Count Down: Ripoti ya Tume ya Wahariri

Paparazi Muwazi

JF-Expert Member
Dec 23, 2007
310
79
Count Down: Ripoti ya Tume ya Wahariri

Kama ambavyo tuliichambua ripoti ya Kamati ya Bomani sasa ni wakati wa kuichambua Tume ya Wahariri iliyoundwa kuhusu habari za kifo cha Wangwe.

1. Muundo wa Tume: je, wajumbe wake ni bora kiasi gani?
2. Hadidu rejea za Tume: kutafuta chanzo cha habari kufanana, kusibitisha kama habari zile ni za kweli. Kuwa palikuwepo Mapanga, Mashoka nk na kwamba Mbowe alitishiwa kukatwa. Na kwamba familia iliamua post mortem baada ya shinikizo la waombolezaji. Kwa kadiri ya Zitto-hapakuwepo mapanga, mikuki nk na wala Mbowe hakutishiwa kuuwawa kwa silaha hizo. Pia uamuzi wa kuahirisha ulifanyika katika kikao cha familia kabla kwa hiyo pale ilikuwa ni kwenda kutangaza tu. Kwa maneno mengine kelele za waombolezaji ziliingilia tu matangazo ya uamuzi ambao ulishafikiwa tayari?
3. Muda: Tume hiyo ina maliza kazi yake lini?
4. Ripoti: iweje, na itakabidhiwa kwa nani? Je itawekwa hadharani?
5. Hatua: nini kitafanyika baada ya ripoti hiyo?

Mimi nadhani ni vyema tume ikafanya upaparazi kubaini mambo mengine ya nyuma ya pazia na kuyaweka wazi. Mathalani, nani aliandika ile habari, nani alituma iandikwe, nani alilipa gharama, je, ni kweli habari iliandikwa kabla ya tukio? Je, ni kweli kulikuwa kuna kikundi kiliandaliwa kiende na mapanga na kwamba kwa bahati mbaya kikaenda na mabango tu wakati habari tayari ilishasema mikuki na mapanga? Je, ni kweli familia ilipewa na kigogo mmoja rambirambi ya milioni 30? Ni kweli Kepa Peter Wangwe, yule aliyekuwa mwenyekiti wa Halmashauri kupitia CCM na Kaka aliyekuwa mpinzani wa Marehemu wakati wote, alilipwa kuratibu zoezi zima la kutangaza kuwa kifo ni cha Risasi? Maana yeye ndiye aliyesema hadharani na pia ndiye aliyenyang’anya bango toka kwa vijana na kulinyosha juu. Je, nini nafasi ya watu kama Waziri Waziri, Vedastus Mathayo(Mb), Mama Kabaka(Mb), Gachuma na Rostam Aziz katika tukio zima? Je, ni kweli msiba mzima ulitumika kama mkakati wa kuivunja CHADEMATarime na kuandaa kampeni za CCM kushinda jimbo hilo? Je, ni kweli viongozi wa TLP, NCCR na CUF walitumia msiba huo kuwapaka matope CHADEMA? Je, nini kinachoendelea Tarime kwa sasa, kwa maana ya habari za mambo yanayojiri? Nini athari za habari zilitolewa kwa wananchi wa Tarime? Hususani suala la Wachagga Vs Makabila mengine Tarime.

PM
 
Count Down: Ripoti ya Tume ya Wahariri

Kama ambavyo tuliichambua ripoti ya Kamati ya Bomani sasa ni wakati wa kuichambua Tume ya Wahariri iliyoundwa kuhusu habari za kifo cha Wangwe.

1. Muundo wa Tume: je, wajumbe wake ni bora kiasi gani?
2. Hadidu rejea za Tume: kutafuta chanzo cha habari kufanana, kusibitisha kama habari zile ni za kweli. Kuwa palikuwepo Mapanga, Mashoka nk na kwamba Mbowe alitishiwa kukatwa. Na kwamba familia iliamua post mortem baada ya shinikizo la waombolezaji. Kwa kadiri ya Zitto-hapakuwepo mapanga, mikuki nk na wala Mbowe hakutishiwa kuuwawa kwa silaha hizo. Pia uamuzi wa kuahirisha ulifanyika katika kikao cha familia kabla kwa hiyo pale ilikuwa ni kwenda kutangaza tu. Kwa maneno mengine kelele za waombolezaji ziliingilia tu matangazo ya uamuzi ambao ulishafikiwa tayari?
3. Muda: Tume hiyo ina maliza kazi yake lini?
4. Ripoti: iweje, na itakabidhiwa kwa nani? Je itawekwa hadharani?
5. Hatua: nini kitafanyika baada ya ripoti hiyo?

Mimi nadhani ni vyema tume ikafanya upaparazi kubaini mambo mengine ya nyuma ya pazia na kuyaweka wazi. Mathalani, nani aliandika ile habari, nani alituma iandikwe, nani alilipa gharama, je, ni kweli habari iliandikwa kabla ya tukio? Je, ni kweli kulikuwa kuna kikundi kiliandaliwa kiende na mapanga na kwamba kwa bahati mbaya kikaenda na mabango tu wakati habari tayari ilishasema mikuki na mapanga? Je, ni kweli familia ilipewa na kigogo mmoja rambirambi ya milioni 30? Ni kweli Kepa Peter Wangwe, yule aliyekuwa mwenyekiti wa Halmashauri kupitia CCM na Kaka aliyekuwa mpinzani wa Marehemu wakati wote, alilipwa kuratibu zoezi zima la kutangaza kuwa kifo ni cha Risasi? Maana yeye ndiye aliyesema hadharani na pia ndiye aliyenyang’anya bango toka kwa vijana na kulinyosha juu. Je, nini nafasi ya watu kama Waziri Waziri, Vedastus Mathayo(Mb), Mama Kabaka(Mb), Gachuma na Rostam Aziz katika tukio zima? Je, ni kweli msiba mzima ulitumika kama mkakati wa kuivunja CHADEMATarime na kuandaa kampeni za CCM kushinda jimbo hilo? Je, ni kweli viongozi wa TLP, NCCR na CUF walitumia msiba huo kuwapaka matope CHADEMA? Je, nini kinachoendelea Tarime kwa sasa, kwa maana ya habari za mambo yanayojiri? Nini athari za habari zilitolewa kwa wananchi wa Tarime? Hususani suala la Wachagga Vs Makabila mengine Tarime.

PM

Baada ya wapinzani kutofautiana katika hili. Sasa ni wakati wa jukwaa la wahariri kufanya kazi yake upesi na kutoa taarifa hadharani ijulikane muongo nani na mkweli nani.

PM
 
hii tume imeundwa kisheria au kwa dhumuni la kijiridhisha tuu??
 
Je hii tume itakuwa ni ya Haki kweli? Jukwaa la Wahariri kweli litafanikisha lolote maana nina imani kwamba baadhi ya wajumbe ni wahusika wa Uhariri katika vyombo ambavyo vilitoa habari hizo tata...
 
Watoe Taarifa Yoyote Hata Kama Ni Ya Hovyo Umma Uwaone Walivyo. Hata Hivyo Sidhani Kama Wahariri Wote Wamenyang'anywa Mapenzi Na Nchi Yao. Tutegee Kitu Pale Wapendwa.

Mtashangaa Itoketaarifa Tamu Ya Kunyamazisha Hata Hilazinazowezatokea Kwenye Uchunguzi Wa Kesi Ambao Labda Polisi Inataka Kufanya Kwenye Upelelezi Wake.
 
Back
Top Bottom