Corona: Mizozo ya mipakani, wa kulaumiwa ni Tanzania

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,825
35,827
Mabibi na mabwana moja kwa moja kwenye mada ili kumfunga paka huyu kengele.

Tunayoyashudia sasa hivi mipakani ni wazi kuwa yataendelea kwa muda mrefu tu na bila ya kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Ni wazi kuwa Tanzania kwa kukataa kuwemo katika protokali za pamoja kuhusiana na ugonjwa huu katika EAC au katika zile za dunia kupitia WHO, hakuna namna yoyote ambayo sisi tunaweza kuwa na mashirikiano au maingiliano na wengine pasipokuwa na migongano.

Tanzania imekuwa ikipotosha kauli na misimamo inayotolewa WHO ambayo kwa hakika imekuwa ikizingatiwa na mataifa takribani yote duniani. Mfano:

1. WHO inatambua ugonjwa huu kuwa ni janga la kimataifa. Kuwa ugonjwa huu ni hatari, unauwa, hauna dawa wala chanjo ya kujikinga nao.

Tanzania badala yake inatambua kuwa huu ugonjwa ni kaupepo tu ambako katapita. Tanzania pia inauona huu ugonjwa kuwa ni vita vya kiuchumi vya mabeberu dhidi yake. Tanzania inatambua kuwa tiba ya ugonjwa huu ipo. Ya kwamba nyungu ya kujifukiza, mitishamba na maombezi vinatambulika rasmi kama suluhu yake kamili.

2. WHO inatambua kuwa ugonjwa huu ungalipo na kuwa kama hatua stahiki za kuudhibiti hakuna, basi utaendelea kusambaa na hali kuwa hata mbaya zaidi.

Hata hivyo WHO inatambua ugonjwa huu utakuwapo kwa muda mrefu na kama jitihada sahihi za kuudhibiti zikiwapo, basi tunaweza kuendelea na maisha hata kama ugonjwa ungalipo hadi pale tiba au chanjo vitakapogunduliwa.


Tanzania kwa upande wake inaamini kuwa ugonjwa huu umeshakwisha hali hakuna hatua zozote zilizochukuliwa au zinazochukuliwa kuumaliza au kuuzuia kuendelea kusambaa. Msisitizo umekuwa zaidi kwenye kulinda uchumi, yaani kwenye kuwataka watu wake kuchapa kazi tu. Ya kuwa corona ni kaugonjwa kadogo tu kanakopita.

Katika EAC wanayatambua yote haya mawili tokea WHO vilivyo, isipokuwa kwa Tanzania tu.

Nchi nyingine zote katika EAC zinatambua umuhimu wa kuwaweka wananchi wao salama dhidi ya ugonjwa huu hata kama ni kwa kuuweka uchumi wa nchi zao hatarini.

Nchi nyingine zote katika EAC haziko tayari kusubiria wananchi wao kufa kwa Corona, bali wako tayari kufa wakati wakipambana nayo.

Nchi nyingine zote katika EAC ziko tayari kuishi na Corona iliyodhibitiwa. Katika hili, nchi hizo haziko tayari kuruhusu mgeni yeyote kuingia katika nchi zao bila ya wao kujiridhisha kwanza kuhusiana hali yake ya Corona ikoje.

Ukiangalia mfululizo wa protocols hizi ni wazi kuwa hapa pana "mwana mkaidi ambaye huyo yeye kufaidi ni mpaka siku ya Iddi!"

Tanzania tunapaswa tujitathmini. Hayupo mchawi bali ni sisi wenyewe. Tumekuwa kama watoto watukutu.

Wala tusimsubiri mno wa kuja kutufunga paka sisi kengele! Mbona sasa tunapitiliza mno?

Choko choko zote hizi huko mipakani, ni wazi kuwa washari ni sisi.

Kama sisi tumeamua kuishi na Corona tukiichukulia poa tusilazimishe hilo na kwa wengine pia.

Kama hatukubali raia wetu waendao kwa wenzetu kupata ruhusa za kuingia kwa kufuata masharti yaliyoko huko, basi na tuifunge tu hii mipaka. Vinginevyo migogoro hii isiyokuwa na tija itaendelea huku mkiwahimiza waathirika wa mitafaruku hii kuwalipa nyie kodi na vitisho vya mafaini juu.

Kwani hamzioni biashara za watu zinavyodorora huko mipakani? Kwani mnadhani wafanyabiashara hao watatoa wapi pesa za kuwalipa nyie kodi tena kwa wakati na kwa shuruti zenu?
 
Duh! Alafu likisuluhishwa mnakuja na kelele zingine.


Mkuu sisi tunachoongelea ni ukweli tu, hata kama ukweli huo ni mchungu kiasi gani:

IMG_20200606_131217_039.jpg


Mwenzio hataki mtu mwenye Corona kuingia kwake. Kwa nini kama nia ni njema haki hiyo ya kumpima mwingiaji kwake asiwe nayo yeye?

Kwa nini unang'ang'ania kuwapimia wewe?

Hata aibu hakuna?
 
Umetumwa na Nani kuandika haya yote

Uzalendo tu uliotukuka tu ndiyo umenituma mkuu. Wewe huoni nilichoandika ni kweli na kweli tupu? Ya kuwa tunapaswa kujitathmini kwa dhati tu kwa maslahi mapana ya nchi yetu?

Au wewe utakuwa umetumwa na nani kuandika ulichoandika hapa kisichokuwa na chembe ya uzalendo hata kidogo?

Aliyekutuma atakuwa hatutakii mema sisi kama nchi. Utakuwa unatumika na mabeberu wewe.

Siyo bure!
 
Makubaliano waliyoingia kati ya Tz na Ke unayafahamu au unaongea tu.

Nakuuliza tena kati ya Tz na Ke nani aliyevunja makubaliano?

Msiwe wapotoshaji..!

Sikia wewe huwezi pata ruksa (viza) ya unakokwenda tokea mamlaka za unakotoka. Hiyo ni common sense tu.

Kwetu nani asiyejua vitu *hewa*? Si ajira, si vyeti, si vibarua nk. Sembuse cheti cha Corona. Tusitake kujidanganya wandugu.

Tusisubiri kukosolewa, tuwe na ujasiri wa kujikosoa wenyewe kwenye mambo ya wazi kama haya.

Ndiyo uungwana huo. Msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Makubaliano kitu gani? Hata makubaliano yakiwa mabovu yaendelee tu? Mbona hata ya mtoto wa Barrick (acacia) na makinikia tulipoona hayalipi tuliyapiga teke mchana kweupe?

Makubaliano yasiyokuwa na tija wala maslahi kuyapiga teke mbona ni wajibu (noble duty)!
 
Uzalendo tu uliotukuka tu ndiyo umenituma mkuu. Wewe huoni nilichoandika ni kweli na kweli tupu? Ya kuwa tunapaswa kujitathmini kwa dhati tu kwa maslahi mapana ya nchi yetu?

Au wewe utakuwa umetumwa na nani kuandika ulichoandika hapa kisichokuwa na chembe ya uzalendo hata kidogo?

Aliyekutuma atakuwa hatutakii mema sisi kama nchi. Utakuwa unatumika na mabeberu wewe.

Siyo bure!
Kwahiyo wewe huoni juhudu zinazofanywa na serikali yako ila unaona za jirani?
 
Kwahiyo wewe huoni juhudu zinazofanywa na serikali yako ila unaona za jirani?

Mkuu mimi naona ukakasi unaofanywa na serikali yangu ya Tanzania. Ningekuwa nimeona kwingine pia ningesema wazi wazi. Hata hivyo sijui ni juhudi zipi au za jirani yupi ambaye wewe ungependa nizione.

Labda kukukumbusha tu, ungejikita kwenye mada ingependeza zaidi kwani tungeweza kuchangia katika kupatikana muafaka bora na wa kudumu. Hii ni kama una chembe yoyote ya uzalendo wa dhati lakini.

Ilikuwa ni katika minajili hiyo hiyo ya haki nadhani hata mzee baba alimpongeza kwa dhati kabisa balozi wa Kenya nchini na hata kuulizia kama alikuwa keshaoa.

Tuepuke kuwa na mawazo mgando. Tujitathmini wakuu. Usimtende mwenzio usichopenda wewe kutendwa. Mbona rahisi tu?
 
Mkuu mimi naona ukakasi unaofanywa na serikali yangu ya Tanzania. Ningekuwa nimeona kwingine pia ningesema wazi wazi. Hata hivyo sijui ni juhudi zipi au za jirani yupi ambaye wewe ungependa nizione.

Labda kukukumbusha tu, ungejikita kwenye mada ingependeza zaidi kwani tungeweza kuchangia katika kupatikana muafaka bora na wa kudumu. Hii ni kama una chembe yoyote ya uzalendo wa dhati lakini.

Ilikuwa ni katika minajili hiyo hiyo haki nadhani hata mzee baba alimpongeza kwa dhati kabisa balozi wa Kenya nchini na hata kuulizia kama alikuwa keshaoa.

Tuepuke kuwa na mawazo mgando. Tujitathmini wakuu. Usimtende mwenzio usichopenda wewe kutendwa. Mbona rahisi tu?
So unataka serikali ifanye unayoyawaza kichwani kwako. To cut story short.
Nini maana ya makubaliano? So wewe kaka zako dada, baba zako kuwa harassed huko mipakani na hao wasiojielewa umeona Ni sahihi..ila serikali yako kuwachukulia hatua hao wanaonyanyasa ndugu zako umeona siyo sahihi..si ndiyo
 
Yaani humu kuna vivulana vingi sana. Hivi wewe baba wa nyumba unasolve matatizo ya nyumba yako kwa kufuata maamuzi ya jirani yako? Wewe utakuwa mtu wa ajabu sana. Kuwa na maamuzi yako kama baba. Na hiyo ndiyo misimamo ya wanaume halisi.

Mizozo iliyoko mpakani ni kuwa Tanzania inataka raia zake yaani sisi tuingie kwenye nchi zingine kwa kuwa tu tuna vyeti tokea Tanzania vinavyosema hatuna Corona.

Kuwa na cheti kuwa huna Corona na kutokuwa au kuwa na Corona mwilini ni mambo tofauti. Sasa katika dunia hii ya kitu kidogo hali inakuwa tata zaidi. Kwa wenzetu imeonekana cheti tokea makwetu haina tija kwa kweli.

Makubaliano si misahafu. Panapokosekana tija maboresho hufuata. Kila mtu si apime mgeni wake anayekuja kama anataka? Shida iko wapi?

Ukiona mahali wazi kama hivi pana shida, ujue pana mtu labda alipanga kuwasambazia wenziwe 'ngwengwe' nao sasa wamestuka.

Mbona sisi barakoa tusizozithibitisha tumezipiga marufuku wakati zetu za kutokea kwa mafundi vyerehani wa chini ya mwembe, ruksa?
 
So unataka serikali ifanye unayoyawaza kichwani kwako..to cut story short..

Soma uzi.

Huoni wenzio kina bia yenu bado wanausoma?

Soma na mawazo wazi - common protocol ni muhimu. There's no long story to cut there.

Jikite kwenye mada.
 
Mizozo iliyoko mpakani ni kuwa Tanzania inataka raia zake yaani sisi tuingie kwenye nchi zingine kwa kuwa tu tuna vyeti tokea Tanzania vinavyosema hatuna Corona.

Kuwa na cheti kuwa huna Corona na kutokuwa au kuwa na Corona mwilini ni mambo tofauti. Sasa katika dunia hii ya kitu kidogo hali inakuwa tata zaidi. Kwa wenzetu imeonekana cheti tokea makwetu haina tija kwa kweli.

Makubaliano si misahafu. Panapokosekana tija maboresho hufuata. Kila mtu si apime mgeni wake anayekuja kama anataka? Shida iko wapi?

Ukiona mahali wazi kama hivi pana shida, ujue pana mtu labda alipanga kuwasambazia wenziwe 'ngwengwe' nao sasa wamestuka.

Mbona sisi barakoa tusizozithibitisha tumezipiga marufuku wakati zetu za kutokea kwa mafundi vyerehani wa chini ya mwembe, ruksa?
Tanzania inataka au ndivyo walivyokubaliana mbona una akili za kijinga Sana we jamaa..Hivi huwa unafuatilia habari kweli au huwa unasubiri kusimuliwa.
 
Mizozo iliyoko mpakani ni kuwa Tanzania inataka raia zake yaani sisi tuingie kwenye nchi zingine kwa kuwa tu tuna vyeti tokea Tanzania vinavyosema hatuna Corona.

Kuwa na cheti kuwa huna Corona na kutokuwa au kuwa na Corona mwilini ni mambo tofauti. Sasa katika dunia hii ya kitu kidogo hali inakuwa tata zaidi. Kwa wenzetu imeonekana cheti tokea makwetu haina tija kwa kweli.

Makubaliano si misahafu. Panapokosekana tija maboresho hufuata. Kila mtu si apime mgeni wake anayekuja kama anataka? Shida iko wapi?

Ukiona mahali wazi kama hivi pana shida, ujue pana mtu labda alipanga kuwasambazia wenziwe 'ngwengwe' nao sasa wamestuka.

Mbona sisi barakoa tusizozithibitisha tumezipiga marufuku wakati zetu za kutokea kwa mafundi vyerehani wa chini ya mwembe, ruksa?

Waambie Kenya kwamba makubaliano yalikuwa kila mtu apimwe nchi yao na mipakani waoneshe vyeti tu. Sasa kwa kuwa wamevunja makubaliano inabidi wao wenyewe warudi upya mezani kuomba suluhu. Na round hii wametupa tena nafasi ya kuongeza trms zetu zaidi maana tuko upande wa ushindi as always kama mwanzo.

Kwa kuvunja makubaliano ya wali tunashukuru sana maana mpaka ufunguliwe tena upya itabidi tuongeze terms nyingine tena mpya na wafate matakwa yetu. Tutazidi kuongoza na wao watafa na watatii tu. Ukigeu geu huko huko kwao.
 
Mabibi na mabwana moja kwa moja kwenye mada ili kumfunga paka huyu kengele.

Tunayoyashudia sasa hivi mipakani ni wazi kuwa yataendelea kwa muda mrefu tu na bila ya kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Ni wazi kuwa Tanzania kwa kukataa kuwemo katika protokali za pamoja kuhusiana na ugonjwa huu katika EAC au katika zile za dunia kupitia WHO, hakuna namna yoyote ambayo sisi tunaweza kuwa na mashirikiano au maingiliano na wengine pasipokuwa na migongano.

Tanzania imekuwa ikipotosha kauli na misimamo inayotolewa WHO ambayo kwa hakika imekuwa ikizingatiwa na mataifa takribani yote duniani. Mfano:

1. WHO inatambua ugonjwa huu kuwa ni janga la kimataifa. Kuwa ugonjwa huu ni hatari, unauwa, hauna dawa wala chanjo ya kujikinga nao.

Tanzania badala yake inatambua kuwa huu ugonjwa ni kaupepo tu ambako katapita. Tanzania pia inauona huu ugonjwa kuwa ni vita vya kiuchumi vya mabeberu dhidi yake. Tanzania inatambua kuwa tiba ya ugonjwa huu ipo. Ya kwamba nyungu ya kujifukiza, mitishamba na maombezi vinatambulika rasmi kama suluhu yake kamili.

2. WHO inatambua kuwa ugonjwa huu ungalipo na kuwa kama hatua stahiki za kuudhibiti hakuna, basi utaendelea kusambaa na hali kuwa hata mbaya zaidi.

Hata hivyo WHO inatambua ugonjwa huu utakuwapo kwa muda mrefu na kama jitihada sahihi za kuudhibiti zikiwapo, basi tunaweza kuendelea na maisha hata kama ugonjwa ungalipo hadi pale tiba au chanjo vitakapogunduliwa.


Tanzania kwa upande wake inaamini kuwa ugonjwa huu umeshakwisha hali hakuna hatua zozote zilizochukuliwa au zinazochukuliwa kuumaliza au kuuzuia kuendelea kusambaa. Msisitizo umekuwa zaidi kwenye kulinda uchumi, yaani kwenye kuwataka watu wake kuchapa kazi tu. Ya kuwa corona ni kaugonjwa kadogo tu kanakopita.

Katika EAC wanayatambua yote haya mawili tokea WHO vilivyo, isipokuwa kwa Tanzania tu.

Nchi nyingine zote katika EAC zinatambua umuhimu wa kuwaweka wananchi wao salama dhidi ya ugonjwa huu hata kama ni kwa kuuweka uchumi wa nchi zao hatarini.

Nchi nyingine zote katika EAC haziko tayari kusubiria wananchi wao kufa kwa Corona, bali wako tayari kufa wakati wakipambana nayo.

Nchi nyingine zote katika EAC ziko tayari kuishi na Corona iliyodhibitiwa. Katika hili, nchi hizo haziko tayari kuruhusu mgeni yeyote kuingia katika nchi zao bila ya wao kujiridhisha kwanza kuhusiana hali yake ya Corona ikoje.

Ukiangalia mfululizo wa protocols hizi ni wazi kuwa hapa pana "mwana mkaidi ambaye huyo yeye kufaidi ni mpaka siku ya Iddi!"

Tanzania tunapaswa tujitathmini. Hayupo mchawi bali ni sisi wenyewe. Tumekuwa kama watoto watukutu.

Wala tusimsubiri mno wa kuja kutufunga paka sisi kengele! Mbona sasa tunapitiliza mno?

Choko choko zote hizi huko mipakani, ni wazi kuwa washari ni sisi.

Kama sisi tumeamua kuishi na Corona tukiichukulia poa tusilazimishe hilo na kwa wengine pia.

Kama hatukubali raia wetu waendao kwa wenzetu kupata ruhusa za kuingia kwa kufuata masharti yaliyoko huko, basi na tujifunge tu hii mipaka. Vinginevyo migogoro hii isiyokuwa na tija itaendelea huku mkiwahimiza waathirika wa mitafaruku hii kuwalipa nyie kodi na vitisho vya mafaini juu.

Kwani hamzioni biashara za watu zinavyodorora huko mipakani? Kwani mnadhani wafanyabiashara hao watatoa wapi pesa za kuwalipa nyie kodi tena kwa wakati na kwa shuruti zenu?
Kamanda umetoka kwenye kupiga ramli sasa hivi lawama.
 
Tanzania inataka au ndivyo walivyokubaliana mbona una akili za kijinga Sana we jamaa..Hivi huwa unafuatilia habari kweli au huwa unasubiri kusimuliwa.

Kwa kutokujikita kwenye mada mjinga mbona utakuwa ni wewe mkuu. Kwa kutokujikita kwenye mada iliyoko hapa hapa wewe mbona ndiyo mwenye kusubiri kusimuliwa. Umeshindwa kusoma na kujikita kwenye mada iliyopo hapa hapa, mfutilia habari utakuwa wewe?

Mbona mu watu wa kujidhalilisha namna hiyo?

IMG_20200606_131217_039.jpg


Haya mbona yameongelewa sana humu? Wewe huoni kama kuna tija yoyote?

Mkuu kama huoni si ubakie tu huko Twitter, Facebook au Instagram? Huko kutakufaa zaidi.

Mkuu akili ndogo kama yako huku itachemsha tu.
 
Kamanda umetoka kwenye kupiga ramli sasa hivi lawama.

Sijaona ramli wala lawama popote. Si katika bandiko hili wala jingine lolote.

Kama hukuelewa, bandiko hili liko wazi:

IMG_20200606_152938_968.jpg


Jikite kwenye mada na unayoandika jiridhishe kuwa hujapotea njia.
 
Back
Top Bottom