DOKEZO Chuo cha KCMC kinataka kuzuia wanafunzi wa mwaka wa nne kufanya mtihani wa semester 1 kama hawajalipa Ada ya semester 2

DOKEZO Chuo cha KCMC kinataka kuzuia wanafunzi wa mwaka wa nne kufanya mtihani wa semester 1 kama hawajalipa Ada ya semester 2

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

goldencrayon

Member
Joined
May 20, 2026
Posts
5
Reaction score
0
Chuo Cha KCMC kimetangaza rasmi kupitia CR wa wanafunzi udaktari (MD) mwaka wa nne kikiwataka kulipa ada ya semester ya pili ilihali bado wako semester ya kwanza na kinatishia kuwa hakitawaruhusu kufanya mitihani wa kumaliza semester ya kwanza (end of semester exam) hata kama ada yao ya mwaka wa kwanza imekamilika.

Na recently waziri mkuu alitoa maelekezo watu wasizuiwe kufanya mitihani. Lakini hapa wanataka kuzuia mitihani Kwa ada ya semester ambayo watu hata bado hawajaianza kwani semester ya kwanza inaishia 13/06/2026 na hawana hoja yoyote wanayoitoa

Huku ni mfululizo wa matukio ya kukosekana Kwa uwazi na uwajibikaji kuhusu pesa wanazolipa wanafunzi kwani hata mwaka jana wanafunzi Hawa wakiwa mwaka wa tatu walilazimika kulipa kiasi tsh 700,000 Kwa ajili ya "community health program" ambayo ilikua program hewa Kwasababu program hiyo huishia mwaka wa tatu tu.

Walipodai waliambiwa pesa hiyo itarudishwa na kuongezewa katika mwaka wa masomo uliofuata lakini chuo kimepiga kimya mpaka Leo na Kila wanafunzi tukiuliza majibu yanatolewa ya kejeli bila vikao rasmi walisema tu kuwa "TCU INAFAHAMU"
 
Chuo cha Ovyo kabisa. Asa kama mtu unalipiwa na HESLB?
 
Chuo Cha KCMC kimetangaza rasmi kupitia CR wa wanafunzi udaktari (MD) mwaka wa nne kikiwataka kulipa ada ya semester ya pili ilihali bado wako semester ya kwanza na kinatishia kuwa hakitawaruhusu kufanya mitihani wa kumaliza semester ya kwanza (end of semester exam)
Pole sana,

Hilo tangazo lao liko wapi? Ungetuonesha hata tangazo la CR wenu daktari.

Kila la kheri.
 
Back
Top Bottom