Mabibi na mabwana, kumekuwa na habari hii kuwa ugonjwa huu ni vita vya kiuchumi. Tena mlengwa ni Tanzania.
Habari hizi zimeendelea kuwapo ikisisitizwa kuwa vita vya uchumi ni ngumu zaidi kuliko vita nyingine zikiwamo tuli zowahi kupigana. Yaani vikiwamo tulivyowahi kushinda kama vya nduli Amini, au hata vya kuwasambaratisha M23.
Kwa bahati mbaya, matamshi haya ambayo wakuu wetu wamekuwa wakiyatoa mara kwa mara, yamekuwa hayana ufafanuzi wa kutosha kiasi kumekuwa na mkanganyiko, zaidi ya kuelewa.
Siri ya ushindi katika vita tulivyopigana tukashinda, ilikuwa ni uwazi wa viongozi wetu ambako ndiko kulikopelekea umoja wetu.
Mfano, sababu za wazi kabisa za kumpiga Amini zilikuwapo. Hivyo nia ikawepo, ikizingatiwa kuwa hata uwezo pia tulikuwa nao.
Katika vita hivi vya uchumi tunavyoaminishana kuwa vipo dhidi yetu, hivi adui yetu hasa ni nani? Tuna uhakika gani na hao tunaodhani kuwa kweli ni adui zetu?
Vipi nia, sababu na hata uwezo wa kuvipigana vita hivyo kama vipo?
Labda tungeanzia hapo kwenye kuwatambua adui zetu kwanza, ili tujengane kiuelewa kama watanzania wote kwanza, kabla ya kujishika kibwe kibwe kumpambania mama Tanzania tukiwa tumegawanyika?
Ninawasilisha.
Habari hizi zimeendelea kuwapo ikisisitizwa kuwa vita vya uchumi ni ngumu zaidi kuliko vita nyingine zikiwamo tuli zowahi kupigana. Yaani vikiwamo tulivyowahi kushinda kama vya nduli Amini, au hata vya kuwasambaratisha M23.
Kwa bahati mbaya, matamshi haya ambayo wakuu wetu wamekuwa wakiyatoa mara kwa mara, yamekuwa hayana ufafanuzi wa kutosha kiasi kumekuwa na mkanganyiko, zaidi ya kuelewa.
Siri ya ushindi katika vita tulivyopigana tukashinda, ilikuwa ni uwazi wa viongozi wetu ambako ndiko kulikopelekea umoja wetu.
Mfano, sababu za wazi kabisa za kumpiga Amini zilikuwapo. Hivyo nia ikawepo, ikizingatiwa kuwa hata uwezo pia tulikuwa nao.
Katika vita hivi vya uchumi tunavyoaminishana kuwa vipo dhidi yetu, hivi adui yetu hasa ni nani? Tuna uhakika gani na hao tunaodhani kuwa kweli ni adui zetu?
Vipi nia, sababu na hata uwezo wa kuvipigana vita hivyo kama vipo?
Labda tungeanzia hapo kwenye kuwatambua adui zetu kwanza, ili tujengane kiuelewa kama watanzania wote kwanza, kabla ya kujishika kibwe kibwe kumpambania mama Tanzania tukiwa tumegawanyika?
Ninawasilisha.