Clouds FM na uchaguzi mkuu wa TFF!

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Nilishindwa kuwaelewa Clouds FM kwa kuamua kukusanya kura za ama KUMKUBALI au KUMKATAA mheshimiwa L. Tenga wakati hoja NZITO ni kwa nini TFF haijatangaza tarehe ya uchaguzi mkuu kama sheria inavotaka.
Mie nionavo hawa TFF wanafanya makusudi kuendelea kwa muda wanaouona wao una maslahi yao ndipo watutangazie tarehe ya uchaguzi. Hebu tujaribu kujiuliza kwa nini chaguzi za mikoani zinavurugwa hivi? Wakati uchaguzi unakaribia wao wanatutangazia ULAJI wa kuteuliwa na CAF kwenye shughuri mbalimbali, sasa wakati RANK ya timu yetu ya taifa ni AIBU wao wanajisifia kwa uteuzi, tujiulize hawa jamaa wapo hapo kwa MANUFAA ya NCHI au YAO binafsi?
Nakumbuka Tenga alichaguliwa 2004 na rais wa jamhuri JK alichaguliwa 2005 na aliwaagiza watafute kocha wa soka na kulipwa na rais wa jamhuri, hawakufanya hivo mpaka JK akahamaki na ndipo alipoletwa Maximo ambaye aliipandisha timu yetu mpaka tukacheza na BRASIL! Sasa angalia walivovurunda na ajabu Clouds FM wanampigia KAMPENI bwana Tenga, hii ni AIBU.
TAFAKARI.
 
kwani ulikuwa hujui TFF ni Tanzania Fitna Federation na tenga tushamchoka hanajipya ndio maana hata kina pele walisema inapopaswa kubadilisha inabidi ubadilishe lakini muwe makini na mabadiliko hayo hapa ni kwamba tenga hana jipya asepe zake..
 
Tatizo clouds wanamaslahi na chaguzi za TFF, wanagombea na kama media ilishafanya biashara na TFF then integrity na maana ya media kuwa fair inakuwa haipo. Kama watangazaji wa vipindi bongo flavour walivyogeuka kuwa mapromota na waimbaji na hawa wa clouds walitakiwa kuacha kutangaza na kwenda kugombea TFF.

Isije kuwa watu wa serikali ndio wanakomaliwa hata hawa wa media binafsi pia wanatakiwa ku declare interest zao binafsi na za wamiliki wao. Very unfair wao wanapata promo na wagombea wengine hawapati. Kama dili la kuprint tickets walianza na wakatoswa baada ya mzabuni mwingine kushinda. Sasa isijekuwa wanajipanga kuingia ili tenda zao zipite bila pingamizi.
 
Back
Top Bottom