Click here to find out how 'Transformers: Dark of the moon' was made

wakati nasoma sekondari shule yetu ilikuwa nzuri sana kwa drama, tulikuwa na mashindano ya drama na shule za wilaya ile. tulikuwa na mwalimu alikuwa mtunzi mzuri sana wa michezo, yaani hata tukiigiza sasa tunaweza tukawa wazuri sana kuliko haya masinema yao.
Nilikuwa pia actor mzuri sana. nakumbuka yaani ni kama somo. mnapewa scripts, unaisoma mwezi mzima, then mnaanza mazoezi, ni kila siku muda ambao wenzenu wanaenda kazi za nje nyie zoezi kwa zaidi ya miezi, yaani mpaka muende mashindano ni ndani ya miezi kadhaa ya kufundishwa na ku-practice. kuna vipaji, yes, lakini kufanya kitu kizuri kunahitaji kufundishwa.

sasa aembu jiulize ni wasanii wangapi wa hapa bongo wamekwenda shule kujifunza sanaa ya uigizaji? Asilimia kubwa wanaishia kudandia treni tena kwa pembeni wala sio kwa mbele tena.
 
Hapo umenkumbusha tena! Kwa mwaka utakuta ray katoa movie 10 so it mean hapo kla movie itakua imeshugulikiwa kwa mwez m1 na siku 6.,. Hapo ubora utatoka wapi.... Kngne unakuta hemed kaweka wave kwenye nywele... Sasa story inakuja eleza kuwa ni baada ya miaka 10... Unakuta bado kaweka wave vile vile... So hapo kauvaa uhusika kivipi

Ndio hapo sasa...hawaoni jinsi wenzetu wanavyoweza kuuvaa uhusika...kama mtu akiigiza kama kijana basi ananyoa midevu yote na kubaki kipara ili aonekane kijana na kama akifia umri wa utu uzima basi anaacha ngozi ichoke choke kidogo na kuachia midevu ili anonekane mtu mzima lakini sisi muvi nzima umeweka kalikiti.
 
Ah ha ha ha, eti anapaa na ungo, aisee umenichekesha. Halafu mwisho wa muvi kwenye credits utakuta:
lighting: Lukansola
location: Lukansola
Costume: Lukansola
Director: Lukansola
na kadhalika...

Kweli mkuu wala sio masihara...mimi huwa muonekano wa mhusika unaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kufikisha ujumbe kwa jamii...Embu pata picha...wewe umeshazoea kuangalia movie za Anorld Schwarzenegger na kila movie zake zote anazocheza huwa ni movie za action na kubeba mijegeja (bunduki)...hii ni kutokana na mwonekano na fani yake halafu ghafla uje umuone Anorld anapaa na ungo hivi huo ujumbe uliokusudiwa kukufikia utakufikia kweli? si utaona hiyo movie kama mzaha?
 
Ya nini kujipa stress wakati ile ni starehe...??? Nadhani tatizo kubwa linalofanya wasanii wetu wasiendelee kwanza kabisa ni tamaa, pili ujuaji mwingi...kila mtu anataka kujifanya anajua kuliko mwenzake, tatu ni kuingia katika fani hii ya kuigiza bila kupata mafunzo. hata kama jamani mtu ana kipaji ili kipaji chake kiweze kukua na kuwa bora laxima apate mafunzo ili kuongeza ujuzi na ufanisi lakini wenzetu huwa tunaokotz tu na kuwapachika matokeo yake tunaishia kuigiza kama ngonjera

na mafunzo yenyewe jamani sio lazima iwe chuoni kama huna uwezo, kwenye mtandao kuna kila kitu unachotaka kujua, jengeni tabia ya kupenda kujisomea, badala ya kuishia facebook ku like piacha, sisemi fb ni mbaya lakini inatumika vibaya, (na wengi wetu)
 
nimeiona umetulia sana, nakubaliana na wewe issue ya msingi hapa ni ujuzi sio mitambo advanved.

tatizo waswahili tunapenda sana 'excuse'.

angalia sinema zetu kwa mfano, kwanza lazima ziwe na majina ya kizungu wakati ndani 99.5% lugha inayotumika ni kiswahili, asilimia .5 inayobaki ni kizungu kibovu kabisa,

kwa mfano ili ijulikane kwamba huyu ni mke lazima mwanamume aseme 'mke wangu' kila anapoongea naye... hiyo nayo tunahitaji mitambo ya kisasa kuirekebisha?

au kutengeneza movie ambayo itamaliza story bila kuwa na part 2 inahitaji mitambo ya kisasa pia?

hata ukiletewa studio ya disney nyumbani, kama huna ujuzi ni kazi bure.

Nasema LIKE!
 
Back
Top Bottom