Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,681
- 1,698
Nilishindwa kuwaelewa Clouds FM kwa kuamua kukusanya kura za ama KUMKUBALI au KUMKATAA mheshimiwa L. Tenga wakati hoja NZITO ni kwa nini TFF haijatangaza tarehe ya uchaguzi mkuu kama sheria inavotaka.
Mie nionavo hawa TFF wanafanya makusudi kuendelea kwa muda wanaouona wao una maslahi yao ndipo watutangazie tarehe ya uchaguzi. Hebu tujaribu kujiuliza kwa nini chaguzi za mikoani zinavurugwa hivi? Wakati uchaguzi unakaribia wao wanatutangazia ULAJI wa kuteuliwa na CAF kwenye shughuri mbalimbali, sasa wakati RANK ya timu yetu ya taifa ni AIBU wao wanajisifia kwa uteuzi, tujiulize hawa jamaa wapo hapo kwa MANUFAA ya NCHI au YAO binafsi?
Nakumbuka Tenga alichaguliwa 2004 na rais wa jamhuri JK alichaguliwa 2005 na aliwaagiza watafute kocha wa soka na kulipwa na rais wa jamhuri, hawakufanya hivo mpaka JK akahamaki na ndipo alipoletwa Maximo ambaye aliipandisha timu yetu mpaka tukacheza na BRASIL! Sasa angalia walivovurunda na ajabu Clouds FM wanampigia KAMPENI bwana Tenga, hii ni AIBU.
TAFAKARI.
Mie nionavo hawa TFF wanafanya makusudi kuendelea kwa muda wanaouona wao una maslahi yao ndipo watutangazie tarehe ya uchaguzi. Hebu tujaribu kujiuliza kwa nini chaguzi za mikoani zinavurugwa hivi? Wakati uchaguzi unakaribia wao wanatutangazia ULAJI wa kuteuliwa na CAF kwenye shughuri mbalimbali, sasa wakati RANK ya timu yetu ya taifa ni AIBU wao wanajisifia kwa uteuzi, tujiulize hawa jamaa wapo hapo kwa MANUFAA ya NCHI au YAO binafsi?
Nakumbuka Tenga alichaguliwa 2004 na rais wa jamhuri JK alichaguliwa 2005 na aliwaagiza watafute kocha wa soka na kulipwa na rais wa jamhuri, hawakufanya hivo mpaka JK akahamaki na ndipo alipoletwa Maximo ambaye aliipandisha timu yetu mpaka tukacheza na BRASIL! Sasa angalia walivovurunda na ajabu Clouds FM wanampigia KAMPENI bwana Tenga, hii ni AIBU.
TAFAKARI.