Corona: "Media tunakufa kizungu na tai shingoni!", asante Waziri Mwakyembe kutambua mchango wetu. Serikali/jamii please do something, tutakwisha

This is rubbish! Total rubbish from Jemedari Mkuu! (not you, pascal) Issue ni kuwa unaweka lockdown kuzuia kusambaa. Ukifankikisha hilo, then unakuwa umejenga uwezo wa hospitali zetu ku handle cases chache zitakazojitokeza. Ukishafika hapo kuwa sasa virus hawasambai, then una ease lockdown. . .. maisha yanaendelea. Kuna some states in the US zimelegeza masharti na LEO maambukizi na hospitalization zimerudi kupanda!
Huondoi woga wa raia kwa kuwa expose kwenye mizinga. Unawaambia kuwa kuna mizinga, itapigwa msiogope, ukisikia mingurumo kimbilia handakini! Tumefundishwa hivyo wakati Id Amin. hapakuwa na taharuki. Tuliambiwa kuna vita fanya moja, mbili, tatu! Hatukuachwa na kuambiwa kuwa hakuna vita!
Mbona woga upo maana watu wanaona watu wanakufa sana! Kila kaya inakwenda kuguswa kama ukimwi ulivyogusa kila kaya, sasa utasemaje hakuna woga?

Big up and kudos!
Mimi huwa nacheka sana ninapomsikia Jiwe akidai kuwa watu wasiwe na HOFU maana hofu ndo inaua kuliko hata Covid-19....!!!
Lakini huyu Jiwe Leo ana zaidi ya mwezi kakimbilia Chattle kwa hofu ya Corona....!!!Mbona hajata?
Jemedari na Amiri Jeshi Mkuu anawahamasisha Wapiganaji wasiwe na HOFU risasi na mabomu zikiwapiga wasonge mbele tu ilhali yeye yuko ndani ya Handaki amejificha! This is purely Kenjikitile policy of confronting the enemy!
What kind of a Commander-in-Chief?
 
Kama siyo " ukanjanja" Pascal angerithi mikoba ya Tido Mhando kwa ubobezi lakini ndio hivyo tena. MC yeye, Mtangazaji yeye, Mwanasheria yeye, Mpiga kampeni yeye, Mgombea ubunge yeye , mwanajeshi yeye nk nk

Na huo ndio ukanjanja wa mtu kutojikita kwenye taaluma!

Mkuu johnthebaptist unadhani tumechelewa sana kumshauri Pascal Mayalla ajikite kwenye taalum yake ili angalau alete ahueni kwenye sekta hii ya Habari ambayo kwa sasa wapiganaji wake wameingia mitini?. Wamebakia wanachungulia kwa Mbali, wakiona hata jani linapeperushwa na upepo wanatimua vumbi.

Nimemkumbuka Mwangosi
 
Well said bro.
Paskali,
Ulimhola bhabha ja mirimo?
Hizo ni salamu za wa kukaya Mwanza- Geita-Chatto.
Kwanza kabisa nianze na hayo malalamiko yako yote yalipaswa kuelekezwa kwa 'homeboyz' wako ambaye amejichimbia Chattle zaidi ya mwezi Sasa na haijulikani yuko likizo ya ugonjwa au amekimbia Covid-19. Tunajua Ikulu rasmi za Head of state Tanzania kwa Sasa ni Dar-es-salaam na Dodoma(Ikulu mpya).
Lakini la pili ni la kuhusu Waandishi wa Habari kukosa UHURU wa kuandika UKWELI wa Covid-19 tangu ianze kuwa reported Tanzania. Kumekuwa na usiri usioeleweka kuhusu janga hili kuhusu idadi Halisi ya Waathirika wa Covid-19, Vifo vingapi na Waliopona wangapi. Hapa ndipo penye tatizo.

Mimi kwanza ndo naskia toka kwako kuwa Kuna Wana media 10 wametangulia mbele za Haki tokana na gonjwa la Covid-19.Lakini homeboy wako hataki hizi habari zijulikane kwa Watz! Hii manake nini kama siyo mbinu ya kuficha udhaifu wa Serikali kwa kushindwa kukabiliana na Covid-19?

Kama ni kweli kuna wanahabari 10 wameondoka kwa Covid-19 unaowajua wewe peke yako, manake ni kwamba the death magnitude ni kubwa sana kuliko hizo Takwimu za Ummy Mwalimu (Vifo 16 tu!) Unless uniambie kuwa Kati ya hivi vifo 16 na hao 10 ni katika idadi hii kitu ambacho siyo kweli.
Kuna Wabunge 3, Kuna Wakuu(W) 2, Kuna masheikh 2 na Kuna Wachungaji 2 na kuwa wale waliokuwa Wanazikwa usiku kwa Ambulance nchi nzima.

Leo ni zaidi ya wiki hatujasikia any Update toka Serikalini! Si Ummy Mwalimu, si Majaliwa, si Suluhu Hassani wala Jiwe mwenyewe!! Wote kimya na huu ukimya una walakini!!
Kuna Hoja dhaifu sana ya ATI M MAABARA YA TAIFA INAFANYIWA MAREKEBISHO....!Hili linashangaza sana. Kigezo kuwa Test Kits za Covid-19 Zina kasoro ni kujaribu kupoteza malengo na kuhamisha mawazo ya Watz kwenye focus ya Covid-19!

Madai ya Jiwe kuwa Kits ni mbovu au zinatumika na Mabeberu kuihujumu Tanzania hazina mashiko! Hizi Kits ziligawiwa kwa nchi zote za Afrika Kama msaada toka kwa Bilionea Jack Maa(China). Nchi za Waafrica wenzetu wanapima kila siku na wanatoa Takwimu every after 24 hours kinyume kabisa na Tanzania Bara. Kwa ndugu zetu wa Tanzania Visiwani wanatumia the same Test Kits na wanatoa update every after 24 hours.

Sisi Tanzania Bara badala ya kupima watu wanaodhaniwa Wana Covid-19 tumeacha na KUANZA kupima Kondoo, Mbuzi, Kware, Mapapai na Mafenesi na sijui nani alimwambia Mkulu kuna Covid-19 mpaka kwenye Mapapai na Mafenesi. Utasema Papai limekutwa na Covid-19. Is it logical? Yawezekana kabisa huyu mtu aliyekwenda kununua hayo mapapai na kuandaa hizo samples alikuwa na Virusi au mwuzaji wa Mapapai Ni mwathirika wa Covid-19, how can you draw a conclusion kuwa Kits Ni mbovu?
But we can put the test the other way round. Kwamba huyu aliyechukua sample za Mapapai na Mbuzi yeye alikuwa amedhamiria kwa maksudi kuonesha kuwa Kits hazifai hivo akapandikiza virus wa Covid-19 ili apate kisingizio kuwa Kits hazifai ili apate hoja ya kukwepa lawama?

Tatizo la Watz wengi kukosa Critical Thinking za kuweza challenge hoja dhaifu toka kwa Watawala. Hapa ndipo Media inapotakowa kuingilia Kati kwa kuhoji issues,kudadavua na kuweka Mambo hadharani. Waandishi Habari wengi wa Kitanzania hawanaga ile kitu inaitwa Critical Analyis au Investigative Journalism na badala yake Waandishi wengi wamebakia kuwa Wapiga Filimbi wa Harmelin tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu johnthebaptist unadhani tumechelewa sana kumshauri Pascal Mayalla ajikite kwenye taalum yake ili angalau alete ahueni kwenye sekta hii ya Habari ambayo kwa sasa wapiganaji wake wameingia mitini?. Wamebakia wanachungulia kwa Mbali, wakiona hata jani linapeperushwa na upepo wanatimua vumbi.

Nimemkumbuka Mwangosi
Hatujachelewa bwashee..... Na vile kwa sasa yuko na Dotto Bulendu anaweza kumakinika zaidi!
 
Big up and kudos!
Mimi huwa nacheka sana ninapomsikia Jiwe akidai kuwa watu wasiwe na HOFU maana hofu ndo inaua kuliko hata Covid-19....!!!
Lakini huyu Jiwe Leo ana zaidi ya mwezi kakimbilia Chattle kwa hofu ya Corona....!!!Mbona hajata?
Jemedari na Amiri Jeshi Mkuu anawahamasisha Wapiganaji wasiwe na HOFU risasi na mabomu zikiwapiga wasonge mbele tu ilhali yeye yuko ndani ya Handaki amejificha! This is purely Kenjikitile policy of confronting the enemy!
What kind of a Commander-in-Chief?
Nimependa argumet yako, perfect!
 
Tundu Lissu aliwahi kusema "Hakuna aliye salama", yani huu utawala huu sijui hata unajihisi uko kwenye karne ya ngapi, Mayalla tatizo lenu waandishi wengi mmekuwa upande wa serikali zaidi mkijua watawalindia taaluma yenu. No One Is Safe.
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko la kuizindua serikali na Jamii, kuikoa sekta ya media, katika hii vita ya janga la Corona, japo sisi waandishi wa habari ni wadau muhimu sana katika vita hii kama ilivyo kwa madakari, manesi na wauguzi, lakini kiukweli sisi waandishi wa habari, haswa ma freelances, na sekta nzima ya Media "Tunakufa Kuzungu Na Tai Shingoni!", tunaangamia kimya kimya, tunamshukuru Waziri wetu wa Habari, Dr. Harrison Mwakyembe kwa kutambua na kuthamini mchango wetu, lakini kiukweli kabisa, media hatujaweza kutimiza wajibu wetu kikamilifu, serikali yetu, taasisi wezeshi kama TCRA, na jamii kwa ujumla, it needs to do something, to help out the situation, vinginevyo media sio tuu tutashindwa, bali pia tutakwisha...!.

Jumamosi iliyopita mimi nikiwa Dar na Dotto Bulendu akiwa Mwanza, tulifanya mahojiano ya live, mubashara na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe, akiwa Dodoma, katika kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, na tulifarijika sana kwa Waziri Mwakyembe, kutambua mchango wetu, na kutupongeza sisi waandishi wa habari, na madaktari, manesi na wauguzi kwa kazi kubwa tunayoifanya, tangu kuibuka kwa janga la Corona, ila akatusifu zaidi sisi waandishi kuwa ni mashujaa wa ajabu, ambao "Tunakufa Kizungu na Tai Shingoni"...
Msikilize Mhe. Waziri



Tangu kuingia kwa janga hili la Corona, ndani ya kichwa changu nina list ya waandishi wa habari zaidi ya 10, tumewazika wengine kwa kutaarifiana rasmi, wengine kimya kimya, naomba nisiwataje majina humu, nikashutumiwa kutoa siri za marehemu kwasababu karibu kila anayekufa sasa, anahusishwa na Corona, hapa naomba kusisitiza sijsema hao waandishi wa habai wote 10, wamekufa kwa Corona, no, ni waandishi wa habari zaidi ya 10, wamekufa tangu kuingia kwa Corona, hivyo sio lazima wawe wamekufa kwa Corona,
Uzi Maalum wa Waandishi wa Habari na Wafanyakazi wa Media Waliotangulia Mbele Tangu Kuingia kwa Corona ila Sio Lazima Chanzo ni Corona!. - JamiiForums
lakini kiukweli wanahabari, tunachomoka, media zinasinyaa, kamba zinazidi kukaza, kwa kada ya sisi waandishi ma freelancers, ndio usiseme kabisa!, hali sii hali, inabidi serikali, TCRA, taasisi wezeshi na jamii kwa ujumla, kuingilia kati, kuisupport media, ili tuweze kutimiza majukumu yetu kikamilifu vinginevyo...

Waziri Mwakyembe " Kila vita ina jemedari wake, katika vita hii, mimi naamini kabisa, Jemedari tunaye ni Mkuu wetu wa nchi, askari wa mstari wa mbele mimi nawachukulia ni makundi mawili, kwanza ni madaktari wetu na watumishi wote wa afya, lakini wa pili ni wana habari". "Wanafanya kazi ambayo, wanaipa jamii elimu, tumefika wapi, na kunaendelea nini, hivyo kwanza naomba kuwapongeza wanahabari, wanafanya kazi nzuri ya kuhabarisha jamii, nchi iko kwenye amani, kila siku tunahabarishwa kinachoendelea, japo taarifa nyingine ni za kugofya sana"

Mwakyembe "Baadhi ya taarifa za Corona, haziendani na mwelekeo wa Jemedari Mkuu, Jemedari Mkuu alichukua hatua moja nzuri sana, tukikabiliwa sana na woga, wasiwasi, dukuduku, watu wengi watakufa kwa dukuduku, wasiwasi na woga"
"Vita ni vita tuu, ukisikia tuu mabomu yanarindima kwa mbali wewe huku unaanguka kwa uoga kwa kudhani yameishakuangamiza".

Mwakyembe "Kwa ujumla kazi ambayo mnaifanya wanahabari ni nzuri, na mimi nawapongeza kwa kazi hii, na mnafanya kazi katika mazingira magumu sana, na hilo lazima tuliangalie wote Watanzania katika hali ya uhalisia. Wakati wengi tunajifungia ndani muda mwingi, kama mimi mmenifuata hapa nyumbani, lakini wana habari, kazi yao ni kutoka nje, wako msatari wa mbele kwenye vita, na mimi nimesikitika kwa muda mrefu, wamiliki wa vyombo vya habari, wana wa expose waandishi wao, wanawaacha wazi, kuweza kupata matatizo mbalimbali, wanatoka ofisini bila barakoa, sanitiser, bila usafiri, nimepita kwenye newsroom, watu wamejaa, wana changia vifaa, siwalaumu, lazima kwanza tuwashukuru kwa kazi nzuri wanayoifanya katika mazingira magumu.

Baada ya Waziri Mwakyembe kulijua hili, sasa naomba kuendesha darasa hili.
1. Hatua ya Kwanza ni kukuelimisha media ni nini na kazi za media.
Media ni vyombo vya habari vinavyotumika katika upashanaji habari. Vyombo hivi vimegawanyika katika makundi mawili, ambazo ni Traditional Formal Mass Media, vyombo rasmi vya habari ambavyo ni Redio, TV na Magazeti, na uhabarishaji hufanywa na waandishi wa habari waliosomea yaani professionals. Kufuatia maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia na utandawazi, kumeibuka modern media ambazo ni online media, na social media zikiwemo Blogs, Online Forums, Facebook, Instagram, Twitter, YouTube, WhatsApp groups etc, ambapo every Tom, Dick and Harry ni mwandishi wa habari, hii inaitwa citizens journalism. Japo TCRA inazitambua online media na kuzisajili, na ma bloggers na Online TV wanapewa press cards, its very unfortunate Waziri Mwakyembe haitambui social media kama ni media, ameiita ni media ya kijiweni!.

2. Kazi za Media
Traditional media ilikuwa na kazi kuu tatu
1. Kuhabarisha Jamii
2. Kuelimisha Jamii
3. Kuburudisha Jamii
Kwa modern Media zimeongezeka
4. Watchdogs of the society, Ku act as 4th Estate

1.Jukumu la 1 la Uhabarishaji.
Kwenye jukumu kuu la kwanza la media kwenye uhabarishaji, Media imetimiza jukumu lake kikamilifu na nimepongeza hatua ya serikali kuweka list ya wazungumzaji rasmi 5 wa Corona kitaifa ambao ni
  1. Rais wa JMT
  2. M/Rais
  3. Waziri Mkuu
  4. Waziri wa Afya
  5. Msemaji Mkuu wa serikali.

  1. Nikasema hatua hii ni mzuri ili taifa lipate taarifa moja iliyonyooka, kama kila mtu ataachwa ajisemee itakuwa chaos, utaratibu huu unaitwa restrictive media reporting na hutumika hata wakati wa vita.
  2. Information is a two way traffic, serikali inatoa tuu taarifa, media ilikuwa ina wajibu wa kufikisha taarifa za serikali kwa umma, lakini hakuna utaratibu wowote wa serikali kupokea mrejesho hao wananchi wanaopelekewa taarifa na maelekezo ya serikali jee wanasemaje?. Wanatekeleza?, Wananawa kwa maji tiririka?. Wanafanya social distancing?. Kwenye eneo hili, media hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu.
  3. Kazi ya hao wazungumzaji wanne ni kutoa update ya Corona. Kwenye eneo hili la media kutoa taarifa za serikali za Corona, media tumetimiza wajibu wetu kikamilifu kabisa na tunastahili pongezi za dhati.
  4. Lakini ukweli Corona ni zaidi ya updates, kila vizara, kila idara, kila Taasisi itakuwa affected na Corona hivyo mawaziri wengine na wakuu wengine wote wana wajibu wa kuizungumzia Corona haswa how to mitigate the after effects, huko sio kutoa update huko ni kuisaidia serikali na Watanzania jinsi ya kukabiliana na madhara ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya Corona. Kwenye eneo hili la kutoa taarifa nyingine zozote kuhusu madhara ya Corona kwa sekta nyingine zote, media hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu.
  5. Watoa taarifa wa serikali wanaisoma taarifa ya maandishi na kuwasomea media hakuna any room kwa media yoyote kuuliza kupata ufafanuzi, matokeo yake media kazi yake ni kulishwa tuu habari, spoon fed, na media kazi yake ni kumeza tuu hizo, habari, hukuna kuzichakata, hakuna news analysis, hakuna news relevance alimradi Msemaji ni serikali na serikali imesema.

2. Jukumu la Pili la Uelimishaji Jamii
Hili pia media imejitahidi ila bado, Watanzania wanahabarishwa vizuri kuhusu Corona lakini kazi ya uelimishaji bado inafanywa kwa kiwango cha chini, hivyo kuna watu wananawa kwa maji tiririka kwasababu ni lazima, lakini kwenye social distancing bado, misongamano bado ipo kila mahali.
Zaidi ya kuripoti zile updates za Corona, hakuna TV yoyote, redio yoyote, au magazeti yenye dedicated Program kuhusu uelimishaji umma wa Corona zaidi ya yale matangazo ya Corona.
Hivyo kwenye jukumu la media za Tanzania katika uelimishaji umma kuhusu Corona bado sana.

Kwa vile Corona haina dawa, Watanzania walipaswa waelimishwe hao wagonjwa huko kwenye vituo walikotengwa wanafanywa nini hadi wengine wanapona kabisa na kuruhusiwa ili wenye uwezo wawatibie watu watu kwa kuzua na sio kusubiri watu waugue wazidiwe wakarudikane kusubiria... wakati watu wangeelimishwa huduma ya kwanza ingeanzia nyumbani.

There's a lot of education inputs kutoka nje kuliko kutoka ndani. Serikali imetoa list ya wataalamu official watakao elimisha kuhusu Corona, sijabahatika kuona hata kipindi kimoja cha wataalamu hao

Vituo vya Redio na TV vitenge dedicated Program za uelimishaji umma kuhusu Corona. Hao wataalamu wawe pro active kwenda kwenye media kuelimisha umma.

The regulator, TCRA, atoe muongozo kwa vyombo vyote vya utangazaji na mitandao ya kijamii kuandaa vipindi elimishi kuhusu Corona

Wakati Wazungu wamehangaika kutafuta tiba, sisi tungewatumia wataalamu wetu wote kuanzia madaktari, tiba mbadaka, tiba asili, ma sangoma, waganga hadi Babu wa Samunge kukijaribishia kikombe.

Hao wachungaji wenye uwezo wa nguvu za uponyaji, waruhusiwe mahospitalini ili tushuhudie uwezo wa nguvu zao na sio kuwakamua masikini Watanzania kwa kusingizio cha kufanya miujiza, Wachungaji wenye uwezo wa kuponya kwa miujiza wajitokeze kuonyesha uwezo wao na serikali iwaruhusu, kama alivyojitokeza Askofu Gwajima, aruhusiwe tuone uwezo wake na miujiza ya Mungu katika uponyaji.

Unapo deal na gonjwa ambalo halina tiba na kuna wagonjwa wamezidiwa mahututi na hatimaye watakufa tuu, what is wrong to turn them into Guinea pigs and test them, we may save them, hata kama kwa kuwajaribishia hizo tiba mbadala na bado wakafa, let it be, at least tumejaribu, hata tusinge jaribu, they were going to die tuu anyway. Let's try to do anything something kuliko doing nothing.

3. Jukumu la 3 la Media ya Tanzania Kubudisha Jamii
Kazi ya tatu ya media ni kuburudisha jamii. Kwenye eneo hili pia media ya Tanzania haijatimiza wajibu wake kikamilifu.
Kwa vile Corona ni janga, na kufuatia kilichotokea Wuhan, Italy, UK na US, Corona imetisha na kuogofya, media nazo zikalipokea hivyo hivyo. Shujaa wa eneo hili ni rais Magufuli aliposema tusitishane, ka Corona ni ka ugonjwa kadogo tuu, tena sio kirusi ni shetani disguise as kirusi, tukamkabidhi kwa Mungu kiboko ya shetani!.
Pamoja na mabalaa yote ya janga la Corona, pia kuna mazuri ya Corona, kuna positives za Corona zilipaswa kuangaliwa. Mwana FA na meneja wa Diamond, Salaa did. Kuna watu wanapona wanaruhusiwa. Media ilipaswa kuwatafuta madaktari waliofanya miujiza tufanye human interest stories za mazuri ya Corona. Kuna watu wamepiga pesa kwa kuziangazia fursa za Corona, hata Diamond alichofanya akiwa quarantine ni jambo zuri, tusiizungumze Corona kwa ubaya tuu, tuizungumze kwa wema. Italy Wazee ni wengi mno na wanaishi sana, hivyo Corona ni kama mkombozi fulani kwa blessing in disguise kwa mifuko ya hifadhi za jamii kwa..., ame fykelea...

Sisi baadhi ya familia, baba na mama ni working class, familia yangu nina watoto 9, wamepishana miaka 2, the oldest ni 24, 22, 20, hawa wako vyuo. Then kuna 18, 16 na 14 wako sekondari, kisha kuna 12, 10 na 8 wako primary. Ukiondoa Christmas Day, there is no any other time watoto wote wako nyumbani. Kwenye Corona wote wamerudi home, baba ni mwandishi wa habari wa mikutano, warsha, seminar, makongamano na events, zimesimamishwa, niko home. Wife ni mfanyabiashara wa safari za nje, zimesimamishwa!, nyumbani kuna Dada wa jikoni, dada wa usafi, kaka wa garden, feeding a family of 15 is not a joke. Ukishinda nyumbani na watoto ndipo unagundua kiukweli hawa wadada wa kazi, walipaswa kulipwa vizuri!.

Hivyo Corona has lots and lots of human interest stories na sio habari tuu za ku stigimize kwa idadi inaongezeka, lakini wanaopona hatuwazungumzi. Kutembelea kambi za quarantine na ku file stories about life in quarantine zitakuwa very interesting stories.

4. Jukumu la 4 la media ya Tanzania as a Watchdogs of the Society kwe janga la Corona
Kazi ya Watchdogs ni wale mbwa wanaofanya kazi ya ulinzi, kazi yao ni kubweka tuu ili kumjulisha mwenye nyumba something is not right.

Hawa mbwa pia wapo mbwa wa aina 3,
1. Shepards Dogs habweki ana ng'ata.
2. Barking Dogs kazi yake ni kubweka tuu ila hang'ati!
3. Lap Dogs kazi yake ni kuchezesha mkia na kukamba lamba, habweki wala hang'ati!

Kwenye janga hili la Corona, the Tanzania media has failed this nation katika role ya Watchdogs.
Toka Corona inaanza kule Wuhan ije December 2019 tungekuwa na serious media, tungeanza kubweka ili kuiandaa serikali yetu for preparedness kwa Corona, angalieni China ilipolipuka tuu Wuhan, mpaka imedhibitiwa haikufika Beijing na wala haikuingia Japan.

Tanzania ndio nyumba yetu, baba mwenye nyumba ni rais wetu na serikali yake, wao wako ndani wamelala, sisi media ndio mbwa ambao tuko macho tunalinda nyumba. Corona ndio mwizi anayekuja kutuibia nyumbani kwetu.

Media ya Tanzania ingekuwa ni Sheppard dog, ingefanya kazi kama gazeti la The Washington Post wakati wa kashfa ya Watergate, naomba tukiri udhaifu kwenye complex issue kama hii ya Corona, media zote za Tanzania hakuna hata moja yenye uwezo kuajiri ma medical journalist wa kuandika story za kina kuhusu Corona ambazo zingeisaidia serikali yetu. Angalieni CNN na Dr. Sunjay Gupta.
Hivyo media ya Tanzania kwenye kuisaidia serikali kwenye hili la Corona ni zero. Naamini kuna madaktari wazuri tuu ambao wanaopenda kuwa watu wa media kama alivyo Dr. Maro kwa Clouds.

Tukija yule mbwa wa pili wa barking Dogs, kiukweli mainstream media pia has failed this nation on this role. Kazi hapa ni kubweka tuu ili kumuansha mwenye nyumba. Media ambayo imelitenda hili ni JF pekee.
Pale rais wa nchi anaposema ka Corona ni ka ugonjwa kadogo tuu na serious media ambayo ni barking Dogs zilipaswa zibwekwe.

Rais Magufuli na serikali yake walipaswa wasaidiwe na media kwa kuwaonyesha good practices elsewhere ambazo zimesaidia.

Rais Magufuli aliporuhusu mikusanyiko ya nyumba za ibada, serious media ilipaswa i bweke kwa kuonyesha kama Roma wenyewe kwenye Ukatoliki wamefunga makanisa, Saudi Arabia wenye Uislamu wamefunga misikiti who are we?. Media tulipaswa kuwaumbua viongozi wa dini wanaohemea sadaka hata kwa kuhatarisha maisha ya watu!.

Hapa Tanzania tulipaswa kuwa na strong independent media yenye uwezo wa kumweleza rais Magufuli na serikali yake kuwa baadhi ya hatua anazosita kuchukua ikiwemo kuendelea kuruhusu mikusanyiko ya nyumba za ibada is wrong. Media ionyeshe jinsi Mungu alivyo Omnipresent yuko popote na mikusanyiko ya nyumba za ibada sio miongoni mwa mikusanyiko muhimu. Kwenye hili angalau sisi jf tulisema.

Kwenye hili media ya Tanzania ni just lap Dogs!. Kazi ya mainstream media zetu haswa za electronics ni kuchezesha tuu mkia na kulamba lamba kila kinachofanywa na serikali, hakuna analysis, hakuna critics na mwendo wa kusifu tuu na kupiga makofi.

Mimi kwenye Programs yangu hii ya Jicho Letu, angalau tumemuita Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndugulile na sasa Waziri wa Habari, Dr. Mwakyembe, maswali yalikuwa mengi muda ulikuwa mfupi ila naomba kukiri udhaifu hata mimi pia ni Lap dog tuu, kwasababu the right to information act inataka tuwaandikie maswali tuwape rasmi lazima maswali yote yangejibiwa.

Hata hivyo bado nina washukuru Dr. Abbas for being available twice at my disposal tukashindwa sisi. Kwa upande wa Dr. Ndugulile kiukweli nilimbwekea ila naye yuko fit sana kukwepa mishale. Hata yeye namshukuru na ni mwana jf mwenzetu ila.... Pia sasa ninamshukru Waziri Mwakyembe kwa kupatikana na ametupatia madini muhimu.

Kitendo cha media ya Tanzania kukubali kuwa lapdog hivyo kushindwa kuitumia position yetu as Mhimili wa Nne, the 4th Estate or The 4th protocol kumepelekea media kudhaurika, kama the Washington Post limewahi kumchoropoa rais fulani Ikulu, media ya Tanzania ingeonyesha uwezo huo kwa kuisaidia serikali kuiambia ukweli wa baadhi ya mipango yake haitekelezeki na kuonyesha matokeo ya serikali kutokusikiliza hoja za serious media, hajafu serikali kweli ikadharau na sasa tunaelekea kwenye hicho media ilichokisema. Kikitokea cha kutokea, ambacho kama serikali ingeshauriwa na kusikiliza, tusinge fika huku tunakokwenda kifika, serikali kama hii ingekuja kuiheshimu media.

Nini Kifanyike, A Way Forward
Asante sana Dr. Mwakyembe kuijua hali yetu na madhila tunayopitia, tunakuomba wewe kama mlezi wa sekta ya habari, please something, Serikali, taasisi, wafadhili, kama inavyowaangalia wahudumu wa Afya, kwa kuwajali kwa hali na mali, pia waijali media, waipe stimulus package, media iwezeshwe iweze kutimiza wajibu wake kikamilifu.

Paskali

Kaka yangu Paskali,
kwa muda mrefu toka JKN ameondoka sekta ya huduma imekuwa kwa kasi sana pasipo uwiano sawa na sekta ya uzalishaji kupitia viwanda.

Sekta ya huduma ni kama real easte, banking, insurance, media, legal, port, logistics ni vitu kama hivyo
Sekta ya ulazima wa uzalishaji (manufacturing) kwa viwanda kukidhi uhitaji wa soko ndani na nje ili service sector ambayo ni suppotive kwa manufacturing ifanye vyema.

Fikiria kidogo kwa mifano mitatu, kama sukari ingezalishwa kwa walau tani laki 7 wakati mahitaji ya ndani ni tani laki 5; bila shaka sekta ya habari na matangazo ingefanya promotion ya kwanini ununue sukari ya "kilimatinde" kwa ujazo wa gm100, gm 250, gm 500.

Sekta ya logistics na distribution watu wangekuwa wanapambana kwanini uwe wakala wa kilimatinde sugar.
Say, tungekuwa na stable sector kuzalisha maziwa na products za maziwa kama maziwa fresh, mtindi, butter, yogurt wingi. Lots promotion za products za maziwa zingefanyika hata kama Covid ingekuwepo; maana bado watu wanakula na kunywa.

Kuna maziwa kama haya toka Oman yanaingia na hayana promotion kwenye any media. Na kuna wakati unayasaka madukani huyapati. Kuna hela inapotea kwa imports kumbe ujanja ni kuzalisha kwa wingi.
1589201870311.png

1589202193470.png
1589202250735.png


1589202020256.png
1589202062661.png

Mzigo hii hapo juu kwa uchache tu, tuna import yote na kuna products katika hizo hakuna kabisa of promo kwa radio, tv, magazeti, twita, instagram au facebook kwa waandishi wa Tanzania.

Sasa basi, JPM anaposema lazima twende kwenye kujenga middle class kwa kutumia viwanda; hata waandishi wa habari wanakosa depth ya analysis maana kuna mambo yanafanyika nchini; media inachukulia poa including ku-import penseli, toothpick.

Hayo mambo yangeshadadiwa sana na media, hata kwa BOT kutoa bank guarantee kwa investments ambazo right away soko lake lipo.

Najua kwa ujumla services sector ita-suffer including media. Ila ili tutoke kwa haraka, chonde chochonde, tumtafuteni huyu mzee wa Chato ili suala la viwanda hasa kwa consumables liwe top priority.



















Wakati Paskali mko Ikulu ninyi wana habari, huyu mzee alisema hivi... Hapa Pasco niambie uko wapi ili tumtafute Msigwa walau tuje na investment ya Sukari kwa kutumia sugar beet kama raw material. Walau tuzalishe hata tani kadhaa.

Tutarejesha mkopo wa uwekazaji na ku-share model kwa wengine nao waingie, kwa soko ambalo lipo wazi kuziba pengp la imports, tutatoa room ya media ku-promote sukari yetu etc etc etc

It breaks my heart baadhi ya biashara including viwanda vingi zinaendeshwa na "wa kuja" na wana roho mbaya kwa jinsi walivyow wabaguzi. Hawana hata nia ya kukupa PPR tangazo maana wanaona utafaidi sana.

Kama vip, twenzetu Chato na project yetu mkononi (ha haaa)
Fred
 
Hili tukio la mkuu wa nchi kukimbizwa kwenda kijijini ni kutangaza kuwa kuna gonjwa la hatari sana.

Tukio la kukimbia toka mjini kutokana na gonjwa ni marudio katika historia ya binadamu katika harakati ya kujiokoa.

Katika muhadhara wa public health katika chuo Kikuu maarufu cha Yale, Prof. Snowden anasimulia.

Hivyo tulioachwa mijini tukio hili tusilichukulie kwa urahisi bali ni ujumbe tosha tuchukue tahadhari kwani mkuu wa nchi ameshauriwa ahame kwa muda toka Dar es Salaam na Dodoma ktk mawe kwani kuna hatari kubwa ya gonjwa hili hatari.

00:00 - Chapter 1. Responses to the Plague and Miasmatism 09:05 - Chapter 2. Individual Measures of Self-Protection and Scape-Goating 18:52 - Chapter 3. Religiosity 25:51 - Chapter 4. Organized Public Health Measures 37:25 - Chapter 5. Did the Public Health Measures Succeed?
Source: Yalecourse
 
Kama siyo " ukanjanja" Pascal angerithi mikoba ya Tido Mhando kwa ubobezi lakini ndio hivyo tena. MC yeye, Mtangazaji yeye, Mwanasheria yeye, Mpiga kampeni yeye, Mgombea ubunge yeye , mwanajeshi yeye nk nk

Na huo ndio ukanjanja wa mtu kutojikita kwenye taaluma!
Duh, mbona kama hili lina ukweli

Ila umenivunja mbavu hapo kwa mwanajeshi.

Anyway, mkuu Pascal unazungumziaje hii hoja ya kada mwaminifu 'Joni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko la kuizindua serikali na Jamii, kuikoa sekta ya media, katika hii vita ya janga la Corona, japo sisi waandishi wa habari ni wadau muhimu sana katika vita hii kama ilivyo kwa madakari, manesi na wauguzi, lakini kiukweli sisi waandishi wa habari, haswa ma freelances, na sekta nzima ya Media "Tunakufa Kuzungu Na Tai Shingoni!", tunaangamia kimya kimya, tunamshukuru Waziri wetu wa Habari, Dr. Harrison Mwakyembe kwa kutambua na kuthamini mchango wetu, lakini kiukweli kabisa, media hatujaweza kutimiza wajibu wetu kikamilifu, serikali yetu, taasisi wezeshi kama TCRA, na jamii kwa ujumla, it needs to do something, to help out the situation, vinginevyo media sio tuu tutashindwa, bali pia tutakwisha...!.

Jumamosi iliyopita mimi nikiwa Dar na Dotto Bulendu akiwa Mwanza, tulifanya mahojiano ya live, mubashara na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe, akiwa Dodoma, katika kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, na tulifarijika sana kwa Waziri Mwakyembe, kutambua mchango wetu, na kutupongeza sisi waandishi wa habari, na madaktari, manesi na wauguzi kwa kazi kubwa tunayoifanya, tangu kuibuka kwa janga la Corona, ila akatusifu zaidi sisi waandishi kuwa ni mashujaa wa ajabu, ambao "Tunakufa Kizungu na Tai Shingoni"...
Msikilize Mhe. Waziri



Tangu kuingia kwa janga hili la Corona, ndani ya kichwa changu nina list ya waandishi wa habari zaidi ya 10, tumewazika wengine kwa kutaarifiana rasmi, wengine kimya kimya, naomba nisiwataje majina humu, nikashutumiwa kutoa siri za marehemu kwasababu karibu kila anayekufa sasa, anahusishwa na Corona, hapa naomba kusisitiza sijsema hao waandishi wa habai wote 10, wamekufa kwa Corona, no, ni waandishi wa habari zaidi ya 10, wamekufa tangu kuingia kwa Corona, hivyo sio lazima wawe wamekufa kwa Corona,
Uzi Maalum wa Waandishi wa Habari na Wafanyakazi wa Media Waliotangulia Mbele Tangu Kuingia kwa Corona ila Sio Lazima Chanzo ni Corona!. - JamiiForums
lakini kiukweli wanahabari, tunachomoka, media zinasinyaa, kamba zinazidi kukaza, kwa kada ya sisi waandishi ma freelancers, ndio usiseme kabisa!, hali sii hali, inabidi serikali, TCRA, taasisi wezeshi na jamii kwa ujumla, kuingilia kati, kuisupport media, ili tuweze kutimiza majukumu yetu kikamilifu vinginevyo...

Waziri Mwakyembe " Kila vita ina jemedari wake, katika vita hii, mimi naamini kabisa, Jemedari tunaye ni Mkuu wetu wa nchi, askari wa mstari wa mbele mimi nawachukulia ni makundi mawili, kwanza ni madaktari wetu na watumishi wote wa afya, lakini wa pili ni wana habari". "Wanafanya kazi ambayo, wanaipa jamii elimu, tumefika wapi, na kunaendelea nini, hivyo kwanza naomba kuwapongeza wanahabari, wanafanya kazi nzuri ya kuhabarisha jamii, nchi iko kwenye amani, kila siku tunahabarishwa kinachoendelea, japo taarifa nyingine ni za kugofya sana"

Mwakyembe "Baadhi ya taarifa za Corona, haziendani na mwelekeo wa Jemedari Mkuu, Jemedari Mkuu alichukua hatua moja nzuri sana, tukikabiliwa sana na woga, wasiwasi, dukuduku, watu wengi watakufa kwa dukuduku, wasiwasi na woga"
"Vita ni vita tuu, ukisikia tuu mabomu yanarindima kwa mbali wewe huku unaanguka kwa uoga kwa kudhani yameishakuangamiza".

Mwakyembe "Kwa ujumla kazi ambayo mnaifanya wanahabari ni nzuri, na mimi nawapongeza kwa kazi hii, na mnafanya kazi katika mazingira magumu sana, na hilo lazima tuliangalie wote Watanzania katika hali ya uhalisia. Wakati wengi tunajifungia ndani muda mwingi, kama mimi mmenifuata hapa nyumbani, lakini wana habari, kazi yao ni kutoka nje, wako msatari wa mbele kwenye vita, na mimi nimesikitika kwa muda mrefu, wamiliki wa vyombo vya habari, wana wa expose waandishi wao, wanawaacha wazi, kuweza kupata matatizo mbalimbali, wanatoka ofisini bila barakoa, sanitiser, bila usafiri, nimepita kwenye newsroom, watu wamejaa, wana changia vifaa, siwalaumu, lazima kwanza tuwashukuru kwa kazi nzuri wanayoifanya katika mazingira magumu.

Baada ya Waziri Mwakyembe kulijua hili, sasa naomba kuendesha darasa hili.
1. Hatua ya Kwanza ni kukuelimisha media ni nini na kazi za media.
Media ni vyombo vya habari vinavyotumika katika upashanaji habari. Vyombo hivi vimegawanyika katika makundi mawili, ambazo ni Traditional Formal Mass Media, vyombo rasmi vya habari ambavyo ni Redio, TV na Magazeti, na uhabarishaji hufanywa na waandishi wa habari waliosomea yaani professionals. Kufuatia maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia na utandawazi, kumeibuka modern media ambazo ni online media, na social media zikiwemo Blogs, Online Forums, Facebook, Instagram, Twitter, YouTube, WhatsApp groups etc, ambapo every Tom, Dick and Harry ni mwandishi wa habari, hii inaitwa citizens journalism. Japo TCRA inazitambua online media na kuzisajili, na ma bloggers na Online TV wanapewa press cards, its very unfortunate Waziri Mwakyembe haitambui social media kama ni media, ameiita ni media ya kijiweni!.

2. Kazi za Media
Traditional media ilikuwa na kazi kuu tatu
1. Kuhabarisha Jamii
2. Kuelimisha Jamii
3. Kuburudisha Jamii
Kwa modern Media zimeongezeka
4. Watchdogs of the society, Ku act as 4th Estate

1.Jukumu la 1 la Uhabarishaji.
Kwenye jukumu kuu la kwanza la media kwenye uhabarishaji, Media imetimiza jukumu lake kikamilifu na nimepongeza hatua ya serikali kuweka list ya wazungumzaji rasmi 5 wa Corona kitaifa ambao ni
  1. Rais wa JMT
  2. M/Rais
  3. Waziri Mkuu
  4. Waziri wa Afya
  5. Msemaji Mkuu wa serikali.

  1. Nikasema hatua hii ni mzuri ili taifa lipate taarifa moja iliyonyooka, kama kila mtu ataachwa ajisemee itakuwa chaos, utaratibu huu unaitwa restrictive media reporting na hutumika hata wakati wa vita.
  2. Information is a two way traffic, serikali inatoa tuu taarifa, media ilikuwa ina wajibu wa kufikisha taarifa za serikali kwa umma, lakini hakuna utaratibu wowote wa serikali kupokea mrejesho hao wananchi wanaopelekewa taarifa na maelekezo ya serikali jee wanasemaje?. Wanatekeleza?, Wananawa kwa maji tiririka?. Wanafanya social distancing?. Kwenye eneo hili, media hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu.
  3. Kazi ya hao wazungumzaji wanne ni kutoa update ya Corona. Kwenye eneo hili la media kutoa taarifa za serikali za Corona, media tumetimiza wajibu wetu kikamilifu kabisa na tunastahili pongezi za dhati.
  4. Lakini ukweli Corona ni zaidi ya updates, kila vizara, kila idara, kila Taasisi itakuwa affected na Corona hivyo mawaziri wengine na wakuu wengine wote wana wajibu wa kuizungumzia Corona haswa how to mitigate the after effects, huko sio kutoa update huko ni kuisaidia serikali na Watanzania jinsi ya kukabiliana na madhara ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya Corona. Kwenye eneo hili la kutoa taarifa nyingine zozote kuhusu madhara ya Corona kwa sekta nyingine zote, media hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu.
  5. Watoa taarifa wa serikali wanaisoma taarifa ya maandishi na kuwasomea media hakuna any room kwa media yoyote kuuliza kupata ufafanuzi, matokeo yake media kazi yake ni kulishwa tuu habari, spoon fed, na media kazi yake ni kumeza tuu hizo, habari, hukuna kuzichakata, hakuna news analysis, hakuna news relevance alimradi Msemaji ni serikali na serikali imesema.

2. Jukumu la Pili la Uelimishaji Jamii
Hili pia media imejitahidi ila bado, Watanzania wanahabarishwa vizuri kuhusu Corona lakini kazi ya uelimishaji bado inafanywa kwa kiwango cha chini, hivyo kuna watu wananawa kwa maji tiririka kwasababu ni lazima, lakini kwenye social distancing bado, misongamano bado ipo kila mahali.
Zaidi ya kuripoti zile updates za Corona, hakuna TV yoyote, redio yoyote, au magazeti yenye dedicated Program kuhusu uelimishaji umma wa Corona zaidi ya yale matangazo ya Corona.
Hivyo kwenye jukumu la media za Tanzania katika uelimishaji umma kuhusu Corona bado sana.

Kwa vile Corona haina dawa, Watanzania walipaswa waelimishwe hao wagonjwa huko kwenye vituo walikotengwa wanafanywa nini hadi wengine wanapona kabisa na kuruhusiwa ili wenye uwezo wawatibie watu watu kwa kuzua na sio kusubiri watu waugue wazidiwe wakarudikane kusubiria... wakati watu wangeelimishwa huduma ya kwanza ingeanzia nyumbani.

There's a lot of education inputs kutoka nje kuliko kutoka ndani. Serikali imetoa list ya wataalamu official watakao elimisha kuhusu Corona, sijabahatika kuona hata kipindi kimoja cha wataalamu hao

Vituo vya Redio na TV vitenge dedicated Program za uelimishaji umma kuhusu Corona. Hao wataalamu wawe pro active kwenda kwenye media kuelimisha umma.

The regulator, TCRA, atoe muongozo kwa vyombo vyote vya utangazaji na mitandao ya kijamii kuandaa vipindi elimishi kuhusu Corona

Wakati Wazungu wamehangaika kutafuta tiba, sisi tungewatumia wataalamu wetu wote kuanzia madaktari, tiba mbadaka, tiba asili, ma sangoma, waganga hadi Babu wa Samunge kukijaribishia kikombe.

Hao wachungaji wenye uwezo wa nguvu za uponyaji, waruhusiwe mahospitalini ili tushuhudie uwezo wa nguvu zao na sio kuwakamua masikini Watanzania kwa kusingizio cha kufanya miujiza, Wachungaji wenye uwezo wa kuponya kwa miujiza wajitokeze kuonyesha uwezo wao na serikali iwaruhusu, kama alivyojitokeza Askofu Gwajima, aruhusiwe tuone uwezo wake na miujiza ya Mungu katika uponyaji.

Unapo deal na gonjwa ambalo halina tiba na kuna wagonjwa wamezidiwa mahututi na hatimaye watakufa tuu, what is wrong to turn them into Guinea pigs and test them, we may save them, hata kama kwa kuwajaribishia hizo tiba mbadala na bado wakafa, let it be, at least tumejaribu, hata tusinge jaribu, they were going to die tuu anyway. Let's try to do anything something kuliko doing nothing.

3. Jukumu la 3 la Media ya Tanzania Kubudisha Jamii
Kazi ya tatu ya media ni kuburudisha jamii. Kwenye eneo hili pia media ya Tanzania haijatimiza wajibu wake kikamilifu.
Kwa vile Corona ni janga, na kufuatia kilichotokea Wuhan, Italy, UK na US, Corona imetisha na kuogofya, media nazo zikalipokea hivyo hivyo. Shujaa wa eneo hili ni rais Magufuli aliposema tusitishane, ka Corona ni ka ugonjwa kadogo tuu, tena sio kirusi ni shetani disguise as kirusi, tukamkabidhi kwa Mungu kiboko ya shetani!.
Pamoja na mabalaa yote ya janga la Corona, pia kuna mazuri ya Corona, kuna positives za Corona zilipaswa kuangaliwa. Mwana FA na meneja wa Diamond, Salaa did. Kuna watu wanapona wanaruhusiwa. Media ilipaswa kuwatafuta madaktari waliofanya miujiza tufanye human interest stories za mazuri ya Corona. Kuna watu wamepiga pesa kwa kuziangazia fursa za Corona, hata Diamond alichofanya akiwa quarantine ni jambo zuri, tusiizungumze Corona kwa ubaya tuu, tuizungumze kwa wema. Italy Wazee ni wengi mno na wanaishi sana, hivyo Corona ni kama mkombozi fulani kwa blessing in disguise kwa mifuko ya hifadhi za jamii kwa..., ame fykelea...

Sisi baadhi ya familia, baba na mama ni working class, familia yangu nina watoto 9, wamepishana miaka 2, the oldest ni 24, 22, 20, hawa wako vyuo. Then kuna 18, 16 na 14 wako sekondari, kisha kuna 12, 10 na 8 wako primary. Ukiondoa Christmas Day, there is no any other time watoto wote wako nyumbani. Kwenye Corona wote wamerudi home, baba ni mwandishi wa habari wa mikutano, warsha, seminar, makongamano na events, zimesimamishwa, niko home. Wife ni mfanyabiashara wa safari za nje, zimesimamishwa!, nyumbani kuna Dada wa jikoni, dada wa usafi, kaka wa garden, feeding a family of 15 is not a joke. Ukishinda nyumbani na watoto ndipo unagundua kiukweli hawa wadada wa kazi, walipaswa kulipwa vizuri!.

Hivyo Corona has lots and lots of human interest stories na sio habari tuu za ku stigimize kwa idadi inaongezeka, lakini wanaopona hatuwazungumzi. Kutembelea kambi za quarantine na ku file stories about life in quarantine zitakuwa very interesting stories.

4. Jukumu la 4 la media ya Tanzania as a Watchdogs of the Society kwe janga la Corona
Kazi ya Watchdogs ni wale mbwa wanaofanya kazi ya ulinzi, kazi yao ni kubweka tuu ili kumjulisha mwenye nyumba something is not right.

Hawa mbwa pia wapo mbwa wa aina 3,
1. Shepards Dogs habweki ana ng'ata.
2. Barking Dogs kazi yake ni kubweka tuu ila hang'ati!
3. Lap Dogs kazi yake ni kuchezesha mkia na kukamba lamba, habweki wala hang'ati!

Kwenye janga hili la Corona, the Tanzania media has failed this nation katika role ya Watchdogs.
Toka Corona inaanza kule Wuhan ije December 2019 tungekuwa na serious media, tungeanza kubweka ili kuiandaa serikali yetu for preparedness kwa Corona, angalieni China ilipolipuka tuu Wuhan, mpaka imedhibitiwa haikufika Beijing na wala haikuingia Japan.

Tanzania ndio nyumba yetu, baba mwenye nyumba ni rais wetu na serikali yake, wao wako ndani wamelala, sisi media ndio mbwa ambao tuko macho tunalinda nyumba. Corona ndio mwizi anayekuja kutuibia nyumbani kwetu.

Media ya Tanzania ingekuwa ni Sheppard dog, ingefanya kazi kama gazeti la The Washington Post wakati wa kashfa ya Watergate, naomba tukiri udhaifu kwenye complex issue kama hii ya Corona, media zote za Tanzania hakuna hata moja yenye uwezo kuajiri ma medical journalist wa kuandika story za kina kuhusu Corona ambazo zingeisaidia serikali yetu. Angalieni CNN na Dr. Sunjay Gupta.
Hivyo media ya Tanzania kwenye kuisaidia serikali kwenye hili la Corona ni zero. Naamini kuna madaktari wazuri tuu ambao wanaopenda kuwa watu wa media kama alivyo Dr. Maro kwa Clouds.

Tukija yule mbwa wa pili wa barking Dogs, kiukweli mainstream media pia has failed this nation on this role. Kazi hapa ni kubweka tuu ili kumuansha mwenye nyumba. Media ambayo imelitenda hili ni JF pekee.
Pale rais wa nchi anaposema ka Corona ni ka ugonjwa kadogo tuu na serious media ambayo ni barking Dogs zilipaswa zibwekwe.

Rais Magufuli na serikali yake walipaswa wasaidiwe na media kwa kuwaonyesha good practices elsewhere ambazo zimesaidia.

Rais Magufuli aliporuhusu mikusanyiko ya nyumba za ibada, serious media ilipaswa i bweke kwa kuonyesha kama Roma wenyewe kwenye Ukatoliki wamefunga makanisa, Saudi Arabia wenye Uislamu wamefunga misikiti who are we?. Media tulipaswa kuwaumbua viongozi wa dini wanaohemea sadaka hata kwa kuhatarisha maisha ya watu!.

Hapa Tanzania tulipaswa kuwa na strong independent media yenye uwezo wa kumweleza rais Magufuli na serikali yake kuwa baadhi ya hatua anazosita kuchukua ikiwemo kuendelea kuruhusu mikusanyiko ya nyumba za ibada is wrong. Media ionyeshe jinsi Mungu alivyo Omnipresent yuko popote na mikusanyiko ya nyumba za ibada sio miongoni mwa mikusanyiko muhimu. Kwenye hili angalau sisi jf tulisema.

Kwenye hili media ya Tanzania ni just lap Dogs!. Kazi ya mainstream media zetu haswa za electronics ni kuchezesha tuu mkia na kulamba lamba kila kinachofanywa na serikali, hakuna analysis, hakuna critics na mwendo wa kusifu tuu na kupiga makofi.

Mimi kwenye Programs yangu hii ya Jicho Letu, angalau tumemuita Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndugulile na sasa Waziri wa Habari, Dr. Mwakyembe, maswali yalikuwa mengi muda ulikuwa mfupi ila naomba kukiri udhaifu hata mimi pia ni Lap dog tuu, kwasababu the right to information act inataka tuwaandikie maswali tuwape rasmi lazima maswali yote yangejibiwa.

Hata hivyo bado nina washukuru Dr. Abbas for being available twice at my disposal tukashindwa sisi. Kwa upande wa Dr. Ndugulile kiukweli nilimbwekea ila naye yuko fit sana kukwepa mishale. Hata yeye namshukuru na ni mwana jf mwenzetu ila.... Pia sasa ninamshukru Waziri Mwakyembe kwa kupatikana na ametupatia madini muhimu.

Kitendo cha media ya Tanzania kukubali kuwa lapdog hivyo kushindwa kuitumia position yetu as Mhimili wa Nne, the 4th Estate or The 4th protocol kumepelekea media kudhaurika, kama the Washington Post limewahi kumchoropoa rais fulani Ikulu, media ya Tanzania ingeonyesha uwezo huo kwa kuisaidia serikali kuiambia ukweli wa baadhi ya mipango yake haitekelezeki na kuonyesha matokeo ya serikali kutokusikiliza hoja za serious media, hajafu serikali kweli ikadharau na sasa tunaelekea kwenye hicho media ilichokisema. Kikitokea cha kutokea, ambacho kama serikali ingeshauriwa na kusikiliza, tusinge fika huku tunakokwenda kifika, serikali kama hii ingekuja kuiheshimu media.

Nini Kifanyike, A Way Forward
Asante sana Dr. Mwakyembe kuijua hali yetu na madhila tunayopitia, tunakuomba wewe kama mlezi wa sekta ya habari, please something, Serikali, taasisi, wafadhili, kama inavyowaangalia wahudumu wa Afya, kwa kuwajali kwa hali na mali, pia waijali media, waipe stimulus package, media iwezeshwe iweze kutimiza wajibu wake kikamilifu.

Paskali



Poleni sana na mlipwe kwa kazi zenu na tuombee kampuni ziwape matangazo kwenye kazi zenu. Sio vizuri kutoa kazi bure kila siku
 
Mimi si walaumu waandishi wa habari bali system ya nchi. Naamini waandishi wana uwezo mkubwa wa kutafuta habari na kufanya analysis lakini kwa hali halisi ya nchi yetu hilo ni gumu. Kwa vile bado demokrasia hatujaweza kuifuata kikamilifu waandishi endeleeni hivyo hivyo kusifia musizitafutie familia zenu matatizo. Hawa viongozi ni makatili sana wao wanawaza matumbo yao tu hivyo hawaoni tabu kutoa uhai wenu. Si tumeona waandishi mahiri walipojaribu kutafuta habari ama kufanya analysis nini kimewapata. Wengine wamepotea na wengine kusweka rumande na sisi wananchi tulibweka wiki mbili tukawasahau. Paskali wewe angalau unatumia real id ila hao wanaokulaumu humu wanatumia fake id.
 
24 May 2016
Public Health Care Communication and Advocacy Systems - Prof. Dr. John Kabudi, Ph.D. AUSN


Public Health Care Communication and Advocacy Systems - Prof. Dr. John Kabudi, Ph.D. AUSN Visiting Professor of Indigenous Knowledge Systems (Faculty of Law, University Dar es Salam, Tanzania) - Public Health Care Communication and Advocacy Systems. Explore scholarships for postgraduate study at American University of Sovereign Nations

Source : American University of Sovereign Nations
 
Pascal Mayalla,

Prof. P. Kabudi : Mtu ni Afya, Mitishamba, Dawa Asili, Tiba-Lishe, Mahali pasipo Daktari ktk muda huu wa Covid-19

Unaona video clip hapo juu Prof. Palamagamba Kabudi ambaye pia ni mwandishi wa habari mstaafu akielezea umuhimu wa kitu kinachoitwa Afya ya Jamii ambayo kazi kubwa wenzetu mabwana / bibi Afya wa halmashauri, wilaya na miji wanaifanya kuhakikisha makaazi yeti hayawi hatari kwetu sisi wenyewe na jirani zetu pia.

Ningependa kuona waandishi wa habari kuwahoji hawa wataalamu wa Afya ya Jamii (Public Health) wanavyopanga na kutekeleza mikakati hii ya kupambana na Covid-19 wakishirikiana na matabibu, waganga, wanasiasa na wadau kama sekta ya Uandishi habari ili tuishinde vita hii.

Hivyo kama Prof. Palamagamba Kabudi kila siku anatukumbusha tusome historia na kuacha kulaumu mfano mbona Prof. Palamagamba Kabudi kenda Madagascar wakati Ummy Mwalimu yupo n.k kumbe Prof. Palamagamba Kabudi ana mambo mengi zaidi ya fani ya sheria na ndiyo maana tunamuona mstari wa mbele ktk hata masuala ya Public Health kupambana na Covid-19
 
Back
Top Bottom