Sikirimimimasikini
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 2,919
- 15,604
CNN yaripoti kuwa hatimae leo Wagner wameukomboa mji wote wa Bakhmut licha ya jitihada kubwa za Marekani + Uingereza + Ujerumani + NATO kutuma kila aina ya silaha walizoziamini (kupitia mahesabu ya kwenye makaratasi) kuwa zingekuwa mwarobaini (a.k.a. game changer) wa kuishinda Urusi vitani.
Silaha hizo zilizoshindwa na kufeli vibaya mbele ya ma-security guards wa kampuni ya ulinzi ya kirusi (Wargner group company) kwenye uwanja wa vita wa Bakhmut ni pamoja na HIMARS na HARM za mMarekani, Leopard 2 tank ya Mjerumani, challenger 2 tank ya Muingereza (hizo ni chache tu kama mifano ila zipo nyingi tele).
Prigozhin, kiongozi wa kampuni ya ulinzi ya Wagner, aliyeonekana leo akiwa ndani ya nguo za kivita kwenye safu za wapiganaji huko Bakhmut, ametangaza kuwa wamehitimisha mapigano ya nyumba kwa nyumba na kuikomboa Bakhmut yote leo mchana wa saa sita. Na akaongeza kuwa wanatarajia kuukabidhi rasmi mji huo wa Bakhmut kwa jeshi la Urusi wiki ijayo tarehe 25 May na kisha wao (Wagner) waondoke wakapumzike na kufanya mazoezi yao ya kivita kujiandaa na majukumu mengine watakayopewa na Putin.
Habari hii imeletwa na CNN pamoja na The Jerusalem Post (chombo cha habari cha taifa teule la Israel)
Cc: MK254
======
Silaha hizo zilizoshindwa na kufeli vibaya mbele ya ma-security guards wa kampuni ya ulinzi ya kirusi (Wargner group company) kwenye uwanja wa vita wa Bakhmut ni pamoja na HIMARS na HARM za mMarekani, Leopard 2 tank ya Mjerumani, challenger 2 tank ya Muingereza (hizo ni chache tu kama mifano ila zipo nyingi tele).
Prigozhin, kiongozi wa kampuni ya ulinzi ya Wagner, aliyeonekana leo akiwa ndani ya nguo za kivita kwenye safu za wapiganaji huko Bakhmut, ametangaza kuwa wamehitimisha mapigano ya nyumba kwa nyumba na kuikomboa Bakhmut yote leo mchana wa saa sita. Na akaongeza kuwa wanatarajia kuukabidhi rasmi mji huo wa Bakhmut kwa jeshi la Urusi wiki ijayo tarehe 25 May na kisha wao (Wagner) waondoke wakapumzike na kufanya mazoezi yao ya kivita kujiandaa na majukumu mengine watakayopewa na Putin.
Habari hii imeletwa na CNN pamoja na The Jerusalem Post (chombo cha habari cha taifa teule la Israel)
Cc: MK254
======