'Classes' zina raha zake, husahaulisha hadi kuhusu wananchi

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,504
Hebu vuta picha kwenye sherehe za kitaifa: kabla hata ya sherehe husika mhusika analetewa mualiko nyumbani kwa bashasha na heshima kubwa. Ukumbini au uwanjani, mhusika anaketi kwenye sehemu ya 'wakubwa na wazito' wenzake kufuatilia kinachojiri huku akichagiza na vistori vya hapa na pale na wakubwa na wazito wenzake.

Kwa pembeni, kuna gari ya maana inamsubiri mhusika. Mhusika anaitwa kwenye mimbari kutoa kaneno kadogo akishangiliwa na wahudhuriaji. Picha za pamoja baada ya shughuli hufuata huku stori zikinoga na wenzake wakiwa wanakumbushana raha na karaha za kazini na hata majuu safarini. Wanacheka na kugonga mikono.

Muda wa misosi unawadia. Misosi na vinywaji kadiri ya avitakavyo vinawekwa mbele ya mhusika. Akiwa nadhifu, mhusika anapita kwenye mstari wa misosi huku akiendeleza vistori vya hapa na pale na wenzake. Anachukua kadiri ya atakavyo na kinywaji akipendacho. Anakula na kunywa atakavyo. Stori tamutamu zinaendelea.

Baada ya yote hapo, gari zuri na la kifahari linasogea. Anawapungia marafikize na kuingia kuelekea nyumbani, ofisini au mahali pengine. Dereva anaondoa gari na wanatokomea kuelekea huko. Raha sana. Ni mambo ya 'classes' hayo. Ndiyo hasa yanayofanya wanasiasa wasahau kwa muda hata shida za wanachi wao.

Ni raha zinazomsukuma mhusika kuhama au kuhamia chama cha kisiasa. Kuwa karibu na marafiki zake na heshima yake ni jambo muhimu. Kuwa sehemu ambayo una uchaguzi wa maneno ili ushangiliwe ni burudani tosha. Kuwa kwenye tabaka lako ni jambo la heri sana. Nani aliye siasani hataki raha hizi? Wananchi myajue haya na kukubali matokeo wakati mwingine.
 
ndio maana Mbowe kajisalimisha kwa CCM, hebu fikiria Mbowe ni kiongozi wa kambi ya upinzani bajeti yake ni milioni 100 kwa mwezi anazolipwa, bado ruzuku ya chama milioni 300 kwa mwezi, bado mshahara wake wa ubunge na marupurupu mengine, akifikiria mwakani vyote hivi havitakuwepo lazima achanganyikiwe, ndio maana CHADEMA wanampigia magoti Magufuli wafanye maridhiano
 
Ndio classes zinanoga! Tusisahau kutoka kuchunga mbuzi wilaya mmoja wapo mkoa wa Geita hadi chama kikongwe kwa ukombozi Afrika kuimba mapambio ya jina lako sio mchezo! Au kutembea na msafara wa magari lukuki na angani helicopter kwa nini kwa mabadiliko hayo usione wewe kama sio mungu basi ni malaika mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ambao wamefika huko kwa msaada wa kafara za kutisha ambazo endapo bwana mshana angeweza kutufunulia tusingethubutu hata kupishana nao barabarani
 
Hebu vuta picha kwenye sherehe za kitaifa: kabla hata ya sherehe husika mhusika analetewa mualiko nyumbani kwa bashasha na heshima kubwa. Ukumbini au uwanjani, mhusika anaketi kwenye sehemu ya 'wakubwa na wazito' wenzake kufuatilia kinachojiri huku akichagiza na vistori vya hapa na pale na wakubwa na wazito wenzake.

Kwa pembeni, kuna gari ya maana inamsubiri mhusika. Mhusika anaitwa kwenye mimbari kutoa kaneno kadogo akishangiliwa na wahudhuriaji. Picha za pamoja baada ya shughuli hufuata huku stori zikinoga na wenzake wakiwa wanakumbushana raha na karaha za kazini na hata majuu safarini. Wanacheka na kugonga mikono.

Muda wa misosi unawadia. Misosi na vinywaji kadiri ya avitakavyo vinawekwa mbele ya mhusika. Akiwa nadhifu, mhusika anapita kwenye mstari wa misosi huku akiendeleza vistori vya hapa na pale na wenzake. Anachukua kadiri ya atakavyo na kinywaji akipendacho. Anakula na kunywa atakavyo. Stori tamutamu zinaendelea.

Baada ya yote hapo, gari zuri na la kifahari linasogea. Anawapungua marafikize na kuingia kuelekea nyumbani, ofisini au mahali pengine. Dereva anaondoa gari na wanatokomea kuelekea huko. Raha sana. Ni mambo ya 'classes' hayo. Ndiyo hasa yanayofanya wanasiasa wasahau kwa muda hata shida za wanachi wao.

Ni raha zinazomsukuma mhusika kuhama au kuhamia chama cha kisiasa. Kuwa karibu na marafiki zake na heshima yake ni jambo muhimu. Kuwa sehemu ambayo una uchaguzi wa maneno ili ushangiliwe ni burudani tosha. Kuwa kwenye tabaka lako ni jambo la heri sana. Nani aliye siasani hataki raha hizi? Wananchi myajue haya na kukubali matokeo wakati mwingine.
Hadithi ya alfu ulelaulela
 
The political elite sio? Wengi wanataka wawe humo. Kuna mmoja leo amewajibu wenzie waliomba maridhiano na demokrasia, kwamba yeye afundishwi demokrasia!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom