Chuo cha Sokoine (SUA) chashika namba moja Tanzania (Citations)

Upepo wa Pesa

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
21,204
34,119
Moja kati ya kazi kuu za chuo chochote duniani ni TAFITI.

Chuo chochote hapa duniani kitaonekana bora kama kina wana sayansi (academicians) bora walio tuliza akili na kuandaa tafiti na ku publish tafiti zao kwenye juornal za kitaifa na kimataifa!

Kwa kuongoza kwenye citation ni ishara wazi kwamba SUA wana wanasayansi wanao fanya tafiti zenye tija duniani!

Na hii ndio sababu kuu wamekamata namba moja Tanzania!

Wakati madokta na maprofesa wa vyuo vingine wakitumia muda mwingi kuunga juhudi na kupiga siasa, hali ni tofauti kwa SUA!

Mimi kama Mtanzania mzalendo nachukua nafasi hii kukipongeza chuo kikuu cha kilimo Sokoine kwa hatua hii!!

Webometrics Ranking: Sokoine University of Agriculture ranked first place in citations

TRANSPARENT RANKING: Top Universities by Citations in Top Google Scholar profiles | Ranking Web of Universities: Webometrics ranks 30000 institutions


Capture.PNG
 
Mbona hizo tafiti hatuzioni kwenye kutatua changamoto za kila siku za wananchi, kwenye statitistics Tz tuko safi ila practically impact Zero, Mwaka unaisha husikie uvumbuzi wowote kutoka katika hivyo vyuo.
 
Nyie madogo mkitokaga na hizo bla bla huko ndio mnakuja kusumbua hakuna kazi, just do what's yours guy. Chuo kishike namba kisishike we soma maliza focus kwenye life yako.. watu hata shule hawajaenda wanasukuma life za maana nyie ni kukomaa na university rankings. Why should you care anyways?
 
"Madogo" ni akili sio umri
Uko sahihi, na mtu mwenye akili ndogo kamwe hawezi kuwa na uthubutu wa kupongeza kitu kinapofanyika kwa ufasaha!

Siku zote mtu mwenye akili ndogo au "dogo" atakua anaangalia maisha yake binafsi badala ya kuwaza na wengine!

Yeye chochote kinacho husu mafanikio au upigaji hatua kama taifa hataona ni cha maana!

Huyo ndiye dogo au kwa jina lingine mtu mwenye akili ndogo kama ulivyosema!!

NB: Sijui nchi za wenzetu zingekuwa wapi kama hawa "madogo" au watu wenye akili finyu wangekua wengi nchi zao! kamwe tusingekaa tuwasikie akina Musk na watafiti kama akina newton, Einstain nk nk.
 
Nyie madogo mkitokaga na hizo bla bla huko ndio mnakuja kusumbua hakuna kazi, just do what's yours guy. Chuo kishike namba kisishike we soma maliza focus kwenye life yako.. watu hata shule hawajaenda wanasukuma life za maana nyie ni kukomaa na university rankings. Why should you care anyways?
Siku zote "dogo" au mtu mwenye akili ndogo (kama ulivyo sema) hawezi ku-care linapokuja swala la maana kama tafiti!
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom