Connect dots hapa kuhusu Jaji Mujulizi na Kikwete

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,983
Habari wadau,

Je, unaikumbuka kampuni ya mawakili ya "IMMA"?

Kampuni hii ndio iliosajili kampuni ya Deep Green Finance inayotuhumiwa kuchota mabilioni kutoka BOT na kumuwezesha mkulu kuingia magogoni.

Kirefu cha IMMA inasemekani ni, I inasimami Ishengoma, M inasimamia Masha, M nyingine Mujulizi na A-Advocates.

Baadae Mujulizi aliteuliwa kuwa Jaji na kuhusu Masha nafikiri unajua.

Sasa leo huyu jaji Mujulizi ndio anatakiwa kuwajibishwa; je hii itawezekana? Tafakari.

Mbali na kutuhumiwa kuchota mabilioni kupitia Deep Green Finance. Pia mtu aitwae Ridhiwan alienda kufanya mazoezi ya sheria(externship) katika kampuni hii ya IMMA.
 
Ni Mtandao wa Kufa Mtu, kwa akili za hakina Kibajaji (Mb) wa Dodoma na Shampa Mshama (Mb) wa Nkenge ambao kila jambo wao wanaliangalia kwa jicho la chuki za kisisa, si rahisi kuunganisha dot...Kumb: Kuunganisha Dot... ni kazi Pevu.

Hakuna lolote wala Chochote wizi na ufisadi mnono ktk nchi yetu hii unaenda Kimtanadao. Taifa hili hatuna sababu ya Kulalamika bali tujilahumu wenyewe kwani tumekubali kuendelea kuibiwa na kuwapigia makofi wezi.

Solution: Kura zetu 2015, ndizo zitaweza kulinusuru taifa hili, eti mtu kapewa 1.6b kwa kutoa ushauri wa kisheria,hivi hii ni sawa kweli si kila mtu angesoma sheria maana hiyo ndyo professional yenye utajiri.

CCM wameliuwa Taifa, Tuchukue hatua kulinusuru kwa njia ya kura za HAPANA kuanzania Katiba ya Chenge (Fisadi # 1) na pia tuseme NDIYO kwa UKAWA kwenye general election 2015, maana bila hivyo tutakuja kupigana muda si mrefu.
 
Alianza Muhongo kumuweka kiporo Rais kwa kumuambia akijiuzuru "nchi itatikisika"
Baadaye akaja Rais akatuambia yeye ndo anayemuweka kiporo Muhongo.

Inaonekana hawa jamaa kila mtu ana kete mkononi na ukichunguza utendaji wa Rais ni wa hofuhofu sana kwa sababu hajui hao wanaodai nchi itatikisika wanaweza kumwaga issue yote hadharani serikali nzima ikaanguka.

Mwakyembe ana kete yake aliyoamua kutuficha kwenye ripoti ya RICHMOND ili kuiokoa serikali yote isianguke.

Filikunjombe ana kete yake, akawaonya wabunge tafadhali tusimuingize mkuu maana nchi itayumba.
Mama Tibaijuka, wewe hukuwa na kete ya kukulinda usijiuzuru kama wenzako? au uliandaliwa kwanza kisaikologia kabla hujatemwa?
 
Mujulizi in jaji kwa hilo jaji mkuu na tume ya mahakama inaweza kushughulika nae. Lakini huyu pia ni katibu wa. Tume ya kurekebisha sheria. Hapa Rais hana kizuizi cha kutengua uteuzi wake. Akiachwa hapo in hatari.
 
Habari wadau,

Je,unaikumbuka kampuni ya mawakili ya "IMMA"?

Kampuni hii ndio iliosajili kampuni ya Deep Green Finance inayotuhumiwa kuchota mabilioni kutoka BOT na kumuwezesha mkulu kuingia magogoni.

Kirefu cha IMMA ni,I inasimami Ishengoma,M inasimamia Masha,M nyingine Mujulizi na A-Advocates.

Baadae Mujulizi aliteuliwa kuwa Jaji na kuhusu Masha nafikiri unajua.

Sasa leo huyu jaji Mujulizi ndio anatakiwa kuwajibishwa na mamlaka yake ya uteuzi;je hii itawezekana?Tafakari.

Mbali na kutuhumiwa kuchota mabilioni kupitia Deep Green Finance,pia mtu aitwae Ridhiwan alienda kufanya mazoezi ya sheria(externship) katika kampuni hii ya IMMA.

Hio ni summary tu,ukitaka habari kamili tafuta gazeti la MAWIO la Alhamisi,Desemba 25-31,2014, kisha nenda ukurasa wa 4 utakutana na makala ya mwandishi Nyaronyo Kicheerem

Wacha uongo, wewe kila uongo unaolishwa unakuja kuutupia hapa, hata hutumii akili yako hata kiduchu basi, Mbona Ruhangisa hujamtaja, au na yeye si jaji? soma:


Azimio la Tano: Linasomeka; “Bunge linaazimia kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aunde Tume ya Kijaji ya Uchunguzi kuchunguza utovu wa maadili dhidi ya Jaji Aloysius Mujulizi na Jaji Profesa Eudes Ruhangisa wa Mahakama Kuu ya Tanzania”

Azimio hili nimelipokea, tumelijadili hata hivyo, itabidi tufuate utaratibu wa kikatiba na kisheria wa kushughulikia masuala ya namna hiyo. Inatakiwa suala kama hili lianzie kwenye Mhimili wa Mahakama yenyewe na siyo kwa Rais au Bunge. Tume ya Mahakama ndiyo yenye mamlaka ya kumtaka Rais aunde Tume ya Kijaji ya kumchukulia hatua Jaji yeyote pale inaporidhika kuwa amepoteza sifa za kuendelea kufanya kazi hiyo. Nashauri suala hili tumuachie Jaji Mkuu wa Tanzania alishughulikie atakavyoona inafaa.

Wala halishghulikii yeye kawawwachia wenyewe mahakama na kaelezea kawaida yake huwaje, majaji watatu, mmoja kutoka nje ya nchi na huyo wa nje ya nchi ndiye anakuwa kiongozi wa hao wengine.

Kikwete angeamuwa yeye si ndiyo ingekuwa mwao. Hapo haingilii Mhimili wa mahakama na mnakuja kudanganya eti "ndio anatakiwa kuwajibishwa na mamlaka yake".


Hamna hata haya?
 
Mujulizi in jaji kwa hilo jaji mkuu na tume ya mahakama inaweza kushughulika nae. Lakini huyu pia ni katibu wa. Tume ya kurekebisha sheria. Hapa Rais hana kizuizi cha kutengua uteuzi wake. Akiachwa hapo in hatari.

Kawawachia mahakama, washughulikie kimahakama, na si huyo pekee na Jaji Ruhangisa jee, mbona mpo kimya?
 
Mijitu mingine haifikirii wala kujiuliza kabla ya kupost. Inapost tu. Nyambaaaaafuuuuuu@salary slip
 
Ni Mtandao wa Kufa Mtu, kwa akiri za hakina Kibajaji (Mb) wa Dodoma na Shampa Mshama (Mb) wa Nkenge ambao kila jambo wao wanaliangalia kwa jicho la chuki za kisisa, si rahisi kuunganisha dot...Kumb: Kuunganisha Dot... ni kazi Pevu.

Hakuna lolote wala Chochote wizi na ufisadi mnono ktk nchi yetu hii unaenda Kimtanadao. Taifa hili hatuna sababu ya Kulalamika bali tujilahumu wenyewe kwani tumekubali kuendelea kuibiwa na kuwapigia makofi wezi.

Solution: Kura zetu 2015, ndizo zitaweza kulinusuru taifa hili, eti mtu kapewa 1.6b kwa kutoa ushauri wa kisheria,hivi hii ni sawa kweli si kila mtu angesoma sheria maana hiyo ndyo professional yenye utajiri.

CCM wameliuwa Taifa, Tuchukue hatua kulinusuru kwa njia ya kura za HAPANA kuanzania Katiba ya Chenge (Fisadi # 1) na pia tuseme NDIYO kwa UKAWA kwenye general election 2015, maana bila hivyo tutakuja kupigana muda si mrefu.

= akili

Hivi wale Maaskofu wa Kanisa Katoliki waliochotewa na Ruge vipi?
 
Hivi na wale Maaskofu wa Kanisa Katoliki waliotajwa na kulamba kutoka kwa Ruge, Kanisa Katoliki linasemaje?

Maana Kikwete karusha hilo, halafu Kikwete kaniacha hoi, eti wachungaji sijui Mashehe, hili yeye hayumo. Kulikuwa kuna shehe pale? kwa vijembe hajambo.
jamani huyu jini mahaba anachangia mada gani?
 
Hivi na wale Maaskofu wa Kanisa Katoliki waliotajwa na kulamba kutoka kwa Ruge, Kanisa Katoliki linasemaje?

Maana Kikwete karusha hilo, halafu Kikwete kaniacha hoi, eti wachungaji sijui Mashehe, hili yeye hayumo. Kulikuwa kuna shehe pale? kwa vijembe hajambo.

Kikwete ni Mweupeee peeee kazi yake ni mipasho na vijembe hotuba zake hazina mashiko!
Nafurahi umeliona hilo
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hivi na wale Maaskofu wa Kanisa Katoliki waliotajwa na kulamba kutoka kwa Ruge, Kanisa Katoliki linasemaje?

Maana Kikwete karusha hilo, halafu Kikwete kaniacha hoi, eti wachungaji sijui Mashehe, hili yeye hayumo. Kulikuwa kuna shehe pale? kwa vijembe hajambo.

Al-shabaab and Mjahidin at work: 24hrs unakalia udini tu.....
 
Mujulizi in jaji kwa hilo jaji mkuu na tume ya mahakama inaweza kushughulika nae. Lakini huyu pia ni katibu wa. Tume ya kurekebisha sheria. Hapa Rais hana kizuizi cha kutengua uteuzi wake. Akiachwa hapo in hatari.

Kwa madhumuni ya kuweka Uhuru wa mahakama Rais hana mamlaka ya kutengua uteuzi wa Majaji
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom