ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
61,957
72,354


Chuo Kikuu Mzumbe kinatarajia Kumtunuku Rais Samia Shahada ya Udakatri wa Heshima katika Uongozi wa Chuo kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kuboresha Elimu ya Juu Nchini hasa miundombinu,Utafiti na kuongeza idadi ya udahili.

Hiyo itakuwa ni Shahada ya 5 Kwa Rais Samia na Shahada ya 1 kutolewa na Chuo Kikuu Mzumbe.

Ikumbukwe Rais Samia ni alumni wa Mzumbe Hongera Rais Samia, jitihada zako zitambuliwe Sasa Ukiwa hai na Kila mtu anaona.👇👇

Leo Jumapili, Novemba 24, 2024 ni mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mkoa wa Morogoro.

IMG_0911.jpeg
Katika mahafali hayo yatakayofanyikia chuoni hapo,
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan atatunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima katika Uongozi ya Chuo Kikuu Mzumbe.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa William Mwegoha amesema hiyo itakuwa shahada ya kwanza ya heshima kutolewa na chuo hicho tangu kuanzishwa kwake.

Shahada hiyo ya udaktari wa heshima itakuwa ya tano Rais Samia kuoewa tangu alipoingia madarakani Machi 19, 2021 akichukua kijiti cha mtangulizi wake, hayati John Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021.

Shahada nyingine nne ametunukiwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Tanzania), Chuo Kikuu cha Zanzibar, Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru (India) na Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki.

IMG_0910.jpeg
Aidha, Profesa Mwegoha amesema suala la usawa wa kijinsia limepiga hatua chuoni hapo akitolea mfano, wahitimu wa mwaka huu,"ni karibu 50/50 kwani asilimia 50.2 ya wahitimu ni wanaume na asilimia 49.7 ni wanawake. Naweza kuona jinsi tunavyopiga hatua kwa vitendo."


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima katika Uongozi ya Chuo Kikuu Mzumbe na Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein kwenye Mahafali ya 23 ya Chuo Kikuu Mzumbe Mkoani Morogoroyaliyofanyika katika eneo la Maekani, Kampasi Kuu Morogoro tarehe 24 Novemba, 2024. Shahada hiyo ni ya kwanza katika ngazi hiyo ya Uongozi kutolewa na Chuo hicho tangu kuanzishwa kwake

samia1.jpg
samia2.jpg
samia3.jpg

Shahada nyingine za Udaktari wa Heshima soma viunganishi hapa chini

Rais Samia atunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu ya Usimamizi ya Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), leo Desemba 28, 2023
Rais Samia Atunukiwa Udaktari wa Uchumi (Doctorate of Economics Degree) Uturuki
Rais Samia atunukiwa Udaktari wa Heshima kutoka Chuo Kikuu cha Ankara, Uturuki, leo Aprili 18, 2024
Rais Samia atunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa, Korea, Juni 3, 2024

My Take
Hata hili Chadema watapinga ila Sasa data za takwimu zinawakataa.

Mfano mzuri ni mradi huu wa kupanua Elimu ya Juu Nchini ambapo taasisi 23 za Elimu ya Juu zinaendelea na kazi ya Ujenzi wa Miundombinu ya Kujifunzia.

Aidha Mikoa 15 ambayo hakikuwahi kuwa na Vyuo Vikuu au Matawi ujenzi unaendelea.Hii ni kazi ya Kutukuka ya Rais Samia. Haya yote yanatokea Chini ya Samia 👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DCr7oyLOtS4/?igsh=MWF5NWIzNHVhcm1mOQ==
 
Chuo Kikuu Mzumbe kinatarajia Kumtunuku Rais Samia Shahada ya Udakatri wa Heshima katika Uongozi wa Chuo kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kuboresha Elimu ya Juu Nchini hasa miundombinu,Utafiti na kuongeza idadi ya udahili.

Hiyo itakuwa ni Shahada ya 5 Kwa Rais Samia na Shahada ya 1 kutolewa na Chuo Kikuu Mzumbe.

Ikumbukwe Rais Samia ni alumni wa Mzumbe Hongera Rais Samia,jitihada zako zitambuliwe Sasa Ukiwa hai na Kila mtu anaona.👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DCvjacQtUGw/?igsh=dnc4ZXRmN3drN2c=

View: https://youtu.be/TrtUv3f9Vqw?si=AL1WHw-cSlXDFJ62

My Take
Hata hili Chadema watapinga ila Sasa data za takwimu zinawakataa.

Mfano mzuri ni mradi huu wa kupanua Elimu ya Juu Nchini ambapo taasisi 23 za Elimu ya Juu zinaendelea na kazi ya Ujenzi wa Miundombinu ya Kujifunzia.

Aidha Mikoa 15 ambayo hakikuwahi kuwa na Vyuo Vikuu au Matawi ujenzi unaendelea.Hii ni kazi ya Kutukuka ya Rais Samia. Haya yote yanatokea Chini ya Samia 👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DCr7oyLOtS4/?igsh=MWF5NWIzNHVhcm1mOQ==

Uchawa unavyoliangamiza taifa😐
 
Samia anatakiwa apewe phd na hata full professor tittle kutoka vyuo vikuu vyote Tanzania ambavyo wiko zaidi ya 30. Wampe hizo phd kadri anavyotaka, wampe tu za kutosha, wampe hata phd tatu tatu kila chuo.

Inatakiwa kila ndaki ama college ya chuo impe samia phd, mfano UD tuanze na udbs, coet na kadhalika wampe phd same na kwa vyuo vyote.

Maprofesa njaa unategemea watafanya nini zaidi ya hicho?
 
Back
Top Bottom