Common Sense Itumike

Mfikirishi

JF-Expert Member
Jan 16, 2012
7,492
8,537
Gari bovu aliruhusiwi kukimbia barabarani..
Ubovu ukizidi mara zote huuzwa kama scrapper..!
Hii ni common sense..!

Shule au chuo kisichokidhi vigezo hufungiwa..! Hii ni common sense..!!

Kwenye usahili au udahili wasiokidhi vigezo utupiliwa mbali..!
Hii ni common sense..!!

Kwa wakulima mashambani; mbegu isiyoleta matunda mazuri ususiwa na wakulima.. Hii ni common sense..!

Katika biashara; bidhaa inayoleta hasara iwapo dukani uachwa mara moja..! Hii ni common sense.!

Katika michezo hususan soka; golikipa au beki ambaye ni uchochoro wa magoli uwekwa benchi au utupiwa virago vyake.. Hii ni common sense..!

Sasa kama ni hivyo; kwa nini tumewaruhusu hawa watawala wabovu waendelee kutawala miaka yote hiyo..??
Hivi tunahitaji muda kiasi gani kubaini kuwa hawa jamaa hawana faida yoyote kwa taifa letu..??

Najua wapo wanaojipa moyo kuwa ipo siku mambo yatakuwa sawa..!!
Anyway; wenye imani hiyo waendelee tu.. Lakini naamini wapo wengi kama mimi ambao hatutegemei kuvuna mahindi kwenye shamba la vitunguu..!!

Common sense itumike kuondoa na kokomesha matatizo yetu..!!
Kama hawa watawala hawafai kila mwaka wanaleta tatizo jipya na hasara kadhaa.. Waondolewe wote na vibaraka vyao..!!

Summary: Common sense ni kuiondoa ccm..!
 
Back
Top Bottom