Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kumtunuku Msekwa shahada ya heshima ya udaktari

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,009
9,874
Katika mwendelezo wa mahafali ya 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Spika mstaafu, Pius Msekwa atatunukiwa shahada ya heshima ya udaktari.

Mahafali hayo yanayoenda sambamba na maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa chuo kikuu hicho pia yatamtunuku shahada ya heshima ya uzamivu Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah.

Taarifa iliyotolewa leo na makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa William Anangisye inasema Msekwa na Nandi-Ndaitwah watakuwa kati ya wahitimu 7,091 watakaotunukiwa shahada zao zikiwamo 82 za uzamivu.

“Chuo kitamtunuku shahada ya heshima ya udaktari Pius Msekwa ambaye alikuwa makamu mkuu wa chuo wa kwanza wakati kinaanzishwa mwaka 1970. Kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 10 chuo kinatoa bure huduma mbalimbali kwa jamii kama sehemu ya maadhimisho ya mahafali ya 50,” amesema Profesa Anangisye.

Licha ya wahitimu wa uzamivu, wanafunzi 608 watapata shahada za umahiri wakati 19 wakipewa stashahada ya uzamili. Wahitimu wa shahada za awali watakuwa wengi zaidi, Profesa Anangisiye amesema watakuwa 6,382.

“Chuo kinawakaribisha wadau wote wa elimu kushiriki maadhimisho haya maalumu,” amesema Profesa Anangisye.

Mahafali hayo yatafanyika kwa siku mbili, Jumanne na Alhamisi katika ukumbi wa Mlimani City ambako Msekwa amesema atatoa hotuba kutathmini maendeleo ya miaka 50 ya elimu ya juu nchini.

Watakaohitimu Jumanne ni kutoka ndaki ya Teknolojia za Habari na Mawasiliano (Tehama), uhandisi na teknolojia, sayansi za kilimo na teknolojia ya chakula, na ndaki ya sayansi asilia na tumizi.

Alhamisi itawahusisha wahitimu kutoka ndaki ya sayansi za jamii, insia, na shule kuu ya elimu, biashara, sheria, uandishi wa habari na mawasiliano kwa umma, taasisi ya taaluma za maendeleo, na ile ya taaluma za Kiswahili.

“Nikuombe uje ukumbini kusikiliza hotuba yangu. Nilikuwa makamu mkuu wa kwanza wa chuo hiki wakati (Mwalimu Julius) Nyerere akiwa mwenyekiti. Tuliweka misingi ya elimu ya juu nchini,” amesema Msekwa alipoulizwa tathmini yake kuhusu maendeleo ya vyuo vikuu nchini
 
Akazie pia lile swala la wabunge waliovuliwa uanachama wa chama cha siasa wanakosa sifa za kuwa wabunge.
 

HONORARY DEGREES: A SHORT HISTORY​

Rosalie Silberman Abella speaking to crowd at podium at Commencement


HONORARY DEGREE RECIPIENT ROSALIE SILBERMAN ABELLA SPEAKS AT COMMENCEMENT 2017.

Honorary degrees appear to have arisen out of the practice of granting dispensations from certain particular academic requirements.

European universities began granting degrees “for the sake of the honor” (honoris causa) in the 15th century, and the first such degree was awarded at Oxford University in 1478 or 1479 to Lionel Woodville, Dean of Exeter, the brother-in-law of Edward IV and the future Bishop of Salisbury. These were essentially academic peerages, entitling the recipient to full privileges in the university, privileges that were much more extensive than now. At the same time universities conferred degrees on certain scholars whose career achievements warranted such recognition.

The first honorary degree awarded in America was an honorary doctor of divinity degree conferred by Harvard University in 1692 on its president, Increase Mather.

Recipients of an honorary doctorate do not normally adopt the title of “doctor.” In many countries, including the United Kingdom, Australia, New Zealand and the United States, it is not usual for an honorary doctor to use the formal title of “doctor,” regardless of the background circumstances for the award. An early and notable exception is Benjamin Franklin, who received an honorary doctorate from the University of St. Andrews in 1759 and the University of Oxford in 1762 for his scientific accomplishments, and thereafter referred to himself as “Doctor Franklin.”

Brandeis University, which awarded its first honorary degrees at its second commencement on June 14, 1953, bestows honorary degrees as a means to acknowledge the singular accomplishments or contributions of individual men and women; to identify the University with the values expressed through the work and accomplishments of the honoree; to draw attention to the University as an institution that respects and encourages such values and the manner in which those values are expressed; and to emphasize its own institutional mission and purposes.

The University honors individuals for distinctive achievement in the creative and performing arts, humanities, social sciences, sciences, public service, philanthropy, business, the learned professions, social justice, Jewish life, international understanding and human rights.

Honorary degree procedures and guidelines​

Criteria and guidelines​

Honorary degrees recognize those who have made profound and enduring contributions to scholarship, culture, and improved quality of life in society at large. Achievements of national or international significance deserve priority consideration. It is important that recipients be persons of great integrity, as the choices we make reflect our values as an institution.

SASA HUYO MSEKWA ANA SIFA ZA HIVYO HATA KAMA SIYO UNIVERSAL? HUYU AMBAYE HONI KASORO KATIAK REGIME HII!
 
Watakaohitimu Jumanne ni kutoka ndaki ya Teknolojia za Habari na Mawasiliano (Tehama), uhandisi na teknolojia, sayansi za kilimo na teknolojia ya chakula, na ndaki ya sayansi asilia na tumizi.
Kiingereza chake please
 
Yani Msekwa wanamfikiria leo wakati yule anayeimba imba sijui anaitwa diamond nilisikia walitaka kumpa hiyo PhD ya heshima miaka minne iliyopita!!!
 
Shahada ya umahili ni ipi?
Ni shahada ya Umahiri na sio Umahili.

Kimtiririko ziko hivi;
1. Astashahada= Certificate
2. Stashahada=Diploma
3. Shahada= Bachelor Degree
4. Stashahada ya Uzamili= Postgraduate Diploma
5. Shahada ya Umahiri= Masters Degree
6. Shahada ya Uzamivu= Philosophical Doctorate (Ph.D)

NOTE: Uzamili= postgraduate studies ambayo inahusisha stashahada ya uzamili, umahiri na Uzamivu.
 
Back
Top Bottom