Chuo Kitakachoanzishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitakua mkombozi kwa chama na Watanzania

Troll JF

JF-Expert Member
Feb 6, 2015
7,804
12,224
Wakuu mlisikia Humphrey Polepole Akisema chama kikongwe chenye Ushawishi Mkubwa nchini kinatarajia kufungua chuo kwa ajili ya kunoa makada wake.

Nikiwa kama Mwananchi nisiye na chama ninaunga Mkono juhudi hizi za CCM za Kuanzisha chuo kwani kitasaidia kuwakuza kisiasa na mwanachama wao kukijua chama na kuweza kutishia uhai wa vyama vinavyoibuka kwa sasa kwani vyenyewe vimekua havina Sera thabiti za kuzisimamia.


Mfano ACT wazalendo wametumia siku nzima Kujadili mambo ya Ujamaa ambayo hayapo katika Ulimwengu wa sasa.

Huku CHADEMA wakionekana wakikosa kile wanachokisimamia hasa.


IMG_20161218_092045.jpg
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Mmeamua kuhalalisha LB7 kabisaaa.
Hongera yenu Tanzania ya Viwanda
 
Back
Top Bottom