CoronaVirus-Tanzania: Unawezaje kuwasaidia Watu wenye Ulemavu katika kipindi hiki?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Watu wenye Ulemavu wanasema hali inakuwa ngumu sana kwao kwa sababu wengi walikuwa wakitegemea biashara za Ujasiriamali ambazo kwa sasa ama zimefungwa au hazifanyi vizuri.

Umoja wa Furaha ya Wanawake Wajasiriamali kwa Viziwi Tanzania (FUWAVITA) umesema zinahitajika barakoa zinazoonesha sehemu ya mdomo kwani kama hakuna Mkalimani wa kuzungumza kwa ishara wao husoma midomo ya mzungumzaji.

Baadhi ya Viziwi wametolea mfano wakiwa sokoni ambapo watu wote wamevaa barakoa inakuwa shida kwao kuwasiliana na wauzaji lakini pia shida hii waanaipata kwa Utingo (Makondakta) wa usafiri wa Umma.

Aidha, wameomba msaada wa chakula, barakoa na Sanitizer kwasababu wao kwa sasa ni ngumu kupata mahitaji hayo.
 
Kazi ipo mwaka huu. Nilidhani huu mwaka wa neema ila umeingiliwa na jinamizi jamaani Mungu pekee atuvushe salama. Kila sehemu kilio kama sio biashara basi wafanyakazi hasa wale waliopunguzwa au kazi zao kufungwa. Serikali yetu iko wapi itupe faraja jamani?Poleni walemavu kama sisi tuu tusio na ulemavu tunaona hali mbaya je nyie? Magufuli toka huko utuambie mipango yako kama marais wengine. Iache wizara itupe updates tujue tunaendeleaje.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom