Tetesi: Conspiracy Theories: TRA na Ukadiriaji Kodi wa Kukomoana na Ukabila

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,240
4,466
Juzi wafanyabiashara jijini Mwanza wamelalamika kwamba biashara zinafungwa kwa sababu makadirio ya kodi ni makubwa kuzidi uhalisia.

Leo nilikuwa Kariakoo, nimewasikia wafanyabiashara fulani wakimjadili mfanyabishara mmoja waliyemuita Iwawa (naamini sikosei jina). Wanadai katika vikao vya wafanyabiashara wa Mbeya na TRA mwaka jana, Iwawa aliwalaumu TRA Mbeya kuwabambikia kodi wafanyabiashara wazawa wa Mbeya kama wanakomoa kwa sababu hawana machungu na biashara zao, na kwamba hiyo ni sababu kubwa ya wafanyabiashara wengi wenye asili ya huko kutowekeza biashara zao kwenye mji wa Mbeya. Inadaiwa ndani ya wiki kadhaa baada ya hicho kikao Iwawa alipelekewa madai ya kodi yanayozidi milioni mia sita (600,000,000/=).

Inawezekana ni tetesi tu, lakini kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusiana na makadirio ya kodi kwa baadhi ya miji, huku wafanyabiashara wa kabila fulani wakidaiwa kutosumbuliwa sana na haya makadirio.

Huwezi shughulikia tetesi zote, lakini tetesi kama hizi zinapaswa kuchunguzwa kwa ustawi wa Taifa.
 
Mkuu sio Iwawa peke yake na sio Mbeya peke yake ambapo hii tabia ipo. Arusha na Moshi biashara zinafungwa kila kukicha kwa sababu ya upuuzi huo huo wa kumkomoa mfanyabiashara kupitia kodi.

Ni ukosefu mkubwa wa ubunifu kuanzia wizara ya fedha mpaka huko TRA. Unapomuumiza mfanyabiashara wa kati, unaikomoa jamii nzima inayomzunguka. Unaua uhai wa familia, na unaowaumiza watakachofanya ni kuichukia serikali.
 
Asikwambie mtu jamaa wa TRA wengi wao hawana hata magenge na kimsingi ukiwa na issue yoyote ya kikodi ambayo ni complex wao ni rahisi sana kukushauri ufunge biashara, kunatofauti kubwa sana kati ya mtu aliekulia kwenye background yenye biashara anaeweza kuchukulia maswala ya kibiashara vizuri zaidi
 
Kinachotuumiza watanzania na waafrika hatuweki hesabu zetu wazi. Kama mtu unatunza hesabu ya biashara yako vizuri huwezi kubambikiziwa kodi. Tatizo lipo watu wanaogopa kuweka wazi biashara zao kwa hofu ya kulipa kodi kubwa wanaishia kubambikiwa kwa makadirio ya macho tu ya TRA. Ni bora ukalipa kodi kubwa lakini sahihi kuliko ukambabikiziwa kodi kubwa kwa kuogopa kulipa sahihi. Ukiwa na data zote, kodi hukatwa kwenye mahesabu sio kwa macho ya TRA. Tujifunze kuweka wazi biashara zetu. Usiri unafanya ukifa hata biashara zako zife maana sio mtoto au mke anayejua hesabu zako, wataendeshaje?
 
Mkuu sio Iwawa peke yake na sio Mbeya peke yake ambapo hii tabia ipo. Arusha na Moshi biashara zinafungwa kila kukicha kwa sababu ya upuuzi huo huo wa kumkomoa mfanyabiashara kupitia kodi.

Ni ukosefu mkubwa wa ubunifu kuanzia wizara ya fedha mpaka huko TRA. Unapomuumiza mfanyabiashara wa kati, unaikomoa jamii nzima inayomzunguka. Unaua uhai wa familia, na unaowaumiza watakachofanya ni kuichukia serikali.
Maumivu ni Kwa wote ni kama chain hata huyo anaeumiza wenzie nao anaathirika pale makusanyo yanapoathirika
 
Wananiacha hoi tu pale wanapojushauri ufunge biashara badala ya kukishauri njia nzuri ya kuondokana na huo mkwamo, nadhan huko vyuoni kuna somo la kumshauri mteja afunge biashara, halaf tra wote wana vitabia vinavofanana
 
Ukifanya audit mapema na kuwapelekea huwezi pigwa kodi kubaa hivo
Sisi no waoga sana wa kufanya audit

Mungu ni Pendo
 
Haya ni kweli mkuu na jamaa kaamua kuhama kabisa mbeya....hii swrikali katiri sn ila wasukuma ndo eti wapiga kura....laana ya ccm hii
Baba wa taifa ambaye ccm walishaacha kumwamini alionya sn kuhusu dhambi ya ubaguzi na huyu phd feki anafanya ubaguzi tena wa wazi kabisa
 
Kinachotuumiza watanzania na waafrika hatuweki hesabu zetu wazi. Kama mtu unatunza hesabu ya biashara yako vizuri huwezi kubambikiziwa kodi. Tatizo lipo watu wanaogopa kuweka wazi biashara zao kwa hofu ya kulipa kodi kubwa wanaishia kubambikiwa kwa makadirio ya macho tu ya TRA. Ni bora ukalipa kodi kubwa lakini sahihi kuliko ukambabikiziwa kodi kubwa kwa kuogopa kulipa sahihi. Ukiwa na data zote, kodi hukatwa kwenye mahesabu sio kwa macho ya TRA. Tujifunze kuweka wazi biashara zetu. Usiri unafanya ukifa hata biashara zako zife maana sio mtoto au mke anayejua hesabu zako, wataendeshaje?
Hakuna mfanyabiashara asiyetunza kumbukumbu sahihi. Tatizo ni kuwa anayeamua kuwa kumbukumbu hii ni sahihi ndo huyo huyo mshika kodi. Hata iwe sahihi na wazi kiasi gani, wakitaka kukuliza wanakuliza tu.
 
Hakuna mfanyabiashara asiyetunza kumbukumbu sahihi. Tatizo ni kuwa anayeamua kuwa kumbukumbu hii ni sahihi ndo huyo huyo mshika kodi. Hata iwe sahihi na wazi kiasi gani, wakitaka kukuliza wanakuliza tu.
Tanzania hii? Mauzo na manunuzi tunaweka wazi? mtaji na turn over ya bidhaa tunaweka wazi? hii Tanzania? labda nchi nyingine
 
Juzi wafanyabiashara jijini Mwanza wamelalamika kwamba biashara zinafungwa kwa sababu makadirio ya kodi ni makubwa kuzidi uhalisia.

Leo nilikuwa Kariakoo, nimewasikia wafanyabiashara fulani wakimjadili mfanyabishara mmoja waliyemuita Iwawa (naamini sikosei jina). Wanadai katika vikao vya wafanyabiashara wa Mbeya na TRA mwaka jana, Iwawa aliwalaumu TRA Mbeya kuwabambikia kodi wafanyabiashara wazawa wa Mbeya kama wanakomoa kwa sababu hawana machungu na biashara zao, na kwamba hiyo ni sababu kubwa ya wafanyabiashara wengi wenye asili ya huko kutowekeza biashara zao kwenye mji wa Mbeya. Inadaiwa ndani ya wiki kadhaa baada ya hicho kikao Iwawa alipelekewa madai ya kodi yanayozidi milioni mia sita (600,000,000/=).

Inawezekana ni tetesi tu, lakini kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusiana na makadirio ya kodi kwa baadhi ya miji, huku wafanyabiashara wa kabila fulani wakidaiwa kutosumbuliwa sana na haya makadirio.

Huwezi shughulikia tetesi zote, lakini tetesi kama hizi zinapaswa kuchunguzwa kwa ustawi wa Taifa.
Mkuu kwa nini unasema hii ni conspiracy theory,mbona sio.Au unapenda saana hiyo concept ya conspiracy theories.Kama unaipenda,basi use it correctly.
 
Kinachotuumiza watanzania na waafrika hatuweki hesabu zetu wazi. Kama mtu unatunza hesabu ya biashara yako vizuri huwezi kubambikiziwa kodi. Tatizo lipo watu wanaogopa kuweka wazi biashara zao kwa hofu ya kulipa kodi kubwa wanaishia kubambikiwa kwa makadirio ya macho tu ya TRA. Ni bora ukalipa kodi kubwa lakini sahihi kuliko ukambabikiziwa kodi kubwa kwa kuogopa kulipa sahihi. Ukiwa na data zote, kodi hukatwa kwenye mahesabu sio kwa macho ya TRA. Tujifunze kuweka wazi biashara zetu. Usiri unafanya ukifa hata biashara zako zife maana sio mtoto au mke anayejua hesabu zako, wataendeshaje?
"Hivi wewe ni mfanyabiashara au unaliskia tu neno biashara, au na wewe Ni miongoni mwa wale wanakabila lisiloguswa?? Ungeguswa na huu mwiba wa makadilio mabovu ya kodi nadhani usingeongea maneno ya kidwanzi kama haya Sisi wahangwa acha tuongee yaliyotukuta na sio izo theories ambazo mlikua mnazikalili mzumbe na Arusha ili muwafurahishe maprofesa msipate sap halafu mje kuajiriwa BOT(katika njozi zenu)
 
"Hivi wewe ni mfanyabiashara au unaliskia tu neno biashara, au na wewe Ni miongoni mwa wale wanakabila lisiloguswa?? Ungeguswa na huu mwiba wa makadilio mabovu ya kodi nadhani usingeongea maneno ya kidwanzi kama haya Sisi wahangwa acha tuongee yaliyotukuta na sio izo theories ambazo mlikua mnazikalili mzumbe na Arusha ili muwafurahishe maprofesa msipate sap halafu mje kuajiriwa BOT(katika njozi zenu)
Anaongea upuuzi huyo, itakuwa hata kibanda cha pipi hana
 
Lkn sheria ya kodi inatoa room kwa mfanya biashara kujikadiria. Lkn kwasababu ya kupenda sifa watakuwekea figisu mpaka ufunge biashara.kwakuwa nina issue nyingine za kipato nikaamua kufunga ili nione nani ataathirika, saivi nimebadili biashara hata hizo wanazikosa
 
Ukipita mpakani ndiyo watakupigaaa, wanashirikiana sana na wenye mabasi ya abiria kuumiza wafanyabiashara. Kondakta akikadiria pesa kubwa ukagomesha kumlipa hiyo pesa tambua kuwa border lazima uchome akaunti.
Na mbaya zaidi wamejenga mazingira ya negotiation na kondakta badala ya kufanya makubaliano na wenye mizigo. Biashara zinakufa sababu ya ubabe wa hao watu...
Tanzania ya uchumi wa kati ni ndoto tena ya mchana kabisa.
 
Back
Top Bottom