Confession: The hurting truth -- natamani kurudi kwenye ushirikina

Fact
@Mshana Jr Chukua Huu Ushauri mkuu. Naamini upo katika Kusaidia watu waepukane na Wajikinge na Ulozi na Ushirikina

Wachawi,Majini,Mashetani Ni Vitu Vibaya Hasa Vikishampa Mtu. Nikuombe Usirudi huko ila Jikite katika kutoa Elimu ya Kuwaepusha Watu na Wabaya Hao na Watumie Nini ili Kujikinga Navyo pamoja Na Nguvu za Mungu Muumba
 
Niliachana kabisa na mambo yote ya kishirikina miezi kadhaa iliyopita, na kuthibitisha hilo niliweka uzi rasmi hapa JF na kumrudia Mola wangu mazima. Na kuna hili ambao sikuwahi kulisema hapa lakini wale ambao niliwaumiza na roho ikaniongoza tusawazishe nilifanya hivyo. Na nikapata amani kubwa moyoni

Naamini nanyi ni mashuhuda wa hili kwakuwa nilipunguza mada za ushirikina kwa asilimia 80 ama 90 hivi. Na kila nilichomiliki chenye viashiria na viasili vya ushirikina ama niligawa au niliviharibu na kuviteketeza kwa moto kwa mikono yangu mwenyewe. Nilihakikisha naishi maisha ya ukamilifu na usafi wa kiroho

LAKINI wapendwa shetani ana nguvu sana sana. Unapokuwa umevaa koti jeupe la mshika dini na asiyependa mambo ya ulozo lakini ndani u mchafu kupitiliza wala sheatani hawezi kukusumbua kabisa lakini once unapomkataa kwa roho na kweli. VITA HUANZIA HAPO! atakujia na washirika wengine SABA kuhakikisha wanakurudisha kwenye himaya yao.

Juzi kati nilikuwa maeneo ya mikwambe Kigamboni kibada mpaka saa tatu usiku hivi wakati naondoka nikagundua kuna watu walikuwa wameniungia body na nilienda nao mpaka Tuangoma halafu wakapotea kusikojulikana

Tangu hapo nimejiwa na msisimko wa ajabu kabisa. Msisimko wa kutafuta zile nguvu za giza tena. Najitambua kiimani na kiroho niko vizuri mno. Lakini sasa naona viashiria vya kunirudisha kilingeni vinazidi kupata nguvu kila uchao.

Tafadhalini naomba msije mkanishangaa in case mkisikia nimerudi Msata Kilingeni penye shina langu. Lakini pia ukiweza na ukipenda kwa utashi wako pls niombee. Kuna shida nyingi huko vilingeni basi tuuu
Kaka mshana samahani naomba unisaidie namba yako ya cm nina shida urgent
 
Back
Top Bottom