Coca-cola Hawalipi Kodi

sakauye

Member
May 20, 2008
27
1
ufisadi tz ni kila sehemu.
hebu fikiria eti coca-cola hawalipi kodi! wakati huo huo wamachinga wanakabwa kufa mtu


Posted Date::6/4/2008
TRA yaorodhesha makampuni yasiyolipa kodi
Na Tausi Mbowe

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imewasilisha serikalini orodha ya makampuni makubwa sugu, ambayo yanakwepa kulipa kodi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, Dk Moselina Chijolinga aliwaambia wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi jana kuwa, mamlaka yake imeamua kupeleka orodha hiyo kwa serikali ili kuomba kampuni hizo zichukuliwe hatua.

''Tumeshapeleka serikalini orodha ya makampuni ambayo hayalipi kodi kabisa na yale yanayolipa kwa kulegalega kwa kuwa yanajulikana,'' alisema Dk Chijolinga.

Hoja hiyo iliamsha ari ya wajumbe wa kamati hiyo ambao ni wabunge, chini ya uenyekiti wake Dk Abdallah Kigoda, ambao waliuliza ni makampuni gani hayo ambayo yanakwepa kulipa kodi.

''Sijui kama sheria inanilinda katika hili, lakini tumeshapeleka barua serikalini inayoonyesha orodha ya makampuni yote sugu kulipa kodi,'' alisema Dk Chijoliga.

Wabunge hao walimtoa shaka Mwenyekiti huyo wa TRA na kumtaka kutaja majina hayo kwa kuwa katika Kamati za Bunge sheria inasema kuwa ana haki ya kutaja chochote.

Baada ya kuambiwa hivyo Mwenyekiti huyo aliidai kuwa kampuni ya Coca-Cola imekuwa hailipi kabisa kodi na baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanalipa kodi kwa kusuasua.

Hata hivyo, Dk Chijoliga alishindwa kutaja idadi kamili ya makampuni hayo mbele ya wabunge hao ambao wengi walionekana wazi kutaka kuzifahamu kampuni hizo.

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omari Mzee aliahidi kuwa serikali italifanyia kazi suala hilo mapema iwezekanavyo.
 
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omari Mzee aliahidi kuwa serikali italifanyia kazi suala hilo mapema iwezekanavyo.

Waziri asituambie atalifanyia kazi, ilibidi aseme kwa nini walikuwa hawajalifanyia kazi swala hilo. Tunataka tujue kama asingejulishwa hiki kitu Wizara yake ingeweza kujua. Tunataka kujua kama kuna makampuni mengine ambayo hayalipi kodi na yeye hajui, au hawezi kujua. Kama anahitaji msaada au vipi. Sio atuambie atalishughulikia tu. Wabunge nao watupu ile mbaya, m-baneni mbavu Waziri huyo!
 
Tanzania kuna makampuni mengi ya coca-cola, mimi nayajua matatu (coca-cola kwanza, Dar; Bonite bottlers, Moshi na African bottlers, Mbeya) sasa ni wapi hao au wote? inamaanisha hata mzalendo Mzee Mengi kampuni yake hailipi kodi? Naomba ufafanuzi tafadhali.
 
Tanzania kuna makampuni mengi ya coca-cola, mimi nayajua matatu (coca-cola kwanza, Dar; Bonite bottlers, Moshi na African bottlers, Mbeya) sasa ni wapi hao au wote? inamaanisha hata mzalendo Mzee Mengi kampuni yake hailipi kodi? Naomba ufafanuzi tafadhali.

Mengi nasikia amefika hapo alipo kwa kukwepa kodi. Hili ni "lisemwalo."
 
Kinachoshangazwa ni mahela wanayomwaga kwenye matangazo .. na vijizawadi ... zingetosha kabisa kulipa kodi.

inabidi tuungane tususe kunywa soda zao kuonyesha msisitizo ... kila mmoja wetu amwambie mwenzie ili tuwapige marufuku watoto, waume , wake ndugu jamaa na marafiki kunywa coca cola huenda ikasaidia kidogo
 
Wafanyakazi wanalipa kodi 20% ya mshahara including walimu, manesi, mapolisi, walinzi ... Wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga wanalipa kodi), wafanya biashara wa kati wanalipa kodi (ingawa ni ndogo kuliko ya wafanyakazi) sasa haya makampuni makubwa, coca cola! makampuni ya simu.. jamani.

Ndiyo maana ya kuteua viongozi wa serekali kuwa wakurugenzi au wanabodi ili wawalinde.
 
...inabidi tuungane tususe kunywa soda zao kuonyesha msisitizo ... kila mmoja wetu amwambie mwenzie ili tuwapige marufuku watoto, waume , wake ndugu jamaa na marafiki kunywa coca cola huenda ikasaidia kidogo

Naomba kutofautiana kidogo hapo.

Kama CocaCola wanakwepa kodi wanavunja sheria. Ni kazi ya Serikali kuchukua hatua. Hatua kali kuzidi kuwagomea soda zao.

Unagomea kampuni kama ikiwa haifanyi vitu fulani vinaitwa Majukumu ya Makampuni kwa Jamii, kama vile wakiwa wanaharibu mazingira, au ikiwa haiwekezi faida zake katika namna inayonufaisha wananchi. Lakini wakiwa wanavunja sheria, hakuna kuwabembeleza kwa migomo. Tuitake Serikali yetu iliyolala fofofo izinduke!
 
Hii Habari Imekaa Kama Udaku Vilee, Haielezi Ni Coca-cola Ipi, Na Huyo Mtu Anaenda Kwenye Kamati Ya Bunge Akiwa Hajui Analoongea Yaani Anataja Coca Tuu Makampuni Mengine Hayakumbuki! Mengi Anavyowabana Mafisadi Sasa Wameanza Kumharibia (sina Uhakika Katika Hilo Ila Inaonyesha Hivyo Kwa Sababu Habari Inataja Kampuni Moja Tuu
 
Nataka Kuongezea Kitu, Hivi Ni Wahindi Wangapi Hawalipi Kodi? Hivi Hamuoni Hoteli Zinavyobadilisha Majina Kila Siku? Maana Nasikia Iliyokuwa Holiday Inn Haipo Tena, Hivi Unadhani Hawajui Ni Nini Wanakifanya? Huyo Mtu Aliyetangaza Anaonekana Ni Mtu Wasiwasi Na Ana Ajenda Ya Siri, Yaani Makampuni Yoote Anataja Moja Tuu?
 
magazeti mengine kuhusu tukio hilo, km daily news wameripoti kuwa makampuni yanayodaiwa kutolipa kodi yamepewa na serikali msamaha huo km masharti yao ya uwekezaji, na mengine yanalipa kodi pungufu kuliko ilivyotarajiwa. Kwa hiyo tatizo ni serikali yenyewe na si makampuni hayo, kwa kuweka mianya ya kutolipa kodi kwa ridhaa yake yenyewe kutokana na ufisadi wa viongozi wenyewe, na kwa serikali kushindwa kusimamia sheria zilizopo.
 
Hii Habari Imekaa Kama Udaku Vilee, Haielezi Ni Coca-cola Ipi, Na Huyo Mtu Anaenda Kwenye Kamati Ya Bunge Akiwa Hajui Analoongea Yaani Anataja Coca Tuu Makampuni Mengine Hayakumbuki! Mengi Anavyowabana Mafisadi Sasa Wameanza Kumharibia (sina Uhakika Katika Hilo Ila Inaonyesha Hivyo Kwa Sababu Habari Inataja Kampuni Moja Tuu

Ahsante.

Ndo maana nikasema Waziri asituambie eti atashughulikia hili suala. Vipi makampuni mengine? Yapo ambayo hayajui?

Kuhusu stori za kidaku daku, tatizo ni Media. Tanzania hatujui ni nini kinaendelea katika nchi yetu kwa sababu hatuna vyombo vya kutupasha habari juu ya nchi inavyoendeshwa, na ni vipi inavyotakiwa kuendeshwa. Na kwa sababu wananchi hatujui kinacho endelea, inakuwa vigumu sana kuchangia kuleta mabadiliko. Kazi ipo!
 
Ahsante.

Ndo maana nikasema Waziri asituambie eti atashughulikia hili suala. Vipi makampuni mengine? Yapo ambayo hayajui?

Kuhusu stori za kidaku daku, tatizo ni Media. Tanzania hatujui ni nini kinaendelea katika nchi yetu kwa sababu hatuna vyombo vya kutupasha habari juu ya nchi inavyoendeshwa, na ni vipi inavyotakiwa kuendeshwa. Na kwa sababu wananchi hatujui kinacho endelea, inakuwa vigumu sana kuchangia kuleta mabadiliko. Kazi ipo!

Nakubaliana nawe,hapa bado "mfupa" tu inatakiwa "nyama"
 
ufisadi tz ni kila sehemu.
hebu fikiria eti coca-cola hawalipi kodi! wakati huo huo wamachinga wanakabwa kufa mtu


Posted Date::6/4/2008
TRA yaorodhesha makampuni yasiyolipa kodi
Na Tausi Mbowe

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imewasilisha serikalini orodha ya makampuni makubwa sugu, ambayo yanakwepa kulipa kodi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, Dk Moselina Chijolinga aliwaambia wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi jana kuwa, mamlaka yake imeamua kupeleka orodha hiyo kwa serikali ili kuomba kampuni hizo zichukuliwe hatua.

''Tumeshapeleka serikalini orodha ya makampuni ambayo hayalipi kodi kabisa na yale yanayolipa kwa kulegalega kwa kuwa yanajulikana,'' alisema Dk Chijolinga.

Hoja hiyo iliamsha ari ya wajumbe wa kamati hiyo ambao ni wabunge, chini ya uenyekiti wake Dk Abdallah Kigoda, ambao waliuliza ni makampuni gani hayo ambayo yanakwepa kulipa kodi.

''Sijui kama sheria inanilinda katika hili, lakini tumeshapeleka barua serikalini inayoonyesha orodha ya makampuni yote sugu kulipa kodi,'' alisema Dk Chijoliga.

Wabunge hao walimtoa shaka Mwenyekiti huyo wa TRA na kumtaka kutaja majina hayo kwa kuwa katika Kamati za Bunge sheria inasema kuwa ana haki ya kutaja chochote.

Baada ya kuambiwa hivyo Mwenyekiti huyo aliidai kuwa kampuni ya Coca-Cola imekuwa hailipi kabisa kodi na baadhi ya makampuni ya simu za mkononi yanalipa kodi kwa kusuasua.

Hata hivyo, Dk Chijoliga alishindwa kutaja idadi kamili ya makampuni hayo mbele ya wabunge hao ambao wengi walionekana wazi kutaka kuzifahamu kampuni hizo.

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omari Mzee aliahidi kuwa serikali italifanyia kazi suala hilo mapema iwezekanavyo.

Sasa hawa TRA watuambie ni muda gani haya makampuni hayajalipa na wao kama Chombo tunachokitegemea kwenye kukusanya mapato walikuwa wapi muda wote huo kuyasema haya na ikiwezekana watuambie ni vigogo wangapi wanalinda maslahi ya Makampuni haya.

Pili, Mheshimiwa Waziri, tunaomba hizi biashara za kusema kwamba mtalifanyia kazi sasa hivi tumeshachoka nasema hivi kwavile najua unayasoma yote yanayoendelea HAPA JF sasa ninachoomba uanze na TRA kwanza uangalie kama kuna haja ya kupunguza watu wasiojua ufanisi wao wa kazi hasa kwenye kukupa ripoti halafu ndio utuhabarishe juu ya haya makampuni na ni kwanini mpk sasa wanaendelea kufanya kazi ikiwa hawalipi kodi.
 
Hii issue iko tatanishi kidogo..

Hivi ni kweli kwa kampuni ya kimataifa kama Coca-cola kutolipa kodi?

Kama ni kweli, basi duh tumeuwawa kifo cha mende...
 
Hii issue iko tatanishi kidogo..

Hivi ni kweli kwa kampuni ya kimataifa kama Coca-cola kutolipa kodi?

Kama ni kweli, basi duh tumeuwawa kifo cha mende...

Mkuu watu huwa siku hizi wanachukua kitu inaitwa FRANCHISE kwa maana unaweza ukaingia mkataba na Kampuni Mama na ukapewa nembo pamoja na Logo ukaendelea kufanya kazi kwa jinsi ninavyojua mimi sasa hawa wanaona they gat nothing to loose aibu inabaki kwa THE COCA COLA COMPANY USA.
 
Mkuu watu huwa siku hizi wanachukua kitu inaitwa FRANCHISE kwa maana unaweza ukaingia mkataba na Kampuni Mama na ukapewa nembo pamoja na Logo ukaendelea kufanya kazi kwa jinsi ninavyojua mimi sasa hawa wanaona they gat nothing to loose aibu inabaki kwa THE COCA COLA COMPANY USA.

Ni kweli. Lakini ishu moja uliyosahau kuhusu Franchise ni kwamba Franchisee anatakiwa ku-operate kutokana na standards zilizowekwa na kampuni mama. Na Franchiser huwa ana monitor closely operation mzima ya Franchisee. NA kwa kampuni ya kimataifa kama Coca-cola, lazima wawe very strictly na operation ya kampuni ya Worldwide.
 
Sasa hawa TRA watuambie ...wao kama Chombo tunachokitegemea kwenye kukusanya mapato walikuwa wapi muda wote huo kuyasema haya na ikiwezekana watuambie ni vigogo wangapi wanalinda maslahi ya Makampuni haya.

Serikali inalaumu sheria ya misamaha. Inaonekana kama TRA walikuwa wanafuata sheria ya Bunge inayowataka watoe misamaha, kwa sababu nao wanasema misamaha ni tatizo. Wabunge wanalaumu CocaCola haijalipishwa kodi lakini wanasema sheria yao ya misamaha ni sheria mbaya. Sasa kosa la nani? Au ni la Media kwa kutowauliza haya maswali wahusika?

Naomba usoma hii taarifa hapa chini halafu unambie kosa ni la nani kati ya TRA, Serikali, CocaCola, Media au Fisadi asiyejulikana...

Coca-Cola yadaiwa hailipi kodi

Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,June 05, 2008 @09:06

...Wakati huo huo, serikali imeeleza kukerwa na misamaha ya kodi inayotolewa kwa taasisi mbalimbali na kushauri zitafutwe njia za kuipunguza kutokana na kile kilichoelezwa kupunguza wigo wa mapato.

Nayo TRA ilikiri kuwa ingawa misamaha hiyo ilikusudiwa kusaidia shughuli za jamii na kuhamasisha uwekezaji, lakini inamomonyoa wigo wa kutoza kodi na inazalisha mianya ya ukwepaji kodi.

Kauli hiyo ya TRA na Serikali, kupitia kwa Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yussuf Mzee, ilichangiwa na wabunge wengi wakitaka itolewe orodha ya kampuni zinazofaidika na pia kushauri sheria zinazoruhusu misamaha hiyo, zipitiwe upya na ikiwezekana, ziondolewe.

Mwenyekiti wa Bodi ya TRA. Marcellina Chijoriga alisema makusanyo halisi ya Idara ya Forodha, Bara, mwaka 2005/06 yalikuwa Sh bilioni 883.6 ambazo kati yake, Sh bilioni 385.5 sawa na asilimia 44, zilisamehewa. Pia mwaka 2006/07 makusanyo halisi Bara, yalikuwa Sh bilioni 1,132.4 na kati yake, Sh bilioni 390 sawa na asilimia 32, zilikuwa za msamaha wa kodi.

Katika kile kilichowashtua wabunge, ni takwimu kuhusu Zanzibar ambako ilionyeshwa kuwa mwaka 2006/07, kati ya Sh bilioni 20.4 zilizokusanywa, Sh 19.6 zilikuwa ni za msamaha.

"Hii inashtua. Zanzibar inakusanya bilioni 20, lakini bilioni 19 ni za msamaha. Hii kodi inamsaidiaje mwananchi? Tumejiandaa na hili kusimama kidete, tufahamu msamaha wa kodi unamsaidia mwananchi, mwekezaji au Serikali?" alisema Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF).

Mohamed ambaye ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni alisema lazima Bunge lichukue jukumu lake la kuhakikisha sheria zinazoruhusu misamaha hiyo zinapitiwa na kubaini kama zina ufanisi au la.

Kulingana na taarifa ya TRA, makundi yaliyopewa misamaha ya kodi Bara, ni wawekezaji binafsi chini ya TIC, taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma, taasisi za dini na zisizo za serikali, miradi ya serikali na wengineo, ambavyo vyote kwa pamoja inafanya zifikie Sh bilioni 359.

Source: Daily News


Na aliye elewa mstari wa mweusi naomba anieleweshe! Billioni 19 zimekusanywa au zimesamehewa? LOL!
 
Serikali style ya ZE COMEDY
hakuna kitu sahihi wanafanya hawa watwana
 
Back
Top Bottom