#COVID19 CNN: After death of Covid-denying president, Tanzania sets roadmap to combat the virus

kuwavimbia kwenye issue ya Corona kulitujengea heshima kubwa

Sasa subiri waje wenyewe kuhakiki wakikuta hiyo inayoitwa Corona haipo ,mitaani watablack list watu kwa utapeli
Heshima.gani tumeonekana wajinga sana .Badala ya kufuata njia sahihi za kujikinga na kutibu tukabaki kama wajima .Ndugu zetu wamekufa kizembe sana mpaka mwendazake naye umemwondoa na ikulu imeadhirika sana.Ona Kenya au Uganda kama kuna kiongozi amekufa kizembe hasa wa ikulu .
 
Sioni Kama Kuna siku watumwa wanaopenda na kushabikia utumwa wao siku moja watakuwa huru nawaona wakiwa watumwa maisha Yao yote
 
CNN wanachofurahi ni soko la chanzo zao kufunguliwa Tanzania nothing else.Magufuli alikomaa kuwa sababu hajuna tiba tuwe na home grown solution ndio tukapiga maombi,piga nyungu kujifukiza na kula zetu tangawizi tukanusurika

Kwa hili wazungu hawakuwa na hamu na sisi sasa hivi lazima wachekeleee soko kupatikana
Hili dudu litakuja tena ku test imani yenu juu ya hizo barakoa, chanjo, sanitizer na social distance zenu. Hapo ndipo kitakapoumana hasa, maana watu wametegwa na kuacha kumtegemea Mungu na kutegemea kazi za mikono ya binadamu. Hili dudu litakuja kuchora mstari, kati ya wale wanaomtegemea Mungu wa kweli na wale wanaomtegemea sanamu.
 
Ungejua hizo chanjo zilivyo bei rahisi usingeandika huu upupu wako, huku nilipo mimi wote tumepewa chanjo bure. Zimbabwe hadi muda huu washapewa chanjo za bure zaidi ya mil. 2,na mtu wa kwanza kuchanjwa alikuwa Mnangagwa, nyie kaeni na upuuzi wenu mliojazwa na marehemu ambaye corona hiyo hiyo ilimuondoa sababu ya kuamini upuuzi kama huu unaoamini wewe.
Ushachanjwa...
Hauko Tanzania...
Sisi wapuuzi...

Sasa kinachokuwasha ni nini ?

Diaspora mna bonge la identity crisis... mmekimbia Tanzania lakini kutwa hamuachi kutufuatilia...
 
Ushachanjwa...
Hauko Tanzania...
Sisi wapuuzi...

Sasa kinachokuwasha ni nini ?

Diaspora mna bonge la identity crisis... mmekimbia Tanzania lakini kutwa hamuachi kutufuatilia...
Mimi ni raia wa Tz, nikimaliza lililonileta huku nitarudi nyumbani, lazima nifuatilie nchi ambayo ndiyo makazi yangu ya kudumu mzee, ukiacha hilo vilevile familia yangu ipo Tz, usalama wa afya yao ni muhimu mno kwangu.
 
Kafa ndio kwani na nyie si mtakufa

ila hiyo michanjo na mibarakoa vaeni wenyewe sisi Mungu alishatushindia
A ha ubishi kama dagaa viongozi wako wenyewe wa dini huko kanisani kwako wanavaa barakoa sasa huyo mungu unayemuomba tofauti na viongozi wa dini yako ni yupi?

Aise nyie watu magufuli aliwaharibu sana vichwa vyenu.
 
Mwendazake aende tu jamani ametukinaishaaaa.....hakuwa focus wala road map uchumi
 
Back
Top Bottom