CIA to M16: Hakikisheni Nyerere Hafanikiwi

Dar_Millionaire

JF-Expert Member
Aug 6, 2008
227
82
Wadau wa JF,

Kuna hii stori nilipata kuisikia kitambo ila sikuweza kufuatilia ukweli wake. Kwa mnaojua undani wake (kama ni kweli au la) naomba michango yenu.

Stori yenyewe ni kwamba baada ya Nyerere kutangaza sera ya Ujamaa huku dunia ikiwa imegawanyika kati ya ubepari na ukomunisti, upande wa ubepari (hususani kinara wao Marekani na mchumba wao Uingereza) walikuwa na shauku ya kujua "Ujamaa" ni kitu gani.

Inasemekana jibu walilopata toka kwa Nyerere ni kwamba Ujamaa sio tafsiri ya moja kwa moja ya ukomunisti kama ambavyo walikuwa wanadhania. Bali ni sera inayolenga kuunganisha jamii kwa kuzingatia utamaduni wa asili wa kushirikiana uliokuwepo miongoni mwa Waafrika. Kwamba lengo sio kuiga sera za nje za kiuchumi bali kujenga nguvu za kiuchumi kwa kuzingatia utamaduni na mazoea tuliyokuwa nayo waafrika hata kabla ya ukoloni.

Inasemekana Wamarekani na Waingereza baina yao walikiri kwamba Nyerere alikuwa amepatia kwa kuzingatia utamaduni na asili za watu katika kutengeneza sera ya kiuchumi. Kwa upande mwingine inasemekana waliona kuwa mafanikio ya sera yake mpya (ambayo walihisi ingefanikiwa) yangesababisha nchi zingine za Afrika kuiga mfumo wa Tanzania na hivyo kutengeneza muungano wa kiafrika ambao wao hawakupenda utokee.

Hivyo inasemekana CIA walitoa classified memo kwenda M16 ikiwa na agizo moja kuu kwamba M16 wahakikishe Nyerere hafanikiwi.

Mdau aliyenipa hii stori anadai memo hiyo iligundulika hivi karibuni baada ya kuexpire muda wake toka kwenye classified materials.

Binafsi ningependa kupata resources za kuthibitisha kama hii stori ni kweli au sio kweli. Wenye data naomba tuhabarishane.

//DM
 
Hakuna lolote hapo....yaani Wanyamwezi wahangaike na kukosa usingizi kisa kanchi kadogo na maskini ka kutupwa kaitwako Tanganyika/ Tanzania....I'm not buying it.....
 
This is the biggest fairly tale I have ever heard! Yes, nchi za Magharibi zilifanya kila kitu kumu-undermine Mchonga kipindi chote cha vita baridi, ila hili la kuogopa maana ya "ujamaa" ni kichekesho cha millenia.
 
msiitupie hoja hiyo pembeni; mngejua tu; nenda kwenye National Archives mtashangaa walichokuwa wanazungumza wamarekani na Britain kuhusu Tanzania. Docs zao nyingi zilikuwa zina ban ya miaka 30; na nyingine miaka 40... za interests hasa ni za wakati wa mapinduzi na muungano na zile za wakati wa Azimio la arusha...
 
msiitupie hoja hiyo pembeni; mngejua tu; nenda kwenye National Archives mtashangaa walichokuwa wanazungumza wamarekani na Britain kuhusu Tanzania. Docs zao nyingi zilikuwa zina ban ya miaka 30; na nyingine miaka 40... za interests hasa ni za wakati wa mapinduzi na muungano na zile za wakati wa Azimio la arusha...

Lately docs nyingi za 50s.60s zinakuwa released kwenye site ya CIA...I enjoyed reading ya Cubam Missile Crisis..bado sijapata ya Tanzania lakini I will keep an eye on that better yet nitamuuliza boy scout mmoja anipenyezee kama ipo.
 
Mimi kuna nilizosoma in late nities... na mwanzoni mwa hii ya 2000.. sijajiupdate. Ila ni docs nzuri sana kwani zinakupa insight ya mtu wa pembeni anayeangalia matukio ya Tanzania kutoka nje. Very interesting. As a matter of fact njia rahisi ya kuanza kama mtu anataka kusearch aende kwenye tovuti ya secretary of state..
 
Hakuna lolote hapo....yaani Wanyamwezi wahangaike na kukosa usingizi kisa kanchi kadogo na maskini ka kutupwa kaitwako Tanganyika/ Tanzania....I'm not buying it.....



kUOGOPWA KWAKE SIO KUWA ILIKUWA NCHI KUBWA AMA NA NGUVU BALI ITIKADI YA UJAMAA ILIONEKANA KUWA INAWEZA KUWA NA NGUVU NA MAFANIKIO.
 
NN angalia hii....
ojhxy1.jpg

2di2fr5.jpg
 
Dar_Millionaire
Siasa saa nyingine ni muhimu kutumia akili...Inawezekana washauri wa mwalimu na wenyewe hawakuwa wazuri sana...Sasa alipowaambia wazungu kuwa ni uatamaduni wa mwafrika na huku yeye ni mkatoliki wapi na wapi?

Halafu ata the same time yeye uchina na ushirikiano na Urusi na Cuba huku akisema hafungamani na upande wowote si ni kujaribu kupaka chokaa na kudai ni rangi?

Mwalimu alitawala kipindi kigumu sana na alikuwa kama sungura mjanja...Lakini sungura mjanja asipopata ushirikiano wa wanyama wengine huko porini maisha yake ni HATARINI.

Kwa kipindi kile vita baridi ndio ilipamba moto.

Pia kama unataka tukuelewe vizuri zaidi..Tunaomba utuambie ujamaa ni nini na ni kivipi unahusiana na utamaduni wa mwafrika...Yani kwenye nyanja gani...Maana utamaduni wa mwafrika umegawanyika kwenye nyanja kuu tatu kama ilivyo kwenye tamaduni zote duniani...Kiuchumi, Kisiasa na kijamii.

Kiuchumi alishirikiana na nani?

Kijamii na kisiasa je?

Pili...Hapo kwenye hiyo info yako kama kweli wewe ni DAR MILIIONAIRE...Nimehighlight hapo kwenye issue ya classified....NIMEONA NIKUPE DEFINTION RAHISI NA SAHIHI KUHUSU HIZO HABARI ZAKO ZILIZOKUWA CLASSIFIED BEFORE...NI KWAMBA KWA MUJIBU WA HAPO KWENYE HIGHLIGHT....HIVI SASA ZIKO DECLASSIFIED...MEANS KWAMBA UNAWEZA UKAZILETA HAPA JF PASIPO MIKWARUZO YOYOTE ILE.

Halafu na Nyie huko bongo pia muanze declassifications.
 
Hapa hamna lolote. Tanzania enzi hizo ilikuwa maskini wa kutupwa. Kama ni kweli Wamarekani walikoseshwa usingizi na sera za Nyerere basi walichemsha. Bado siamini....hizi ni stori tu.
 
Kama Unakumbuka , baada ya Uhuru na Baada ya Waisrael Kujenga Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, Nyerere aliwafukuza kwasababu walikuwa wameshaanza kujemege nchi.

As you know matatizo mengi unayoyaona Duniani yanasababiswa na Intrest za waisrael, Kwahiyo Nyerere aliwekwa kwenye Kundi la anti-sematic. Na ndio maan Nyerere kafanya mambo mengi sana Kuliko mandela lakini mandela ni maarufu kukiko Nyerere.

Ukitaka kujua How waisrael wanaicontrol Dunia go to this paper was published by Havard University it has enough information

http://ksgnotes1.harvard.edu/Research/wpaper.nsf/rwp/RWP06-011/$File/rwp_06_011_walt.pdf
 
LeoKweli,

Interest gani hizo za Waisrael? Watu wenyewe kwanza hata hawajaendelea hivyo sasa hizo interest zao zinazosababisha hayo matatizo ya dunia ni zipi? Wamarekani kila mwaka wanawapa mabilioni ya dola. I smell a kind of anti-semitism here blame the Jews for everything...
 
Hapa hamna lolote. Tanzania enzi hizo ilikuwa maskini wa kutupwa. Kama ni kweli Wamarekani walikoseshwa usingizi na sera za Nyerere basi walichemsha. Bado siamini....hizi ni stori tu.

Duhh, hii imetulia kweli kweli!!!!!! Swali la kwanza lilikua na jibu, just kuonyeshwa tu cover, sasa nadhani lazima ufungue ndani na kuona kwamba na Tanzania (Nyerere) ilikuwamo (na imo) katika list ya majukumu ya CIA
 
nyani ngabu,read between the lines,mpaka barack obama anaenda kuomba kura za americans,of all places in israel,na ana backtrack on some issues in favour of israel should give you an idea of the cloat israel is carrying on world affairs and happenings.AGAIN CIA were intrested in tanzania cause this was the height of the COLD WAR-either you were east or west.tanzania falling in the hands of the east was creating great discomfort in western capitals
 
nyani ngabu,read between the lines,mpaka barack obama anaenda kuomba kura za americans,of all places in israel,na ana backtrack on some issues in favour of israel should give you an idea of the cloat israel is carrying on world affairs and happenings.AGAIN CIA were intrested in tanzania cause this was the height of the COLD WAR-either you were east or west.tanzania falling in the hands of the east was creating great discomfort in western capitals

Hiyo clout ya Israel iko overrated!! Israel bila Marekani haipo....
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom