachai wa Malagasi ni dawa, na kwamba majani tu yaliyoota uani kwako ni dawa ya Corona.
 
Nguruvi3.
Ulipokuwa unatetea kila takwa kuwa HAKI ulikuwa unalinda maslahi ya nani? Sasa unahamisha magoli tena, kuwa kuna Takwa la Kutaka tu, na Takwa lililojengwa katika misingi ya maridhiano na mafungamano yetu. Hiki ndicho nilichokuwa nakuambia, bado ukashupaza shingo yako.

Sasa bado nitakufafanulia vema zaidi kuhusu hili, ili usiwe unabebabeba tu mambo usiyotaka kuyaelewa kiundani na kuyasema hovyo kwa watu.....
Unapotosha kufikiri Haki haiombwi Bali ni Kudai tu, unajikanganya tena kwa mfano wako wa mwajiriwa na mwajiriwa. Kwamba Nyongeza ya mshahara ni haki yake, wewe unayedaia haki haiombwi unataka mwajiriwa akae katika majadiliano, na mwajiri wake kujadili haki yake!
Kwanini Asiichukue tu, kwanini Asiidai tu mahakamani kwa sababu ni Haki na haipaswi kuombwa?
Unaweza kututofautishia majadiliano ya mwajiri na mwajiriwa, juu ya nyongeza ya mshahara na maombi ya haki ya nyongeza ya mshahara?
Je, huo unatafakari vema unachoandika au unachojali ni kuwasilisha hisia zako tu hadharani?

Nikujuze tu... Dhana nzima ya HAKI ni Batili, ni KIINI MACHO, ni Upofu....Ndio maana mnapata tabu kuitetea. Mmelishwa Ubatili, mnajivunia hadharani, ni Wanafiki na Wasaliti.

Serikali kutojishughulisha na kilichomo chumbani, ni hoja ya kitoto ambayo ulipaswa kuionea aibu kuitamka. Hili mdsnganyane wenyewe huko katika harakati za upofu wa kiitwacho Haki.
 
Nguruvi3.
Ulipokuwa unatetea kila takwa kuwa HAKI ulikuwa unalinda maslahi ya nani? Sasa unahamisha magoli tena, kuwa kuna Takwa la Kutaka tu, na Takwa lililojengwa katika misingi ya maridhiano na mafungamano yetu. Hiki ndicho nilichokuwa nakuambia, bado ukashupaza shingo yako.
Nilipotetea takwa la haki nilikuwa nalinda maslahi ya wanaotaka chanjo , wanaonyimwa bila sababu za msingi.

Hoja usiotaka na wasiotaka kuijibu watetezi wa 'vita ya uchumi' ni hii;
Mtoto afikishapo miaka 5 mwili wake unachanjo za kutosha nimeorodhesha, kipi kinachunguzwa katika COVID-19?

Kuhusu takwa, hili nilidhani linaeleweka kwamba takwa linalohitajika ni lile lililojuu ya misingi ya ufungamano wetu. Kwamba, kuna takwa la dawa asili basi takwa la chanjo ni sehemu ya haki kama haki nyingine.

Mtu mmoja kwa fikra zake hawezi kufikiri kwa niaba ya watu wote. Hatuwezi kuishi katika udwanzi wa kudanganyana hii ni vita ya uchumi tukiwanyima haki wanaotaka kuzisalimisha nafsi zao kwa hiari na haki zao
Sasa bado nitakufafanulia vema zaidi kuhusu hili, ili usiwe unabebabeba tu mambo usiyotaka kuyaelewa kiundani na kuyasema hovyo kwa watu.....
Nitasema kwasababu kukemea upotoshaji ni sehemu ya msaada kwa jamii.
Hatuwezi kuambiwa Virus wa mapafu wanaondoka mwilini kwa mapambio.

Hatuwezi kuambiwa chanjo inatoka kwa mabeberu wakati mikononi mwetu tukiwa tumebeba Biblia zilizoandikwa na mabeberu. Hatuwezi kukaa kimya tukiambiwa virus wanaotafuna mapafu eti ni vita ya uchumi.
Unapotosha kufikiri Haki haiombwi Bali ni Kudai tu, unajikanganya tena kwa mfano wako wa mwajiriwa na mwajiriwa. Kwamba Nyongeza ya mshahara ni haki yake, wewe unayedaia haki haiombwi unataka mwajiriwa akae katika majadiliano, na mwajiri wake kujadili haki yake!
Haki haiombwi, inadaiwa. Period
Kwanini Asiichukue tu, kwanini Asiidai tu mahakamani kwa sababu ni Haki na haipaswi kuombwa?
Unaweza kututofautishia majadiliano ya mwajiri na mwajiriwa, juu ya nyongeza ya mshahara na maombi ya haki ya nyongeza ya mshahara?
Je, huo unatafakari vema unachoandika au unachojali ni kuwasilisha hisia zako tu hadharani?
Kukaa meza moja kati ya mwajiri na mwajiriwa ni takwa na ni haki.
Si haki au takwa kwasababu tunasema, ni kwasababu imeanishwa katika miongozo yetu ya kijamii chini ya sheria.

Kulipa fedha kwa vyama vya wafanyakazi ni wajibu, lakini wajibu unaambatana na haki . Kazi ya vyama vya wafanyakazi ni kukaa meza moja na mwajiri kujadiliana kuhusu masilahi ikiwemo mishahara.

Ikiwa hakuna maafikiano kuna haki ya mwajiriwa kuchukua hatua zaidi dhidi ya mwajiri, ima kwenda mahakamani au kugoma au kufanya jambo litakalomlazimu mwajiri kurudi mezani. Hiyo ni Haki na haiombwi inadaiwa

Ututusa kwamba haki inaombwa upo Tanzania tu, na kwa haya ninayosoma safari bado ni ndefu.
I can imagine yule 'commoner' sijui upeo wake utakuwaje ikiwa 'at least elite hawajui haki ni takwa si ombi' Sad
Nikujuze tu... Dhana nzima ya HAKI ni Batili, ni KIINI MACHO, ni Upofu....Ndio maana mnapata tabu kuitetea. Mmelishwa Ubatili, mnajivunia hadharani, ni Wanafiki na Wasaliti.
Haki haina ubatili isipokuwa tu inadaiwa wapi. Huko duniani haki ni takwa la mtu, Tanzania ni ombi
Kupata chanjo ni takwa na ni haki, kama ile ya mapambio na kuchemsha nyasi
Serikali kutojishughulisha na kilichomo chumbani, ni hoja ya kitoto ambayo ulipaswa kuionea aibu kuitamka. Hili mdsnganyane wenyewe huko katika harakati za upofu wa kiitwacho Haki.
Ni hivi serikali ina mipaka yake! kuna mambo yapo katika level tofauti kabisa. Kwa wenzetu walioendelea serikali ina miapaka kuanzia serikali kuu, serikali za majiji na na manispaa, serikali za mitaa hadi kwa '' serikali ya mtu'
Kuna mipaka ya maisha binafsi na maisha ndani ya jamii kwa ufungamano wa serikali. Usichanganye

Hoja zote zinaishia katika swala moja, tueleze kwanini chanjo ya COVID-19 inapigwa danadana?

Je, bado unaamini Corona ni vita ya uchumi au umeungana nasi kuamini ni Virus wanaoshambulia mapafu!

Je, bado unaamini uchemshaji wa nyasi ni dawa ya Corona au umeungana nasi kuijali sayansi!

Je, bado unaamini kazi ya serikali ni kuhamasisha mapambio , sala na maombi au umeungana nasi kuamini kuwa imani ni suala binafsi na linaanza na kuishia kwa mtu nyumbani na chumbani kwakwe na si wajibu wa serikali!

Tukatae unajisi dhidi ya akili zetu! tunaweza kufikiri vizuri na kwa mantiki ! Tulipotezwa sasa turudi katika mstari
 
Takwa la Chanjo halijakidhi vigezo vya serikali kufanya kuwa HAKI bado au haitotokea kabisa. Ukiona unacheleweshewa Dai Takwa lako mahakamani au omba uraia wa nchi nyingine yenye kutimiza Takwa lako. Kwa sasa ni Takwa tupu, Halina Mashiko.

Udwanzi na Uduni wa kufikiri, ni kufikiri kuwa Dunia inaendeshwa kwa ustaarabu na unyenyekevu. Ni udwanzi kufikiri kuwa kila uambiwacho au kukiona kiko vile uambiwavyo au ukionavyo. Dunia haiko vile muaminishwavyo na wale ambao mna mahaba nao.

HAKI na UHURU ni viini macho, havijawahi kuishi ila tu mawazoni mwa wasiopenda kuumiza vichwa. HAKI na Uhuru ni dhana za Kusadikika, haziwezi kudhihirika labda kwa kujidanganya.

Kauli za "Huko duniani..." ukitofautisha na Tz zinakuchora u mtu wa namna gani! Kinachouma na kukera zaidi ni kuona ukijionea fahari na ushujaa fikra ulizonazo kichwani, kiasi cha kujipa uhalali wa kuwasemea watu. Sad!

Kama Takwa lako ni sheria tayari, kwanini mkae chini kulijadili? Kama unachoita haki ni lazima kukipata, majadiliano ya nini wakati tokeo linapaswa kuwa moja tu, kupewa utakacho? Why kuwe na nafasi ya majadiliano wakati kuna mahakama? Ni kwamba Majadiliano yanaweza kukukaribisha kujua kuwa, Takwa lako halitekelezeki kwa maana si kitu Upaswacho kupata kwa wakati huo, hata kama itaitwa ni Haki yako.

Katika kulinda Masilahi ya Umma hiyo mipaka haipo, usichoelewa nini? Hakuna serikali yenye mipaka duniani.

Tuambie wewe kwanza, Kwanini chanjo isipigwe danadana, wakati huna hakika ya matokeo yake hata baada ya mwaka tu?

Uelewa wako upoje hivi? Mbona unakuwa mpotoshaji kiasi hicho? Vita ya Uchumi au Kirusi Kweli ndio alternatives gani hizi za kulinganisha mbele za watu? Sasa ingekuwa dai lako ni la kweli, kwanini watu waambiwe wajifukize? Mnajitoaje Ufahamu kiasi hiki ili Kupotosha?
Corona virus kuwa sehemu ya vita vya kiuchumi mimi sina ushahidi nalo moja kwa moja, lakini siwezi kutoa Uwezekano wake. Na kama litakuwa kweli ni smartest players tu ndio watatoboa, si wakurupukaji.

Swali la nyasi nikushauri tu... Kama upo Tz tafuta watu waliowahi kuumwa corona halafu wakuambie waliponaje. Halafu ukae uwaambie huu upotoshaji wako kama watakuelewa.

Kama ni kweli uliona mapambio, sala na maombi tu, hoja zako ni sahihi juu ya wajibu wa serikali. Binafsi sikujitia upofu na kushindwa kuona yaliyoambatana na hayo mengi, mwishiwe nakuona u mpotoshoji wa makusudi. Sijui ni kwa masilahi ya nani.

Nikuambie tu, baada ya Mbowe, wewe ni mtu wa Pili kumsikia analilia Chanjo. Matakwa yenu bado kukomaa, na msitudanganye kuwa corona iliwahi kuwa tishio kubwa. Tunaishi hapa, tunasafiri, tuna ndugu kila kona. Tunajua uzito wa kilichotokea, si kwa kusimuliwa.
Nilishawahi kukuuliza, Je, upo Tz?

Anayefikiri amerudi kwenye mstari hana lake, wala hapajui pake. Anaokota na kuokota kila atupiwacho. Kinachojiumiza zaidi, anajionea fahari na kujihesabia werevu katika Unajisi huo.

Safari ni ndefu mno. Ni heri kwani Ilishaanza mapema.
 
Tuambie wewe kwanza, Kwanini chanjo isipigwe danadana, wakati huna hakika ya matokeo yake hata baada ya mwaka tu?
Nani hana uhakika na matokeo?
Uelewa wako upoje hivi? Mbona unakuwa mpotoshaji kiasi hicho? Vita ya Uchumi au Kirusi Kweli ndio alternatives gani hizi za kulinganisha mbele za watu?
Kumbuka kuna aliyelinganisha sisi wengine tunasema kilicholinganishwa

Bandiko lako lina mengi. Tubaki kwenye mada, hilo ni muhimu.

Baada ya miaka 5 watoto wana chanjo zaidi ya 4 na zitaendelea maishani mwao.
Hatujawahi tilia shaka, leo tunashaka na chanjo nyingine! Hili hulijibu

Pili, lini haki ya kuamini na kuabudu ikawa jukumu la serikali ? Si tulisema serikali ni secular?

Tatu, unatiliaje shaka chanjo ukiwa huna uthibitisho bali kauli tu za nyasi kuponya watu?

Nne, kama Corona si tishio , mbona tunaanza kuvaa mask wenzetu wakizivua?

Tano, hapo nyuma ulinieleza 'hoja zinaweza kusimama bila mipasho au bezo''
Rudi usome bandiko hapo juu ujiridhishe kuwa ni wewe uliyeshauri siku za nyuma.
 
Mkuu, je wewe unayo matokeo ya chanjo baada ya mwaka mmoja?

Hayo mengi katika bandiko hakuna lililotoka nje ya hoja zako. Ni sahihi unapoamua kuyakwepa, lakini werevu wanatusoma.

Hujawahi tilia shaka chanjo za watoto wewe na Nani? Kuna chanjo yoyote inayokuwa anayotolewa bila Mamlaka kuidhinisha? Kwanini isiwe kwa hii ya corona!? Hakuna chanjo inayopokelewa tu, na nyingi tumeshafahamu matokeo yake hata ya makumi ya miaka mbele. Tuambie ni nani anayeweza kukuhakishia chanjo ya korona ni salama hata baada ya mwaka tu, kama sio miaka?

Lakini pia nikuulize, Je, hizi shakashaka juu ya nyendo za corona ni kwa Tz tu? Huzioni huko kwingine? Hata kwa uwaaminio sana kuwa ni wajuzi peke yao? Kama unaziona unafikiri zinatokea wapi? Na kwanini isiwe sahihi kwetu kuwa nazo?

Kuabudu hakuna mahusiano na dini, serikali yetu kutokuwa na dini haimaanishi kuwa haifanyi ibada. Sikiliza wimbo Taifa, BUNGE huanza kwa maombi, hujiulizi kukimbiza mwenge, nk... Tafuta maarifa yaliyo nje ya mifumo uliyolishwa, nimekusihi sana hili.
Nitakuambia tena cha kuzingatia.... Si kila Usikiacho na Kuoneshwa kiko tu vile usikiavyo au uobeshwavyo. Dunia ina mengi sana nyuma ya pazia. Tafakari.

Hueleweki sasa, Unajua Sina Uthibitisho halafu unanihoji why natilia shaka, ulitakaje sasa? Je, niwe kama wewe kuamini vitu nisivyoweza kuthibitisha? Halipo.

Corona Tz hazijaanza kuvaliwa Bongo, tangu inaanza wapo waliovaa, na wapo ambao hawajawahi kuvaa hata mara moja mpaka sasa, na wako poa! Hujiulizi?

Wakati fulani wengi hupenda kujifunza kwa njia ngumu, nawe ni mmoja wao. Hope utasimamia hoja sasa.
 
Leo watoto wanachanjwa DPT(Diptheria , Pertussis and Tetanus), halafu kuna Measles, Rubella, Polio etc
Huko hatusikii mbwembwe za uchunguzi, ikija COVID kuna uchunguzi. Kigugumizi cha nini?
Nimeshindwa kujizuia , hivyo nimelazimika hoji maelezo yako haya.
===
Kwa hiyo haujui utaratibu uliotumika kuruhusu matumizi ya chanjo hizo kwa watoto hapa nchini !?

Hakuna cha mbwembwe, chanjo za corona kwa sasa hazijafikia ubora wa kuaminika. Ndiyo maana nyingine zinazuiwa kutumika wakati zimeishafika kwenye maeneo ya matukio. Hatari hasa ipo kwa chanjo za kuja Africa.
 
Mkuu, je wewe unayo matokeo ya chanjo baada ya mwaka mmoja?
Yes! kama huna habari za dunia tafuta. Israel wamefungua nchi. Huko Israel kwa Mnazaret wanachanja, huku kwetu tunatumai mapambio, tena kutoka ubeberuni halafu hutataki kuchanja.

Marekani vifo vimepungua, wanaelekea kufungua nchi. UK vifo vimepungua wanaelekea kufungua nchi.
India walikaidi , wana kipindi kigumu. Nao kama Tanzania waliamini 'mapambio' ya Ganjes yatawakasa
Nchi za dunia zinatumia chanjo hata majariani zetu . Tumekumbatia ushamba!
Hujawahi tilia shaka chanjo za watoto wewe na Nani?
Haya nani kayasema? Nilisema ''hamjawahi' kutilia shaka chanjo za watoto.
Kuna chanjo yoyote inayokuwa anayotolewa bila Mamlaka kuidhinisha? Kwanini isiwe kwa hii ya corona!? Hakuna chanjo inayopokelewa tu, na nyingi tumeshafahamu matokeo yake hata ya makumi ya miaka mbele. Tuambie ni nani anayeweza kukuhakishia chanjo ya korona ni salama hata baada ya mwaka tu, kama sio miaka?
Hoja ya kukataa chanjo iliyotolewa mwaka jana ni kuwa hii ni vita ya uchumi na hizo chanjo zina hila. Umeelewa
Tukaambiwa hata mask nazo zinaletwa zikiwa zimepandikizwa vitu! Wanaojua ''siri za nchi walisema''

Hapa ndipo swali linakuja, ikiwa ni hivyo kwanini basi tuamini chanjo za watoto za kila siku?
Ikiwa mabeberu wanataka kutudhuru kwa vita ya uchumi, hivi ni wapi pazuri pa kuanzia !Corona au chanjo za kila siku za watoto hadi miaka 5?
Hii ndio hoja iliyopo mezani ! kwamba, kuamini ni vita ni ushamba tu! wakitaka watatupiga na chanjo za kila siku

Lakini kwa wenye akili na mantiki kuna jambo la kujiuliza.
Hivi tuna mashine ndogo ya gene sequencing, unafanyaje uchunguzi wa vaccine?
Yaani uchunguzi unatumia data za walizotengeneza , unadai umechunguza.

Mashine za kupimia tu ambazo sasa zinapatika majumbani (home kit) kwingine duniani sisi tunaagiza.
Inachukua wiki kupata majibu. Katika ukonokono huu tunatathmini chanjo kwa uwezo upi?
Ni akili tu na logic inayoweza kukupa jibu, siyo maombi na mapambio!
Kuabudu hakuna mahusiano na dini, serikali yetu kutokuwa na dini haimaanishi kuwa haifanyi ibada. Sikiliza wimbo Taifa, BUNGE huanza kwa maombi, hujiulizi kukimbiza mwenge, nk... Tafuta maarifa yaliyo nje ya mifumo uliyolishwa, nimekusihi sana hili.
Si jukumu la serikali kutangaza dini! Katiba inasema serikali yetu ni ''secular''
Maombi , mapambio n.k. ni huko kunakohusika si kazi ya serikali wala Rais. Imani ni suala binafsi
Corona Tz hazijaanza kuvaliwa Bongo, tangu inaanza wapo waliovaa, na wapo ambao hawajawahi kuvaa hata mara moja mpaka sasa, na wako poa! Hujiulizi?
Ok, wapo poa! Kwa waliozika na kusafirisha, kwa wajane na mayatima kauli hii ni kejeli!
Nimezungumzia sana moral decay and lack of empathy mabandiko ya nyuma

Na hoja yako ya mwisho ni kwanini sijibu baadhi ya hoja. Well, hoja ni kitu chenye maana na mantiki
Kwa kawaida kama sina sababu huwa sijibu, au matusi sina ujuzi nayo! lakini mara nyingi sana sijibu non sense
 
Mkuu Nguruvi3 , una matokeo ya mwaka mmoja mbele ya chanjo ambayo tangu ianze kutolewa haijafikisha mwaka!!!!?????? UNALIPWA NA NINI KUTETEA UBATILI KWA GHARAMA KUBWA HIVYO?
Umepoteza integrity ya majadiliano, naomba nikuache kwa kukumbia hivi...

Si kila Ukionacho kiko vile Uonavyo, Dunia imejaa Viini Macho. Iwe ni Sayansi, Imani, Mila, Teknolojia, mazingira,nk.


Hakuna sehemu nimekuhoji kwamba kwanini hujibu baadhi ya hoja, kama ipo nioneshe. Sifanyi hivyo kwasababu najua Si kila nisemacho kinabeba Uzito unaoweza kuhimiliwa na ufahamu wako, achilia mbali Hulka zako. Mengine ni ya kutafakari nyumbani, Usijilazimishe kuyafanya hadharani.

Thanks!
 
Back
Top Bottom