Wananchi kwa Cote D'Ivoire walifanya uchaguzi 31 Oktoba 2010 baada ya miaka 10 bila kufanyika uchaguzi. Kulikuwa na wagombea nafasi ya uraisi 14. Na matokeo yametoka jana na kuwa katika hao 14, mmoja amepata 38% na mwingine 32% na waliobakia wamepata chini ya 30%. Hivyo uchaguzi utarudiwa mwisho wa mwezi huu kwa hao wawili waliopata above 30%.