Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,370
- 39,186
Makala hii imetoka kwenye Tanzania Daima leo. Kwa bahati mbaya kwenye tovuti yao haionekani (kama ilivyo kwa makala nyingine). Kwa faida ya wasomaji, mashabiki na wakosoaji ninaiweka hapa kama ilivyo.
M. M. Mwanakijiji
Hii itakuwa ni makala yangu ya kufungia mwaka (isipokuwa kama kuna jambo la dharura kabla ya mwaka mpya). Katika kumaliza mwaka huu jambo ambalo limenigusa mno ni majaribio yasiyoisha ya kuzuga wananchi yaliyofanywa na serikali ya CCM na viongozi wake. Majaribio hayo dhaifu na yasiyoenda shule yalikuwa ni burudani tosha kwa wananchi hasa wale ambao hawakuwa tayari kuzugika.
Kuna matukio mengi ambayo tukianza kuyahesabu tunaweza kucheka lakini kwa hakika Watanzania wanakumbuka jinsi ambavyo viongozi wetu walivyochemsha mara kadhaa na kujikuta kuwa wananchi wamewashtukia. Binafsi nilifikia mahali pa kuweka manyanga chini na kukubali yaishe tu. Nilifikia mahali pa kuona kuwa serikali yetu imeziba masikio yake na ingawa inaimba wimbo wa kukubali kukosolewa kimsingi haina lengo la kusahihisha makosa au udhaifu wake na badala yake imejitahidi kuuelezea na kuuhalalisha.
Lakini ambacho kilinikera zaidi mwaka huu siyo masuala ya mikataba ingawa hilo lilinikera; siyo suala la nishati ingawa hilo lilinikera; siyo masuala ya wanafunzi wa Ukraine ambayo kwa hakika yalinikera sana; na kwa hakika siyo maamuzi mbalimbali ya kisiasa ambacho yamechukuliwa mwaka huu, ambayo nayo pia yalinikera. Binafsi kati ya yote ambayo serikali ya Kikwete imejitahidi kuyafanya na kushindwa vibaya sana ni uzugaji makusudi wa wananchi bila wananchi wenyewe kuzugika.
Tulipoanza na suala la vijana wetu waliokwama Ukraine ambao serikali iliwakubalia mkopo na kuwapa baraka zote waende kusoma huko kilichonisikisha na kunitisha siyo adha na matatizo ya watoto wetu wale hadi wakapiga kambi nje ya Ubalozi wa Uingereza bali ni majibu ya kizugaji ya serikali yetu. Licha ya kuwapa nafasi viongozi wote wakuu wa serikali yetu kuanzia Rais Kikwete hadi Wabunge wote kwa woga waligwaya kushughulikia suala hili na badala yake wakaja na majibu ya kizugaji.
Prof. Msolla na timu yake iliyojaa wazembe na viongozi wenye kujipenda wenyewe kuliko utumishi wao kwa taifa hili wakasema kuwa tuliwapa ushauri wasiondoke, hawakusikiliza. Hakuna kati yao kwa mwaka mzima aliyeweza kusema ni lini na ni nani aliyewapa vijana hao ushauri huo wa kutokwenda Ukraine lakini wakaenda. Na kwa kutumia ubavu mkubwa wakawalazimisha vijana wale kurudi nyumbani na kukatisha masomo. Wiki iliyopita Prof. Msolla bila soni anadiriki kuuambia ulimwengu kuwa Tanzania iko nyuma katika elimu ya juu!! Uzugaji juu ya uzugaji.
Rais Kikwete na Waziri wake Mkuu walipopewa nafasi ya kufanya maamuzi ya kijasiri na kishujaa wakagwaya na kuona kuwa tunashindana na serikali. Rais Kikwete yeye akasema kama Wizara wangeshindwa wangeniambia na Mhe Lowassa yeye alipopewa nafasi ya kuonesha uongozi akasema ninaenda kula. Bodi mbovu ya mikopo ambayo ni chanzo cha matatizo makubwa ya elimu ya juu na mfumo duni wa utoaji wa mikopo hiyo unaosimamiwa na Nyatega vyote bado vipo na mwaka ujao Watanzania muendelee kusubiri uzugaji juu ya uzugaji.
Tukawaonesha jinsi gani bodi ya mikopo inachota fedha na kushindwa kusimamia utoaji wa mikopo na hivyo kutengeneza mwanya mkubwa wa ufisadi na majina tukawapa. Kina Gesimba na wenzao wakakurupuka kutoka idara yao ya uzugaji na kujaribu kuelezea upotofu huo. Wakajaribu kutoa majibu ya nini kilifanyika kuhusu vijana wa Ukraine na tulipowabana wakaomba Taasisi ya Kuzuga kuwasaidia. Ndipo Bw. Edward Hosea na TAKUKURU wakajjitokeza na kusema kuwa wanafanyia kazi madai ya ufisadi kwenye Bodi ya Mikopo. Wananchi tukazugwa.
Wakati wa kikao cha bajeti Waziri Mkuu akiwa na jazba zake na akizungumza kwa sauti ya kupaa kama msanii wa bongo flava akatangaza Bungeni kwa mbwembwe zote kuwa Tanzania imepaa na wananchi tushangilie. Nikaandika wakati ule juu ya Ndege ya Lowassa iliyopaa na abiria walioachwa wameduwaa iliyoambatana na kikatuni kizuri kabisa. Mabingwa wa uzugaji wakakurupuka kuja na majibu yasiyo na kichwa wala mguu ambayo ndani yake wakatupa sisi wengine ukimbizi wa reja reja. Tukawajibu kimahiri bila kuwaonea soni kama vile kumkoma nyani giledi! Tukawaonesha kuwa wamekurupuka na waliposoma majibu yetu wakanywea na kuelewa kuwa uzugaji wao wa zamani hauna nafasi leo hii.
Yakaja masuala ya Buzwagi na Karamagi. Mjadala ukazuka na tukaona ni jinsi gani Taasisi yao ya Uzugaji imekosa nguvu kwani hata kitengo chao cha chama kinachoshughulikia Uzugaji kilishindwa kulitetea jambo hili. Walipomwadhibu Mhe. Zitto na kumfungia wao walitarajia wananchi watashangilia na Zitto aliposimamishwa kama shujaa katika Taifa hili wakajua uzugaji wao hatimaye umefikia kikomo. Wakawatuma kuanzia kina Mhe. Anna Makinda na wapambe wao toka Bungeni ili wawaeleweshe wananchi juu ya Adhabu ya Zitto na kwanini imestahili. Wakajaribu kuzuga weeeee lakini wapi, Zitto akawa Mzitto habebeki! Taasisi yao ya Uzugaji chini ya Hosea ikaingilia kati tena, wakasema tunachunguza rushwa wakati hakuna mtu aliyedai kulikuwa na rushwa!
Kabla hawajakaa sawasawa Ushirika wa wapinzani wakaja na kile ambacho naamini ni jambo kubwa kabisa katika historia ya nchi yetu mwaka huu nako ni kutajwa kwa orodha ya aibu ya ufisadi ambapo watumishi 11 katika serikali yetu wakatajwa kuwa kwa namna moja au nyingine wameshiriki katika ufisadi. Alitajwa kuanzia Rais Kikwete hadi mtu wa mwisho. Kama vile mbogo waliojeruhiwa watawala wetu wakaanza kukurupuka na majibu ambayo kwa hakika mfano wake hakuna. Wakaanza kujaribu kutuzuga. Akatumwa Kingunge, Bomani, Warioba na wenzao huku watuhumiwa wakitishia kwenda mahakamani.
Watu tukashangazwa imekuwaje hadi Warioba kutumiwa katika uzugaji? Kumbe yalikuwa maji marefu. Walizoea kutuzuga sisi wananchi wa kawaida lakini mwisho mjomba wetu kule Ulaya akaingilia kati, uzugaji wao haukufanikiwa kama walivyotaka wakajikuta hawana budi kuruhusu uchunguzi huru.
Wakitumia ujuzi wao wa siku nyingi wa uzugaji wakaamua kutuma timu yao nzima kama kikosi kwenda mikoani kuzuga wananchi kwa kile ambacho wao walikiita kuelezea bajeti. Masikini wa Mungu wakajitahidi! Lakini wakienda huku wanazomewa, wakirudi kule wanazomewa! Hawakuelewa ni kitu gani kimewaingia Watanzania! Wakabakia wanaulizana ilikuwaje? Cha kusikitisha ni kuwa uzugaji wao ulifikia mahali pabaya hadi kuomba msaada wa mtuhumiwa wa mauaji Brother Ditto ambaye naye kwa kushindwa hoja akajikuta anatukana wake za watu! Kumbe cha kuvunjda hakina ubani!!
Wakiwa katika uzugaji huo ndipo kwa mara nyingine Watanzania tukaona jinsi gani nchi yetu imejaliwa wasanii. Kama ilivyokuwa wakati wa uvamizi wa Wamarekani nchini Iraq miaka karibu minne iliyopita, ambapo wananchi walishuhudia Umahiri wa Waziri wa Habari wa Saddam Bw. Mohammed Said al Sahaf. Waziri yule ambaye katika miaka ya hivi karibuni bila ya shaka anashikilia rekodi ya propaganda duniani aliweza kuiteka mioyo ya watu kwa kutumia kipaji chake cha maneno kuzuga watu. Mojawapo ya uzugaji wake mkubwa wakati wa vita ni madai kuwa majeshi ya Marekani hayako Baghdadi na askari wa Marekani wanauliwa malangoni mwake. Wakati anasema hayo majeshi ya Marekani yalikuwa mita chache toka alipokuwapo Waziri huyo. Ni kutokana na uzugaji huo magazeti ya magharibi yakampachika jina la comical Ali yaani mchekeshaji Ali wakimtofautisha na msaidizi mwingine wa Sadam aliyejulikana kama Chemical Ali.
Ndipo na sisi Watanzania wakati wa sakata la orodha ya ufisadi tukapata mchekeshaji wetu. Waziri wetu wa Habari na Utamaduni (cheo kama cha Comical Ali) Bw. Mohammed Seif Khatib alipoonesha uzugaji wake. Mheshimiwa huyo alikana kabisa kuwa viongozi hawazomewi, zote hizo ni propaganda za Wapinzani.
Uzugaji ukaendelea mwaka mzima na hasa pale ilipouunda Kamati ya Ushauri kuhusu Sekta ya Madini. Wananchi walifurahia kweli kuwa hatimaye Rais kafanya kweli. Wananchi wakadhania kuwa sala zao zimejibiwa kumbe walichoshuhudia ni uzugaji wa hali ya juu. Hisia hizo kuwa tumezugwa zikathibitishwa na idara ya CCM ya uzugaji wa Hali ya Juu inayoongozwa na Mhe. John Chiligati. Yeye bila wasiwasi akawaambia wananchi kuwa Rais hakuunda tume ya uchunguzi! Wakatuzuga tukazugika.
Sasa uzugaji huu ukaendelea kwenye mambo mengi na kama nilivyosema kuyaorodhesha yote tutakesha. Hata hivyo nimeshindwa kujizua kuelezea uzugaji uliofanywa na Comical Khatib wetu mara ya mwisho. Yalipotolewa matokeo ya utafiti wa REDET kuhusu serikali ya Kikwete vyombo mbalimbali vya habari vikaelezea ni jinsi gani matokeo ya utafiti huo siyo mazuri kwa CCM. Mheshimiwa Khatib akitumia mbinu ya Comical Ali akajaribu kuelezea kwanini matokeo hayo ni mazuri kwa CCM kwa kuangalia neno kuridhika. Akajaribu kutuzuga.
Sasa, CCM na wapambe wake wataendelea kutuzuga hadi lini? Hivi wanaposimama na kusema mambo ambayo hayana mantiki kweli wanafikiria wananchi hawatashtukia? Leo hii Ofisa Ugavi toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma anawatangazia madiwani kuwa kuanzia sasa wanaweza kuomba Tenda katika halmashauri zao na wasikataliwe kwa vile tu wao ni madiwani wa halmashauri hizo. Bw. Athuman Ngwalo amesema kwa vile wao madiwani siyo watumishi wa umma (msiniulize wanamtumikia nani) basi hata kama wana makampuni yao mbalimbali sasa wanaweza kushindanisha tenda kwenye halmashauri zao kwani hakuna sheria inayowakata kufanya hivyo. Kama vile Rais wao Mkapa alivyofanya akiwa Ikulu sasa halmashauri zetu zimepewa leseni za kutengeneza pesa! Kuzuga wanakotuzuga.
Sasa, tunapoelekea mwaka huu mpya nina ombi moja tu kwa CCM na watendaji wake. Chonde chonde sana na tafadhali mno, kuwa mwaka ujao wa 2008 mtakapoamua kutuzuga jaribuni kutuzuga tukazugika. Jinsi ambavyo mmejaribu mwaka huu kwa kweli mmefeli mno na kwa neno moja mmetia aibu. Kama uzugaji mliofanya mwaka huu ndio mtakaourudia mwakani basi kama watani zangu wanavyosema kule Mbeya Mbombo ingafu. Mna kazi mwakani kama uzugaji mtakaofanya unakaribiana kwa kiasi chochotena ule wa mwaka huu.
Mtakapoamua kutuzuga mwakani hakikisheni mnatuzuga hadi tunazugika maana mkituacha na maswali ya ziada au mkitoa majibu yanayozua maswali zaidi basi mtakuwa mmeshindwa katika fani uzugaji. Kama Rais ataamua kuunda upya baraza lake ni bora ahakikishe kuwa kitengo cha Uzugaji kina watu wanaoweza kuimuda nafasi hiyo na mtindo mlioanzisha sasa wa Mawaziri kuzungumza na wananchi ni mzuri. Ila nawashauri mwakani wale wasemaji wenu watakapokuwa wanatoa taarifa rasmi watengenezeeni beji zenye herufi ya M ili wananchi wajue. Haitoshi kumwaga takwimu, haitoshi kulalamika magazeti hayaandiki mazuri na haitoshi kujaribu kuvinyima vyombo vya habari vinavyowakosoa biashara toka serikalini kwa vile tu hawakubali uzugaji wenu. Mkiamua kutuzuga mwakani mtuzuge tuzugike!
Vinginevyo, mwaka ujao tutaendelea kuwakalia kooni kama nira na kama ndege wanavyotua juu ya wanyama malishoni ndivyo na sisi tutavyotua katika migongo yenu. Tutawadonoa kwahoja na kuwaparua hadi makupe na viroboto yaishe kati yenu. Kama mwaka huu mmetushinda kwa kuwarudisha vijana wetu toka Ukraine kusoma na kuwaacha Solemba, na mkatangaza ushindi, basi mwaka ujao ni zamu yetu! Tunawatangazia mapema kuwa kama mlifikiri Tanzania ni yenu peke yenu na sisi wengine ni wakimbizi tu na wahamiaji mjue kuwa wakati wa njozi yenu hiyo umefikia kikomo! Unapokuja mwaka mpya, hatutakubali tena kuzugwa kwani kuzuga kwa miaka 46 iliyopita kumetosha na wananchi wanajiandaa kwa mwaka 2010! Mmepewa nafasi nyingi ya kusahihisha na kujisahihisha na mara zote mmekuwa na majibu na mikakati ya kizugaji. Watanzania wamechoka, na wakati waja na tena upo ambapo wataonesha uchovu wao kwenye sanduku la kura. Safari ya kuelekea huko ndiyo imeanza. Mtatuzuga tena? I dont think so!
Kwenu nyote wasomaji, Eid Mubarak, Heri ya Krismasi, na Fanaka za Mwaka Mpya usio na uzugaji wa 2008! Tukutane wiki ya kwanza ya 2008
Niandikie: mwanakijiji(at)jamboforums.com
M. M. Mwanakijiji
Hii itakuwa ni makala yangu ya kufungia mwaka (isipokuwa kama kuna jambo la dharura kabla ya mwaka mpya). Katika kumaliza mwaka huu jambo ambalo limenigusa mno ni majaribio yasiyoisha ya kuzuga wananchi yaliyofanywa na serikali ya CCM na viongozi wake. Majaribio hayo dhaifu na yasiyoenda shule yalikuwa ni burudani tosha kwa wananchi hasa wale ambao hawakuwa tayari kuzugika.
Kuna matukio mengi ambayo tukianza kuyahesabu tunaweza kucheka lakini kwa hakika Watanzania wanakumbuka jinsi ambavyo viongozi wetu walivyochemsha mara kadhaa na kujikuta kuwa wananchi wamewashtukia. Binafsi nilifikia mahali pa kuweka manyanga chini na kukubali yaishe tu. Nilifikia mahali pa kuona kuwa serikali yetu imeziba masikio yake na ingawa inaimba wimbo wa kukubali kukosolewa kimsingi haina lengo la kusahihisha makosa au udhaifu wake na badala yake imejitahidi kuuelezea na kuuhalalisha.
Lakini ambacho kilinikera zaidi mwaka huu siyo masuala ya mikataba ingawa hilo lilinikera; siyo suala la nishati ingawa hilo lilinikera; siyo masuala ya wanafunzi wa Ukraine ambayo kwa hakika yalinikera sana; na kwa hakika siyo maamuzi mbalimbali ya kisiasa ambacho yamechukuliwa mwaka huu, ambayo nayo pia yalinikera. Binafsi kati ya yote ambayo serikali ya Kikwete imejitahidi kuyafanya na kushindwa vibaya sana ni uzugaji makusudi wa wananchi bila wananchi wenyewe kuzugika.
Tulipoanza na suala la vijana wetu waliokwama Ukraine ambao serikali iliwakubalia mkopo na kuwapa baraka zote waende kusoma huko kilichonisikisha na kunitisha siyo adha na matatizo ya watoto wetu wale hadi wakapiga kambi nje ya Ubalozi wa Uingereza bali ni majibu ya kizugaji ya serikali yetu. Licha ya kuwapa nafasi viongozi wote wakuu wa serikali yetu kuanzia Rais Kikwete hadi Wabunge wote kwa woga waligwaya kushughulikia suala hili na badala yake wakaja na majibu ya kizugaji.
Prof. Msolla na timu yake iliyojaa wazembe na viongozi wenye kujipenda wenyewe kuliko utumishi wao kwa taifa hili wakasema kuwa tuliwapa ushauri wasiondoke, hawakusikiliza. Hakuna kati yao kwa mwaka mzima aliyeweza kusema ni lini na ni nani aliyewapa vijana hao ushauri huo wa kutokwenda Ukraine lakini wakaenda. Na kwa kutumia ubavu mkubwa wakawalazimisha vijana wale kurudi nyumbani na kukatisha masomo. Wiki iliyopita Prof. Msolla bila soni anadiriki kuuambia ulimwengu kuwa Tanzania iko nyuma katika elimu ya juu!! Uzugaji juu ya uzugaji.
Rais Kikwete na Waziri wake Mkuu walipopewa nafasi ya kufanya maamuzi ya kijasiri na kishujaa wakagwaya na kuona kuwa tunashindana na serikali. Rais Kikwete yeye akasema kama Wizara wangeshindwa wangeniambia na Mhe Lowassa yeye alipopewa nafasi ya kuonesha uongozi akasema ninaenda kula. Bodi mbovu ya mikopo ambayo ni chanzo cha matatizo makubwa ya elimu ya juu na mfumo duni wa utoaji wa mikopo hiyo unaosimamiwa na Nyatega vyote bado vipo na mwaka ujao Watanzania muendelee kusubiri uzugaji juu ya uzugaji.
Tukawaonesha jinsi gani bodi ya mikopo inachota fedha na kushindwa kusimamia utoaji wa mikopo na hivyo kutengeneza mwanya mkubwa wa ufisadi na majina tukawapa. Kina Gesimba na wenzao wakakurupuka kutoka idara yao ya uzugaji na kujaribu kuelezea upotofu huo. Wakajaribu kutoa majibu ya nini kilifanyika kuhusu vijana wa Ukraine na tulipowabana wakaomba Taasisi ya Kuzuga kuwasaidia. Ndipo Bw. Edward Hosea na TAKUKURU wakajjitokeza na kusema kuwa wanafanyia kazi madai ya ufisadi kwenye Bodi ya Mikopo. Wananchi tukazugwa.
Wakati wa kikao cha bajeti Waziri Mkuu akiwa na jazba zake na akizungumza kwa sauti ya kupaa kama msanii wa bongo flava akatangaza Bungeni kwa mbwembwe zote kuwa Tanzania imepaa na wananchi tushangilie. Nikaandika wakati ule juu ya Ndege ya Lowassa iliyopaa na abiria walioachwa wameduwaa iliyoambatana na kikatuni kizuri kabisa. Mabingwa wa uzugaji wakakurupuka kuja na majibu yasiyo na kichwa wala mguu ambayo ndani yake wakatupa sisi wengine ukimbizi wa reja reja. Tukawajibu kimahiri bila kuwaonea soni kama vile kumkoma nyani giledi! Tukawaonesha kuwa wamekurupuka na waliposoma majibu yetu wakanywea na kuelewa kuwa uzugaji wao wa zamani hauna nafasi leo hii.
Yakaja masuala ya Buzwagi na Karamagi. Mjadala ukazuka na tukaona ni jinsi gani Taasisi yao ya Uzugaji imekosa nguvu kwani hata kitengo chao cha chama kinachoshughulikia Uzugaji kilishindwa kulitetea jambo hili. Walipomwadhibu Mhe. Zitto na kumfungia wao walitarajia wananchi watashangilia na Zitto aliposimamishwa kama shujaa katika Taifa hili wakajua uzugaji wao hatimaye umefikia kikomo. Wakawatuma kuanzia kina Mhe. Anna Makinda na wapambe wao toka Bungeni ili wawaeleweshe wananchi juu ya Adhabu ya Zitto na kwanini imestahili. Wakajaribu kuzuga weeeee lakini wapi, Zitto akawa Mzitto habebeki! Taasisi yao ya Uzugaji chini ya Hosea ikaingilia kati tena, wakasema tunachunguza rushwa wakati hakuna mtu aliyedai kulikuwa na rushwa!
Kabla hawajakaa sawasawa Ushirika wa wapinzani wakaja na kile ambacho naamini ni jambo kubwa kabisa katika historia ya nchi yetu mwaka huu nako ni kutajwa kwa orodha ya aibu ya ufisadi ambapo watumishi 11 katika serikali yetu wakatajwa kuwa kwa namna moja au nyingine wameshiriki katika ufisadi. Alitajwa kuanzia Rais Kikwete hadi mtu wa mwisho. Kama vile mbogo waliojeruhiwa watawala wetu wakaanza kukurupuka na majibu ambayo kwa hakika mfano wake hakuna. Wakaanza kujaribu kutuzuga. Akatumwa Kingunge, Bomani, Warioba na wenzao huku watuhumiwa wakitishia kwenda mahakamani.
Watu tukashangazwa imekuwaje hadi Warioba kutumiwa katika uzugaji? Kumbe yalikuwa maji marefu. Walizoea kutuzuga sisi wananchi wa kawaida lakini mwisho mjomba wetu kule Ulaya akaingilia kati, uzugaji wao haukufanikiwa kama walivyotaka wakajikuta hawana budi kuruhusu uchunguzi huru.
Wakitumia ujuzi wao wa siku nyingi wa uzugaji wakaamua kutuma timu yao nzima kama kikosi kwenda mikoani kuzuga wananchi kwa kile ambacho wao walikiita kuelezea bajeti. Masikini wa Mungu wakajitahidi! Lakini wakienda huku wanazomewa, wakirudi kule wanazomewa! Hawakuelewa ni kitu gani kimewaingia Watanzania! Wakabakia wanaulizana ilikuwaje? Cha kusikitisha ni kuwa uzugaji wao ulifikia mahali pabaya hadi kuomba msaada wa mtuhumiwa wa mauaji Brother Ditto ambaye naye kwa kushindwa hoja akajikuta anatukana wake za watu! Kumbe cha kuvunjda hakina ubani!!
Wakiwa katika uzugaji huo ndipo kwa mara nyingine Watanzania tukaona jinsi gani nchi yetu imejaliwa wasanii. Kama ilivyokuwa wakati wa uvamizi wa Wamarekani nchini Iraq miaka karibu minne iliyopita, ambapo wananchi walishuhudia Umahiri wa Waziri wa Habari wa Saddam Bw. Mohammed Said al Sahaf. Waziri yule ambaye katika miaka ya hivi karibuni bila ya shaka anashikilia rekodi ya propaganda duniani aliweza kuiteka mioyo ya watu kwa kutumia kipaji chake cha maneno kuzuga watu. Mojawapo ya uzugaji wake mkubwa wakati wa vita ni madai kuwa majeshi ya Marekani hayako Baghdadi na askari wa Marekani wanauliwa malangoni mwake. Wakati anasema hayo majeshi ya Marekani yalikuwa mita chache toka alipokuwapo Waziri huyo. Ni kutokana na uzugaji huo magazeti ya magharibi yakampachika jina la comical Ali yaani mchekeshaji Ali wakimtofautisha na msaidizi mwingine wa Sadam aliyejulikana kama Chemical Ali.
Ndipo na sisi Watanzania wakati wa sakata la orodha ya ufisadi tukapata mchekeshaji wetu. Waziri wetu wa Habari na Utamaduni (cheo kama cha Comical Ali) Bw. Mohammed Seif Khatib alipoonesha uzugaji wake. Mheshimiwa huyo alikana kabisa kuwa viongozi hawazomewi, zote hizo ni propaganda za Wapinzani.
Uzugaji ukaendelea mwaka mzima na hasa pale ilipouunda Kamati ya Ushauri kuhusu Sekta ya Madini. Wananchi walifurahia kweli kuwa hatimaye Rais kafanya kweli. Wananchi wakadhania kuwa sala zao zimejibiwa kumbe walichoshuhudia ni uzugaji wa hali ya juu. Hisia hizo kuwa tumezugwa zikathibitishwa na idara ya CCM ya uzugaji wa Hali ya Juu inayoongozwa na Mhe. John Chiligati. Yeye bila wasiwasi akawaambia wananchi kuwa Rais hakuunda tume ya uchunguzi! Wakatuzuga tukazugika.
Sasa uzugaji huu ukaendelea kwenye mambo mengi na kama nilivyosema kuyaorodhesha yote tutakesha. Hata hivyo nimeshindwa kujizua kuelezea uzugaji uliofanywa na Comical Khatib wetu mara ya mwisho. Yalipotolewa matokeo ya utafiti wa REDET kuhusu serikali ya Kikwete vyombo mbalimbali vya habari vikaelezea ni jinsi gani matokeo ya utafiti huo siyo mazuri kwa CCM. Mheshimiwa Khatib akitumia mbinu ya Comical Ali akajaribu kuelezea kwanini matokeo hayo ni mazuri kwa CCM kwa kuangalia neno kuridhika. Akajaribu kutuzuga.
Sasa, CCM na wapambe wake wataendelea kutuzuga hadi lini? Hivi wanaposimama na kusema mambo ambayo hayana mantiki kweli wanafikiria wananchi hawatashtukia? Leo hii Ofisa Ugavi toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma anawatangazia madiwani kuwa kuanzia sasa wanaweza kuomba Tenda katika halmashauri zao na wasikataliwe kwa vile tu wao ni madiwani wa halmashauri hizo. Bw. Athuman Ngwalo amesema kwa vile wao madiwani siyo watumishi wa umma (msiniulize wanamtumikia nani) basi hata kama wana makampuni yao mbalimbali sasa wanaweza kushindanisha tenda kwenye halmashauri zao kwani hakuna sheria inayowakata kufanya hivyo. Kama vile Rais wao Mkapa alivyofanya akiwa Ikulu sasa halmashauri zetu zimepewa leseni za kutengeneza pesa! Kuzuga wanakotuzuga.
Sasa, tunapoelekea mwaka huu mpya nina ombi moja tu kwa CCM na watendaji wake. Chonde chonde sana na tafadhali mno, kuwa mwaka ujao wa 2008 mtakapoamua kutuzuga jaribuni kutuzuga tukazugika. Jinsi ambavyo mmejaribu mwaka huu kwa kweli mmefeli mno na kwa neno moja mmetia aibu. Kama uzugaji mliofanya mwaka huu ndio mtakaourudia mwakani basi kama watani zangu wanavyosema kule Mbeya Mbombo ingafu. Mna kazi mwakani kama uzugaji mtakaofanya unakaribiana kwa kiasi chochotena ule wa mwaka huu.
Mtakapoamua kutuzuga mwakani hakikisheni mnatuzuga hadi tunazugika maana mkituacha na maswali ya ziada au mkitoa majibu yanayozua maswali zaidi basi mtakuwa mmeshindwa katika fani uzugaji. Kama Rais ataamua kuunda upya baraza lake ni bora ahakikishe kuwa kitengo cha Uzugaji kina watu wanaoweza kuimuda nafasi hiyo na mtindo mlioanzisha sasa wa Mawaziri kuzungumza na wananchi ni mzuri. Ila nawashauri mwakani wale wasemaji wenu watakapokuwa wanatoa taarifa rasmi watengenezeeni beji zenye herufi ya M ili wananchi wajue. Haitoshi kumwaga takwimu, haitoshi kulalamika magazeti hayaandiki mazuri na haitoshi kujaribu kuvinyima vyombo vya habari vinavyowakosoa biashara toka serikalini kwa vile tu hawakubali uzugaji wenu. Mkiamua kutuzuga mwakani mtuzuge tuzugike!
Vinginevyo, mwaka ujao tutaendelea kuwakalia kooni kama nira na kama ndege wanavyotua juu ya wanyama malishoni ndivyo na sisi tutavyotua katika migongo yenu. Tutawadonoa kwahoja na kuwaparua hadi makupe na viroboto yaishe kati yenu. Kama mwaka huu mmetushinda kwa kuwarudisha vijana wetu toka Ukraine kusoma na kuwaacha Solemba, na mkatangaza ushindi, basi mwaka ujao ni zamu yetu! Tunawatangazia mapema kuwa kama mlifikiri Tanzania ni yenu peke yenu na sisi wengine ni wakimbizi tu na wahamiaji mjue kuwa wakati wa njozi yenu hiyo umefikia kikomo! Unapokuja mwaka mpya, hatutakubali tena kuzugwa kwani kuzuga kwa miaka 46 iliyopita kumetosha na wananchi wanajiandaa kwa mwaka 2010! Mmepewa nafasi nyingi ya kusahihisha na kujisahihisha na mara zote mmekuwa na majibu na mikakati ya kizugaji. Watanzania wamechoka, na wakati waja na tena upo ambapo wataonesha uchovu wao kwenye sanduku la kura. Safari ya kuelekea huko ndiyo imeanza. Mtatuzuga tena? I dont think so!
Kwenu nyote wasomaji, Eid Mubarak, Heri ya Krismasi, na Fanaka za Mwaka Mpya usio na uzugaji wa 2008! Tukutane wiki ya kwanza ya 2008
Niandikie: mwanakijiji(at)jamboforums.com