CIA Hawakufahamu Uwepo Wa Che Dar

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Leo Oktoba 9 ni miaka 40 tangu kuuawa kwa mwanamapinduzi Che Guevara nchini Bolivia. Nimepata kukisoma kitabu kiitwacho " The African Dream"- The diaries of the revolutionary war in the Congo. Ama hakika ni kitabu chenye maelezo yenye kusisimua, kufurahisha na kusikitisha juu ya mwanamapinduzi huyu na harakati zake za mapambano ya ukombozi wa kimataifa.

Che aliingia Dar April 1965, alikutana na Nyerere na kupata baraka zake. Aliingia Mashariki ya Congo akiwa na kikosi cha askari 100; Hawa ni Wa-Cuba weusi waliopata mafunzo ya kijeshi Havana bila kuelewa kuwa walikuwa wanakwenda Congo. Uwepo wa Che Guevara jijini Dar April 1965 haukufahamika na wengi.

Hata CIA hawakuelewa hilo. Hadi mwaka 1990 CIA waliamini kuwa Che Guevara aliingia Congo akitokea Congo Brazaville. Kwamba Che Guevara alikuwa Dar kwa juma moja na zaidi unadhihirisha ukweli wa simulizi kuwa Che Guevara alitembelea mgahawa wa Zahir ( Sasa New Zahir Restaurant) mtaa wa Msikiti. Che alikuwa na mazoea ya kunywa chai na kula chakula mahala hapo.

New Africa Hotel kulikuwa na mgahawa maarufu kule juu kabisa, lakini pale pangemfanya aonekane kirahisi hata na mawakala wa CIA. Che Guevara anamweleze Laurent Kabila ( Baba yake Joseph Kabila) kama mtu ambaye hakuwa makini katika kuendesha harakati za mapambano.

Che anaandika; kuwa Kabila alipenda sana pombe, hakuonekana kwenye uwanja wa mapambano, mara nyingi alituma ujumbe wa mdomo au maandishi kutoa maelekezo. Che alikwenda na kikosi chake Mashariki ya Kongo bila ya mwenyeji wake, Laurent Kabila. Kiumri, Laurent Kabila alikuwa na miaka 26 tu wakati huo. Kuhusu umri wa Kabila Che Gueavara anandika hivi; " Kabila is young, and it is possible that he will change. But I have very great doubts about his ability to overcome his defects in the environment in which he operates".

Nisimalize utamu wa kitabu; tafuta kitabu hiki ukisome. Kinatoa picha tofauti na kutusaidia kuelewa baadhi ya sababu zinazopelekea vita vinavyochukua muda mrefu katika ukanda wa Maziwa Makuu.

Kwa habari zaidi katika picha tembelea; http://mjengwa.blogspot.com
 
Nafikiri CIA walikuwa wanajua mizunguko ya Che kwani kwa walikuwa wamo kwenye mipango ya kumkamata ambapo kwa wakati ule yeye alikuwa bado ni waziri wa viwanda na mkurugenzi wa benki kuu ambapo pia alikuwa akisaini noti kwa jina lake la "che" tokea mwaka 1961 hadi 1965.

CIA wana kitengo maalum "task force" cha kushughulikia mtu au watu wanaokwamisha juhudi za kibepari mahali popote pale duniani na ushahidi tumeuona pale walipokiri mwaka jana kama sikosei kwamba wakihusika na kifo cha Patrice Lumumba ambae ile hotuba alioitoa siku Congo ilipopata uhuru, iliwaudhi sana mabepari.

Ernesto "Che" Guevara de la Serna, alijiuzuru kazi hiyo April mwaka 1965 na kuwa kiongozi wa uasi katika nchi ya Bolivia. Ni katika kipindi hicho ndio alipata nafasi ya kuja kuona namna ya kusaidia harakati za kimapinduzi barani Afrika na kuona kwamba waafrika ni watu vulnerable na tusio na msimamo katika kutekeleza baadhi ya maamuzi ambayo hupangwa.

Katika kitabu chake cha "Guerrilla Warfare" cha mwaka 1960 anasema nanukuu –

"The guerrilla band is an armed nucleus, the fighting vanguard of the people. It draws its great force from the mass of the people themselves. The guerrilla band is not to be considered inferior to the army against which it fights simply because it is inferior in fire power. Guerrilla warfare is used by the side which is supported by a majority but which possesses a much smaller number of arms for use in defense against oppression" – mwisho wa kunukuu.

Alipokuwa Congo alikuwa akiliandaa kundi la "Lumumba Batallion" ambalo lilishiriki katika vita vya waasi dhidi ya serikali ya Mabutu. Hata hivo hakupendezwa na utendaji wa kazi wa Laurent Kabila ingawa mwanzoni alipenda na aliandika katika "diary" yake kwamba nanukuu- "Africa has a long way to go before it reaches real revolutionary maturity,"- mwisho wa kunukuu.

Hizo sehemu mbili kuhusu mtazamo wa comrade "Che" kwa Afrika ni muhimu sana kwa sisi waafrika lakini kwa sasa sidhani kama nguvu ya ubepari inaweza kuzimwa kabisa, ingawa maraisi Hugo Chavez wa Venezuela na Morares wa Bolivia wamejaribu kutumia njia inayoitwa "a third way" ambayo haiwapokonyi mali mapebari mali zao moja kwa moja bali kukaa nao mezani na kuwapa sera zako za kiuchumi na zinazoonesha kuzingatia maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.


Kuna vitabu vingine vingi tu ambavyo kama kuna mtu anapenda kusoma mawazo ya "Che" ambavyo naviorodhesha hapa chini:

The African Dream: The Diaries of the Revolutionary War in the Congo, 2001 (trans. by Patrick Camiller)
Che in Africa: Che Guevara's Congo Diary by William Gálvez (1999
Guerrilla Warfare (1961)
Guerrilla Warfare: A Method (1963)


Ila namalizia kwa kutoa onyo kwamba hapa sitoi shauri namna yoyote ile ya kuwa muasi bali ni kusoma tu kazi za comrade "Che" na kutafakari maisha ya leo ya mkulima na mfanyakazi wa Afrika popote pale alipo.
 
Sounds like Tanzania is already in a guerilla warfare, the weapon used is the voice of the oppressed which they are using to boo their oppressors. There is every indication that the weapon is very effective.
 
Back
Top Bottom